Kesi ya Mbowe: Shahidi mwingine naye asema hakuona viashiria vya ugaidi

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia, BJ, leo tarehe 24 Januari 2022.

Jaji ameingia Mahakamani saa 4 na dakika 55

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na wakili

Pius Hilla

Abdallah Chavula

Jenitreza Kitali

Nassoro Katuga

Esther Martin

Tulimanywa Majige

Ignasi Mwinuka

Wakili Peter Kibatala: ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala Wakili wa Mshtakiwa wa Nne, Nipo Pamoja na Wakili

Nashon Nkungu

Faraji Mangula

Dickson Matata

Michael Mwangasa

Idd Msawanga

Sisty Aloyce

Seleman Matauka

Jaji: anaita Washitakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na tupo tayari Kuendelea

Jaji: Wakili wa Utetezi

Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari Mheshimiwa Jaji

Jaji: Shahidi Nakukumbusha Siku ya Ijumaa Uliapa, Na Leo Utaendelea Kutoa Ushahidi Wako Chini ya Kiapo

Wakili Dickson Matata ananyanyuka na Kuendelea

Matata: Shahidi Habari

Shahidi: Salama

Matata: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulisema Wakati Mnafanya Ukamataji We Ulikuwa Detective Coplo

Shahidi: Siyo Sahihi

Matata: Ulikuwa nani

Shahidi: Detective

Matata: Utakubaliana na Mimi Kwamba Kwa nafasi hiyo Ulikuwa Unatakiwa Kufuatilia Vyombo Vya Habari na Bunge Ilikupata Taarifa za Ndani na Nje ya Nchi

Shahidi: Kufuatilia Habari ni Jambo la Kawaida Kabisa Kama Unataka Kufuatilia

Matata: Kama Ulikuwa Unafuatilia Uliwahi Kusikia Habari Ya Mtu Kupigwa Risasi Mkoani Dodoma anaitwa Tundu Antiphas Lissu

Shahidi: Ndiyo Niliwahi Kusikia

Matata: Unafahamu Kwamba Tundu Antipas Lissu ni Kiongozi za Chadema

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Na Kwamba alipigwa Risasi akiwa Kwenye Shughuli za Bunge, Dodoma

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Je Ulifuatilia Kuhusu Report ya Tukio hilo kutoka

Shahidi: Sijawahi Kufuatilia

Matata: pia Ushawahi Kusikia Kuvamiwa na Kuulizwa Kwa Freeman Mbowe Dodoma

Shahidi: Nishawahi Kusikia

Matata: Na Je Unafahamu Kwamba Freeman Mbowe ni Kiongozi wa Chadema

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Kwa hiyo Unathibitisha Kwamba Tundu Lissu na Freeman Mbowe ni Viongozi wa Chadema?

Shahidi: Ndiyo ni Viongozi Wa Chadema

Matata: Sasa Shahidi Kwa Ufahamu Wako Baada Ya Mtu Kama Tundu Lissu Kupigwa Risasi 16 anaruhusiwa Kuwa na Ulinzi au hatakiwi

Shahidi: Suala la Ulinzi ni La Mtu Binafsi, akiamua anakuwa na Ulinzi

Matata: Je unafahamu Kwamba Mmoja ya mtu Mliye Mkamata Rau Madukani ni Mlinzi Wa Mbowe? 

Shahidi: Sifahamu

Matata: Kwani Tukio la Rau Madukani lilifanyika lini? 

Shahidi: Tarehe 05 August 2020

Matata: Je Kipi Kilianza Kati ya Tukio la Lissu na Rau Madukani

Shahidi: Sifahamu

Matata: Je unafahamu Kwamba Washtakiwa Wanashtakiwa kwa Kula Njama za Kutenda Matendo Ya Ugaidi? 

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Moja ya shutuma pia, Ni kutaka Kumdhuru Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya

Shahidi: Ndiyo

Matata: Kwa kuwa Ole Sabaya alikuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Je Freeman Mbowe alikuwa mbunge wa wapi? 

Shahidi: Sifahamu alikuwa mbunge wa wapi, sijui kati ya SIHA au MOSHI ila najua alikuwa mbunge tu..

Matata: Je, hjawahi kusikia kiwa Freeman Mbowe alikuwa mbunge wa jimbo la Hai? 

Shahidi: Ndiyo maana nimesema nilikuwa sifahamu ni SIHA au wapi ila najua ni Machame…

Matata: Uliwahi Kusikia Kwenye Vyombo Vya Habari Kuwa SABAYA alisema 2020 Freeman Mbowe hawezi Kushinda Ubunge Hai.?

Shahidi: Sijui

Matata: Kazi Maalum Maana Yake ni nini, Uliposema Kwenye Ushahidi Wako Juzi

Shahidi: Haina Utofauti na kazi za Kawaida

Matata: Kwakuwa Umekiri Kuwa Kazi Maalum haina Utofauti na kazi za kawaida, kwanini wewe na Wenzako Mlipokuwa Mnakuja Hapa Mnasema kazi Maalum

Shahidi: Kwa Nature ya kesi, ilikuwa ni Kuzuia Uhalifu

Matata: Sasa Shahidi Nikisema Kwamba Kazi Maalum Ilikuwa Ni Kumdhoofisha Mbowe kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020 ili asiweze Kushinda Ubunge

Shahidi: Si Kweli, Ndiyo Maana Walikamatwa Wenyewe

Matata: Kwani Unaposema Walikamatwa Wenyewe, Hapa Mahakamani Hayupo na Mbowe? 

Shahidi: Mheshimiwa Mbowe naye Yupo

Matata: Wakati Unatoa Ushahidi Ulisema Wanataka Kufanya Ugaidi Kiongozi wao alikuwa Freeman Mbowe

Shahidi: Hapana Siyo Kiongozi Wao, Nilisema anayeratibu alikuwa Freeman Mbowe

Matata: Na Taarifa Za Kwamba anaratibu Ulizifahamu Mapema

Shahidi: Nilifahamu Tarehe 04 August 2020

Matata: Kama ulizipata, Je kwa Kawaida Mtu anayeratibu ni Mtuhumiwa au siyo Mtuhumiwa

Shahidi: Ni Mtuhumiwa

Matata: Kama ni Mtuhumiwa Ikumbushe Mahakama Mbowe alikamatwa lini

Shahidi: Sikumbuki Lini, ila ni 2021

Matata: Tukihesabu Tangu umezifahamu hizo Taarifa, Mpaka anakamatwa 2021 imepita angalau Miezi Mitano? 

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Kwa Hiyo Kwa Muda wote huo alikuwa hajakamatwa

Shahidi: Ndiyo alikuwa hajakamatwa

Matata: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulieleza ni Kwanini Mtu anayeratibu Ugaidi, ni kwa nini alikaa Miezi zaidi ya Mitano Bila Kufikishiwa Kwenye Vyombo Vya Dola

Shahidi: Sikueleza

Matata: Baada ya hilo Jibu lako bado Unakataa suala la Kuwakamata Walinzi Wa Mbowe haikuwa Kumdhoofisha Mbowe Wakati Wa Uchaguzi Mkuu wa 2020

Shahidi: Haikuwa hivyo

Matata: Wewe ni Polisi Wa Kituo Gani

Shahidi: Central Arusha

Matata: Wakati Unawakamata Ulikuwa na Cheo gani

Shahidi: Constable Wa Polisi

Matata: Wakati Mpo Central Arusha na mkaenda Kuwakamata Watuhumiwa Rau Madukani Mkoa Mwingine Wa Kilimanjaro

Shahidi: Ni sahihi

Matata/ Na Kwa Mujibu wa Utaratibu Wa Kipolisi, Polisi anapokuwa anaenda Mkoa Mwingine anatakiwa Kuwa na MOVEMENT ORDER

Shahidi: Ndiyo ni sahihi

Matata: Na Hiyo Movement Order Ndiyo inaonyesha Umetoka Mkoa Wako Kwenda Mkoa Mwingine Kufanya kazi fulani

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Na Ukikosa hiyo Movement Order Unakuwa unaenda Kufanya Kinyume na Taratibu

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Je Shahidi Wewe Umeleta Movement Order Hapa Mahakamani

Shahidi: Sijaja nayo

Matata: Baada ya Kufanya Mliyofanya Moshi Mkaelekea Dar es Salaam ambapo ni Mkoa Mwingine

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Ulileta Movement Order Kwamba Umekuja Dar es Salaam

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Matata: Ulisema Kwamba Ulikuwepo Kwenye Ukamataji pale Rau Madukani

Shahidi: Ni kweli

Matata: ulisema katika Ukamataji Ule Watuhumiwa walikuwa watatu, Ila Mmoja aliweza Kutoroka, ambaye anaitwa Moses Lijenje

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Je Umezungumzia Katika Ushahidi Wako Kwa Yoyote Kuendelea Kumtafuta Moses Lijenje

Shahidi: Sijazungumzia 

Matata: Mpaka Mnaleta Kesi Mahakamani, Upelelezi Ulikuwa Umekamilika

Shahidi: Mimi sifahamu kwa sababu Siyo Mpelelezi

Matata: una taarifa zozote za Moses Lijenje

Shahidi: Sina Taarifa

Matata: anatafutwa au hatafutwi? 

Shahidi: Taarifa za kuwa anatafutwa zipo na nazifahamu

Matata: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulieleza Mahakama Kwamba anaendelea Kutafutwa?

Shahidi: Nilieleza za Kwamba anaendelea Kutafutwa

Matata: Kwa Maelezo yako akikamatwa atakuja kuunganishwa Kwenye hii Kesi

Shahidi: Mpaka akamatwe

Matata: Je Shahidi Unafahamu Kwamba Makosa ya Ugaidi ni Makosa Makubwa Sana

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Na Je Unafahamu Kwamba suala la Ugaidi ni la kidunia

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Matata: Je unafahamu Kwamba Mtu anayetuhumiwa kwa Ugaidi ni Hatari Sana

Shahidi: Mpaka Mahakama ithibitishe

Matata: Je kati ya Mtu anayetuhumiwa kwa Kuiba Kuku na Mtu anayetuhumiwa Kwa Kufanya Ugaidi, nani ni Mtu hatari

Shahidi: Yote ni Makosa na Wote wanaweza Kuwa Hatari

Matata: Wakati unahojiwa na Wakili hapa, Ulizungumzia chochote Juu ya Moses Lijenje Kwamba Uchunguzi unaendelea, ikiwa kumtangaza Kwenye Gazeti ili Raia wema wasaidie?

Shahidi: Sijazungumzia

Matata: Kuhusu kumtangaza Kwenye Tv

Shahidi: Sijazungumzia

Matata: Kwakuwa Moses Lijenje alikuwa Mwanajeshi Ulizungumzia Chochote Kuhusu Kushirikiana na Jeshi liweze Kusaidia

Shahidi: Sija +zungumzia

Matata: Ulizungumzia kuhusu kushirikiana na Interpol Ili Kumkamata

Shahidi: Sijazungumzia

Matata: Ulizungumzia Kuhusu Kuongea na Vyombo Vya Kimataifa kama BBC ili Kuweza Kumkamata Moses Lijenje

Shahidi: Sijazungumzia

Matata: Ulizungumzia Kuhusiana Kuongea na Ofisi za mabalozi kuhusu Kumkamata Moses Lijenje

Shahidi: Sija zungumzia

Matata: Kuhusu Vyombo Vingine Vya Kimataifa Vya kupambana na Ugaidi

Shahidi: Sijazungumzia

Matata: Nilisikia Kwamba Mlipofika Central Police Moshi Mahita na Jumanne Ndiyo Walishuka

Shahidi: Ndiyo

Matata: Na Kwamba Mahita na Jumanne, Walipo rudi ndiyo Mkaenda Kumtafuta Moses Lijenje

Shahidi: Ni sahihi

Matata: Wakati Mpo Central Police Moshi, Je Mlikuwa na Mashahidi huru

Shahidi: Walikuwa Kwenye Gari Nyingine

Matata: Je Ulisema lolote Kwamba Mashahidi huru Walishuka kwenda Kuandika Maelezo

Shahidi: Walikuwa Kwenye Gari Nyingine

Matata: Je Ulieleza Mahakama kwamba uliwaona Mashahidi huru Wakishuka Central Moshi Kuandika Maelezo

Shahidi: Hiyo Sikueleza

Matata: Nikumbushe Mkiwa pale Rau Madukani Mlimkamata nini na wewe Ulimkabidhiwa nini

Shahidi: Tulimkamata Simu, Madawa ya Kulevya, Silaha na Risasi

Matata: Wewe Ulimkabidhiwa Vitu gani

Shahidi: Silaha na Simu

Matata: Wewe Ulijaza Hati za Kukamatia Mali?

Shahidi: Alijaza Afande Jumanne

Matata: alijaza Ngapi

Shahidi: Alijaza Mbili Mbili kwa Kila Mtuhumiwa

Matata: Wewe Ulishuhudia

Shahidi: Niliona, sikushuhudia

Matata: tulianza na Hati ya Kukamatia Mali za Adamoo, Je Hati ya Kwanza Ilikuwa na Nini na Nini

Shahidi: Ya Kwanza Ilikuwa na Simu na Silaha

Matata: Ya Pili ilikuwa na Nini

Shahidi: Ya Pili ilikuwa na Madawa ya Kulevya

Matata: Twende Kwa Mshitakiwa Wa Tatu Mohammed Ling’wenya, Ya Kwanza Ilikuwa na nini

Shahidi: Ya Kwanza Ilikuwa na Simu na Ya Pili ilikuwa na Madawa ya Kulevya

Matata: Sasa Shahidi Wakati unatoa Ushahidi Wako, Ulielezea Kwanini ziliandikwa zilitofautishwa kwa sababu ipi

Shahidi: Sikueleza

Matata: Shahidi Wewe Sasa Ulitoka na Vitu gani Mpaka Ukaja navyo Dar es Salaam

Shahidi: Simu na Silaha

Matata: Na Ulipofika Dar es Salaam Uliambiwa Ukabidhi Vielelezo Pale Central Polisi

Shahidi: Ndiyo

Matata: Na pale Ulimkabidhi Vitu gani Afande Nuru

Shahidi: Silaha na Risasi

Matata: Kwa hiyo Nuru Ndiyo Mtunza Vielelezo Pale Central polisi

Shahidi: Sahihi

Matata: Ukasema Simu Ulimkabidhi Afande Swila

Shahidi: Sahihi

Matata: Ulielezea Hapa Mahakamani Kwanini Simu alipewa Swila na siyo Mtunza Vielelezo

Shahidi: Hapana Sikueleza

Matata: Mheshimiwa Jaji ni Hayo tu

Kibatala: una elimu gani?

Shahidi: Degree

Kibatala: Chuo gani?

Shahidi: Open University

Kibatala: degree gani?

Shahidi: Sociology 

Kibatala: advance umesomea wapi?

Shahidi: Karatu

Kibatala: ulipata divisheni ngapi

Shahidi: Divisheni 3

Kibatala: Point ngapi?

Shahidi: 21

Kibatala: nikisema kwamba majibu yako yaendane na digrii nitakuwa nakukosea?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Msingi wa upelelezi unatakiwa uwe ProActive siyo mpaka ipate maelezo?

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Uwe umeshika silaha hujashika silaha wewe ni mpelelezi

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Ukasema Mahita alikwambia Kwamba Unaitwa na RCO ukachukua Silaha

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Katika Ushahidi Wako Kuna Mahala Yoyote ulisema Kwamba Kuna Kiongozi Yoyote alikwambia Majukumu yako ya Upelelezi yapo Suspended

Shahidi: Hakuna

Kibatala: Nilisikia Wakili amakueleza hapa Kuwa SMG ni Function au siyo Function

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je inategemewa Afisa wa Juu wa Polisi asema Kwamba Kuna Silaha inaitwa AK47 au SMG

Shahidi: Inategemea

Kibatala: Kwa hiyo Kinacho tofautisha Silaha ni Jina na siyo Function

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je hii Bunduki aina ya Luger ni A5340.?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ndiyo ilikamatwa kwa Adam Kasekwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wakati una wa Describe wale Watu Mahakamani, Kuna Mahala Kwenye Ushahidi Wako pia alijitambulisha kwenu la Adamoo

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wala Hukusema Kwamba Adam Kasekwa pia ni Adamoo

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Pia Hukusema Kwamba Mohammed Ling’wenya ndiye DOYI

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Ulimtaja Kakobe wala Siyo Moses Lijenje

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Moses Lijenje Katika Ushahidi Wako hukumtaja

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa Ushahidi Wako wewe Mlikuwa mnatafuta Kakobe

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Bunduki aina ya Luger A5340 Je ni Moja wapo ya silaha inayotolewa kwa maafisa wa Juu

Shahidi: Sijawahi kuona zaidi ya ile

Kibatala: Je Maafisa wa Juu anapewa bastola za aina gani

Shahidi: Chinese Pistol

Kibatala: Hakuna bastola zinaitwa Chinese Pistol,

Kibatala: Brand name yake ni nini

Shahidi: Sifahamu, mie najua zinaitwa Chinese Pistol

Kibatala: Je Unafahamu kwamba Bidhaa kama Simu ya Samsung Inaweza kutengenezwa Nchi Nyingine Kama Brazil kwa Makubaliano

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Baada ya Zoezi la Kukamata Silaha, Ukaenda Kuchukua Seizure Certificate kwenye Gari

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je ni kweli ulipokwenda kwenye Gari hukuambatana nao Kwenda kwenye Gari.?

Shahidi: Sikuambatana nao

Kibatala: Na Wakati unaenda Kwenye Gari hukuambatana na Washitakiwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na Ulipo rudi ulipatia tena Jumanne hiyo Bunduki

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: kwa hiyo Mmebadirishana na Jumanne Mara Mbili

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa mlisaini Hati ya Kukabidhiana na Jumanne Mara ngapi

Shahidi: Mara Moja tu

Kibatala: Mlisaini Hati ya Makabidhiano Baada ya Yeye kuKupatia, Mwanzo au Baada ya Kusaini Seizure Certificate?

Shahidi: Baada ya Kusaini Seizure Certificate

Kibatala: Kwa hiyo Mwanzo alipokupa Uende kwenye gari Hukusaini Makabidhiano?

Shahidi: Ndiyo alikuwa amenipa tu

Kibatala: Je Mshitakiwa Adam Kasekwa, alipewa nafasi ya Kurekodi namba ya Ile Silaha

Shahidi: alisomewa, Hakuandika

Kibatala: Je Wala Mashahidi huru Walipata nafasi ya Kurekodi ile namba ya silaha

Shahidi: Walisomewa, Kama Kuishika Kichwani inategemea Uwezo wao

Kibatala: Katika ile Seizure Certificate Je yaliwekwa Maneno CZ 100

Shahidi: Sikushuhudia

Kibatala: Je Kama Hukushuhudia Kilicho andikwa Pale Rau Madukani kwenye Seizure Certificate, Details zilizowekwa Kwenye Seizure Certificate Pale Rau Madukani ndiyo Details hizo hizo mlizokabidhiana na Nuru

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Naomba Kielelezo Namba 36

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji iwapo mahala popote kama kuna majina Adam Kasekwa maarufu kama Adamoo, kwenye hiyo kielelezo namba 36

Shahidi: Hakuna majina

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Upekuzi Uliopelekea Kukamatwa kwa hiyo Silaha Umefanyika Kwa nani kwenye Kielelezo namba 11

Shahidi: Kwa Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo

Kibatala: Na Wewe Ukisema hujawahi Kusikia Neno Adamoo

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Unafahamu Kwamba Nuru uliye Mkabidhi Vielelezo ina description ya CALLIBRE 9, CZ 100

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Unafahamu kwamba description ya kielelezo kinatakiwa kuwa vilevile kama Ilivyokatwa

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala Kama Nuru kaweka Maneno CZ 100 Ndiyo anajua Maneno haya ya ziada yaliyoongezwa?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: na hapa katika seizure certificate Chini Kuna Maneno Yamesema kwamba silaha Iliyochukuliwa kutoka Adam Kasekwa kama kuna Maneno CZ 100

Shahidi: Hakuna

Kibatala: Na Silaha hiyo Ndiyo inamuunganisha Adam Kasekwa na hii Kesi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Nilikusikia Katika Ushahidi Wako Ulisema kuhusu Silaha AK 47

Shahidi: sahihi

Kibatala: Je hii Silaha Ina Uhusiano wa Moja kwa Moja Kuhusu Kuwalinda Washtakiwa

Shahidi: Ina Umuhimu katika Ushahidi

Kibatala: Silaha inatolewa Je Kwa Utaratibu au Kama Pipi

Shahidi: Unachukua Kwa Kuandika Pale Chumba Cha Silaha

Kibatala: Je Hapa Mahakamani Umekuja na Makaratasi ya hiyo Silaha Hapa Mahakamani

Shahidi: Kwa Leo Sijaja nayo, Yakihtajika nitakuja nayo

Kibatala: Je Baada ya Kuja Dar es Salaam Kukabidhi Silaha, Ujawahi Kukabidhi popote

Shahidi: Ndiyo unaenda nayo hadi Nyumbani

Kibatala: Ndiyo Mafunzo Mliyopewa CCP

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wakati Watuhumiwa Wanafika DAR ilikuwa Saa Ngapi

Shahidi: Saa 12 kasoro

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba nini Kilikufanya Usikabidhi Kielelezo Saa 12 Kasorobo

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Katika Ushahidi Wako tunaona Ukienda Kunawa Uso Ukiwa na Vidhibiti

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Katika Ushahidi wako Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulimkabidhi Saa ngapi hiyo Silaha Siku ya Tarehe 07 August 2020

Shahidi Nilimwambia

Kibatala: Katika Kielelezo namba 36 Kuna Muda Unaomekana kwamba Mlikabidhiana Saa ngapi?

Shahidi: Hapana Muda hauonekani

Kibatala: Wewe huoni sasa Kwamba Kwa Kwenda Kuzurula na Silaha ambayo ni Kidhibiti, Imepelekea Nuru Kuongeza Maneno Mengine ya CZ 100? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Umwambia Jaji Kwamba Wakati wa Makabidhiano, Risasi zilitolewa Katika magazine mkahesabu

Shahidi: Hapana Sikusema

Kibatala: Kwamba Kuna Risasi Tatu Ndani ya magazine ulimwambia Wewe?

Shahidi: Hapana aliona yeye, Kwa Sababu ya Kuna Vitabu Vingine Vya kujaza,

Kibatala: Vitaje vitabu Vingine ni Vipi

Shahidi: anavijua Mtunza Kielelezo

Kibatala: Vitaje hivyo Vielelezo

Shahidi: Kuna Kitabu Kinaitwa PF 16

Kibatala: Je Ulionyeshwa kwenye Extract ya PF16 Kwamba Ndicho Kile Kilicho andikwa kwenye Seizure Certificate

Shahidi: Hapana Sikuonyeshwa

Kibatala: Wakati Upo Rau Madukani, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Afande Jumanne alitoa namba za Zile Risasi akawasomea Mashahidi huru

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: aje unafahamu kwamba Katika Uchunguzi wa Ballistic, Makabaki ya Risasi Mbili Kwenye kitako zina namba

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: Wakati Mpo Rau Madukani ukisikia Maneno Kati ya Kingai, Jumanne au Mahita Kwamba Adam Kasekwa ana haki ya Kuita , Ndugu, Jamaa au Rafiki

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ndiyo Maana Katika Kielelezo namba 11 sehemu ya Adamoo Kuweka Mashahidi Wake Pako wazi

Shahidi Pako wazi

Kibatala: Mnasema Wale Mashahidi walikuwa Mashahidi huru

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwamba Mmoja alikuwa Mmiliki wa ile Grocery

Shahidi: Hapana Siyo Mmiliki

Kibatala: Ulisema Kwamba Wakati Afande Kingai Alimtuma Mahita Kuangalia Kama Watuhumiwa Walikiwepo, Ulisema aliwakuta wapi Vile? 

Shahidi: Kwenye Grocery

Kibatala: Na bado hapo hapo huyo Mwenye Grocery Mnasema Shahidi Huru? 

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: unajua maana ya shahidi huru?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je unafahamu kuwa shahidi huru hatakiwi kuwa mtu mwenye mahusiano na mtuhumiwa kwa namna yoyote? 

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Vipi kama Adamoo alipishana kauli na kugombana na mwenye Grocery, Je atakuwa shahidi huru huyo? 

Shahidi: Hakunaaaaaaaa Bhanaaaaaaaa.. 

Mahakama: Kichekoo

Kibatala: Tutoke Kwenye Bunduki Twende Kwenye Simu

Kibatala: Kwanza Ulisikia kutoka kwa Kingai, Jumanne au Mahita Kuitwa kwa Viongozi Wa Serikali ya mtaa pale

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je unafahamu Kwamba Seizure Certificate ni Nakala tatu

Shahidi: Nafahamu ni Nakala Mbili

Kibatala: Je Ulishawahi Kushuhudia Adam Kasekwa akipewa Nakala yake ya Seizure Certificate

Shahidi: Ndiyo niliona

Kibatala: Nakala Nyingine Kabaki nayo nani

Shahidi: Ikabaki Kwenye Vielelezo Kwa Afande Jumanne

Kibatala: Wale Mashahidi Hawakupewa

Shahidi: Hawakupewa

Kibatala: Wewe ulipoenda Kwenye Gari Ulimkabidhiwa ngapi

Shahidi: Nilipewa Kwenye Bahasha, Si kuweza Kufahamu

Kibatala: Aliyekabidhi wa Kituo cha Polisi zile Seizure Certificate ni nani

Shahidi: Sijui nilizikuta Kwenye Gari

Kibatala: Ulizikagua Ulipoitoa Kwenye Gari

Shahidi: Si Kukagua

Kibatala: Kwahiyo Ka zilishajazwa Hujui

Shahidi: Hazikujazwa

Kibatala: zilijazwa Seizure Certificate ngapi kuhusu Madawa ya Kulevya

Shahidi: ilijazwa Moja na Nakala yake

Kibatala: Ile copy Ilienda Wapi

Shahidi: Alipewa Mtuhumiwa

Kibatala: Mtuhumiwa alisaini wapi Kwamba kapewa Seizure Certificate

Shahidi: Hakuna anaposaini

Kibatala: Hebu tuchoree Jiographia ya Pale

Shahidi: Barabara ya Lami, Kuna Glocery alafu Kuna Uchochoro

Kibatala: Mahala mlipo waweka Watuhumiwa Palikuwa na uchochoro

Shahidi: Ndiyo palikuwa na Uchochoro

Kibatala: Gari Mliyoenda nayo ilikuwa ya Namba Gani

Shahidi: Toyota Land Cruiser

Kibatala: Ilikuwa na Vioo Vya giza au Hakuna

Shahidi: ilikuwa navyo

Kibatala Twende Kwenye Simu sasa, Unasema Ulimkabidhi Inspector Ndowo lini

Shahidi Nilikabidhi 07 August 2020

Kibatala: Ulimkabidhi nani

Shahidi: Swila

Kibatala: Kwa Hati ya Makabidhiano

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: hiyo Hati ya Makabidhiano ipo hapa Mahakamani

Shahidi: Haipo Hapa Mahakamani

Kibatala: Hati ya Makabidhiano ndiyo ingeonyesha sasa IMEI namba

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Hati hiyo ya Makabidhiano ndiyo Ingekuwa na IMEI namba za Simu na IC CID

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Na wewe hapa Mahakamani hujataja IMEI namba

Shahidi: Sijataja

Kibatala: na SimCard mlizokabidhiana Haijataja ICCID namba

Shahidi: Sijataja namba

Kibatala: Wala unasema kwa Mheshimiwa Jaji Kwamba 07 August 2020 Kama Kweli Mlikabidhiana na Inspector Swila tulimtegemea tuone IMEI NAMBA na ICCID wakati wa Makabidhiano Tarehe 13 August 2020

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Na wala hujamwambia Jaji Kwamba Ulilinganisha

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: Umeleta Hati ya Makabidhiano ya Barua iliyofungua Uchunguzi pale Forensic Beaural?

Shahidi: Hapana Sijaleta

Kibatala: Baada ya Kufika Pale Forensic Beaural, Kwa Inspector Ndowo Ilikuwaje Makabidhiano

Shahidi: Tulikabidhiana kwa Hati ya Makabidhiano

Kibatala: Umeleta Hati ya Makabidhiano ya wewe na Ndowo

Shahidi: Hapana Sijaona Hapa Mahakamani

Kibatala: Inspector Ndowo anasema aliingiza Vielelezo Kwenye Kitabu Cha Register na siyo Hati ya Makabidhiano, Tusaidie Sasa mlijaza nini pale

Shahidi: Tulijaza Hati ya Makabidhiano na Kwenye Register

Kibatala: Je Register Ambayo Inspector Ndowo alijaza Kuhusu Vielelezo, Je Umeonyeshwa hapa Mahakamani

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwanini hizo Hati tatu za Makabidhiano ujazileta Mahakamani

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwanini Ujaleta Register Mahakamani

Shahidi: Sijamwambia Mheshimiwa Jaji

Kibatala: Na wala hujamwambia Jaji Kwamba mlibadilishana Namba na Inspector Ndowo

Shahidi: Hapana Sija Mwambia

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Siku Moja Ulipiga Siku Kwamba Umepata Dharula, badala yake aMkabidhi inspector Swila

Shahidi: Hapana Sija Mwambia

Kibatala: Wala hujamwambia Kwamba ni nani aliyetoa Maelekezo Kwamba akachukue Inspector Swila

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: na wala hujamwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Baada ya pale Swila Kupokea Vielelezo ulilinganisha Hati za Makabidhiano

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: Na wala hujamwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba ni lini Uliacha wala Kusimamia Majukumu Yako ya Kutunza Vielelezo, na akapewa Inspector Swila

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: Shahidi nakuonyesha maelezo yako yaliyochapwa soma KWA SAUTI

Shahidi: ANASOMA

Lakini kama anashtuka Mwenyewe hivi na kuhamaki.. 

Shahidi: Sikumbuki Kama Niliandika hivi,

Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba kupata maelezo yake halisi

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji ilishawahi kujitokeza na ikatolewa ruling kwenye proceedings hizi hizi

Kibatala: Mhe Jaji Tumekuwa too Much Technical, Kama hawana siyo tatizo la Mahakama wala letu

Jaji: Haipo Kwenye Possession Yao Bali ipo Upande wa Mahakama

Kibatala: nitaendelea, Wakati wa Break nitaomba wenzangu waifuate

Kibatala: Twende Kwenye simu na SimCard za Bwire

Kibatala: Nilisikia sahihi Kwamba Simu za Bwire zilichukuliwa na Kingai

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Seizure Certificate ya simu za Bwire Ulishawahi kuiona

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Simu na Simu Card Ulikabidhiwa kwa Makabidhiano

Shahidi: Hapana Nilipewa nizishike tu

Kibatala: kutoka Chang’ombe Mpaka Central Dar es Salaam ulikuwa Umezishika tu

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ulikuwa na Mashahidi huru Wakati wote Ukiwa Njiani kutoka Chang’ombe Mpaka Central

Shahidi: Hapana Sikuwa na Mashahidi huru

Kibatala: Ulikuwa na Bwire

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wakati Unamkabidhi Swila, Bila Seizure Certificate alipata nafasi ya kulinganisha

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Unafahamu Kwamba Swila Alihifadhi wapi hizo Simu

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Akaja Kukukabidhi tena simu na SimCard Tarehe 13 August 2020

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: umepewa Simu 8 na Swila 13.8.2020, Kuna Simu zilizo katwa Rau Madukani Tarehe 05 August 2020, na Zile za BWIRE zilizo Kamatwa za Bwire Siku ya Tarehe 10 August 2020

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: kwa hiyo Uwezi Kujua Kama Simu na Sim Card za Simu mbili ni Zenyewe au Siyo

Shahidi: Ndiyo siwezi Kufahamu

Kibatala: Turudi tena Moshi Kidogo

Kibatala: Mlipofika Central Police Station Moshi, nyie mlibaki ndani ya Gari

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ni wakati gani Mliwauliza kuhusu Mwenzao

Shahidi: Tulipo kuwa tunakaribia Kituoni

Kibatala: ulisikia Mtu yoyote ndani ya Gari a kwamba Nawauliza Lakini Mkijibu inaweza Kuchukuliwa ni sehemu ya Maelezo yao

Shahidi: Hapana Hakuna aliyesema

Kibatala: Je, unafahamu Kwamba Mtu ana haki zake Za Kujulishwa Makosa na Kumwambia Haki ya kunyamaza wakati wa Mahojiano?

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Kabla ya Mahita na Jumanne Kushuka Kwenye Gari, Mlikuwa Mmeshaaamua Kurudi Kumtafuta Kakobe au Bado hamjaamua? 

Shahidi: Tulikuwa tumeshaamua

Kibatala: Kuhusu ile Bahasha Kwenye Seizure Certificate, unajua ilitoka wapi

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Kamati anayejua Kuhusu ile Bahasha ni Afande Jumanne

Shahidi: Sifahamu

Kibatala’ Kabla ya kuanza Safari, Mlienda Aishi Machame Hotel

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Na kule Rau Madukani aliyeshuka pale ni Kingai au Mahita

Shahidi: Ni Mahita

Kibatala: Wakati Unatoa Maelezo yako Mwanzo a Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Unatoka CID ARUSHA

Shahidi: Hapana Sikumwambia

Kibatala: Katika Kielelezo namba 36 unasema umetoka wapi

Shahidi: CID ARUSHA

Kibatala: Uliongozwa Ukatoa Kielelezo namba 36, pamoja na kwamba wakati wa Utambulisho wako wewe ni Mpelelezi, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba CID ARUSHA ni nini

Shahidi: Sikufafanua

Kibatala: Uliwahi kusikia kuwepo Kwa njama zozote Sabaya akiwa Arusha? 

Shahidi: Ndiyo Tarehe 04 August 2020

Kibatala: kabla ya Tarehe 04 August 2020

Shahidi: Sijawahi kusikia

Kibatala: Ulishawahi kusikia njama za kumdhuru Sabaya ukiwa CID Ausha? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je uliwahi kusikia intelijensia kama mpelelezi njama za kufanya maandamano ya siyo na kikomo? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ulishawahi kusikia njama za kuchoma bituo vya mafuta Arusha ukiwa kama mpelelezi? 

Shahidi: Hapana, SIJAWAHI KUSIKIA

Kibatala: Na kama ungesikia unge’ report na kufanyia Kazi kwa sababu hayo ndiyo mambo ya kufanya Askari apandishwe cheo

Shahidi Hapana sijawahi kusikia

Kibatala: Ulishawahi kusikia kwamba Freeman Mbowe alikuwa anapanga njama za matendo ya kigaidi 

Shahidi: Hapana… Sijawahi kusikia

Kibatala: Unafahamu kuhusu kamati za ulinzi za wilaya na mkoa? 

Shahidi: ndiyo

Kibatala: Je Ulishawahi kusikia malalamiko Kutoka kamati za ulinzi za wilaya na mkoa kuhusu njama za Freeman Mbowe na matendo ya kigaidi? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Unafahamu kwamba Sabaya alikuwa Ndiyo mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya ya Hai? 

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je Sabaya alishawahi kuwalalamikia Kuhusu njama za kutaka kudhurika? 

Shahidi: Hapana sijawahi kusikia

Kibatala: Mheshimiwa Jaji naona saa saba Imefika, naomba kutoa hoja ya kuhairisha kwa muda

Wakili wa serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi 

Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba kukumbushia kidogo kuhusu ombi letu la maelezo ya shahidi 

Jaji nahairisha mpaka Saa 7 na dakika 45

Jaji anatoka

Jaji ameingia Mahakamani

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: kwa Upande wa Mawakili Wa Jamhuri tupo Kama Awali

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Upande wetu tupo Kama Awali, Isipokuwa Wakili Seleman Matauka amepata Dharula Kidogo

Jaji anaandika Kidogo palee

Mahakama ilikuwa kimya kwa muda..

Shahidi amerejea kizimbani, amekaa kwa unyonge sana.. Sio kama Asubuhi alivyokuwa na bashasha

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba kwa Hisani ya Mahakama hii Tukufu Nikumbushwe Nilipo Ishia

Jaji: Kama alifahamu Jinsi ambavyo Sabaya angedhuriwa, akasema Hapana

…….

Kibatala: Wewe upo Arusha, Mnabadilishana Taarifa na Arusha na Mikoa Mingine ya Kipolisi

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Ulishawahi Kupata Taarifa Kabla ya Tarehe 04.8.2020 ulisikia chochote kutoka kwa wapelelezi Wenzako wa Moshi Kuhusiana na Kikundi kinachopanga kufanya ugaidi?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je uliwahi kufahamu wewe na wapelelezi wenzio kuhusu kikao huko Moshi ikiwa ajenda ni kupanga matendo ya Ugaidi? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je uliwahi kusikia Aishi Hotel na mmiliki wake kuwekwa chini ya uangalizi na nyendo za pale sababu ya Ugaidi? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: hata baada ya tarehe 04 August 2020 ulishawahi kupata taarifa kwamba kuna kazi ya kufuatilia nyendo za Hotel na watu wa pale kuhusu Hotel yao kufanya ugaidi? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Baada ya Timu yenu Kuundwa, Na Baada ya Pale Kutoka Moshi hujawahi Kushughulika na Ile hotel tena? 

Shahidi: Sijawahi

Kibatala: Na Hata Wenzako hujawahi Kusikia Wakishughulika na Ile Hotel tena? 

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Timu yenu ya watu Sita akiwemo Dereva, Kuna Taarifa Nyingine ambazo Walikuwa wanazifahamu Kingai na Jumanne tu au Mlikuwa mazifahamu wote

Shahidi: Tulikuwa tunafahamu Taarifa zote kwa Pamoja

Kibatala: na Ungeshangaa Kama Kama Kuna wengine Wangekuwa wanawaficha Taarifa?? 

Shahidi: Tulikuwa tunafanya Kazi wote Kwa Pomoja

Kibatala: Je task force yenu Ilishawahi Kumuweka Freeman Mbowe chini ya uangalizi wakati wote kwa tuhuma za ugaidi? 

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je uliwahi kufahamu kwamba kuna Polisi wengine walimuweka Freeman Mbowe chini ya Surveillance kwa niaba yenu? 

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je Uliwahi kusikia kwamba washtakiwa wamepanga ku’ block barabara? 

Shahidi: Sijawahi kusikia

Kibatala: Je umewahi kusikia Kingai au Jumanne wakizungumzia kwamba washtakiwa walipanga ku’ block barabara fulani fulani? 

Shahidi: Hapana

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Katika Mambo yote haya, Adam Kasekwa aliwahi Kuwaambia Ile Bastola Ile Luger A5340 alipata Kwa nani

Shahidi: hajawahi kutuambia 

Kibatala: Je Kingai? 

Shahidi: Sijasikia

Kibatala: ufahamu wala kusikia ni namna gani alipanga kutumia bastola hiyo katika kutekeleza yale wanayoshtakiwa nayo na washtakiwa wenzie? 

Shahidi: Sijawahi kusikia

Kibatala: Je Unafahamu kuwa katika vitu Ulivyotaja kuwa mlikamata kwa Bwire, kama uniform za Jeshi zilikataliwa hapa mahakamani 

Shahidi: Hapana sifahamu

Kibatala: Shahidi Mlikabidhiana Na Stafff Sarjent Nuru, Je Ulieleza Lolote kuhusu Saini zako wewe na Nuru

Shahidi Hapana

Kibatala: Je Kuna Saini Zako wewe na Nuru

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ipo wapi

Shahidi: H4347

Kibatala: Soma Hapo Juu

Shahidi: Jina na Sahihi ya anayekabidhi

Lakini hii Ndiyo signature ya Kijeshi

Kibatala: ulimueleza Jaji hivyo

Shahidi: sikumueleza. 

Kibatala: Kielelezo namba P 37 na Yenyewe haina Saini yako

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: na yenyewe Ulimfafanulia Jaji Kuhusu hiyo Saini ya Kijeshi

Shahidi: Hapana Sikutoa Ufafanuzi

Kibatala: Katika Kielelezo hicho Kuna sehemu anayetuhumiwa Kuna Deshi na Makosa Deshi

Ukasema Majina hayapo Kwa Sababu Kuna File namba, Je unafahamu Kuwa Kesi hii Ina Washitakiwa Wanne, na wote wanashea Kesi namba Moja

Shahidi: Kama wote wanatumiwa Kwa Kosa Moja Lazima Majina yawe yote

Kibatala: hiyo Kumbukumbu namba si lazima niende Kwenye Faili

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Sasa hilo Kesi lipo wapi Hapa Mahakamani

Shahidi: Sijaliona

Kibatala: Mlikabidhiana Bastola na Risasi Wewe na Nuru Mara Mbili

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Tarehe 25 November 2020 kabla ya Kukabidhiwa Bastola na Nuru, Kwamba Mli Cross check Kwa Pamoja Kuona Kama Risasi zinafanana, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji? 

Shahidi: sikumwambia

Kibatala: Je ulimwambia mheshimiwa Jaji kwamba tarehe 25 November 2020 kwa pamoja na kulinganisha, magazine na risasi? 

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: Ile Seizure Certificate Pale Rau Madukani, Unafahamu Alianza Kusaini nani akafuata nani? 

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: Rau Madukani, Mnasema Kulikuwa na Mashahidi huru, Je Kuna mtu aliye Muuliza Huyu Dada aliye toka Grocery, Je Kuna Yoyote kati yenu aliye Muuliza huyu Dada Kuhusiana na Mmoja aliyetoroka? 

Shahidi: sifahamu

Kibatala: Majukumu ya Ulinzi Ulipewa wapi

Shahidi: Pale Rau Madukani

Kibatala: Ni nani aliyeambiwa na Kingai Kwamba Wewe Utakuwa Mpelelezi?

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Hati ya Makabidhiano ya Bunduki Kwa Ushahidi Wako Ilijazwa Kwenye Gari

Shahidi Mie Nilisaini Kwenye Gari

Kibatala: Je unafahamu alijaza wapi

Shahidi: Kwenye Gari

Kibatala: Mlikabidhiana Kwenye Gari?

Shahidi: Tulikabidhiana Chini, Tukasaini Kwenye Gari, Shahidi aliweka Afande jumanne

Kibatala: Je aliweka Lebel Kwenye Vielelezo Vipi

Shahidi: Aliweka Kwenye Simu tu siyo Silaha

Kibatala: Hizo Lebel Zina Rangi gani

Shahidi: Sizikumbuki

Kibatala: Ulionyeshwa hizo Simu Hapa Mahakamani

Shahidi: Ndiyo nilionyeshwa na Mheshimiwa Malya

Kibatala: Malya Ni Wakili Wa Serikali

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Vielelezo (dhibiti) Vinavyokamatwa palepale Vinawekwa Label

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: wewe Ulijiridjisha Kama Vielelezo Vyote Vina Label

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je ulifafanua Kwa Mheshimiwa Jaji kwanini Jumanne hakuweka Label Kwenye Silaha

Shahidi: Hapana Sikufafanua

Kibatala: aliye wakamata Watuhumiwa na Kuwaambia wapo Chini ya Ulinzi ni nani

Shahidi: alikuwa ni Afande Mahita

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji ile Gari ya Pili ilifika Saa ngapi

Shahidi: Nilieleza

Kibatala: Ulielezea Nani alikuwa anaendesha Gari ya pili

Shahidi: Hapana Sikueleza

Kibatala: aje Uliwahi kuhudhuria kozi yoyote ya kuhusu viashiria vya ugaidi 

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wapi

Shahidi: CCP Moshi

Kibatala: nitajie viashiria vitatu 

Shahidi: Kuhusu Kula Njama, State of Mind

Kibatala: ambapo wewe hukuona popote 

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ya Pili

Shahidi: Nimesahau

Kibatala: Ya tatu

Shahidi: Nimesahau

Kibatala: Seizure Certificate Afande Jumanne alikuwa anajaza kwenye Nini Meza au Mkono?

Shahidi: Aliweka Mguu kwenye Jiwe akawa anaandika Kwenye Diary Juu

Kibatala: Seizure Certificate Afande Jumanne alikuwa anajaza kwenye Nini Meza au Mkono?

Shahidi: Aliweka Mguu kwenye Jiwe akawa anaandika Kwenye Diary Juu

Kibatala: Je Unafahamu Afisa wa Polisi ambaye aliwakabidhisha hawa Polisi

Shahidi: Sikumbuki, Nilikuwa Nje

Kibatala: Je Ulishuhudia Sasa? 

Shahidi: Niliona lakini sikushuhudia

Kibatala: Na Mbweni Je? 

Shahidi: Niliona Waliingia Kituoni lakini sikushuhudia

Kibatala: Kwa Maana hiyo huwezi Kufahamu Kwamba Seizure Certificate zake aliziandika katika PPR? 

Shahidi: Sikuona, Sifahamu

Kibatala: lakini Unafahamu kwamba Mshtakiwa anatakiwa Kuandika Vitu Vyake katika PPR hata Seizure Certificate

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Je unafahamu Kwamba Timu yenu Ili kuwa Ina report kwa nani? 

Shahidi: Kwa Afande DCI

Kibatala: Je Kwa Ufahamu Wako Wewe DCI anafahamu Kwamba Mlikabidhiana Simu za Bwire Bila Hati ya Makabidhiano?? 

Shahidi: Sifahamu kama anafahamu Lolote

Kibatala: Katika Maelezo yako Unakumbuka Ulisema chochote Kuhusu Wewe Kupewa Majukumu ya Ulinzi pale Rau Madukani

Shahidi: Ndiyo niliandika

Kibatala: na katika Maelezo yako Unakumbuka Ulisema ulifika Saa Ngapi Dar es Salaam Central police? 

Shahidi: Saa 12 Kasorobo

Kibatala: Siyo Saa 12 kamili

Shahidi: Yote ndiyo yake Yale

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Sina Swali zaidiMWISHO

Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji nitauliza Maswalia Machache

Wakili wa Serikali: Shahidi Nakuuliza Maswali Kwa ajili ya Ufafanuzi

Wakili wa Serikali: Kuna Swali Uliulizwa Juzi Kuhusu Watuhumiwa Kuwekwa Kwenye Dr, Ukasema Ni sahihi, Ulikuwa Una maanisha Nini

Shahidi: unapopelekwa Kwenye Charge Room, lazima Uwekwe kwenye DR

Wakili wa Serikali Uliulizwa Swali Kuhusiana na Mtunza Vielelezo Ukasema Siyo lazima kumkabidhi

Shahidi: ndiyo siyo lazima Kwa sababu unaweza Kumkata Mtuhumiwa hapa Ukazipeleka kwa Mtunza Vielelezo Baadae

Wakili wa serikali: Uliulizwa Kuhusu Raiding Kwamba lazima Uwe Umetoa Taarifa Kituo cha karibu Ukasema Ndiyo,

Shahidi: Ndiyo sisi tulienda Kufanya arrest siyo Raiding

Wakili wa Serikali: Malya alikuuliza Kwamba Ulipotea Vielelezo, Ukasema Hapana, Tufafanulie

Shahidi: Si Kupoteza Vielelezo, + ulikuwa Unamaanisha nini

Shahidi: Si Kupoteza Vielelezo

Wakili wa serikali: Mallya alikuuza Kwamba Baada ya Kuwakamata Watuhumiwa Mlienda CCP Moshi Kuwatesa, Ukasema Kweli

Shahidi: Ni Kwa Sababu Hakuna Mahala Tumesema Watuhumiwa Walienda CCP kwenye Mateso

Wakili wa serikali: Leo Sasa Mahojiano na Kibatala, Kwamba Washtakiwa Ni Walinzi Wa Mbowe, ukasema Si Kweli

Shahidi: Hatukuwa kamata Sababu ni Walinzi Wa Mbowe

Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Ndugu wa Mtuhumiwa Wakati Wa Mshtakiwa anakamatwa, akasema Eneo la Ndugu Lipo wazi

Shahidi: Sababu sehemu ya Kuchukulia Mali ina Sehemu anajaza Maafisa Wawili, Lakini Hapa Yupo Mmoja na Katajwa Namba Moja tu

Wakili wa Serikali: Kwenye Swali hilo hilo Uliulizwa kuhusu Ndugu kuhusika

Shahidi: Ni Matakwa ya Mtuhumiwa Mwenyewe

Wakili wa Serikali Robert Kidando: anaendelea

Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kuhusiana Kama Mshitakiwa Khalfani Bwire, Zaidi ya Kuwekwa Mahabusu ya Chang’ombe, Ukasema Ufahamu

Shahidi: Kwa sababu Baada ya Kukamatwa Siku Ile Chang’ombe, Tuliondoka Na Kilicho Endelea ni Kazi ya Mpelelezi

Wakili wa Serikali: Ulionyeshwa Hati namba 36 na 37 ambapo Sehemu ya Sahihi ilisoma. Namba yako ya Kijeshi badala ya Saini

Shahidi: Askari Wa Cheo Cha Chini Harusiwi kukoroga

Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Hayo ni Mambo Mapya, Sisi tulifafanua au Lah

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kweli alisema ali fafanua

Jaji: Mimi Nilisikia alitoa Ufafanuzi

Wakili wa Serikali: Robert Kidando Je ulitoa ufafanuzi gani

Shahidi: Nilitoa Ufafanuzi Kuwa H4347 DC Goodluck Ndiyo Sahihi yangu na Jina langu

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia Hapo

Jaji: tunakushukuru Shahidi Kwa Ushahidi Wako

Wakili wa serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji huyo ndiye shahidi tuliyekuwa naye kwa leo, Hivyo tunaomba hairisho la kesi hii mpaka tarehe 26 January mheshimiwa Jaji

Kwani shahidi ambaye tulikuwa tumempa taarifa, tulimtegemea awe amefika leo ili aweze kuendelea kesho,

Ametupa taarifa mchana huu kuwa amepata dharula.. Hivyo hajaweza kusafiri leo, atasafiri kesho Kuja Dar es Salaam…

Wakili wa serikali: Katika Mazingira hayo Mheshimiwa Jaji, Ilikutoipotezea Mahakama Muda, Tunaomba Iridhie shauri hili lihairishwe mpaka tarehe 26 January 2022 badala ya kesho

Kibatala: Mheshimiwa Jaji nawakumbusha wenzetu kuwa washtakiwa wanasubiri kujua hatima yao, wafikirie kama ingekuwa ni wao au ndugu zao, wangefanya hayo wanayofanya?

Jaji: Kuhusu maombi ya hairisho hujasema kitu 

Kibatala: Naiachia mahakama Mheshimiwa Jaji

Jaji anaandika

Shahidi ameshuka kutoka kizimbani sasa, na ameketi katika pahali pa-Mawakili wa Serikali, ameloana Jasho Mgongoni kweli kweli, na sehemu za makwapani pia kuna jasho la kutosha..

Jaji: Naelekeza Jamhuri Kuleta mashahidi siku ya tarehe 26 January 2022

Washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza 

Jaji anatoka na kuondoka 

Like
5