Kesi ya Mbowe: Shahidi aliyekuja kubainisha uwongo wa mashitaka aibua mazito

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia BJ, leo tarehe 30 Novemba 2021.

Jaji ameingia Mahakamani Muda huu Saa 4 na Dakika 12 ya Tarehe 30 November 2021

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Tulimanywa Majige

WAKILI PETER KIBATALA Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naomba Kuwatambulisha

John Malya
Nashon Nkungu
Fredrick Kihwelo
Paul Kaunda
Seleman Matauka
Michael Lugina

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa, Naomba tupatiwe Nyaraka ilikuweza Kuzikagau

Wamekabidhiwa Nyaraka na Kuanza Kukagua Moja baada ya Nyingine

Mahakama ipo Kimya Wakiendelea zoezi la Kukagua

Wakati wanakagua Leo Mahudhurio siyo Makubwa Sana, Huenda Sababu ya Hali ya hewa

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Tunamapingamizi Kuhusiana na Upokelewaji Wa Nyaraka hizo Nne Zinazotaka Kutolewa na Shahidi Wa Pili
Mheshimiwa Jaji tumeandaa Mapingamizi ngamizi ifuatavyo

1.Mwenendo wa Kesi( Case Proceedings, Hati ya Mashitaka (Charge Sheet) pamoja na Barua inayo Daiwa Kuandikwa Kwa Hakimu wa Mahakama Mkazi Kisutu,

Nyaraka hizi haina Relevance Katika Shauri Linalo endelea Kuhusu Mshitakiwa Wa Tatu

Kwa hiyo Nyaraka hizi tunazipinga
Mheshimiwa Jaji Kuhusiana na Nyaraka nikizozitaja hapo Juu, Kuna Cha Kuongezea Kuhusiana na Hati Ya Mshitakiwa, Kwamba Kilicho letwa Mahakamani hapa ni Copy ya Hati ya Mashitaka, ambayo Kwa Mujibu wa Sheria Copy haiwezi Kupokelewa kabla ya Kukidhi Vigezo Vya Kisheria Kama Vilivyotakiwa katika Vifungu Vya 65, 66, na 67 ya Sheria ya Ushahidi Sura ya Sita

Mheshimiwa Jaji Kuhusiana na Dispatch, Shahidi aliyepo Mahakamani siyo Competent Witness Kuweza Kuitoa hiyo Dispatch

Mheshimiwa Jaji sisi tupo tayari Kuendelea na Hizo Hoja zetu za Kisheria kwa Maana Kufanya Submission na ataanza Pius Hilla

JAJI: Kwa hiyo ni Mapingamizi Matatu

WAKILI WA SERIKALI Pius Hilla:
Mheshimiwa Jaji Nyaraka ambazo Wenzetu Wanataka Kutender Kwenye Ushahidi

JAJI: Hapo unamaanisha Dispatch

WAKILI WA SERIKALI Pius Hilla: KUHUSU RELEVANCE Nyaraka Wanazotaka Kitumbukiza Kwenye Ushahidi Barua, Proceedings, na Charge sheet

Ukizitazama Zinahusiana Criminal case namba 77 /2020 kuhusu Jamhuri Vs Lembrus MCHOME Kesi ambayo ilikuwa Mahakama Ya Kisutu

Mheshimiwa Jaji Hakuna Namna yoyote Ile, Nyaraka hizi zikahusiana na Shauri Lililopo Mbele yako

Hakuna Namna yoyote Ile Mheshimiwa Jaji Nyaraka hizi Kuhusiana na D/C Msemwa Ambaye ni Shahidi namba 3 wa Shauri Dogo Ndani ya Shauri kubwa
Nyaraka hazina Uhusiano wowote Ule na Hoja ya D/C Msemwa Kuwepo Central Police au Hatakuwepo Oysterbay Police
Nyaraka hazina Indicator Zozote zile kama D/C Msemwa aliwahi Kufanya Kazi Kituo cha Polisi Oysterbay kipindi cha Mwezi May 2020

Mheshimiwa Jaji Nyaraka hizi pia hazina Bearing yoyote ile za Ukamatwaji Wa Ling’wenya, Uandikaji wa Maelezo Ya Ling’wenya, Mambo ambayo Ndiyo Issue Iliyopo Mbele Yako
Nyaraka hizi pia Mheshimiwa Jaji hazina Bearing yoyote ile Kwamba Lembrus MCHOME (DW2) Kuwa amewahi Kukaa Kituo cha Police Oysterbay

Mheshimiwa Jaji Jaji Kwa Mujibu wa kifungu cha 7 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6, Kwamba Ushahidi Mheshimiwa Jaji, Utatolewa na Kupokelewa Mahakamani Kama Upo Relevant
Na wala Siyo Vinginevyo
Mheshimiwa Jaji Mahakama Yako hii inaongozwa na Sheria, Kwamba Kila Kinachofanyika Mahakamani lazima Kifanyike Kwa Mujibu wa Sheria

Kila kitakachopokelewa lazima Kiwe na connection (Uhusiano)
Mheshimiwa Jaji Kesi ya DPP VS SHARIF MOHAMMED ATHUMAN AND SIX OTHERS Criminal appeal namba 74 ya Mwaka 2016 katika Ukurasa Wa 6 Aya ya Mwisho

Mahakama Ya Rufaa Ilipata Kusema Kwamba, Ushahidi ambao ni Irrelevant ni inadmissible
Mheshimiwa Jaji Page ya 7 ya Hukumu hiyo paragraph Ya Kwanza
Mahakama Ya Rufani Inasema Kwamba fact inakuwa Relevant kama Inakusudia Ku Prove au Ku disaprove Ushahidi

Bila Kuzingatia hayo Mahakama Ingaletewa Mambo Mengi ya siyo Ya Msingi
Mheshimiwa Jaji Mahakama Inapaswa Kuletewa Mambo ambayo ni Relevant
Mheshimiwa Jaji Barua inayo taka Kuletwa Mahakamani inatoka TANAFRICA LAW imesainiwa na Wakili Peter Kibatala Imeelekezwa kwa Hakimu Mkazi Kisutu imenakiliwa kwa Lembrus MCHOME na Kwa Deputy Registar wa Mahakama hii Kuomba Proceedings

Haiongelei Ukamatwaji Wa Ling’wenya Wala Haiongelei Uandikaji wa Maelezo wa Ling’wenya
Kwamba Barua Mheshimiwa Jaji Haijaongelea Kwa Jambo Lote Lote lile Kuhusiana na Shauri Lililopo Mahakamani
PW2 Hajaongelea Kwa Namna Yoyote ile anahusiana na Ling’wenya
PW2 Hajaongelea lolote Kuhusiana na hii Barua Kama inahusiana na Ukamatwaji na Uandikaji wa Maelezo wa Ling’wenya
PW2 haja eleza Kwa namna gani, Barua hii, Proceedings na hata Charge Vinahusiana Vipi na Yeye Kuwepo pale Oysterbay Police

Mheshimiwa Jaji Charge Sheet na Proceedings Zinahusiana na Mashitaka, Publication of photographs
Shahidi aliyepo Mahakamani alikamatwa kwa Kupigwa Picha Fulani Kwa Kiongozi Fulani akashtakiwa Kwa Matumizi Mabovu ya Mtandao

Mheshimiwa Jaji Swali la Kujiuliza ni Je Shauri hili lina Uhusiano gani na Matumizi Mabovu ya Mtandao, Ya Uhusiano gani wa a Kupiga Picha Kiongozi Fulani au Taasisi fulani
Mashitaka haya ya Publication of Photograph Yana Uhusiano gani na D/C Msemwa Kuwepo Oysterbay police
Mheshimiwa Jaji Nyaraka zinatakiwa kujiongelea Zenyewe

Ni Wasilisho letu Kwamba Nyaraka hizi haziongelea Chochote Kuhusiana na Ishu iliyopo Mahakamani
Nyaraka zinaongelea Vitu Vingine kabisa
Nyaraka hazina Uhusiano na Ukamataji na Uchukuliwaji wa maelezo ya Ling’wenya
Na zaidi zaidi Nyaraka haziongelei kabisa Kuwepo Kwa Lembrus Oysterbay na Kuonana na D/C Msemwa
Mheshimiwa Jaji Tunawasilisha Kwamba Shahidi Ndiyo anaye Lay Foundation Juu ya Upokelewaji Wa Ushahidi Wake Mahakamani

Alitakiwa a ieleze Mahakama Yako Tukufu Kwenye Hizo Nyaraka Kuna Moja Mbili Tatu Kuhusiana na D/C Msemwa
Mheshimiwa Jaji Shahidi alijaribu Kueleza Mahakama Yako tukufu Kwamba alikaa na Msemwa Kwa Muda
Hicho siyo Kigezo Cha Kuleta Hizo Nyaraka
Nyaraka zilitakiwq zijitambukishe Zenyenwe na Shahidi aongee Kuzitambulisha

Kwa Kifupi pasipo Kuwa chosha Mahakama Yako tukufu Nyaraka hizi ni Irrelevant, Hazina Sifa za Ku pokelewa Nyaraka hizi
Kwamba Kitendo Cha Shahidi Kutokuongelea ni Kitu gani kwenye Nyaraka Kinahusiana na D/C Msemwa Inabainisha Kwamba Wala Hana Knowledge Ya Kile Kilichopo Katika hii Nyaraka

Mheshimiwa Jaji nizungumzie Sasa Kuhusiana na Charge Kuwa Nakala
Mheshimiwa Jaji Kinacho letwa Mbele Yako Hakuna Ubishi it’s a photo Copy
Tunasema Hakuna Ubishi Kwa Sababu Shahidi Mwenyewe Alianza Kwa Kusema Hivyo
Rules of Evidence zinademand Kufuatwa Kwa Procedures ili Kuleta Ushahidi
Mheshimiwa Jaji ni Wasilisho Letu kuwa Nyaraka hii Imeletwa kwenye Violation
Ni Violation ya kifungu cha 63 Mpaka 66 ya Sheria ya Ushahidi Sura ya 6
Kwamba Kwakuwa Walifahamu Kwamba Nyaraka ni Photocopy (Secondary) Walitakiwa Mheshimiwa Jaji Wa Comply na Masharti
Mheshimiwa Jaji Ushahidi Ambao ni Photocopy (Secondary) it’s a General Rule Kuwa ni Adminsible

Mheshimiwa Jaji baada ya Kusema hayo naomba Wakili Mwenzangu Abdallah Chavula aendelee pale Nilipo Ishia, ata Kuja kwa Swala la Dispatch

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji ni Kama alivyo tangu Lia a Kusema Mwenzangu
Nitaanzia Hapa Alipoishia Yeye
Na Yeye Aliishia Kwamba hii Hati ya Mashitaka Imekiuka Kifungu namba 63 Mpaka 66
Mheshimiwa Jaji Kifungu cha 63 kimatoa Ruhusa kwa Nyaraka kwa namna mbili
Kwa primary Evidence na Secondary Evidence
Na Kifungu ha 64 limeweka Bayana Kwamba Primary ni Documents
Mheshimiwa Jaji Shahidi akaweka Bayana kwamba alipewa Photocopy
Kwa hiyo siyo Primary Evidence, Kwa Maana hiyo anataka Kuijulisha Mahakama Hii ni secondary Evidence
Mheshimiwa Jaji Kifungu cha 65 ya Sheria ya Ushahidi Sura ya 6, kinasema kwamba
ANASOMA
(a), (b) (C), (d), na (e)
changed this group’s settings to allow only admins to send messages to this group

Mheshimiwa Jaji Katika Ushahidi Wake haja eleza Mahakama Kwamba Nyaraka hii Imekuwa Certified na Ukatazama Nyaraka Yenyewe Pia Hazijawa Certified
Shahidi ajieleza Mahakama Kwamba Nyaraka hii Imetengenezwa Kutoka Kwenye Nyaraka

Hajaileleza Mahakama Mheshimiwa Jaji Kwamba Baada Ya Kufanyiwa Photocopy Wali ringanisha Kujiridhisha Kwamba Kilichopo humu ndiyo Kipo kwa Original Charge Sheet

Vilevile Haja elezea Kwa mdomo Kwamba hii ni sehemu ya Ile Original Document

Mheshimiwa Jaji Ni Hoja yetu Kwamba Shahidi huyu wakati wa Kuomba Kutoa Nyaraka Hajakidhi Matakwa ya Kifungu cha 65
Twende Mbele zaidi, Fungu la 67 Kinaweka Masharti Kwamba Secondary Evidence Inatapaswa Kutolewa Mahakamani
Ni Maoni yetu Siye kwa Madai Ya Kwamba Eti Kule Mahakamani Kisutu Kwamba walielezwa Nyaraka Ya Mashataka ipo Moja tuh
Kwa Bahati Mbayo siyo Sababu Iliyo Tajwa Kisheria Kuleta Nyaraka hiyo
Ni Maoni yetu Vigezo Vilivyomo Katika Kifungu cha 65 vinakosekana kwa Ushahidi na Shahidi Mwenyewei
Na hii ya Kupewa Photocopy Haikamiilishi Kifungu
Kifungu Cha 68 Kinachotaka Wao Kufanya Ku Introduce hiyo Documen na Wao hawakufanya
Na Kwa Sababu Hawa Kutumi hiyo nafasi, Basi Maombi yao ya nakuwa Batili Mbele ya Mahakama hii
Mheshimiwa Jaji naomba tuelekee Kwenye Pingamizi La Dispatch
Mheshimiwa Jaji ni Msimamo Wa Sheria na Katika Nyakati tofauti Tofauti

Tumekuwa tulielekeza Mahakama Yako Kwenye Shauri la JAMHURI Vs CHARLES GAZILABO NA WENZAKE Katika Ukurasa Wa 12, Na Pia Kesi ya DPP VS MIZIRAHI
Mahakama ili weka Vigezo na Vigezo Hivyo Ni knowledge na Kama Ushahidi Ulishawahi Kuwa kwenye Himaya Yake

NASHON NKUNGU: Mheshimiwa Jaji Kuna Kesi Zinatajwa hapa Kama Rejea Naomba Nasisi Tungapatiwa

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji alikuwa afuatilii Kwa Sababu nilikuwa nasema tuh Kuhusu hizo Kesi, ila pia tuliwapa
Nashukuru Kaka Yangu Kibatala anasema aniendelee

Mheshimiwa Jaji hapa Kuna Swala la Knowledge
Ilikuwa ni Lazima Kuonyesha Mahakama Kwamba alishawahi Kumiliki Kielelezo hiki
Sisi ni Maoni yetu Kwamba Kuna Eneo Muhimu Sana ambalo tunaona ni lazima Mahakama itambue
Wakati anaeleza Kuhusu Barua, alieleza Barua ile Ina Reference namba, Mheshimiwa Jaji Shahidi a Kwenda Mbele na Kutuambia hizo Reference Nmab ni zipi Ni Maoni yetu Kwamba Shahidi ameshindwa Kunukuu Reference namba za Barua ambazo yeye Anada Kwamba hazikamiliki
Ni Maoni yetu Kwamba Shahidi hana Knowledge ya Kielelezo ambacho anataka Kukitoa

Na Vilevile Kwamba Kielelezo hicho Hakina Uhusiano na Kesi iliyopo Mahakamani

NASHON NKUNGU: OBJECTION Mheshimiwa Jaji tungejikita na P. O zile tatu naona hii ni P. O Mpya

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Shahidi alieleza Mahakama Kwamba Dispatch Hii Ililetwa na Msaidizi Wa TANAFRICA LAW naye Baada ya Kuleta Barua, na haya ya Kupeleka Barua yakifanywa na Mtu anaitwa FAITH kwa Mujibu wa Ushahidi Wake
Na Yalifanyika Tarehe 23 November Mwaka huu, na Yeye alikuja Tarehe 24 November 2021, Hakuna Sehemu alitaka Kwamba FAITH Alimkabidhi Dispatch
Lakini hajaileleza Mahakama Kwa Namna alivyo Kihifadhi Kielelezo Hicho
Haja eleza Mahakama Kwamba Mpaka anafika hapa Kielelezo hicho Kilivyo kuwa wapi na Kilikuwa kinatunza kwa namna gani

Naomba Nielekee Mahakama Yako Kwenye Kesi Ya DPP Vs SHARIF MOHAMMED ATHUMAN na Wenzake

WAKILI JOHN MALYA: OBJECTION naona Wakili analeta Jambo Jipya, Sababu Hapa P. O ilikuwa ni Kuhusu Competence ya Shahidi Juu ya Kielelezo

WAKILI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji nafikiri Wakili angetukia kwanza anisikilize na Mahakama Yako iniachie nafasi Nionyeshe Natokea wapi

WAKILI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Ilitakiwa Ionyeshwe Kwamba Kielelezo Kile akijachezewa Mpaka Kuja Mahakamani

Katika hili hili Kesi ya DPP VS SHARIF MOHAMMED ATHUMAN AND SIX OTHER Ishu Ilikuwa ni Shahidi Wa Jamhuri Kuonyesha Chasis Namba ya Gari na Kwa Bahati Mbaya Shahidi alishindwa Kufungua Bonet ilioneshe Ushahidi Wake

Na Wakati Wa Ushahidi Wale alisema Anatokea Himo wakati Gari Ipo Moshi Ndiyo zikatokea Hizo Ishu

Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji Shahidi Ilikuonyesha Kwamba Alilioata wapi Kielelezo na alikaa nacho ilikuweza kukileta Kielelezo
Hilo Haku fanya na wala Hakuileza Mahakama Hiki Kielelezo alikabidhiwa na nani
Ni Hoja yetu Kwamba Kukosekana Kwa Ushahidi huo
Kwa hayo tuliyoyaeleza ni Maoni yetu Kwamba Kielelezo Hiki (Dispatch) haiwezi Kupokelewa

Mheshimiwa Jaji naomba Kumalizia Kwa Kurejea kwenye Hati ya Mashitaka,
Hati ya Mashitaka I akin ana na Ushahidi Wa shahidi
Pale anaposema alikamatwa na Kufunguliwa Mashitaka kwa Makosa aliyo fanya Wilaya ya Mwanga
Hati anayotaka Kuleta Yeye inaongelea Makosa Yaliyofanyika Dar es Salaam
Hakuna Sehemu aliyo weza Kulinganisha Kosa akilofanya Wilaya ya Mwanga na Makosa aliyoshtakiwa Dar es Salaam

Haya yote Kwa Ujumla hayana Sifa Ya Kupokelewa na Mahakama hii, Ni Maoni yetu Kwamba Katika Mazingira haya Tunaomba Mahakama Isipokee Vielelezo hivyo
Ni Hayo tuh Mheshimiwa Jaji

JAJI: Mmemaliza..?

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Ndiyo

JAJI: Nakukumbusha Wakili Nashon Nkungu Kwemye Sababu Zako Za a Kuunga Mkono Usijibu Hoja ambazo zimetolewa na Upande Wa Mashitaka

NASHON NKUNGU: Sawa Mheshimiwa Jaji, Ingawa napata Ugumu, Naomba Mahakama Univumilie naona Hoja Nyingi Zinakuwa against na Hoja zao

JAJ: I Ndiyo Changa Moto tunazopata Eneo hili

WAKILI wa SERIKALI Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Naomba Kuwakumbusha Kwamba Siyo Haki yao Kujibu

Huyu siyo Mtu aliye leta Motion

Jaji Nakukumbusha Mr. Hila Kwamba Hilo siyo Jambo Jipya, nimemkumbusha Kwa sababu Hakwepo Mahakamani

NASHON NKUNGU: Mheshimiwa Jaji Naunga Mkono Upokelewaji wa Vithibiti hivi Kwa Pamoja kwa sababu Nimeona vimekidhi Matakwa Makubwa Matatu ambayo ni RELEVANCE, MTERIAL na COMPETENCE

Sijaenda Kwa Haraka Haraka kwenye Proceedings Za Mahakama hii

Lakini niliona ina Case Namba, Ina jina la Mshitakiwa

JAJI: Hiyo ni Nyaraka gani

WAKILI NASHON NKUNGU: Court Proceedings

NASHON NKUNGU: Pia Nikihamia Kwenye Charge sheet, Sitoenda Kwenye Content nitajikita Hasa yake Maeneo alisema ni Copy, Nimeona kweli ni Copy Nimeona namba ya Kesi namba 77 ya 2020 na Relevance InaKuja Kwa sababu akishatueleza Kwamba alipelekewa Oysterbay na Kwa kutumia Charg Sheet hii alipelekewa Mahakama ya Kisutu

Kwa Swala la Relevance Kwa Mujibu Wa Kifungu cha

WAKILI WA SERIKALI: OBJECTION Mheshimiwa Jaji anachokifanya Wakili anajibu

JAJI: Mr. Hila anachokisema Unaenda Ndani Sana

NASHON NKUNGU: , Sawa Mheshimiwa Jaji, Kingine Kinachoifanya niunge Mkono ni Kesi ya DPP VS MIZIRAHI Ukurasa wa 8

JAJI: We Unayo hiyo Nakala ya MIZIRAHI Kwa Maana Nakumbuka Ina chukuliwa a kutoka. Kwenye kesi ya ABEL GAZILABO

NASHON NKUNGU: Mimi ninayo tutawapatia pia, neona Kwenye kesi hii Inasisitiza Knowledge Wala Siyo Sufficient Knowledge
Kwa hayo Machache, Naomba Sababu za Kuunga Mkono Zichukuliwe

WAKILI JOHN MALYA: Mheshimiwa Jaji Nita ongea akwa Kifupi Sana na Kwa Bahati Nzuri sikuwa nawasikikiza Upande wa Mashitaka
Swala la Kwanza la Barua ni, Naona Lazima Barua Isomwe na Charge Sheet na Proceedings kwa hiyo Barua ni Relevant

Zaidi Mheshimiwa Jaji Kifungu cha 8 cha Sheria Ya Ushahidi, Kwamba Matters ambazo zipo Connected at anytime zinaweza kuibuliwa

Shahidi alieleza Ni Muda gani Kila Nyaraka aliiimiliki, kwa Madhumuni gani na alishughulikia Vipi, kwa Hiyo naona ni Shahidi Competent

Kwa sababu hiyo tunaomba Nyaraka aza Shahidi Zipokelewe Bila Wasiwasi wowote

WAKILI PETER KIBATALA: Mheshimiwa Jaji Kwa niaba ya Mshitakiwa Wa Nne tunafunga Mkono, Kupokea Kwa Set Ya Nyaraka zote Nne, Kwa Maana Nyaraka zote zimekidhi Vigezo Vya Msingi

Na Yeye Mwenyewe ameweza Kutengeneza Misingi ya hizo Nyaraka
Ameeleza Kwa namna alivyokaa na Vielelezo Vyote kuanzia alipokabidhiwa
Na sisi Washitakiwa wanne tunasubiria Kujanakuzijaribu Velacity yake Mbele ya Safari wakati wa Cross Examination

WAKILI FREDRICK KIHWELO: Mheshimiwa Jaji Kwa niaba ya Mshitakiwa Wa tatu ataanza Wakili Matata Na Baadae nitafuata Mimi

WAKILI DICKSON MATATA:, ASANTE Mheshimiwa Jaji

Upande wa Jamhuri waliweka Mapingamizi Matatu, Moja ikiwa kwa Nyaraka ambazo Shahidi anaomba Kuingiza a Mahakamani kwa Maana Barua, Charge sheet, Proceedings na Dispatch hazina Relevant
La Pili Ni kwamba Hati Ya Mashitaka ni Photocopy na Kwamba haijakidhi Kifungu Cha 66 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6
Na Pingamizi la Tatu Kwamba Dispatch, Shahidi Siyo Competent Kuweza Kutender Dispatch
Mheshimiwa Jaji nitajibu Kwa Ujumla na Wakili Mwenzangu atakuja Kujibu pale Nitakapo Ishia

Mheshimiwa Jaji nianze na Swala la Relevance
Mheshimiwa Jaji ipo katika Kumbukumbu Za Mahakama hii Kupitia Shahidi Kwamba Jana alieleza Mahakama Kwamba alipata Taarifa za Shahidi D/C Msemwa ambaye alikuwa Shahidi Wa Jamhuri Katika Shauri Dogo

Kwamba alikuja kutoa Ushahidi, Ambao Ushahidi Ule Kimsingi Ulionyesha Kwamba D/C Msemwa Wakati Mtuhumiwa Namba 3 anakamatwa na Kuletwa Dar es Salaam alikuwa Central Police Dar es Salaam

SHAHIDI: anasema hiyo Hakuwa Kweli Kwasababu yeye Mwaka Jana Tarehe 14 May 2020 baada ya Kukamatwa Mwanga na Kuletwa Dar es Salaam alipokelewa na D/C Msemwa

Sitaki Kuzuia ngumza Sana Kuhusu D/C Msemwa Pale Oysterbay, Itoshe Kusema Kwamba a baada ya Kuongea Sababu hiyo na Kwamba Kwa Sababu anajua D/C Msemwa alikuwa Oysterbay aliamua Kuja Kujitolea Kuja Kutoa Ushahidi Ili Kuja Ku Disaprove alichokisema D/C Msemwa

Na akasema ili Kudhibitisha Hayo, aliwasilina na Wakili wake (Peter Kibatala) alisema Kwamba Ni Wakili aliye husika Kutetea Mwaka Jana Kwamba ni Kesi namba 77 ya Mwaka 2020 ambayo ni Jamhuri Vs Lembrus MCHOME ambayo ilikuwa Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu

Aliwasilina na Wakili wake ili aweze Kupata Charge sheet na Proceedings Za Kesi hiyo na Alisema Kwamba Sababu ya Kuomba Nyaraka hizo
Ilikuwa ni Kuthibitisha Kwamba aliwahi Kufika Kituo cha Polisi Oysterbay Na Baada ya Hapo Ndiyo alipelekewa KwabHakimu Mkazi Kisutu
Na Kwamba a alipokuwa Kituo cha Polisi Oysterbay Ndiponalipokutana na D/C Msemwa

Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji Ni Wasilisho letu Kwamba Nyaraka hizi ni Relevant na Kwasababu Malengo ya Nyaraka hizo ni Kutaka Ku Disprove Kile alichokisema D/C Msemwa

Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji Pingamizi walilileta Upande wa Serikali Kwamba Nyaraka hizi siyo Relevant, Tunaona ni Pingamizi ambalo halina Mashiko
Kwa Sababu Hakuna Namna D/C Msemwa angeweza a kuwa Oysterbay na wakati huo huo akawa Polisi Central Dar es Salaam Wakati ni Vituo tofauti

Na Mheshimiwa Jaji Bila hata Kuingia Kwenye Barua yenyewe, ilikuwa ni Barua ya Kuomba Nyaraka Kuja kutumika Kwenye Kesi hii
Mheshimiwa Jaji nije kwenye Swala la Photocopy, ni Pingamizi la JAMHURI Kwamba Hati ya Mashitaka ni Photocopy na Kwamba Imekiuka Kifungu cha 66 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6 Kama Ilivyofanyiwa marekebisho Mwaka 2019

Na Wamesema Kwamba Imekiuka Kifungu Cha 65,66,67 na 68
Mheshimiwa Jaji Nianze Kwa Kusema Kwamba Shahidi Alianza Kwa Kulay Foundation Vizuri kwa kuieleza Mahakama ni Kwanini amekuja na Photocopy
Ni Maelezo ya Shahidi Kwamba Yeye Mwenyewe akiwa na Dada anayeitwa FAITH
Baada ya Kukabidhiwa Barua Kama Nyaraka Walizooomba Mahakama Ya Kisutu
Kwamba alienda Kisutu akiwa na FAITH na Alipofika Alikutana na Mmama Kwenye Chumba ambacho alikitaja
Na Kwamba Baada ya Kufika alimkabidhi Barua aliyopewa na Peter Kibatala ya Kuomba Nyaraka hizo, na Kwamba Yule Mama baada ya Kujiridhisha inafana na Barua iliyopo Pale Mahakamani
Alimpitia Lembrus MCHOME Court Proceedings na akampa Photocopy ya Charge sheet
Shahidi akauliza mbona nimeomba Certified Copy, Mama akajibu Kwamba hii Ndiyo tuliyonayo
Mheshimiwa Jaji ni Wasilisho letu Kwamba Fault ya Kupewa Photocopy haijatokana na Mteja wetu ni Fault Ya Mahakama
Sisi tunaona Pingamizi Halina Mashiko
Kwa sababu Kifungu cha 67 ya Sheria ya ushahidi Sura ya 6 Kama Ilivyofanyiwa Marekebisho Mwaka 2019 Inaruhusu Kutumiwa Kwa Photocopy pale ambapo Kuna Mazingira kama Yaliyotokea Kwenye kesi hii

Naomba Nikisome
67(a)Secondary Evidence May be given…………………

ANAENDELEA KUSOMA
11/30/21, 10:29 – Irene Lema: Naomba Kusisitiza 67(c) When the Parties Offers Evidence of its contents not for other Reason……………

Mheshimiwa Jaji ni Wasilisho la Upande wa Jamhuri Kwamba tulitakiwa Kuomba Notice to Produce Chinese ni ya kifungu cha 68
Mheshimiwa Jaji ni Wasilisho Letu Kwamba Kifungu Hiki awajakitazama kwa usahihi, Katika Mazingira ya kesi yetu
Ilikifumgu cha 68 ya Sheria ya Shahidi Kiweze Kutumika ni pale ambapo Masharti Yaliyowekwa Katika Kifungu (a) Mheshimiwa Jaji naomba kukisoma
Mheshimiwa Jaji Kwa Kifupi Kifungu cha 68 kina Sema Kwamba Uwezi Kutumia Evidence ambayo ni Secondary Kama Inaangukia Kwenye Kifungu 67(a)
Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji ni Wasilisho letu Kwamba Kielelezo Kinacho Ombwa Kuingia Mahakamani Kipo sahihi na akija Kosa Sifa yoyote ya Sheria Ya Ushahidi

Mheshimiwa Jaji Kwa namna Nyingine Kwamba, Tufanye Kweli Tulitakiwa Kutoa Notice to Produce Kitu ambacho nakipinga Kwa Nguvu zote

Lakini Bado Mahakama Inayo Uwezo Wa Kupokea Secondary Evidence Kwa Kutumia Kifungu hicho hicho cha 68 68(g)

Mheshimiwa Jaji Kwa kuzingatia Kwamba Photocopy hii alipewa na Mahakama na Kwa Kuzingatia tupo Kwenye Ndogo inayohitaji Uharaka
Na Kwa kuzingatia Kipengele (g) Mahakama Inayo Mamlaka ya Kukipokea
Ni Wasilisho letu Kwamba Pingamizi hilo halina Mashiko na litupiliwe Mbali
Mheshimiwa Jaji nije kwenye Swala la Competence
Na specifically nitazungumzia Kuhusu Dispatch
Mheshimiwa Jaji Ni Submission ya Shahidi Kwamba alipofika Dar es Salaam alienda Kuonana na Wakili wake Peter Kibatala
Na Baada Kuonana na Wakili wake, Wakili wake alimkabidhi Barua na Dispatch akiwa yeye Shahidi Na Mtu anaitwa FAITH
Na Kwamba Baada ya Kukabidhiwa yeye na FAITH waliongozana Kwenda Mahakama Ya Kisutu Wakiwa na hiyo Barua na Dispatch
Na ni Ushahidi Wake Kwamba kwanza Alipopewa Dispatch na Barua alijirodhisha Kama Dispatch na Barua Zinahusiana na Kesi namba 77 ya 2020
Na Kwamba waliofika Mahakamani Walienda Kuonana na Mmama Katika Chumba ambacho alikitaja yeye Shahidi akiwa na Barua na Dispatch

Na Kwamba waliofika Mahakamani Walienda Kuonana na Mmama Katika Chumba ambacho alikitaja yeye Shahidi akiwa na Barua na Dispatch

WAKILI WA SERIKALI Pius Hilla :Mheshimiwa Jaji tumevumilia Sana Lakini Sasa Wakili asitoe Ushahidi, Hakuna Sehemu Shahidi alisema alienda akiwa na Dispatch alisema alienda na Barua

WAKILI DICKSON MATATA: Naomba Mahakama itukumbushe, Mimi Nilisikia Kwamba Walienda na Barua pamoja na Dispatch
Jaji napekua Faili lake

Jaji anasoma ila Hakuna Sehemu Jaji Kaandika Kuhusu Dispatch

Kumbukumbu za Jaji Hakuna Sehemu Dispatch imetajwa

JAJI: Mimi Niliandika Kwamba alikabidhiwa Barua sioni sehemu ya Dispatch

WAKILI PETER KIBATALA: Kuna Mahala Tunalinganisha Hapa KWAMBA, Paonyesha majibu ya Wakili na Shahidi

Kibatala ANASOMA

JAJI: Unalinganisha Wapi Kwenye Live..?

Mahakama kichekoooooo

KIBATALA: Sawa lakini Kama Mahakama Haiku andika atuwezi Kufanya lolote

Kwamba Hakusema Swala la Dispatch

JAJI: Mbeleni Mpaka Wanafika Mahakamani hapa Walikuwa na Dispatch Ila sijaona sehemu Kwamba FAITH Alimkabidhi Barua na Dispatch, Ila Baadae alikuwa na Dispatch

WAKILI WA SERIKALI Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Kwa Hiyo Dispatch ipo au Haipo

JAJI: Dispatch ipo kwa Sababu Mbeleni huku naona Kuna sehemu alisema Kwamba awalipo fika hapa walikuwa na Dispatch

WAKILI WA SERIKALI: Lakini haionyeshi Dispatch alipata wapi na Ilikuwa Kwenye Custody yake tangu saa ngapi?

WAKILI DICKSON MATATA: Mheshimiwa Jaji Shahidi aliweza Kusema Kwamba alikabidhiwa Barua na Dispatch na Aliweza Kutaja Kuwa Ilikuwa na Rangi ya Pinki, Juu Imeandikwa Classic Dispatch Book
Inamaneno yameandikwa COURT 2
Ndani yake ina
anuani ya Mahakama

Kwa Maoni yetu shahidi aliweza Kusema Kwamba alipata wapi na alikaa nayo, Ni Ushahidi Wetu Kwamba Shahidi ni Competent
Kwa sababu Pingamizi lao Lilikuwa linahusiana na Competence na siyo Swala la Chain of Custody
Tunaiomba Mahakama Inapokuwa inatoa Maamuzi Juu ya Competence
Ijielekeze kwenye Kile Kilicho amriwa Katika Kesi Ya DPP VS MIZIRAHI na wenzake Watatu Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam, Criminal appeal namba 293 ya Mwaka 2016, Ukurasa wa Saba na Nane aya ya kwanza

Iliposema posseser anaweza Ku tender Document
Inasema…….. ANASOMA
Shahidi alionyesha ana hiyo Knowledge na aliposess Nyaraka hiyo tunaomba Mahakama Imuone ni Competent na Tunaomba Mahakama Itupile mbali Pingamizi hilo

Mheshimiwa Jaji naomba Wakili Mwenzangu amalizie

WAKILI FREDRICK KIHWELO: Mheshimiwa Jaji Mimi nitakuwa na Jambo Moja
Mheshimiwa Jaji Wakili Wa Serikali Wakati anazungumzia Swala la Dispatch , alisema Kutoka Kutajwa kwa Reference namba kwenye Dispatch

Kwa Maoni yangu Mheshimiwa Jaji alikuwa anazungumzia Authentication ya Dispatch hiyo
Mheshimiwa Jaji Wakati Shahidi anatoa Ushahidi Wake, Alizumgumzia Kidogo Kuhusu Dispatch hiyo kwa Kutaja Features Mbalimbali kama Rangi, Jina Lililopo Juu Kwa Maana Classic Dispatch Book na COURT 2

Naalikwenda Mbali Kwamba Ndani palikuwa na Tarehe, Anuani ya Barua na Sahihi ya Mpokeaji
Kwa Maoni yangu Kwamba aliweza Ku authenticate

Mheshimiwa Jaji Pia naomba nizungumzie Kuhusu Swala la Hati ya Mashitaka
Kwamba Shahidi Ameleta Nakala Na Shahidi alieleza kwamba Kwanini alileta Nakala

Kwakuwa Shahidi amesema Kwanini Shahidi Ameleta Nakala, Ni Submission Yetu Kwamba Ushahidi Wa Shahidi Unapaswa Kuchukuliwa akwa Uzito unaostahili

Na hilo pia lipo Katika Sheria Kesi Ya GOODLUCK KYANDO Vs REPUBLIC Criminal appeal 118, ya 2003 ipo kwenye Tanzania Law Report Kwenye Ukurasa wa 363 na Specifically 367
Mheshimiwa Jaji Kwa hili na yake ambayo yemezungukzwa na Wakili Mwenzangu Dickson Matata Naomba, Itupilie Mbali Mapingamizi na Ikubali Vielelezo Vilivyoletwa Mbele Yako

Ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji

JAJI: Jamhuri

WAKILI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Kwa Ufupi sana Naanza na Hoja ya Wakili Msomi Dickson Matata

Alianza Kujibu Hoja ya Relevance
Wakati anazungumzia Hoja ya Relevance
Ni kweli Shahidi alieleza hayo, lakini Hoja yetu ya Msingi ni Hayo aliyiyasema alipaswa aoanishe kwenye Hizo Nyarak
Tunaimbaia Mahakama Kwamba Vitu anavyosisema Vilipaswa Pia Kwa al Kuangalia hizo Nyaraka utayakuta
Kwa Ushahidi Mwingine sasa Yeye Kuunganisha
Yeye anasema Hakuna Uwezekano wa DC Msemwa Kupatikana Oysterbay na Mwaka huo huo Kuwa Central Police Dar es Salaam
Ingelikiwa anasema Kwa Siku hiyohiyo Sisi tuna Isingewezekana kwa Swala hili sisi tunasema hakuna Muunganiko

Akaenda ambali akasema Kwamba Nyaraka zile zimelenga Katika Kuthibitisha Kwamba DC Msemwa Hakuwa Kuwa Central Police Dar es Salaam
Walitakiwa Sasa Kuonyesha Nyaraka ambazo Ndani yake Ukizisoma Zina onyesha Kwamba DC Msemwa alikuwa Oysterbay Police
Sasa Kwakuwa Nyaraka hizo Kwa Hati ya Mashitaka na Proceedings zinaonyesha Mashitaka Ya phonograph

WAKILI PETER KIBATALA: OBJECTION Wakili anaruhusiwa Kwenda Ndani tena ya Proceedings

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Eneo Lingine Mwenzetu aligusia Swala la Secondary Evidence
Mwenzetu alielekeza Mahakama Kifungu cha 67 1(c) na aakaisomea Mahakama Kwa Ufasaha

Katika Hiki Kifungu, Wenzetu hawawezi Kupata Hifadhi hapa
Walitakiwa Kuieleza Mahakama Kati haya Matatu, Nyaraka Halisi either Imepokea, ama Nyaraka halisi imeharibika, ama kwa Sababu ambazo hazitokani na wao Wameshindwa Kuleta Nyaraka hiyo Ndani ya wakati
Sasa Kusema Pekee Kwamba aliyetuhudumia akituambia Kwamba hii Ndiyo Nyaraka pekee, haitoshi kwa Kusema

Badala yake Walipaswa Waonyeshe Jitihada Walifanya Nini Baada ya Kuambiwa Hivyo
Badala yake wanaitupi Mahakama Lawama Badala ya Kusema Walifanya nini
Kwa Maoni yetu siyo Sahihi
Vilevile Mheshimiwa Jaji Mwenzetu anaomba Mahakama Ipokee Nyaraka hiyo kwa kutumia Kifungu Cha 68(g)
Huu siyo Wakati wake,
Alipaswa aiombe Mahakama Kabla hatuja weka Mapingamizi

KWA hiyo Kitendo cha Kuomba Mahakama Ipokee Nyaraka hiyo Wakati wa Mapingamizi, Kwa Maoni yetu Siyo Sahihi
Mwenzetu Hakusema kwamba Nyaraka hii Kwa Mujibu kwa Kifungu cha 65 ni Secondary Evidence
Kitendo Cha Kuto Jibu Maana yake Wenzetu wamekubali na hawana Kipingamizi nalo
Vilevile Wenzetu Wamezungumzia Kuhusiana Na Swala la Competence Ya Dispatch
Wamezungumzia Competence Ya Shahidi Yenye Connection Na Dispatch
Mheshimiwa Jaji hapa tunaona Wenzetu wakichanganya Mambo mawili Kwa Wakati Mmoja

Wenzetu Wanasema Kwamba Kwa Sababu Shahidi ameweza Ku Identity Unique Features basi ana Knowledge
Mheshimiwa Jaji Utambuzi wa Nyaraka na Kilichopo ndani ya Nyaraka Ni Vitu Viwili tofauti
Kutambua Nyaraka Peke yake Haitoshi
Kwa Maoni yetu Kutambua Nyaraka Na Kujua Kilichopo ndani ya Nyaraka Ni Tofauti
Ugomvi wetu ni Kwamba Shahidi hajaweza Kutuambi Kilichopo Ndani ya Nyaraka ni nini
Sisi tunasema Hakuna Ushahidi Wa Shahidi Unaonyesha Kwamba FAITH Ali transfer Dispatch Kwa Shahidi

Connection hii inakosekana
Wenzetu Walitakiwa Wajibu Hoja yetu Katika Misingi huu, Kitu ambacho hawajafanya
Mwisho Wenzetu Wameielekeza Mahakama Katika Kesi Ya GOODLUCK KYANDO, Kitu ambacho sisi tunasema Principle hii haiwezi Kutumika hapa Kwenye kesi hii Wanaongelea Kielelezo ambacho Kipo Kwenye Kumbukumbu za Mahakama
Sisi tunasema Hoja za Wenzetu hazijajibu Hoja zetu
Sisi tunaomba Mahakama Isizingatie Hoja zao Kwa Sababu Hazina Nguvu Kisheria
Mheshimiwa Jaji Samahani, Walizungumza Pia Kesi ya DPP VS MIZIRAHI

Kwamba Ku possess Kukikuwa Kunatosha Kuonyesha Kwamba Kiliwwza Kuwa Kwenye Miliki yake
Sisi hatuja kataa, Bali tunasema Hicho anachotaka Kukitoa Ndiyo cha Faith
Kwa Hiyo Kesi zote Mbili hazina Connection na Kesi hii
Maombi yetu ni Vielelezo Hivi visipokelewe na Hoja za Wenzetu Kuhusu Mapingamizi zisitiliwe Mkazo

Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Jaji anaandika Kidogo, Wakati pande zote mbili Wamemaliza Kuwasilisha Hoja zao

JAJI: nimewasikia Pande zote mbili kwa Hoja zote mbili nahitaji Ku digest
Nahitaji Muda wa Dakika 45 kama naweza Kuwaita Mapema nitawaiteni
Tutarudi Saa Nane na Dakika 25

Jaji anatoka

Jaji amerejea Mahakamani Muda huu Saa 9 na Dakika 17

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena Mahakamani

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando:Upande wa Jamhuri Quorum ipo vile vile na tupo tayari

WAKILI PETER KIBATALA: na sisi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari na Quorum ipo Vilevile haijabadirika

JAJI: Muda Mfupi Uliopita kabla Mahakama Kupumzika
Niilisikiliza Hoja za Pande zote mbili
Sasa Uamuzi ni Kama Ufutavyo
Shahidi Wakati anatoa Ushahidi Wake ambapo ni Barua Kutoka Kwa Wakili Wake Peter Kibatala Kwenda Mahakama Ya Hakimu Mkazi, Dispatch na Mwenendo Wa Kesi pamona na Hati ya Mashitaka Kutaka Kuingia Kama Kielelezo
Jambo ambalo lilipingwa na Mawakili wa Serikali Kwamba Moja Nyaraka hizo hazina Uhusiano na Kesi (Relevance)
Na Pia Kwamba Hati Ya Mashitaka Ilikuwa ni Nakala na siyo Nakala Halisi

Tatu ilikuwa Kwamba Shahidi ajaonyesha Kwamba anaifahamu Dispatch
Mahakama Kwa kuzingatia Hoja zote za pande Mbili
Na Mahakama Ikazingatia Kwamba Nyaraka hizi Zinazoombwa Kuingia zitaishia Kwenye kesi hii Ndogo
Pia Kwamba Shahidi ana tatizo la kina Ki Afya
Na Kwamba Ni Kweli Kwamba Nyaraka zinatumika Kuuliza Maswali lakini Mahakama Inayo Muda wa Kuzichunguza
Kwa Sababu hiyo Mahakama Imeona izipokee Nyaraka kuzingatia Uamuzi Wake autaokuja Kutoa Mbele

Mahakama Inapokea Barua Kwenda Kwa Hakimu Mkazi Kisutu kama Kielelezo Namba 1
Mahakama Inapokea Dispatch Kama Kielelezo Namba 2

Mahakama Inapokea Nakala ya Hati Ya Mashitaka ambayo ilikuwa imefunguliwa Mahakama ya Kisutu Jamhuri Vs Lembrus MCHOME
Mahakama Inapokea Pia Mwenendo Wa Kesi hiyo namba 77 ya Mwaka 2020.
Kama nilivyosema Kwamba Mahakama Itatoa Uamuzi Juu ya Nyaraka hizi wakati Maamuzi wa Kesi Ndogo

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando; Naomba Kwa Record Juu ya Namba, Kuna Kielelezo Cha Goodluck

JAJI: Basi naomba Kubadirisha Namba,

Barua itakuwa D2
Dispatch Itakuwa D3
Hati ya Mashitaka ni D4
Na Mwenendo ni D5

JAJI: naomba Sasa Shahidi akabidhiwe aweze Kusoma

JAJI: Shahidi Nikikumbushe Kwamba Uliapa, na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo

WAKILI FREDRICK: Isome Barua hiyo

Shahidi… ANASOMA BARUA Kutoka TANAFRICA LAW kwenda kwa Hakimu Mkazi Kisutu

Shahidi anasoma kwa Kingereza kile cha Ndani Ndani kabisa (BBC ENGLISH)

Mahakama Imetulia Vizuri Kabisa inasikilizwa Kingereza Kinachovuti Kwa Namna anavyotamka Maneno Ya Kingereza (Pronunciation)

Nafikiri ni Mpare Wa Pili Kumsikia Kuongea Kingereza kizuri baada ya Waziri Mkuu Cleopa Msuya

Jaji Soma na Dispatch Book

Shahidi anasoma Dispatch Book.

WAKILI FREDRICK: naKukabidhi Hati ya Mashitaka Shahidi

Shahidianasoma Hati ya Mashitaka pia Kwa Kingereza

WAKILI FREDRICK: Nitakukabidhi Mwenendo Wa Kesi na nitataka Usome Page ya Kwanza na Ya Mwisho

Shahidi anasoma Pia Case Proceedings Kwa Kingereza Pia

Anasoma Page ya Mwisho Sasa….!!!

Shahidi amemaliza Kusoma Vielelezo Vyote, Lakini Mawakili wa Serikali Wanamshangaa Mwonekano kano wake na Kingereza chake ni Vitu Viwili

WAKILI Fredrick KIHWELO: Shahidi Ulisema Kwamba Oysterbay Ulikaa Siku 14 Je Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nikipofikishwa Oysterbay Mara ta Kwanza Nilikaa Siku Tano Kuanzia Tarehe 14 May Mpaka Tarehe 15 May 2020
Nilipo pelekwa Kisutu

WAKILI FREDRICK: Baada ya Hapo, Nikisomewa Kesi Na Kunyimwa Dhamana Nakutakia kwenda Magereza nikarudi Shwa Oysterbay Siku 14
Ilikuwaje Ukarudi Shwa Oysterbay

SHAHIDI: Baada ya Kukosa Dhamana, Hakimu alisema Nipelekwe Keko, Lakini Wakati Ule Palikuwa na Corona Siku pelekwa Magereza Badala Yake nikapekwa Oysterbay tena

WAKILI FREDRICK: Kwanini Sasa Hawakukupeleka Magereza Kama Hakimu alivyosema?

SHAHIDI: Kwa Uelewa Wangu Sababu ya Corona

WAKILI FREDRICK: Ulipimwa lini Corona
11/30/21, 13:41 – Irene Lema: Shahidi Siku ya Tarehe 19 May 2020
lini tena Ulipima Corona?

SHAHIDI: Hakuna zaidi Ya Kusubiri Majibu ya Corona

WAKILI FREDRICK: lini Ulirudishwa tena Mahakamani

SHAHIDI: Siku ya Tarehe 19 ambapo Hakimu alikataa Kunipokea Kwa Sababu Nilikuwa Nimtokea Polisi na siyo Magereza kama alivyoagiza

WAKILI FREDRICK: Siku ya Tarehe 03 nini Kilitokea

SHAHIDI: Siku niliyopelekwa Magereza

WAKILI FREDRICK: Na Siku ya Tarehe 05 June nini Kilitokea

SHAHIDI: Nilisomewa Mashitaka Kwa Njia Ya Mtandao na Hakimu akasema Kwamba Naweza Kupata Dhamana

WAKILI FREDRICK: Na Tarehe 08 June, Nini Kilitokea Siku ambayo nilipata Dhamana Maana Siku ya Tarehe 05 June sikukamlisha Masharti ya Dhamana
Umetaja Tarehe Nyingi Nyingi Je zote zipo Kwenye Mwenendo Wa Kesi

SHAHIDI: Ndiyo zote zipo

Tarehe 03 Mwezi Wa Sita Utaipata Ukurasa wa Ngapi

SHAHIDI: Ukurasa wa Tano

WAKILI FREDRICK: Tarehe 08 June 2020 Utaipata Ukurasa Upi?

SHAHIDI: Kwenye Ukurasa Wa Sita

WAKILI FREDRICK:
Nini Kilitokea Mwezi wa 10 August 2020

SHAHIDI: Hakimu aliniachia Kwa kifungu 225 baada Ya Upelelezi Kutokamilika

WAKILI FREDRICK: Nini Kilitokea tena

SHAHIDI: Nili kamatwa na kurudishwa tena Oysterbay

WAKILI FREDRICK: Uliwakuta Askari Gani

SHAHIDI: Mkuu wa zamu alikuwa Afande Msemwa, Hadija na Sam

WAKILI FREDRICK: Umekuwa Ulimtaja Afande Msemwa wa Oysterbay

SHAHIDI: Mwonekano kano wake ni Mweusi Kidogo kwangu, Anamwili kunizidi Kidogo.
Kitu Kingine ni Namba Yake

WAKILI FREDRICK: Namba gani?

SHAHIDI: Namba Yake Ya ajira

WAKILI FREDRICK: ambayo ni namba Ngapi?

SHAHIDI: H4323

WAKILI : Wakati Unajitambulisha Umesema Wewe Ni Mkulima, Ukiachana na Kilimo unafanya Shughuli Gani Nyingine

SHAHIDI: Najihusisha na siasa

WAKILI FREDRICK: Kule Mwanga Ulihojiwa Kwa Kosa gani

SHAHIDI: Kwa Makosa ya Kupiga Picha Gari ya Kiongozi Fulani wa Taasisi Fulani Tanzania

WAKILI FREDRICK: Ukashtakiwa kwa Makosa gani?

SHAHIDI: Kwa Makosa ya Kimtandao, Kitu ambacho Kilinishangaza

WAKILI FREDRICK: Unasema Ulitambua Afande Msemwa Kwa Namba Yake, Je Ilikuwa sehemu gani

SHAHIDI: Upande wa Kulia Kifuani

WAKILI FREDRICK: Wakati Unahojiwa hapa ulisema Kwamba Mwanga huku andika Jina Popote na Ulipokuwa Moshi pia Huku andikwa Popote

SHAHIDI: Watu wengi wana fikishwa Vituo Vya Polisi bila Kuandikwa Mahali Popote

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hayo ni Maoni yake

WAKILI FREDRICK KIHWELO: Naondoa Mheshimiwa Jaji

Na huo utakuwa Mwisho Wangu

WAKILI NASHON NKUNGU: Shahidi Ulisema Kwamba Askari walikuja Nyumbani Kwako Kukukamata, Je Walikuja nyesha Arrest Warrant.?
.
SHAHIDI: Hapana

NASHON NKUNGU: Nilisikia Pia Unasema Waliruka Geti

SHAHIDI: Ndiyo

NASHON NKUNGU: Je Walikuja na Kiongozi yoyote Wa Mtaani Kwako

SHAHIDI: Hapana

NASHON NKUNGU: Nilisikia Unasema Ulishtakiwa Kwa Matumizi Mabaya Ya Mtandao

SHAHIDI: Ndiyo

Nilisikia Ulikamatwa Kwa a Kupiga Picha Kiongozi Fulani Mkuu wa Taasisi Fulani hapa Nchini

SHAHIDI: Ndiyo

NASHON NKUNGU: Nilisikia Unasema Kuhusu Askari Msemwa hapa Mahakamani, Je Mnaugomvi

SHAHIDI: Hatujawahi Kuwa na Ugomvi

NASHON NKUNGU: Nilisikia Pia Kwamba Uliletewa Dar es Salaam Tarehe 14 May 2020

SHAHIDI: Ni sahihi

NASHON NKUNGU: Ulimuona Afande Msemwa Siku hiyo

SHAHIDI: Ndiyo

NASHON NKUNGU: Alikuwa Wapi

SHAHIDI: Mapokezi Oysterbay

NASHON NKUNGU: Ulikuwa Unapata Huduma Za Kibinadamu

SHAHIDI: Ndiyo

NASHON NKUNGU: kama Nini

SHAHIDI: Kama Chakula na Maji

NASHON NKUNGU: Nani alikuwa anakuhudumia Chakula

SHAHIDI,: Mimi nilikuwa Simfahamu Kwa sababu Nilinyimwa Kuonana Na Ndugu zangu

NASHON NKUNGU: Askari gani alikuwa anakuhudumia Kule Mahabusu

SHAHIDI: Askari wengi akiwemo Msemwa

NASHON NKUNGU: Asante Mheshimiwa Jaji

WAKILI MALYA:
Sasa Umesema Wewe Mwanasiasa Je Wa Chama Gani?

SHAHIDI: Wa Chadema

JOHN MALYA: Je Nikisema Wewe Mwanachama Umekuja Kusema Uongo Mahakamani Kumuokoa Mwenyekiti Wako Mahakamani?
Nitakuwa nasema Uongo.?

SHAHIDI: Uongo Mkubwa

JOHN MALYA: kwanini

SHAHIDI: Kwa sababu hata Ingekuwa Mtu wa CCM anatoa Ushahidi Wa Uongo ningekuwa Kuisaidia Mahakama

JOHN MALYA: Je Namba ya Msemwa Iko Kwemye Nini

SHAHIDI: Beji Kama Chuma Kifuani

WAKILI JOHN MALYA: Asante Mheshimiwa Jaji

WAKILI PETER KIBATALA: Shahidi Oysterbay ipo sehemu gani au Unakitu gani Kimepakana nacho?

SHAHIDI: Ubalozi Wa Marekani

KIBATALA: Asante Mheshimiwa Jaji sina Swali lingine

WAKILI WA SERIKALI Roberts Kidando: Shahidi Hebu tutajie Majina yako?

SHAHIDI: Lembrus Kapuya Mchome

WAKILI WA SERIKALI: Ulisikia Mtu anaitwa Mchome Je ni Ndugu yako

SHAHIDI Hapana, Utakuwa ni Ukoo labda

WAKILI WA SERIKALI: Kinachotofautisha MCHOME wewe na Wengine ni nini?

SHAHIDI: Maboma ya Kifamilia

WAKILI WA SERIKALI: Unamaanisha Nini

SHAHIDI: Ukoo Mkubwa au Kuna wachome Wengine Wala Hatufahamiani

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Umetuambia Kwamba Ulikuwa Unafuatilia Mwenendo wa kesi Hii kwa Mtandao na Magazeti

SHAHIDI: Sahihi

WAKILI WA SERIKALI:
Ulimaanisha Mtandao ni Mitandao ya Kijamii

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Katika Social Media unatumia Mtandao Ipi

SHAHIDI: Twitter

WAKILI WA SERIKALI: Unatumia Majina gani?

SHAHIDI: Lembrus MCHOME

WAKILI WA SERIKALI: Umesema pia wewe ni Mwanasiasa

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Katika Sasa unanafasi gani?

SHAHIDI: Ni Katibu Wa Chadema Wilaya ya Mwanga na Pia Katibu Wa Bavicha Mkoa wa Kilimanjaro

WAKILI WA SERIKALI: na utakuwa Mwanachama Hai,wa Chadema W
Kwa Muda gani?

SHAHIDI: Kwa Muda wa Miaka 11 Sasa hivi

WAKILI WA SERIKALI Katika Muda wote wa Kuwa Mwanachama Mwenyekiti Wako ni nani?

SHAHIDI: Ni Freeman Aikael Mbowe

WAKILI WA SERIKALI: Nitakuwa Sawa Nikisema Kwamba Kwenye Nyanja za Kisiasa Mnafahamiana Sana

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Unapendezwa na Uongozi wake

SHAHIDI: Sana

WAKILI WA SERIKALI: Kwenye Kesi hii, Ya Uhujumu Uchumi namba 16 ya 2021
Unafahamu alishitakiwa lini

SHAHIDI: Hapana Sikumbuki

WAKILI WA SERIKALI: ya Mwaka huu au Mwaka Jana

SHAHIDI: Mwaka huu

WAKILI WA SERIKALI: Wakati unashtakiwa Hati yako inasema Kwamba Unashtakiwa Kwa Publication of Ponograph

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Unasema Kwamba Kesi hiyo ili maliza Tarehe 10 Mwezi 08 2021

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Wakati Huo Freeman Mbowe ameshashrakiwa tayari

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Baada Ya Kuwa Umeshaaachiwa Je Ulifunguliwa Kesi Nyingine tena

SHAHIDI: Hapana

WAKILI WA SERIKALI: utakubaliana na Mimi Kwamba Kwa Kipindi hicho kabla ya Kufahamu

Kwanza Nikuulize Swali

Je Ni kweli Ulifahamu Msemwa alitoa Ushahidi Kupitia Mitandao

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Ni kweli Kwamba, Kabla ya Kuona Taarifa hizo na Ulichukulia Kwamba Shitaka lako limefutwa, Kabla ya Hapo Ulikuwa Ujawahi Kuomba Kupatiwa Mwenendo na Hati ya Mashitaka

SHAHIDI: Hapana

WAKILI WA SERIKALI: Katika Mitandao ya Kijamii Haswa Twitter Ambapo Unajulikana Kama Lembrus MCHOME
Namna ya Kutuma Ujumbe Unautengeneza Mwenyewe yani (User generator)

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Ukitaka Kuchukua Ujumbe wa Mtu Mwingine yani Retweet Unafahamu

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Kwenye Mtandao Wa Twitter, Kama Naelewa Utanifahamisha, Ni Information Ambazo Mtu anaweza Kuona zile ambazo umetweet na Kuziona

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Sasa na Mara Nyingine Umekuwa Uliandika Ujumbe Unaohusiana na Kesi hii Kule Twitter

SHAHIDI: Ndyo

WAKILI WA SERIKALI: Katika Moja wapo ya Vitu Ulivyotweet Ukasema “kesi Mikazo, Mashahidi wa Michongo” ulikuwa unamaanisha nini

SHAHIDI: Maana yake ni Mashahidi Wa Kuunga

WAKILI WA SERIKALI: Vipi Kuhusu Mawakili wa Serikali wa Michongo na Majaji wa Michingo

SHAHIDI: Kwasababu Mawakili wa Serikali Wanateta Mashahidi Wa Uongo

WAKILI WA SERIKALI: Na Vipi Kuhusu Majaji wa Michongo

SHAHIDI: Ndiyo Kuna Hukumu ambazo Wanatoa hazipo Sawasawa

Mahakama kichekoooooo

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo Unamalalamiko Kuhusu Kesi hii

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo wewe ni Shahidi Mwenye Malalamiko

SHAHIDI: Ninayo Malalamiko Kwa Sababu Mahakama inadanganywa

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo Unatamani Siku Moja Mawakili Wa Serikali unaowataka Wewe

SHAHIDI: Nataka Haki itendeke

Wakili wa Serikali Jibu swali Langu

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo Unatamani Siku Moja Mawakili Wa Serikali unaowataka Wewe

SHAHIDI: Ambao Watakuwa Wapo Sahihi Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Ni kweli Watu walikuwa wa nakupa Pole Kwenye Mitandao yako
Baada ya Kupata Ajali

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Walikuwa wa nakupa Moyo Kamanda Nenda Kapambane

SHAHIDI: Hiyo sijaona

WAKILI WA SERIKALI: Kitu Kilichokufanya Uje Kutoa Ushahidi, Unamfahamu linamuhusu Mshitakiwa Yupi?

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Nano

SHAHIDI: Katika Shitaka hili Dogo ni Mohammed Ling’wenya

WAKILI WA SERIKALI: Wakati Unaongozwa na Wakili Dickson Matata Na Fredrick Kihwelo Ni kweli Hukutoa Ushahidi huyu Mohammed Ling’wenya Mnafahamiana Lini na Wapi

WAKILI WA SERIKALI: Ni kweli Kwamba Wakili Peter Kibatala ambaye Ulimpa Maelekezo Kwamba aandike Barua Kwenda Kisutu, Yeye Siye anayemwakilisha Mohammed Ling’wenya

SHAHIDI: Ndiyo nafahamu

WAKILI WA SERIKALI; Kama unafahamu Sema sasa ni Lini sasa Ulifahamu Kwamba Peter Kibatala amuwakikishi Mohammed Ling’wenya

SHAHIDI: Kwenye VYOMBO Vya Habari

WAKILI WA SERIKALI: Na Unafahamu Kwamba Peter Kibatala Anamwakilisha Freeman Mbowe

SHAHIDI: Nafahamu Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Mwanzoni Nilikuuliza Kuhusiana na Jina Mchome, Turudi Sasa Kwa Jina la Msemwa
Je litakuwa na Watu wengi wanaoitwa hivyo

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Katika Ushahidi Wako Tangu Unaongozwa Jana Hukutoa Ushahidi Kwamba Kwa Jina hilo la Msemwa Wapo Watu Wengi Kwa jina la Msemwa

SHAHIDI: ndiyo

WAKILI WA SERIKALI Na Hukusema hawa watu wa Jina la Msemwa Wapo Wangapi Kwa Jeshi la Polisi

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Kwa Sababu Ulikuwa Ukifuatilia Kesi hii, Unafahamu Kwamba hii ni Kesi Ndogo Ya Pili

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Unafahamu pia Kwamba Katika Kesi Ndogo Ya Adam Kasekwa Msemwa alitoa Ushahidi

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Ulifahamu Lini Siku hiyo hiyo au

SHAHIDI: Sikumbuki

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Shahidi Katika Ile Barua iliyopo lelewa Mahakamani ilivyoandikwa na Kibatala Kwenda Kisutu, Ni kweli Kwamba haina Jina la Mohammed Ling’wenya Popote pale

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Kutokana na Jinsi ilivyoandikwa ndiyo inaakisi Kile Ulicho Muelekeza Peter Kibatala

Shahidi Ndiyo
SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI 6wa SERIKALI: Sasa Kwa Mazingira hayo hata Katika Ushahidi huu, Ni Mamubaliano Yako Kuja Baina yako na Peter Kibatala

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Wenzangu Waendelee

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula:
anasimama

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Naomba nianzie alipoishia Mwenzangu
Mheshimiwa jaji naomba ni Muonyeshe Shahidi Exhibit D2
Umeona Enheeeeeee
Nyaraka I naelekeza akwa nani

SHAHIDI: I naelekezwa Kwa Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu

WAKILI WA SERIKALI: Ni sahihi Ilimfikia huyo Hakimu Mkazi Kisutu

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Nyaraka hiyo Wamepewa nani na nani

SHAHIDI: Lembrus Mchome
Na Naibu Msajili Wa Mahakama hii

WAKILI WA SERIKALI: anapaitika Wapi

SHAHIDI: Mahakama hii

WAKILI WA SERIKALI: Yupo humu Ndani

SHAHIDI: Hapana

WAKILI WA SERIKALI: Nitakuwa Sahihi Kwamba Umekuja baada ya Kusikia, DC Msemwa Kusema Kwamba alimpokea Mohammed Ling’wenya Pale Kituo cha Polisi Central

WAKILI WA SERIKALI: Reference namba zinamuhusu Nani

SHAHIDI: Mbowe

WAKILI WA SERIKALI: Wakili Wako ni nani

SHAHIDI: Peter Kibatala

WAKILI WA SERIKALI: Anamwakilisha Nani katika hili Shauri

SHAHIDI: Freeman Mbowe

WAKILI WA SERIKALI: Nitakuwa Sahihi nikisema Freeman Mbowe anaitambua Barua hii

SHAHIDI: Hilo silijui

WAKILI WA SERIKALI: Ni kweli Kwamba Mohammed Ling’wenya atakuwa anajua Barua hiyo

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI DICKSON MATATA: Mheshimiwa Jaji Napinga Swali na Jibu sababu Lina Suggest Opinion

JAJI: Ngoja tumsikie

WAKILI WA SERIKALI: Swali langu Kwamba Hiyo Barua haionyeshi Kumfikia Bwana Mohammed Ling’wenya

JAJI: ni Wakati gani hapo Opinion,

WAKILI DICKSON MATATA: Kauliza Ni kweli Kwamba Mohammed Ling’wenya Ajui kuhusu Barua hiyo

JAJI: Basi Wakili wa Serikali Rudia Swali

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Ni kweli Kwamba Kwa Maudhui ya Barua hiyo haionyeshi Kumfikia Mohammed Ling’wenya

SHAHIDI: Hilo sijui

WAKILI WA SERIKALI: kuanzia Siku ya Jana Mpaka Leo Hii hakuna Sehemu yoyote Uliyo eleza Kwamba Uliwasiliana na Mohammed Ling’wenya

SHAHIDI: Ni sahihi

WAKILI WA SERIKALI: Ni sahihi Kwamba Mahakama Haijaonyesha Kwamba Mohammed anaufahamu wako wewe Kuwepo Mahakamani

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo nitakuwa nakosea Nikisema Wewe Umeletwa Kwa Madhumuni fulani fulani

SHAHIDI: Sana

JAJI: Shahidi Umesema

SHAHIDI: Sawa

WAKILI DICKSON MATATA: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ameshajibu

WAKILI WA SERIKALI: Hakuna Kurudia Swali

JAJI: Miye Mwanzo nimesikia Sana

WAKILI DICKSON MATATA: Namimi nimesikia Sana

JAJI: Wakili wa Serikali, Kwa Maslahi Ya Haki hebu rudia Swali

WAKILI WA SERIKALI: Habu Soma hii Nyaraka Paragraph Ya Pili

SHAHIDI: Shahidi anasoma Kwa Kingereza

WAKILI WA SERIKALI: Hebu ijibu Mahakama Mr. Freeman Aikael Mbowe ndiyo Mohammed Ling’wenya

SHAHIDI: Hapana

WAKILI WA SERIKALI: Hebu I ambie Mahakama Ni sehemu Gani imeandikwa Kwamba hizo Taarifa unazoomba Umelenga Kuthibitisha Kwamba Mr. MSEMWA Hakwepo Central
SHAHIDI: Hakuna

WAKILI WA SERIKALI: Katika hiyo Barua ni sehemu Gani Inaeleza Kwamba Ulikuwa Kituo Cha Polisi Oysterbay

SHAHIDI: Hakuna

WAKILI WA SERIKALI: Ni wapi Katika Barua hiyo Sehemu Inavyoonekana Kwamba Wakili anaye Mwakilisha Mohammed Ling’wenya Kwenye hiyo Barua

SHAHIDI: Hakuna

WAKILI WA SERIKALI: Ulisema Tarehe 14 Maya 2020, Wakati Umefikishwa Oysterbay Polisi, Miongoni Mwa Askari Aliyekuhudumia alikuwa na DC Msemwa

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Na Ulisikika Ukisema Kwamba ulimtambua DC. Msemwa kupitia Beji yake aliyo vaa

SHAHIDI: Hapana

WAKILI WA SERIKALI: Nitakuwa Sahihi Nikisema Kwamba Huyo DC Msemwa Uliyemtambua wewe alikuwa amevaa Uniform

SHAHIDI: ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Kwa hiyo nitakuwa Sahihi Nikisema Ulimtambua DC Msemwa Baada ya Kuona Beji yake yenye namba yake 4323

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Toka Umeanza Kutoa Ushahidi Wako Siku ya Jana Mpaka Leo Hii Hakuna Mahala Umesema Kwamba alikwambia ni wakati Gani anaitwa DC Msemwa na Hukusema ni Wakati gani ulipata Kujua

SHAHIDI: Ndiyo

WAKILI WA SERIKALI: Kwa Kushindwa Kusema Ulijuaje anaitwa DC Msemwa, Mahakama ipo gizani

SHAHIDI: Si Kweli

WAKILI WA SERIKALI Abdallah Chavula: Kwa Ruhusa Yako tunaomba tuendelee Kesho Kwa sababu Muda hautoshi

WAKILI PETER KIBATALA Mheshimiwa Jaji Tulishaliomgea hilo Kwenye Briefing Kwamba Tumlimde Shahidi Haki yake ni Mtu aliye Pata Ajali
Na Kwamba tulimuomba Mpaka Kwa Wazazi wake, Shahidi Ni Magonjwa na Haki yake inaonekana

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Magereza Waliomba Asubuhi Kwamba tujitahidi tumalize Saa 11 ili Wapate Muda wa Kuwahi Kurudi Magereza

JAJI: ni Kweli Kwamba tulikaa pamoja Asubuhi Kwamba Kuna Jambo hilo la Hali ya Shahidi
Ni swala linahusu Haki

Haki Upande wa Mashitaka Kusikilizwa

Na Hali ya Shahidi Tunaona pia

Je Shahidi Unaweza Kesho kuwepo

Nikuombe Shahidi, Je Uwezi Kuja Kesho

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji Haki yangu inaniwia Ngumu, Ila Kwa Sababu ni Ombi lako inanibidi nikubali

JAJI: jitahidi tuh, tuh ni Ombi kutoka kwa Jaji
Na hilo nimekuomba wewe Binafsi Siyo Kupitia Kwa Wakili

WAKILI WA SERIKALI Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Hairisho Mpaka Kesho Tarehe 01 Mwezi wa 12 ilituweze Kuendelea na Cross Examination

JAJI: Upande Wa Utetezi Mnaye Shahidi Mwingine

WAKILI PETER KIBATALA: Tunaye Mmoja

JAJI: Shahidi Baada ya Kuwa Nimekuomba na Umenikubalia naomba Kesho Uje

Washitakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi

Saa 3 Asubuhi

Basi nawatakia Jioni Njema

Jaji anatoka

Like