Kesi ya Mbowe: Shahidi kutoka Tigo akiri mitambo ya simu yaweza kuingiliwa, kuchezewa

Mtobesya: Sikusikia ukisema kwamba Servers zinaweza kuingiliwa na Mahakama?

Shahidi (Tigo): Sahihi

Mtobesya: Wakati Jaji akiandika elezea HACKERS ni Watu gani

Shahidi (Tigo): Ni Wataalamu wa mitandao ambao wanasoma mfumo au wanakuwa wanaufahamu mfumo na wanatabia ya kujaribu kuingia kwenye mfumo, kuchukua ama kuharibu taarifa ama mfumo Wenyewe.

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema wakati unaongozwa na wakili wa serikali hukusema kama palikuwa na possibility ya hackers kuingia kwenye mfumo?

Shahidi (Tigo): Ndiyo Sikusema

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema hackers wana uwezo wa kuingia na kucheza na taarifa za READ ONLY kama alivyokuwa anakuongoza wakili wa serikali?

Shahidi (Tigo): Ndiyo uwezekano upo

Kutoka mahakamani kama ilivyowasilishwa na ripota rais, BJ, leo tarehe 02 Novemba 2021.

Jaji ameingia Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe Imeshatajwa

Wakili wa Serikali Robert Kidando Anatambulisha

  1. Pius Hilla

2. Nassoro Katuga

3. Abdallah Chavula

4. Ester Martin

5. Jenitreza Kitali

6. Tulimanywa Majige

Kibatala anatambulisha Jopo lake

1. Michael Mwangasa

2.Seleman Matauka

3.Nashon Nkungu

4.Alex Massaba

5.Michael Lugina

6.Maria Mushi

7.Hadija Aron

8.Dickson Matata

9.Jonathan Mndeme

10.Fredrick Kihwelo

11. John Malya

Jaji Mashtakiwa 1,2,3 na 4 Wananyanyuka kuashiria uwepo wao

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tunashahidi Mmoja Kwa Leo Lakini Kabla ya Kuendelea Leo tuna ombi, Na Maombi yetu yatamuhusu Shahidi Wa Leo Mheshimiwa.

Jaji: Wakati wa Kufile Mashahidi tuliorodhesha Majina Kama Frank Kapala

Jaji: Ndiyo

Wakili wa Serikali: na Kule Kwenye Comito Proceedings Katika Ukusara wa 32 wa zile proceeding za Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zilitaja Kama Frank Kapala Lakin kama tulivyo leta information Barua ya 11 August 2021 Ndiyo alitaja kama Frank Kapala Mheshimiwa Jaji Kwa Usahihi ….Shahidi huyu anaitwa Frank kapara.

Wakili wa serikali: Kwa hiyo tunaomba Kumbukumbu sahihi za Mahakama zi-note kama Frank Kapara Kwa kifungu 264 Sura ya 20 cha CPA Rev Ya 2009 Na Kwa sababu Ushahidi wa Shahidi huyu ulisomwa wakati wa Comito Proceedings tunaomba turuhusiwe Kuendelea na Shahidi huyu.

Jaji: Kifungu gani?

Wakili wa Serikali: 264 Sura ya 20 kama Ilivyofanyiwa marekebisho Mwaka 2009

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Maombi yetu ni hayo tu

Mtobesya: Tumesikia Maombi ya Upande wa Mashitaka na Kwa sababu Wanasema Substance ndiyo Iliyo contain Ushahidi Wake tangu Maelezo yake Polisi. Kwa Upande wetu hatuoni Kama inaathiri Haki za Mteja wetu, Hatupingi hilo Ombi Kwa niaba ya Mshitakiwa Wa Kwanza. Asante.

Wakili John Mallya: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili hatuna Pingamizi.

Wakili Fredrick Kihwelo: hatuna Pingamizi Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu.

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi Kwakuwa wameleta Maombi Rasmi.

Jaji: Samahani Kidogo, Unachotaka Kirekebishwe Unaweza Ku-Spell

Wakili wa Serikali: FREDY KAPALA

Jaji: Basi maombi ambayo yameletwa Kurekebisha Kumbukumbu za Mahakama Kuwa Shahidi alikuwa Frank Kampala na Sasa atafahamika kuwa ni FREDY Kapala Na hiyo ndiyo Itakuwa kumbukumbu Mpya ya Mahakama, NATOA AMRI. Mawakili wote Wananyuka na Kukubaliana na Jaji.

JAJI: Shahidi aletwe sasa

Wakili wa Serikali: Ameenda Kuitwa

Jaji: Anakuwa Shahidi Wa Ngapi huyo

Wakili wa Serikali: Shahidi 05

Jaji: Utetezi Ndiyo..?

Kibatala: Ndiyo

Jaji: Majina yako

Shahidi: Naitwa Afredy Kapala

Jaji: Umri

Shahidi: 38yr

Jaji: kabila

Shahidi: Mpare

Jaji: Shughuli yako

Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya Tigo

Jaji: Dini yako

Shahidi: Mkristo

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni Kweli, kweli tupu Eenheeeee Mwenyezi Mungu nisaidie.

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Wakili Nasorro Katuga atamuongoza

Wakili wa Serikali Nasorro: Nitakuuliza Maswali

Wakili wa Serikali: Umesema Unashughulika na nini?

Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya kibiashara inaitwa TIGO

Wakili wa Serikali: Kwanini Unasema Kampuni ya kibiashara

Shahidi: Kwa sababu kampuni iliyosainiwa Brela ni MIC Tanzania

Wakili wa Serikali: Jina la Kibiashara ndiyo

Shahidi: Tigo

Wakili wa Serikali: Kampuni ya MIC Tanzania Ltd Inafanya Shughuli gani?

Shahidi: Mawasiliano ya Simu pamoja na Mihamala ya Kifedha

Wakili wa Serikali: Mwambie Mheshimiwa Jaji Umeajiriwa lini

Shahidi: March Mwaka 2012

Wakili wa Serikali: Umeajiriwa kama nani?

Shahidi: Kama Mwanasheria wa Tigo

Wakili wa Serikali: Katika Kitengo Kipi

Shahidi: Kitengo cha Sheria

Wakili wa Serikali: Umesema Kampuni yako inajishughulisha Kutoa Mawasiliano ya Simu na Mihamala ya kifedha Iambie Mahakama kwa nani?

Shahidi: Kwa Wateja Ambao wanamiliki line za Mitandao ya Simu

Wakili wa Serikali: Hawa wateja Wa Tigo Wanapatikana Vipi?

Shahidi: Wanapatikana Kwa Kununua line za Tigo na Wakaitumia basi Wanakuwa Wateja wetu. Na ili ifanye kazi lazima ifanyiwe Usajili.

Wakili wa Serikali: Kwenye Kusajili mnasajili Kitu gani?

Shahidi: Kwa mtu ambaye ana kitambukisho cha NIDA tunatumia NATIONAL IDENTIFICATION NUMBER. Mtu anaye sajili ataingiza Namba ya Kitambulisho Cha Taifa Itasoma Taarifa.

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama process za Manunuzi ya Line kama zipo?

Shahidi: Mtu yoyote anaweza Kufika kwenye Duka au sehemu ambayo kuna Wakala anauza hizo line za Tigo akiwa na Kitambulisho Cha Taifa, Lakini pia Kuna Wageni ambao wanatakiwa kutumia passport….

Wakili wa Serikali: Mtu anaye jua atafanya nini?

Shahidi: Ataweke Kidole Kigumba, Zitasoma Taarifa zote ambazo zipo Kwenye NIDA, Kama Jina Na tarehe ya kuzaliwa Kwa hiyo Taarifa hiyo itachukuliwa Na kuhifadhiwa Kwenye Mfumo wa Tigo kama Taarifa za Owner au Mtumiaji wa hiyo line.

Wakili wa Serikali: Mtu asiyejua NIDA, unaposema Zinaenda Kutally na Taarifa za NIDA unamaanisha Nini?

Shahidi: NIDA nimfumo wa Usajili wa Vitambulisho Vya Taifa ambao unatunzwa na Authority

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama unaposema Taarifa zile zitachukukiwa na Kuhifadhiwa Tigo, Nani atazichukua

Shahidi: Tunasema Ki Electronic kuna Mfumo wetu ikizipata na Ikatally inatunza Kwetu, Kwa hiyo Mifumo inawasiliana

Wakili wa Serikali: Jinsi ya Kusajili line Taratibu ziko Vipi

Shahidi: Ukishanunua Laini na Kwamba wewe sasa Unawasiliana, Tuna kutumia Meseji Kuwa kama Unataka Kutumia huduma ya Mihamala ya Fedha, Ukisema Okey tunakupa Vigezo na Masharti.

Wakili wa Serikali: Hiko Kitendo Mnakiitaje?

Shahidi: Umejiregister Kwenye Huduma ya Tigopesa

Wakili wa Serikali: Nikurudiahe kwako sasa wewe Mwenyewe, Tigo Umeajiriwa kama Mwanasheria Je Majukumu yako ni Yapi

Shahidi: Kushauri Viongozi Maswala Yanayohusu Sheria, Kutengeneza Kusoma, kupitia na Kusaini Mikataba Kufuatilia, Kusimamia Kesi zote zinazohusiana na Tigo …Kumsaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama Katika Kupata Taarifa Mbalimbali Kutoka kwa Wateja zinapohitajika.

Wakili wa Serikali: Jingine, Baada ya kutoa hizo Taarifa

Shahidi: Kama Kuna Jinsi Yoyote Kusaidia Chombo chochote Katika Kutafuta Taarifa, Naweza Kusaidia Siyo VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama tu Bali hata Mtu Binafsi anaweza kupata Msaada wangu.

Wakili wa Serikali: Ni Vipi Mtu Binafsi, Mtu X anaweza kupata Taarifa za Mtu Y

Shahidi: Mtu Mmoja Kupata Taarifa za mtu Mwingine HAIWEZEKANI

Wakili wa Serikali: Kwa mujukumu hayo uliyoyataja, Unamajukumu gani au Ujuzi gani inayo Kusaidia katika Kutekeleza Majukumu yako

Shahidi: Kama Mwanasheria wa kampuni Nina Digrii ya Sheria, Nimesomea India JSS law college. Under MYSORI University, Ambayo niliipata 2009 Nilisoma Pia Advanced Computer Course, MYSORI University India 2007. Nilisoma Pia Advanced Diploma in Practice Nilimaliza Mwaka 2012 Baada ya hapo Kuna Training mbalimbali ambazo Nimezipata Nikiwa kazini 2012 nilipoanza Kazi

Wakili wa Serikali: Zitaje Training gani

Shahidi: Nilipopata kazi ilikuwa ni Majukumu yangu Nilikuwa nimeingia Kampuni ya Telecom Nilipata Training Ya Mwezi na nusu

Wakili wa Serikali: Ulisomea nini ktk hiyo Training

Shahidi: Mifumo ya Kujifunza Kutumia, ilikupata Taarifa Wa kwanza ni oracle Wa Kusaidia Kupata Taarifa mbalimbali zilizopo Sehemu za Kazi.

Shahidi: Kuna system Nyingine ambayo CONVIVER iliyokuwa Inasaidia Kupata Mihamala Yote ni soft ware BILL QUERY Iilikuwq Inasaidia Kujua matumizi Mbalimbali ya Mteja Upande wa Vocha Na SMAP ni Mfumo Sawa QUERY Kwa hiyo nilikuwa nasaidia VYOMBO Vya Ulinzi Na Usalama Kupata …Information.

Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka Ulikuwa unafanyiwa na nani

Shahidi: Ofisini na Mtu anaitwa Mr…..

Wakili wa Serikali: Ofisi za Tigo ziko wapi

Shahidi: Ofisi za Tigo Zipo Makumbusho DERM COMPLEX

Wakili wa Serikali: Unakumbuka Training Nyingine

Shahidi: 2015 palikuwa na Training Nyingine Baada ya Mifumo Kubadilika Baada ya oracle ikaja SQL Server CONVIVER ikaja Kubadirishwa Ikaja TELVIVER IKAJA ENVIVER ambayo sasa Ikaja Information Mbayo Ukiingia Unaona Matumizi …na Kila Kitu. Wanakufundisha Kule Unakoenda Kuchukua zile Information Siyo Kila amtu anaruhusiwa Kwenda Kuchukua Unafundishwa Jinsi gani ya Kuzilinda.

Wakili wa Serikali: Baada ya Mifumo Kubadilika sasa

Shahidi: Ikabidi tupate Training, Jinsi zinavyofanya kazi na Tabia zake

Wakili wa Serikali: Katika Training zako ulipata Lolote Kuhusiana na Information ambazo unaenda kufanyia Kazi

Shahidi: Wanakufundisha General Overview

Wakili wa Serikali: Umetaja Training za 2012 na 2015 Je una Training Nyingine

Shahidi: Zipo Nyingine hizo ni Major Kila Siku Dunia Ikileta System Mpya tutaambiwa tu Kuna Training za Kila Siku Katika Majukumu ya kazi

Wakili wa Serikali: Nikurudishe Nyuma Wakati Unataja Majukumu Yako Unasema Unasaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama. Je Ni VYOMBO gani

Shahidi: VYOMBO Vyote Vya Usalama Ukijumlisha Polisi, Jeshi, Kama ni Anga kama ni Ardhi na VYOMBO Vyote Vinavyofanya Uchunguzi wa Kisayansi. 2.Taarifa za Mihamala ya Fedha, Kutuma na Kupokea fedha 3. Kuna Recharge ya Vocha na Kutumia pamoja na Matumizi yake 4. Taarifa za Usajili 5. Taarifa Nyingine zote zinazoambatana Kama NIDA, LOCATIONS, BILL MBALIMBALI ANAZOLIPA

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama sasa Unawasaidia Kuwapa Taarifa, Je ni Taarifa zipi Mnawapa, ulikuwa unatumia Neno zinazoruhusiwa Kisheria

Shahidi: Zozote ambazo zitakuwa zinahitajika sisi tunazo 1.Kuna Kupiga na Kupokea Simu, Za wateja wetu zinaitwa Call Details …

Wakili wa Serikali: Shahidi Iambie Mahakama Hizo Taarifa wewe unazitoa wapi

Shahidi: (Tigo) Taarifa zote za kampuni pamoja na Wateja wake Zinakuwa Stored Kwenye Server

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Nani anaitoa Taarifa kwenye Server

Shahidi: (Tigo) Taarifa zote Zinakuwa Served Automatically Mtu anapo piga Simu Mnara Unasima na Taarifa zinashuka na Zina switch kwenda Automatically Kwenda Kwenye Server Kuwa stored. Lakini pia Kuna watu ambao ni Observers wa kungalia na Ku Audit kazi Nzima ya Server

Wakili wa Serikali: hizo Taarifa unazozitoa Unasema Zinakuwa self Generated, Je kiuadilifu kuwa hizi ni zile zilizojitengeneza, Uadilifu wake kwenye Server?

Shahidi: (Tigo) Kama kampuni ina Mifumo ya tofauti ilitengenezwa Mahususi Kulinda hizi Server na The Whole System

Wakili wa Serikali: Unaweza kuwa unaijua hiyo Mifumo

Shahidi: (Tigo) Yeah Naweza kukujibu Kuna Mfumo Obeservit, Server au Kutoka Kwenye Switch yanyewe inakuwa na Catalist Na Kuna HUAWEI pia

Wakili wa Serikali: Unajishughulisha na nini na unafanyaje kazi?

Shahidi: (Tigo) ni software ambayo kazi yake ni Kucheki Kama Kuna Mtu au kitu kili Intend Kuingia. Kuna Firewall ni Mfumo wa kuulinzi Pale kwetu wanatumia SISQO Kuchuja kinachoingia Na Kutoka Kwenda kwenye ….

Shahidi: (Tigo) Kuna Kitu Kinaitwa AUDIT Kuangalia nani na nani Kachukua nini na Kapita wapi Kingine kuna VAPT Volumeability Acess And Penetration Test Hizi Test zinafanywa na Watu ambao ni Very Profesional lakini ni Independent Office ambapo Mnawapa Kazi Ya Kuingia …. Kwenye Mifumo yenu So It’s the test Ukitaka Unamleta Unamwambia Vunja Mifumo yako Akijaribu anakwambia Wapi pana Udhaifu na wapi Mtu anaweza Kupita Inabidi Kufanya Test Mara kwa mara ili Ujue.

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Ili Usitujaze sana, Wewe Umeyajuaje

Shahidi: (Tigo) Training niliyopata, Kazi nilizofanya, uzoefu niliyopata, na Matatizo ya kila Siku (Challenge).

Wakili wa Serikali: Unaiambia Mahakama ndiyo yaliyokupa Ujuzi

SHAHIDI: (Tigo) Training, Experience ya 9yrs na Matatizo Computer nitakayopewa, nitapewa Acess kwa kuombewa Access Kwamba Mtu tuliyemuajiri anahitaji Kupata Access ili utendaji wake wa Kazi uwe Rahisi

Wakili Wa Serikali: Iambie Mahakama wewe Kwakuisaidia VYOMBO Pelelezi au VYOMBO Vya Ulinzi wewe Unafanyeje

Shahidi: (Tigo) Ukipata Kazi tuh, Kwa Maana ya kuajiriwa Kuna Vitendea Kazi kama Computer na simu ya Kwanza, Ni Vitu Vinavyo Configure Namaanisha Simu nitakayopewa na ..

Wakili wa Serikali: Unapoombewa Acess Unapewa Vitu gani?

Shahidi: (Tigo) wakati Unapewa Access Kuna SERVICE NOW system ambayo inampa Ruhusa Boss wako Ruhusa ya kuthibitisha kwamba unakuja Kufanya Kazi Fulani Kuna watu ambao ni IT security wanatakiwa kuangalia. Naingia Mara ya Kwanza Kwa Laptop lakini Kuna System Nyingine itaniambia Kama tunataka Password Yako Kuverify Either Inipigie Simu au Itumie sms, itatuma Alafu itatuma sasa Code ili niweze Kufungua Sasa Kwenye System.

Wakili wa Serikali: Sasa Umeshakuwa Approved Kwamba Huyu Mtu anafaa, Iambie Mahakama sasa Vitu gani Unakabidhiwa

Shahidi: (Tigo) Laptop Ukishapewa na Simu Kuna Vitu Vinakuwa vinawekwa ndani ya Laptop ambapo Kuna System Nyingine itaniruhusu Mimi Kuingia Mimi kwenye hiyo Computer.

Wakili wa Serikali: Code Unapewa Mara Moja unapo ajiriwa.?

Shahidi: (Tigo) Kila Ninapotaka Kuingia

Wakili wa Serikali: Nini Kitafuata

Shahidi: (Tigo) ndiyo nitakuwa na Uwezo wa Ku Access Emails, Kufungua Systems yoyote ile

Wakili wa Serikali: Nataka Kujua Sasa Jinsi ya Kuingia Kwenye Server

Shahidi: (Tigo) Kuna Mifumo sasa Nilitaja Mfumo wa SQL Itanisaidia ku-Commicate Kupata Taarifa mbalimbali

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Unaweza Je Kujua hapa umezipata na Utafanya nini

Shahidi: (Tigo) nikishaingia na kama nimezipata Kuna Button ya ku-Execute itazileta Kwenye Screen ya Laptop Yangu Kwamba naziona lakini siwezi ku-editi (READ ONLY) Kwamba naweza Kuziona tu ..nikitaka itaniruhusu Kuzi Print.

Wakili wa Serikali: Ishu ya kuvisaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama Utaratibu Ukoje

Shahidi: (Tigo) Kila Chombo Cha Ulinzi Kinahitaji Kuwa na Hizo Document iwe Amri au Ombi lazima iwe In Writing

Wakili wa Serikali: In Writing Unamaanisha nini?

Shahidi: (Tigo) iwe na Proper heading, naIwe na Nini wanataka

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ni Barua, lazima iwe hivyo

Shahidi: (Tigo) NI Barua au Order ya Mahakama

Wakili wa Serikali: Kwa kumbukumbu zako Mnamo tarehe 02 Mwezi 07 2021 ulikuwa wapi

Shahidi: (Tigo) nilipata Barua Mbalimbali za Maombi, Katika Barua hizo Kuna Barua ilitoka Kwa Kamishina wa Upelelezi wa Kisayansi Ikihitaji Taarifa za Namba ya mteja.

Wakili wa Serikali: Ulisema kuna aina Mbili Za Maombi kuwa kuna Maombi na Amri. Je hiyo ilikuwa nini?

Shahidi: (Tigo) Ilikuwa ni Requeast

Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka Ilikuja kwa Maombi Ya Kuomba Taarifa fulani za Namba fulani, Je unaweza Kukumbuka.? Hiyo namba uliyoombewa Kwenye Hiyo barua

Shahidi: (Tigo) Baada ya Kuifikiria Sana anaitaja 0719933386

Wakili wa Serikali: hilo Ombi lilikuwa ni Maombi Mangapi

Shahidi: (Tigo) yalikuwa Maombi ya Mihamala ya Fedha na KYC

Wakili wa Serikali: KYC unamaanisha nini

Shahidi: (Tigo) Usajili.

Wakili wa Serikali: baada ya Kupokea Sasa, Nini Ulifanya Kuhusiana na Ombi hilo

Shahidi: (Tigo) nilipopokea ombi Kutoka kwa kamishina, Niliingia Kwenye Computer yangu Nikaweka Credentials Zangu Nikafunga Screen Server Nikaingiza namba ya Simu kwenye Procedure Ambayo…Inaniruhusu Kupata Tigo Pesa.

Wakili wa Serikali: Unakumbuka Ilikuwa ni wakati gani?

Shahidi: (Tigo) walitaka Taarifa za mihamala ya Fedha kutoka 01 June ya 2020 Mpaka 31 June ya 2020 Nikaingia Kwenye Computer Nikaziona

Wakili wa Serikali: Baada Ya Kuziona

Shahidi: (Tigo): Nikaziprint

Wakili wa Serikali: Kabla ya kuziprint

Shahidi (Tigo): nili-execute Kuona Ni Yenyewe Nikaingiza Namba sehemu ambayo itanipa Usajili. Server yenyewe ilitoa Majibu Ambapo Taarifa Inapokaa iliweza Kutoa hiyo Taarifa ambayo niliweza Kuiomba.

Wakili wa Serikali: Na huko Unatumia Mfumo gani?

Shahidi(Tigo): SQL server

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Utendaji kazi wa Siku hiyo Ulikuwaje

Shahidi (Tigo): Laptop yangu ilikuwa Kwenye condition Nzuri Inafanya kazi Kawaida SQL sever ilikuwa Inafanya kazi Vizuri ….

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama hicho ulichokifanya, watu wapi wa Kitengo gani wanaweza Kuwa na Access ya Server kama wapo?

Shahidi: (Tigo) kila Mtu anapata Access Kutokana na Kazi anayoifanya ambapo Kuna watu wanaangalia ile server Kama Inapata Moto Kila wakati ili iweze Kufanya kazi yake

Wakili wa Serikali: Kama watu gani?

Shahidi (Tigo): Kama Legal Department Ambapo tulipaswa Kuwa na Access Ya Kuingia Kutokana na Order za Mahakama ni watu tunaoweza Kufanyia Kazi Haraka Kuna watu Wanaitwa Order Audit, Watu wa IT security Kuna watu pia wa Data warehouse …

Wakili wa Serikali: Nyinyi Legal Department Mnapewa Access ya Kufanyaje

Shahidi (Tigo): Kusaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama na lazima Muhuri wa MIC Tanzania Ltd

Wakili wa Serikali: Turudi Kwenye namba uliyotaja, Baada ya kuprint Ukafanya nini?

Shahidi (Tigo): Niliandika Barua kumjibu Kamishina wa Makosa ya kisayansi alichokuwa anakitafuta, nikamrudishia Katika Barua nilisha Print lazima Nigonge Muhuri na Signature yangu ….

Wakili wa Serikali: Ukiambatanisha na nini hiyo Barua?

Shahidi (Tigo): Cover later, Barua ya kamishina, Mihamala ya kifedha na KYC

Wakili wa Serikali: Ukafanya nini?

Shahidi (Tigo): Nikazipeleka Ofisi ya Cyber

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Leo hii Ukionyeshwa hiyo Barua na Hizo Print Out kama utaweza Kuzikumbuka.

Shahidi (Tigo): naweza Kuzimbuka kwa Barua yangu ambapo Cover later ipo kwenye headed Paper. Cover later Ya Tigo Nimesaini Nimegonga na Muhuri

Wakili wa Serikali: Barua Ukiona Utakumbuka

Shahidi (Tigo): Nitakumbuka kwa namba Niliyofanyia Kazi

Wakili wa Serikali: Namba ngapi

Shahidi (Tigo): Nimesahau

Wakili wa Serikali: Tarehe?

Shahidi (Tigo): Nimesahau ila ni 2020

Wakili wa Serikali: ambapo ulisema hiyo namba ni ngapi

Shahidi (Tigo): 0719933386

Wakili wa Serikali: Kingine

Shahidi (Tigo): Mihamala ya Fedha pia ninaweza kutambua Kwa sababu niligonga Muhuri wa MIC Tanzania Ltd

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Kwa ridhaa ya Mahakama naomba nimuonyeshe Shahidi Documents fulani Kama anaweza Kuzitambua.

Wakili wa Serikali: Anamkabidhi Makaratasi

Wakili wa Serikali: Nakupa hii Nyaraka Ishike iangalie Moja badala ya Nyingine

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Kama umeweza Kuitambua

Shahidi (Tigo): nimetambua Barua ya juu ambayo ni Cover later ambapo ina later Head ya Tigo

Wakili wa Serikali: Kingine

Shahidi (Tigo): Nimeona Muhuri Niliogonga na namba ambavyo Nililetewa kwenye Barua ya kamishina

Wakili wa Serikali: na KYC

Shahidi (Tigo): Same same Ina namba na pia nimegonga Muhuri za Usajili wa namba hiyo, Ziwe Kielelezo katika Kesi hii

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Sasa Unaiomba nini Mahakama

Shahidi (Tigo): Naomba Mahakama hii Ipokee Barua niliyoandika kwa kamishina Uchunguzi wa Kisayansi, Barua iliyokuwa inahitaji Taarifa alizokuwa akihitaji Mihamala ya Fedha ya namba iliyokuwa anaiombea na Taarifa …

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza hatuna Pingamizi

Malya: kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili hatuna Pingamizi

Fredrick Kihwelo: hatuna Pingamizi Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu

Peter Kibatala: na sisi pia kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi

Jaji: tunaweza Kukiita Kielelezo namba ngapi

Wakili wa Serikali: Namba 05 Mheshimiwa jaji

Mahakama ipo Kimya kwa Dakika 10 Sasa

Jaji: Mahakama Imepokea Barua ilivyoandikwa Kutaka Taarifa ya Uchunguzi wa Kisayansi kama Kielelezo namba 06 Napokea Barua ya Tigo, Majibu yao Kama Kielelezo namba 07 Napokea Print Out Kama Kielelezo namba 08 Na Mwisho Nyaraka ya KYC kama Kielelezo Namba 09.

Jaji: Sasa Naomba Shahidi utusomee Kila Kielelezo

Shahidi (Tigo): anasoma Barua ya Ombi la Kupatiwa Uchunguzi wa Kisayansi

Shahidi (Tigo): anasoma Barua ya majibu yao Kwa Kamishina wa Upelelezi wa Kisayansi Kwa niaba ya MIC Tanzania Ltd Ni matumaini Yangu Taarifa tuliyowapatia Itawasaidia

Shahidi (Tigo): anasoma Taarifa ya Mihamala ya Kifedha.

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji nafikiri Shahidi (Tigo) hawezi Kusoma hiyo Nyaraka yote tutakesha hapa Wao Wamuongoze na Kisha Tukubaliane kuwa Nyaraka ilisomwa.

Jaji: upande wa serikali

Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Jaji

Wakili wa Serikali:Shahidi tufafanulie Maneno Ya Juu kama Sender Maana yake nini

Shahidi (Tigo): Send My Op namba 0719933386 Receiver 0787555200 Miamala wa Tarehe 20 Kiasi 500,0000 Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 21na Balance Ilikuwa 2.3M

Wakili wa Serikali: Twende kwenye hii KYC Kielelezo namba 09

Shahidi (Tigo): Imeanza na namba pale Juu Jina la Kwanza Jina la Katika, Taifa, Jenda na Vitu Vinginevyo Mstari unaofuata 0719933386 Jina Freeman Last name Mbowe Nationality Tanzanian From Kilimanjaro

Shahidi (Tigo): Kuna namba ya Tigo ya O719933386 imetuma kiasi cha fedha Tsh 500,000 kwenda kwa namba ya Airtel namba 0787555200

Wakili wa Serikali: IOP Maana Yake nini?

Shahidi (Tigo): Kitu Kimetumwa kutoka Namba hiyo

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa hayo ndiyo maeneo ambayo tulikuwa tunaomba Shahidi ayasome

Wakili wa Serikali:Kielelezo namba 7 iambie Mahakama ni nini?

Shahidi (Tigo): Barua iliyotoka kwa Kamishina Ikiwa inataka taarifa za mteja

Wakili wa Serikali: Tarehe 20.7.2020 inaonekana nini.

Wakili wa Serikali: Sender City maana yake nini?

Shahidi: Mnara wa mtu aliyetuma Pesa alikuwa wapi?

Wakili wa Serikali: Fafanua Sender One Mikocheni

Shahidi: aliyetuma fedha alikuwa Mikocheni na alikuwa Kinondoni

Wakili wa Serikali: Fafanua hapo Kwamba Mikocheni ipo Kinondoni

Shahidi (Tigo): hapana, MIKOCHENI ni KITONGOJI

Wakili wa Serikali: Kielelezo namba 9 Kuna Kitu Umesema First name na Middle name Na ulianzana namba

Shahidi: 0719933386 ni namba ya Tigo

Shahidi: First name Freeman, Middle name Aikael, Last name Mbowe

Wakili wa Serikali: Maana yake

Shahidi (Tigo): namba inamilikiwa na Mtu anaitwa Freeman Aikael Mbowe

Wakili wa Serikali: chini ni nini

Shahidi (Tigo): Tarehe ya kuzaliwa

Wakili wa Serikali: ID proof Maana yake nini?

Shahidi (Tigo): Kitambulisho kilichotumika Kusajilia namba

WS: Mwenye namba hii alisajili kwa alama za Vidole tarehe ngapi?

Shahidi (Tigo): 16.9.2019

Wakili wa Serikali: hizi Null Null Null fafanua kidogo

Shahidi (Tigo): System haipati Taarifa za Usajili wa wakati Ule wa zamani

Shahidi (Tigo): Nilienda Kutoa Maelezo yangu katika Taarifa nilizozitoa

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu, Namuacha Mikononi Mwa Mahakama

Shahidi (Tigo): alinipigia Simu Kwamba yeye ni Askari Polisi na Kwamba nahitaji kutoa Maelezo

Wakili wa Serikali: Alikuambia nini?

Shahidi (Tigo): aliniambia Kuhusiana na Taarifa zako ambazo Ulizotoa

Wakili wa Serikali: Wewe Ukafanya Nini

Wakili wa Serikali:Tarehe 08 July 2021 Unakumbuka nini?

Shahidi (Tigo): Nikitakiwa kutoa Maelezo kituoni, kituo cha Polisi Central, Si kuandika Maelezo

Wakili wa Serikali: Ulitakiwa na nani?

Shahidi (Tigo): Kuna Inspector wa Polisi alinitafuta

Wakili wa Serikali: alikutafutaje

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Kabla hatujaanza maswali ya dodoso nilikuwa naomba Mahakama itambue uwepo wa wakili mwenzangu Nashon Nkungu

Jaji anaandika Kidogo..

Mtobesya: Nilikuwa naongea na wenzangu kama Tutapata mapumziko ya Afya lakini naomba Niulize mimi Japo kwa nusu saa tu baada ya Hapa Nina kesi mahakama ya Rufani nitaacha wenzangu waendelee

Jaji: itakuwa vizuri ukitumia dakika 20

Mtobesya: Shahidi Wakati naongozwa na wakili wa serikali ulielezea kwa urefu sana namna ambavyo mnafanya kulinda mfumo wenu Pamoja na Server. Je Ni sahihi?

Shahidi: Ni sahihi

Mtobesya: Lakini Hukuiambia Mahakama Mpaka Wakati Unatoa Taarifa hapakuwa pamefanyika Audit ya namna gani na Kwamba System Ilikuwa Vizuri.

Shahidi: Sahihi

Mtobesya: Sikusikia Ukisema Kwamba Servers zinaweza kuingiliwa na Mahakama?

Shahidi (Tigo): Sahihi

Mtobesya: Wakati Jaji akiandika elezea HACKERS ni Watu gani

Shahidi (Tigo): Ni Wataalamu wa mitandao ambao wanasoma mfumo au wanakuwa wanaufahamu mfumo na wanatabia ya kujaribu kuingia kwenye mfumo, kuchukua ama kuharibu taarifa ama mfumo Wenyewe.

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema wakati unaongozwa na wakili wa serikali hukusema kama palikuwa na possibility ya hackers kuingia kwenye mfumo?

Shahidi (Tigo): Ndiyo Sikusema

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema hackers wana uwezo wa kuingia na kucheza na taarifa za READ ONLY kama alivyokuwa anakuongoza wakili wa serikali?

Shahidi (Tigo): Ndiyo uwezekano upo

Mtobesya: Ofisi ya Tigo ulisema ni nini

Shahidi (Tigo): Jina la Kibiashara

Mtobesya: Ofisini kwenu kuna wanasheria Wangapi?

Shahidi (Tigo): Kwa Ujumla au Legal Department.?

Mtobesya: Legal Department

Shahidi (Tigo): Watatu

Mtobesya: Nilisikia Ulisema wanaweza Kuingia Kwenye Mfumo ni watu wa Mantainance na Audit, Je Kuna lolote Umetoa lenye Jina lako kwamba wewe ndiyo ulishughulikia Taarifa hizi?

Shahidi (Tigo): Mbali na Barua kwa kweli Hakuna

Mtobesya: na Barua pia haina Jina?

Shahidi (Tigo): Ndiyo haina Jina

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Barua ithibitishe hiyo

Mtobesya: Nitakuwa sahihi Nikisema Kwenye Taarifa ya KYC (KNOW YOUR CLIENT) haihitaji Barua za Utambulisho kama Serikali za Mitaa?

Shahidi (Tigo): Hapana haihitaji

Mtobesya: tuweke Record sawa kwa hiyo hata Photocopy Ya Kitambulisho Cha NIDA haihitajiki

Shahidi: NI Scanned ID

Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema KYC inatakiwa iambatane na hiyo Image ya Kitambulisho Cha NIDA

Shahidi (Tigo): Siyo lazima

Mtobesya: Nitakuwa sasa Kwenye Kielelezo namba 09 Cha Mtu Uliye Sema ni Freeman Mbowe Taarifa zake Hazipo Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 09

Mtobesya: Nionyeshe Jina la Mtumishi aliyesajili

Shahidi (Tigo): Siyo Mtumishi ni Mtu Mwenye Device

Mtobesya: Ndiyo huyo huyo Nionyeshe Jina lake

Shahidi (Tigo): Halipo

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema hata Mtu aliye sajili haionekani alisajilia wapi?

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Shahidi (Tigo): Legal Department

Mallya: Ulitaja Department Zingine Kwenye Ushahidi wako

Shahidi (Tigo): Ndiyo Kama IT Security

Mallya: Kazi zake?

Shahidi (Tigo): Ulinzi wa Taarifa za Mfumo na Taarifa zote zinazoshughulika na wateja

Mallya: Shahidi wewe ni Wakili siyo

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Umekuwa admitted kwenye bar mwaka gani?

Shahidi (Tigo): 2013

Mallya: Tigo Umeajiriwa lini

Shahidi (Tigo): 2012

Mallya: na Uliajiriwa department gani?

Mallya: Hiyo Department ya Security Bwana Yahaya Zahoro ndiye anayeshughulikia taarifa kama hizi?

Shahidi (Tigo): Yeye ni Internal Investgation Officer

Mallya: yeye ndiye anaye Shughulikia Maswala kama haya

Shahidi (Tigo): Siyo haya

Mallya: Upi Ulianza

Shahidi (Tigo): Ulianza CONVIVER Ukaja Telepin

Mallya: kwanini waliondoa CONVIVER

Shahidi (Tigo): Kwa sababu ya Mabadiliko ya muda na Technology

Mallya: kuna Department inayoshughulika na Masuala External Investigation

Shahidi (Tigo): hatuna, hiyo labda ni Polisi na Serikali

Mallya: Ulizungumza lolote kuhusu Telepin

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Ulisema ni nini

Shahidi (Tigo): Mfumo Mmoja Ulikuja Kure place Mwingine

Mallya: Wakati Unatoa Exhibit P8 suala la Miamala ya Fedha Ulielezea Mahakama Kwamba Ulizungumza Kutoka Kwenye Software gani?

Shahidi: Screen Server

Mallya: Wakati Unaona hizi Taarifa Ulisema Umetumia Mechanism Gani Kugenerate hii Print Out

Shahidi: Nilichagua Option ya Kuprint

Mallya: Kwanini Ulichagua Kwanini Uliacha Option Ya Screenshort ukaamua Kuprint?

Shahidi (Tigo) Ilikuwa ishu ya Choice tu

Mallya: Kuhusiana na Jina lako Mwanzoni palikuwa na Maombi ya Kubadili Kutoka Frank Kwenda FREDY,

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Mallya: Je Kapala ni R au L Mwishoni

Shahidi (Tigo): NI L Mwisho

Mallya: Kwa hiyo huyu Kapara siyo wewe

Shahidi (Tigo): Inaweza Kuwa wamechanganya

Mallya: Wewe ni Wakili unajua Madhara ya kukosewa Jina

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Life cycle ya Simu Card unaweza Kupata Wapi?

Shahidi (Tigo): SQL server

Mallya: Mimi ninao Ushahidi inapatikana Kwenye SMAP

Shahidi (Tigo): Ndiyo inapatikana pia

Mallya: Unababilisha Jibu eeh!

Shahidi (Tigo): Hapana Kote unaweza Kupata Kote

Mallya: Taarifa uliyoileta KYC ni Taarifa Accuracy?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unataka Mahakama Ikueleweje ukisema Accuracy?

Shahidi: Nimezipata Kwa Njia iliyokamilika sina Wasiwasi nazo

Mallya: Hapo Kuna Mpangilio wa Taarifa Je umeelezea Sababu Ya Kupanga hivi?

Shahidi: Hapana

Mallya: Kuna City imeandikwa Kilimanjaro Je Ulimwambia Jaji hiyo Kilimanjaro City Unaifahamu

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Hiyo Kilimanjaro City unaifahamu

Shahidi (Tigo): Hakuna Kilimanjaro City

Mallya: Kuna District inaitwa Kinondoni, Je huko Kilimanjaro inaweza kuwa District ya Kinondoni?

Shahidi (Tigo): SAMAHANI KIDOGO

Mallya: NISHAKUSAMEHE

Shahidi (Tigo): RUDIA SWALI

Mallya: Kuna City ya Kilimanjaro, kuna District ya Kinondoni

Shahidi (Tigo): Hakuna

Mallya: Kuna sehemu hapo imeandikwa Region, Region gani?

Shahidi (Tigo): Kimyaaaaaaaaaa

Mallya: Je huko Dodoma Kuna Sehemu Inaitwa Kilimanjaro City?

Shahidi (Tigo): Hakuna

Mallya: Unasemaje Kuhusu hizo Taarifa?

Shahidi (Tigo): Kuna Taarifa ambazo zipo NIDA so Ukiweka Kidogo Nauliza Mfumo wa NIDA, Mtu Mwenye Jina hili na Fingerprints hizi Zina Match Zinasoma anaitwa nani, na Taarifa zake zote zinakuja,Kama hazipo zinakuja Kuhuishwa siyo Za NIDA Kama hazipo ni za kwetu sisi.

Mallya: kama Taarifa hakuna Je Freeman Mbowe alijisajili Mwenyewe?

Shahidi: Nahisi Wakili hatuelewani katika hili, Nilisha Sema Kama Taarifa zilizotakiwa Kuchukuliwa NIDA kama Hawana Sisi tulipaswa kuchukua NIDA

Mallya: Kielelezo 09 kimetoka kwenu au NIDA?

Shahidi: kwetu

Mallya: Kwa hiyo Hiyo Mitambo ya kuprint ipo NIDA au Ofisini Kwenu?

Shahidi (Tigo): Ofisini Kwetu

Mallya: Aliyemsajili Mbowe nani kama Kweli Mbowe ana namba ya Tigo?

Shahidi (Tigo): Simjui

Mallya: Kwanini humjui?

Shahidi (Tigo): Sababu Kwenye Taarifa hiyo Sijamuona

Mallya: Nitakuwa sahihi Nikisema Taarifa Yenu Haipo Kamili nitakuwa Sahihi?

Shahidi (Tigo): Haupo Sahihi

Mallya: Pale Ofisini Kuna Department ya Tigo Pesa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Ulizungumzia kuhusu Tigo Pesa Department.?

Shahidi (Tigo): Sikuzungumzia.

Mallya: Mimi siijui kama namba ni ya Freeman Mbowe au Lah, lakini hebu niambie Pale Kwenu Kuna Kitengo cha Business to Business kama Post paid?

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Ulizungumzia Hiyo?

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Hii namna ya Kujibu Mabarua ni Standard Form au Kila Barua na namna yake?

Shahidi (Tigo): NI Standard Form

Mallya: Lengo la Kuweka ENEO la Kujaza Kosa la Mteja wenu wanalomchunguza nalo?

Shahidi (Tigo): NI Format ya Kuweka Kosa wanalo mchunguza nalo

Mallya: Je Polisi Wakitaka Uwape Taarifa ya kuchunguza Girl Friend wake we utatoa taarifa?

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Je wewe Ulipata Kuuliza Wana mtuhumu Kwa Makosa gani?

Shahidi (Tigo): Hapana Sikuuliza

Shahidi (Tigo): Siyo lazima pawe na kosa la Jinai, Kazi yangu ni kuona Kama Wamekidhi vigezo

Mallya: Ni Mara yako ya Kwanza Kupata Barua Kutoka Forensic Bureau?

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Kwa hiyo wewe Ukatoa Taarifa hata kama Mtu anataka Kujua anamtumia pesa Mpenzi wake

Shahidi (Tigo): Siyo Utaratibu wangu wa Kazi

Mallya: Kwa hiyo nyie Tigo mnataka Kutuambia Kuwa Polisi Wakitaka Taarifa hata kama hawana Kosa la Kuchunguza Mtawapa?

Mallya: Kwani Forensic Bureau Wanahusika na masuala ya ndoa na matunzo ya watoto?

Shahidi (Tigo): Mimi naangalia namba na kutoa taarifa

Mallya: Hukuona umuhimu wa kujua kosa..?

Shahidi ( Tigo): Siyo kazi yangu kujua makosa

Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Jaji; anaandika Kidogo

Jaji; Tutaenda break Dakika Ngapi?

Kibatala: Ngoja tushauriane

Jaji; Sawa Wakili wa Serikali; Tumekubaliana na Wenzetu Tubreak Kwa Dakika 40 turudi saa 08 kamili

Jaji; basi tunabreaka kwa Dakika 40 tutarudi Saa 08 kamili, Naomba tutunze Muda

Jaji ameingia tena Kesi inatajwa tena.

Kibatala: Naomba Wakili Dickson Matata Kwa Ruhusa yako aingizwe Katika column Nilimuombea Ruhusa Kwamba atachelelewa na Kwa Sasa ameshafika Namualika Wakili wa Mshtakiwa wa 03 aweze Kuuliza Maswali ya Dodoso

Matata: Nilikusikia Kwamba Kwenye Kitengo Cha Sheria Mpo watatu

Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili wa Serikali Ukusema nani Mkuu wa Idara Yenu

Matata: Na Hukusema Wewe licha ya Kuwa Mwanasheria Ni Mkuu wa Idara, Kweli siyo kweli

Shahidi: (Tigo) +/ Siyo Kweli

Matata: licha ya Kuwa Wewe Mwanasheria Hukusema Wewe unanafasi gani Nyingine

Shahidi: Siyo Kweli Matata Ikae hivyo hivyo Mheshimiwa Jaji

Matata: Wewe Ndiyo umepokea Barua, wewe Ndiyo umeprint Taarifa, na Wewe Ndiyo Umepeleka Majibu Polisi

Shahidi (Tigo): Sijaelewa

Matata: Wewe Ndiyo ulipokea Barua

Shahidi (Tigo): Sahihi

Matata: wewe Ndiyo uliandika Barua

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Nitakuwa sahihi nikisema wewe Ulifanya Kila Kitu Kwa Niaba ya Tigo

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Ulielezea mahakama kwamba kwanini wenzio 3 hawakushiriki katika hiyo kazi?

Shahidi (Tigo): Siyo kweli

Matata: Kampuni yenu mnasera ya Usiri?

Shahidi (Tigo): Upo sahihi

Matata: ambapo Mawasiliano ya mteja yanakuja ni Siri kati ya Mteja na Nyinyi

Shahidi (Tigo): Sahihi

Matata: Kwamba nitakusa sahihi nikisema Moja ya Sababu Ya Kuvunja Usiri ni endapo panahitajika Kufanya Uchunguzi Kwa VYOMBO Vya Uchunguzi

Shahidi (Tigo) Sahihi

Matata: Na Utoaji huo Wa Taarifa unalindwa na Sheria

Matata: Na wewe ni Mwanasheria

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Na Mimi nimekusikia Mtatoa Taarifa Endapo Mtaombwa au Kwa Amri ya mahakama

Shahidi (Tigo): Sahihi

Matata: Kwa kuzingatia Umuhimu wa Usiri wa mteja Nisomee Kifungu cha 34 cha Sheria Ya Makosa ya Mtandao

Shahidi (Tigo): 34(i) Disclosure of Data………

Matata: Utakubaliana na Mimi kwamba Pale panapohitajika Taarifa Ya Uchunguzi Police ambaye ni Ofisa anaweza Kuomba Taarifa Kwenu?

Shahidi (Tigo): Hapo anaongelea Ongoing Trafficking Data siyo Stored Data

Matata: Mh Jaji naomba Kielelezo

Matata: hiyo Barua Wametumia Kifungu gani?

Matata: Kwa Mujibu wa Maelezo yako walitaka Uwapo Data Trafficking Ya Siku hiyo Siyo Stored Data

Matata: Naomba Unisomee hapa

Shahidi kutoka( Tigo_TZ ) Anasoma kwa sauti sheria tajwa

Shahidi (Tigo): Kifungu cha 34 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao

Matata: Na Mimi nimekuuliza Usome Kifungu gani?

Shahidi (Tigo): Kifungu hicho hicho cha 34

Matata: Kwa hiyo utakubaliana na Mimi wewe Umeombwa Kitu Kingine na wewe Ukatoa Kitu Kingine

Matata: Utakubaliana na Mimi kwamba Kama Mtu ameombwa Taarifa na akakataa na Yule Police Officer alitakiwa kwenda Mahakamani Kuomba Court Order

Shahidi (Tigo): NI sahihi

Matata: Naomba Unionyeshe Kwenye hii Barua ni wapi Pameonyeshwa Kosa Kwenye hiyo Barua ambapo hiyo namba Inatuhumiwa kwenye Kosa la Jinai

Shahidi: Hakuna

Matata: Kuna Kosa Umeandika hapa Wakati Unajibu Barua hii Kuhusiana na Uchunguzi

Shahidi (Tigo): Kuna Dash Hakuna Kosa

Shahidi (Tigo): Hapakuwa na Haja hiyo

Matata: Kwa hiyo Polisi Wakikuandikia Barua ya Kutaka Taarifa Bila Kukutajia Makosa

Shahidi (Tigo): Nitampa

Matata: Kwenye kampuni yenu haitaji la Kutuma Meseji au Kupiga Simu Kwenu ni Kosa?

Shahidi (Tigo): Hapana Siyo Kosa

Matata: Kwa hiyo Hakuna Kosa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Pamoja na Barua kuja Bila Kutaja Kosa na Wewe Ukatoa Taarifa hiyo bila Kutaja Kosa kama Inavyosema katika Kifungu 34 Je Hukuona hilo ni Jambo lisilostahili ili uwakatalie Waende Mahakamani Kulinda Usiri wa wateja wenu?

Jaji: wakili wa mshtakiwa namba 4

Kibatala: Nyie Kama (Tigo_TZ) MIC Tanzania Ltd Priority ni nini, USIRI wa MTEJA au Kufuata MASHARTI ya POLISI?

Shahidi (Tigo): Tuseme COMPLIANCE na SIRI za MTEJA

Kibatala: Sawa tuweke hivyo Kwenu Kipaumbele ni nini?

Shahidi (Tigo): COMPLIANCE

Kibatala: Unafahamu Kuwa Mtu uliyemtolea Ushahidi Kama Freeman Mbowe Kuwa ni Kiongozi wa CHADEMA kama Kiongozi wa Chama Cha Upinzani

Shahidi (Tigo): Simfahamu

Kibatala: Umekuwa Wakili tangu lini?

Shahidi (Tigo): 2013

Kibatala: Bado unataka tukubali kuwa humfahamu Freeman Mbowe kama Kiongozi wa CHADEMA, chama kikuu cha upinzani Tanzania?

Shahidi (Tigo): Ndiyo sifahamu, Wapo wengi

Kibatala: Barua ilisema Kwamba iwe ni Siri sana Mteja asijue?

Shahidi (Tigo): Haikusema hivyo

Kibatala: Ulimtaarifu Mteja Mwenyewe kwamba Kuna Taarifa zako za Kiuchunguzi zinahitajika?

Shahidi: Hapana.

Kibatala: Kama Kampuni Mlichukua Hatua yoyote ya Kumlinda Mteja Kwa kwenda Mahakamani Kupinga au Kuandika Barua kwenda TCRA, Mlichukua hatua kama hiyo?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Hakuna Polisi Wana abuse power zao

Shahidi (Tigo): Sifahamu

Kibatala: mlichukua hatua gani kumlinda mteja?

Shahidi (Tigo): Hiyo siyo kazi yetu, Hakuna hatua tuliyoichukua kumlinda mteja

Kibatala: Mnafahamu Angalau kuwa Kuna Tasisi Mbili angalau zinahusika Kulinda Maslahi ya Mteja

Shahidi (Tigo): Ndiyo nazifahamu

Kibatala: Zitaje

Shahidi (Tigo): TCRA na FCC

Kibatala: Barua Yako uliyoitoa Mahakamani, Je Mahakama Ikitaka Kujua Kuwa nini wewe Mmiliki wa Barua, Ina angalia Wapi?

Shahidi: Kielelezo namba p6

Kibatala: Msaidie Mheshimiwa Jaji akiangalia Wapi ataona Barua hii Umesaini wewe FREDY Kapala

Kibatala: Je Uliongozwa na Wakili wa Serikali Kutoa Nyaraka Nyingine Kufanya Ulinganifu kwamba hii ni Saini yako?

Shahidi (Tigo): Sikuyatoa

Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa Hatuna sehemu ya Kulinganisha Signature Yako

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Tuchukulie Kwamba Barua Iliandikwa na Polisi na wewe hii ni Saini Yako, Je ni wapi Mheshimiwa Jaji akiangalia anaweza Kuona Barua hii Ilipita kwa Wengine Tigo kwamba Ufanye kama kwa Ku’ minute

Shahidi (Tigo): Sijaelewa

Kibatala: Unafahamu Kuwa baadhi ya Ofisi Barua inatembea na kupelekwa kwa Mhusika baada ya Kupita kwa wengine Ulimwambia Jaji kama Nyie Tigo hamna Utaratibu huu?

Shahidi (Tigo) Ningeweza Kujibu Lolote

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Unakubaliana Barua Yako ya Tarehe 02 Haielei hewani Ndiyo Maana Inaviambatanishi?

Kibatala: Ni sahihi kwamba Jalada ulilonukuu wewe ni tofauti ambalo hata polisi wamekuletea?

Shahidi (Tigo): Hapana

Kibatala: Ulitoa ufafanuzi wakati unaongozwa na wakili wa serikali kwamba umeulizwa barua kwa Jalada A wewe ukajibu Jalada B

Shahidi (Tigo): Hapana Sikusema

Kibatala: Twende eneo lingine, umetoa kielelezo namba P6 ni KYC. Nimesikia mnaulizana rekodi za NIDA Vs Tigo_TZ Kwa kuwa Taarifa za Freeman Mbowe zipo NIDA, ni sahihi?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: kwa hiyo kimsingi NIDA ndiyo Primary Source za Freeman Mbowe

Shahidi: Haupo sahihi

Kibatala: Basi niambie Uhusiano wa Tigo na NIDA katika KYC

Shahidi (Tigo): Kwa sababu sisi tuna chukua Data Kwao kimtandao

Kibatala: Kwa hiyo utakubaliana na Mimi NIDA ni Primary Source

Shahidi (Tigo): Hapana

Kibatala: Usajili wa Tigo unaweza kutambulika bila Mtu Kusajiliwa NIDA?

Shahidi (Tigo): Hapana

Kibatala: Katika Ushahidi wako umezungumzia Lolote Kuhusu wewe Kusomea Mambo ya Data za NIDA

Shahidi (Tigo): Hapana Sikuzungumzia

Kibatala: Wewe unaweza Kuzungumzia suala la Server ya NIDA Kama siyo Administrator wa NIDA?

Shahidi (Tigo): Hapana

Kibatala: Kuna aina Ngapi za Server?

Shahidi (Tigo): Email Based, Data Based Server

Kibatala: Nikisema LINU server unaelewa

Shahidi (Tigo): Ndiyo naifahamu

Kibatala: Ni nini?

Shahidi (Tigo): Maelezo yake sifahamu

Kibatala: Ni Lenox au Linux

Shahidi (Tigo): Linux

Kibatala: Huku Taja Window Server

Shahidi (Tigo): Sikusema

Kibatala: SQL Server Foft ware

Shahidi (Tigo): Fost ware

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Server ni Software au Hardware

Shahidi (Tigo): Hard Ware

Kibatala: Kuna Version kadhaa za SQL Software

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Tutajie The Latest SQL version Shahidi

(Tigo): Siwezi Kujua Kwa kweli

Kibatala: Sasa aliyemtajia Jaji Mambo ya SQL fotware ulilenga nini?

Shahidi (Tigo): Kumuonyesha Jaji ni wapi nilipata Hizo Nyaraka

Kibatala: Wewe Hukutaka kabisa Jaji ajue Uimara, Uadilifu na Uimara wa hizo Software

Shahidi (Tigo): Sikumwambia

Kibatala: Je unajua The SQL Software 2019 ndiyo The best wewe utakataa?

Shahidi: SIWEZI KUJUA NDIYO MAANA NIMESEMA SIWEZI KUELEZEA HIYO

Kibatala: Kwa Maelezo yako SQL Server Mnayotumia ni ya 2015

Shahidi: Nilisema ile ndiyo nilisoma Kozi ya introduction, tume update juzi

Kibatala: Sasa ulimwambia Mheshimiwa Jaji..?

Shahidi (Tigo): Siku Mwambia Exactly

Kibatala: Hatuna Kumwambia Exactly Wanasheria

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Umeupdate Juzi?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: VAPT ni nini?

Shahidi: NI Watu wakujaribu Umadhubuti wa mifumo

Kibatala: Kutokana na Umuhimu huo ndiyo Maana Mkawafuata Ernest & Young Taasisi Kubwa, Mmechukua Kwa ajili ya Ulinzi wa Mifumo?

Kibatala: Unafahamu DB2 software

Shahidi (Tigo): Siifahamu

Kibatala: Kwa hiyo wewe nikikwambia DB2 ndiyo madhubuti duniani kwa uwezo wake, huwezi kujua?

Shahidi (Tigo): Siwezi Kujua Kwa kweli

Kibatala: Na Unajua Kuwa SQL ni moja software ya bei rahisi duniani?

Shahidi (Tigo): Inayoweza Kununulika (affordable)

Kibatala: Unafahamu Kwamba Tigo ni Reportimg Institution

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Mlishawahi Ku’ report Mambo yasiyofahaa Kuhusu Hiyo namba za simu

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Unafahamu Kuwa PEGASUS ni SoftWare Hatari sana Duniani Kwa ajili ya Kuingilia Mawasiliano wa mtu?

Shahidi (Tigo): Hilo sifahamu

Kibatala: Makao Makuu ya Tigo yapo Karibu kabisa na Eneo la Usalama wa Taifa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Unafahamu Kuna Pesa Za Mteja Zimeibwa Kwenye huduma ya Kibubu ya tigo, Na Mwanasheria Pacience Mlowe ameleta Demand Notes kwenu?

Shahidi (Tigo): Hapana Sifahamu

Kibatala: Nakupeleka Kwenye Detail ya Miamala ya pesa

Kibatala: Kuna Originating Number na Terminating Namba

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Wewe Ulionyeshwa hapa Mahakamani Kwamba hii Ndiyo Terminating Namba.?

Shahidi (Tigo): Sikuonyeshwa

Kibatala: Unafahamu kuwa kuna Huduma ya Kurudisha Miamala?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo hatuwezi Kusema Details za kuanzia Tarehe 01.8.2020 kama tunazo hapa?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo hatujui Kama Pesa hiyo huenda mbele Ilirudishwa, Si Ndiyo

Shahidi: Ndiyo Hatujui

Kibatala kamaliza kuuliza maswali ya Dodoso.. Anasimama sasa Wakili wa Serikali Kwa ajili ya Re examination..

Wakili wa Serikali: Nitakuuliza Kwa ufafanuzi na Pole Kwa Maswali.

Wakili wa Serikali: Wakati Unaulizwa Maswali na Mawakili wasomi hasa Mtobesya kama umeiambia Mahakama kuhusiana na Watu Wanaitwa Hackers, na akakuuliza servers zinaweza Kuingiliwa na Hackers Ukajibu ni sahihi Na wakati Ulikuwa una generate Data Kama Mfumo ulikuwa Umeingiliwa

Shahidi (Tigo): Mantiki ya kuwa na Mifumo ya kulinda na Kutoa Taarifa, ni ili Mfumo wa kila wakati unapotumika Uwe Salama

Mallya: OBJECTION ni swali Jipya

Wakili wa Serikali: Nimetoa katika Maswali Mengi Labda Kama Mtobesya Mwenyewe angekuwepo

Jaji: Shida siyo Maswali shida ni Majibu

Shahidi: Wakati nafanya system hizo zilikuwa Inplace na zinalindwa na Mfumo kwa wakati wote

Wakili wa Serikali: Kama nilikuelewa Vizuri Ulikuwa Unaulizwa Kama Barua ya Polisi Ilikutaja, na Ofisi inachunguza nini

Shahidi: Kuhusiana na Tuhuma za Jinai

Wakili wa Serikali: Ambayo ni Kumbukumbu ya Nini hiyo?

Shahidi: Kumbukumbu ya Jalada

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Ulikuwa unamaanisha nini Katika kutokubadili Mfumo?

Kibatala: OBJECTION siyo Sawa wakili anachotaka kufanya

Wakili wa Serikali: Alitaka Kufafanua Maana ya convenience zile ambazo hazipo Kwenye Mfumo wa NIDA na huzipati

Wakili wa Serikali: Uliulizwa na Kibatala kuhusiana na Utambulisho Kwamba Usajili wenu Primary Source yenu ni Nida. Ukasema Kula NIDA ni ku verify

Shahidi: Ilipofika kutafuta Kitambulisho Cha Taifa sehemu Nyingi Zina Verify Taarifa za NIDA tu

Jaji: Unawasiwasi Mahakama Haijaelewa Kuhusu Conviniance?

Wakili wa Serikali: Samahani Mheshimiwa Jaji

Wakili wa Serikali: Umeulizwa kwenye KYC Kuhusu Mbowe kama yuko Ukasema hayumo, ipe Mwanga Mahakama

Shahidi: Taarifa zinazoonekana zimepatika Kwenye Server Ya Tigo, information ambazo zimeandikwa Null ni zile ambazo hazipo Kwenye Mfumo wa NIDA

Wakili wa Serikali: Elezea alipokutaka Kuelezea Kuhusiana na Utofauti na Namba kumbukumbu hasa kwenye Miaka, Elezea Mahakama Haya yakijitokeza Vipi?

Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji

Wakili wa Serikali: Wakati unaandika Exhibit P6 ulikuwa unajibu nini?

Shahidi: Nilikuwa na Barua Kutoka kwa kamishina

Wakili wa Serikali: alikuuliza Kibatala Endapo Kumfanyika Mfananisho wa Signature yako, Ukasema Hukuweka Ikumbushe Mahakama Uliweka Saini ya nani

Shahidi: Saini Yangu

Wakili wa Serikali:: ni wakati gani sahihi ufananishwa

Kibatala: OBJECTION swali hilo subiri wakati wa Submission

Wakili wa Serikali: Sawa

Shahidi (Tigo): Kutafuta Miamala Ya Fedha Kutoka June Mpaka July Wakati Kifungu cha 34 kinazungumzia interpretation

Matata: Mheshimiwa Jaji OBJECTION Kusema Kilikuwa Misquoted ni Fact Mpya, miye Nilisoma Barua tuh

Shahidi: Kifungu kimenukuliwa tofauti na kile ambacho Barua Imetoka Reqiest

Wakili wa Serikali: umelitoa wapi, exhibit gani hiyo

Shahidi: P07

Wakili wa Serikali: Ilikutaka Kufanya nini

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji, Naomba Wakili Chavula ana maswali Kadhaa ya kuuliza

Wakili wa Serikali:: Ulikuwa Unaulizwa Kuhusu Cyber Act Kuhusu Kifungu 34 na 36 Hii report yako Ilikuwa kwa ajili ya Trafficking, Fafanua sasa Relevance ya vile Vifungu kile Ulichoombwa Kufanya

Shahidi (Tigo) Niliombwa Kutoa taarifa ya Miamala Kutoka June Mpaka July nisingeweza Kwenda zaidi ya Hapo

Shahidi (Tigo): ni Kwa sababu NIDA hawana Majina ya Trama Leader na wala Watu wanaosajili kutoka kwetu

Wakili wa Serikali: Shahidi ieleze Mahakama kuhusu pesa hizo kama zilirudishwa kwa aliyetuma….. Kwani wewe Kwa Mujibu wa Kielelezo Cha Mahakama uliombwa Kufanya nini?

Wakili wa Serikali: Tufafanulie katika hicho Kielelezo Imejitokeza Kwamba KYC Hakutaja Jina la Aliyemsajili Freeman Mbowe

Shahidi: Sijaelewa Swali

Wakili wa Serikali:: Tufafanulie katika hicho Kielelezo Imejitokeza Kwamba KYC Hakutaja Jina la Aliyemsajili Freeman Mbowe

Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Maneno City Kuna Kilimanjaro, District Kinondoni na Region ni Dodoma hebu ifafanulie Mahakama

Shahidi (Tigo): NI Classification yetu sisi

Wakili Malya: OBJECTION hiyo ni New Fact

Wakili wa Serikali: Hatuoni hapo Kama Kuna Jambo Jipya

Wakili wa Serikali: Mimi kwa Uelewa Wangu Kitu kinachotakiwa Kuwa Objected ni Maswali tu siyo Majibu Shahidi anaweza Kuongea Kitu Jipya, hawezi Kuongea Maneno yaleyale

Wakili wa Serikali: Chavula Kwa kuongeza tutazame Kifungu Kidogo ha 147 cha Sheria ya Ushahidi Maswali yetu yakijielekeza Kwenye yaliyojili kwenye Cross examination Na kazi yetu nikufukia Mashimo yaliyojitokeza Kwenye Cross Examination Tunaomba Shahidi wetu apewe Nafasi ya Kufafanua

Jaji: Ninaona ni kitu Jipya kwa hiyo na kubaliana na Maoni ya wakili Malya Unaweza Ukalitengeneza Ukauliza Kivingine

Jaji: Wote tunakubaliana Hairuhusiwi Kufanya Mambo Mapya kwenye Re examination kwa sababu utatoa Fursa ya Upande wa pili Kurudi tena Ninachokiona mimi hapa tunabishana Kama Jambo ni Jipya au lilikuwa mwanzoni

Wakili wa Serikali: Kwenye City inaonekana Kilimanjaro na Kwenye Region panaonekana Dodoma na Kuna District Kinondoni

Shahidi (Tigo) Hizo ni Permanent Adress na Zingine ni Temporary Adress nadhanu niishie hapa

Wakili Malya: Mimi Siku uliza Mambo ya Adress anachokileta ni Kitu Kipya, aseme kama Ilivyo Kilimanjaro City

Jaji: Wote tunakubaliana ni Jukumu la Mahakama Ku’ Control Process Wote tunakubaliana Jambo la Kuleta Mashahidi

Wakili wa Serikali: Sheria haikudhamiria kubana shahidi kuongea Hapa, Lakini si kuzuia kuongelea masuala walioyaibua wao Mheshimiwa Jaji Kwa mfano hapa hakuna sehemu Kinondoni kwenye Kilimanjaro Sisi tunaona basi bora tunyimwe kabisa haki hii Ni hayo tu, lakini nakaa kwa hasira.

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naona Wenzetu Wameibua Malalamiko na wanaelekeza Kwa Mahakama Wakili wa Serikali Kwanza Aondoe hilo, Hakuna anayelalamika sisi tumeleta Hoja

Kibatala: hii Statue inatoa Jibu, imesema Question and Answers lakini kwenye hili wameita Re-examination

Jaji: Akielekeza Majibu ambayo hayaibui Maswali Mapya tunayapokea. Na Shahidi Mpaka Sasa Kajibu mambo Mengi. Na suala la Msingi hapa Shahidi ajielekeze Kwenye Kutoleta Mambo Mapya Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana Jaji.

Wakili wa Serikali: Chavula Mheshimiwa ni hayo tuh Sina Cha Ziada

Jaji: Eneo hili limeleta Maswali Mengi na Mkanganyiko

Wakili wa Serikali: Shahidi Kwanini Kwenye exhibit P9 kuna Kilimanjaro City huku hakuna Kilimanjaro City

Shahidi: Tuseme Kwa Urahisi Ndiyo Inavyo kuwa Lebelled Kwa Upande wa Kuandika hizo Data

Wakili wa Serikali: Na Kilimanjaro kuna Wilaya inaitwa Kinondoni lakini Kwenye Exhibit, Kuna Region Imeandikwa Dodoma

Shahidi (Tigo): NI sehemu Tatu Tofauti

Jaji: Nina swali Moja tuh Je hizi Taarifa ambazo Zimeleta Mkanganyiko Sorce yake ni wapi?

Shahidi (Tigo): NIDA

Jaji na wewe Sasa unaweza Kuzisemea

Shahidi (Tigo): Zikiwa Upande wetu, zinakuja Kwa Mteja kama Mmiliki baada ya Finger prints

Jaji: Nakushukuru Kwa Ushahidi Wako

Wakili wa Serikali, Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka kesho tarehe 3 ilituweze kuendelea na usikilizwaji wa shauri hili

Jaji: Utetezi

Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi kwenye hili

Jaji anaendelea kuandika

Jaji: Maombi ya hairisho yamekubaliwa na Shauri linairishwa Mpaka kesho tarehe 3. Upande wa Mashitaka mnaamriwa Kuleta Mashahidi. Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande Mpaka Kesho saa 3 Asubuhi. Jaji anatoka.

Like
3