Kesi ya Mbowe: Shahidi wa Jamhuri augulia kizimbani

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia, BJ, leo tarehe 17, Januari 2022.


Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa leo Jumatatu ya Tarehe 17 Januari 2022

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo Pamoja na

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka Wote Mawakili Wa Serikali Waandamizi

Pamoja na Tulimanywa Majige

Wakili Peter Kibatala ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na Mawakili

Jeremiah Mtobesya
John Mallya
Faraji Mangula
Dickson Matata
Seleman Matauka
Michael Mwangasa
Khadija Aaron

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja na tupo Tayari Kuendelea

Wakili Peter Kibatala: Nasisi pia Tupo Tayari Kuendelea

Shahidi anakwenda kuitwa

Anakuja Kwa Mbali Shahidi Wa Kiume

Jaji: Majina

Shahidi: Inspector Innocent Ndowa

Jaji: Umri

Shahidi: 37

Jaji: Kabila

Shahidi: Mchaga

Shahidi: Mimi Inspector Innocent Ndowa Naapa Kuwa Ushahidi nitakaotoa utakuwa wa kweli tupu Eehee Mwenyezi Mungu Nisaidie

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ataongonzwa na Wakili Pius Hilla

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Majina Yako Kamili ni nani

Shahidi: Naitwa Inspector Innocent Ndowa

Wakili wa Serikali: Unafanya Kazi gani

Shahidi: Mimi ni Askari Polisi

Wakili wa Serikali: Tangu lini Shahidi: Mwaka 2012

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kituo chako Cha Polisi cha Kwanza

Shahidi: Makao Makuu ya Polisi Ya zamani

Wakili wa Serikali: Ulisema Ya Zamani Una manisha Nini

Shahidi: Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam, posta Kabla hayajaamishiwa Dodoma

Wakili wa Serikali: Kazi yako ni Ipi huko Polisi

Shahidi: Wakati Naanza Kazi nilikuwa Katika Kamisheni ya TEHAMA Makao Makuu

Wakili wa Serikali: Ulifanya Kazi hadi lini

Shahidi: Mwaka 2014

Wakili wa Serikali: Mwaka 2014 kilitokea Kitu gani

Shahidi: Nikahamishiwa katika Kamisheni ya Uchunguzi wa Kisayansi

Wakili wa Serikali: Ipo wapi

Shahidi: Makao Makuu ya Polisi Ya Zamani

Wakili wa Serikali: Kamisheni Ya Uchunguzi Wa Kisayansi upo Kitengo Gani

Shahidi: Nipo katika Uchunguzi Wa Makosa ya Kimtandao, Yaani Cyber Crime

Wakili wa Serikali: katika Hilo Kitengo Una Muda gani

Shahidi: Kwa sasa Nina Miaka 8

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kwamba Kitengo hicho cha Cyber Crime Kina husika na Nini hasa

Shahidi: Kina Husika na Uchunguzi Wa Vifaa Vya Ki Electronics Ambavyo vinadhaniwa Kutumika Katika Matukio Mbalimbali ya Kihalifu

Wakili wa Serikali: Sasa wewe ni nani Katika hicho Kitengo

Shahidi: Mimi ni Computer and Mobile phone Forensic Analyist

Wakili wa Serikali: Wewe Ukiwa kama Computer and Mobile phone Forensic analist Majukumu yako ni Yapi

Shahidi: Kupokea Vifaa Kama Computer na Simu ambavyo vinatuhumiwa Kuhusika katika Matukio Mbalimbali. Kazi ya Pili ni Kufanya Uchunguzi Mbalimbali Kufuatia Maombi Ya Taasisi Mbalimbali, Kuandaa Ushahidi

Wakili wa Serikali: Fafanua Hilo Jukumu la Kuandaa Ushahidi

Shahidi: Inapotokea Kifaa kimekuja, Kuna Utaratibu Wa Kuandaa Ushahidi Wa Namna Kifaa Kilivyo kuja, Jukumu hilo ni la Kwetu la Kiuchunguzi Jukumu lingine ni Kuandaa report ya Uchunguzi Jukumu lingine ni pale ninapohitajika Kutoa Ushahidi Basi naenda Kutoa Ushahidi

Wakili wa Serikali: Wewe Shahidi Ni Analyist, Sasa Ifahamishe Mahakama Unautaaluma gani

Shahidi: Kwaka 2009 nilihitimu Katika Chuo CHA usimamizi wa Fedha IFM katika… 2012 nilijiunga katika Jeshi la Polisi 2014 nilifanya Certificate in Ethical Hacking, Taasisi Ya Uingereza Ipo DSM, Upanga

August 2014 nilifanya Kozi inaitwa Penetration Testing, Chini ya Taasisi inaitwa ATU ikifanyika Dar es Salaam Chini ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania November 2014 ndiyo Niliingia Forensic bureau

Nilienda Kozi Nyingine India ambayo inaitwa Certificate course in Networking, ilifanyika katika Chuo kinaitwa UTL Technology Limited Mwaka 2016 June Nilifanya Training Nyingine Dar es Salaam inaitwa Identification and Seizure of Digital devices ambayo ilitolewa na Taasisi ya Chini ya Ubalozi wa Marekani ambayo inaitwa BUREAU OF DIPLOMATIC SECURITY July 2016 nilifanya Training Nyingine ambayo inaitwa Network Security administration Version 4 ambayo ilitolewa na Link Academy

Kozi Nyingine Chini ya Ubalozi wa Marekani ambayo inaitwa Terrorist Crimes Scene Investigation September 2016 nilikwenda Nchini Egypt kufanya Kozi inaitwa CRIMINAL INVESTIGATION AND CRIME SCENE

Shahidi: Mwaka huo huo November Chini ya Ubalozi Wa Marekani Nikifanya Kozi INAITWA DIGITAL LABORATORY FORENSIC MENTORSHIP PROGRAM. Mwaka 2018 March Nchini RWANDA nikafanya Kozi inaitwa CYBER CRIME INVESTIGATION

Mwezi may Mpaka June 2018 Nilienda Nchini Uganda Kufanya Kozi inaitwa CYBER SECURITY Mwaka 2021 nilifanya Kozi Nyingine Katika UNIT ACADEMY ambapo nilifanya Kozi ya Certificate of Hacking, Version 12

Wakili wa Serikali: Shahidi Umeeleza Vyema Kuhusu Ujuzi na Taaluma Yako, Eleza Mahakama Taratibu za Upokelewaji wa Vielelezo Vya Ki Electronics

Shahidi: Utaratibu wa Upokelewaji Wa Vielelezo Vya Ki Electronics Unaanza Katika Kitengo Chetu ambapo Pale Unakutana Na Mapokezi Ukiwa na Barua na Kielelezo Husika, Unamkabidhi Ofisa wa zamu

Wakili wa Serikali: Ifahamishe Mahakama sasa Upo pale na Kielelezo Kimefika

Shahidi: Jukumu la Ofisa wa Zamu, Ni Kwanza Kukagua Kielelezo na Barua Husika

Wakili wa Serikali: Unakaguaje?

Shahidi: Kwa kufanya Identification, Barua Ka Ina Kifaa kama Simu lazima Iwe namba Kama IMEI namba, Unakagua kama Ipo

Shahidi: Baada ya Identification Ofisa Amejiridhisha Wajibu wake ni Kuvipa Usajili Wa Maabara

Wakili wa Serikali: Usajili Unafanyikaje

Shahidi: Unafanyika Kwa Mwaka Husika, Kwa Reference namba ya Barua, Useme Imetoka Himaya ya nani, Tarehe iliyofika Kwako na Vielelezo Vilivyofika kwako

Wakili wa Serikali: Una sajili Kwenye nini

Shahidi: Kwenye Kitabu Cha Maabara Kutoa Lab Namba

Wakili wa Serikali: Hiyo Lab Namba Inapatikanaje

Shahidi: Inatolewa In sequencial Series Pale ambapo Mwaka Unaanza unasajili namba moja

Wakili wa Serikali: Hatua Inayofuata ni nini

Shahidi: Hatua Inayofuata ni Kifungua Jalada

Wakili wa Serikali: Jalada linafunguliwa kwa Madhumuni gani

Shahidi: Kwa Kuangalia Vielelezo na Kutunza Vielelezo, na Kama Kazi Ifanyika

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine kinafanyika

Shahidi: Kielelezo Chenyewe Kinatakiwa Kutunza Kwenye Roka lake, Kwa ajili ya Kutunza Kielelezo, na Baadae Jalada lina enda kwa Commanding Officer na Baadae kwa Kamishina Kwa ajili ya Kutolea Maelekezo na Kupanga kazi

Na Baadae ndipo linarudi Kwa ajili ya Kufanya Kazi na Kuchukua Vielelezo hivyo..

Shahidi: Ni Kufanya Uchunguzi, Kwa Mujibu wa Ratiba yake, Wajibu wake ni Kutunza na Kufanya Kazi ya Uchunguzi

Shahidi: Ni Kufanya Uchunguzi, Kwa Mujibu wa Ratiba yake, Wajibu wake ni Kutunza na Kufanya Kazi ya Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Tuongelee Uchunguzi Wa Hivi Vifaa, Uchunguzi wa hivi Vifaa Vya Ki Electronics vinachunguzwa Vipi, Kwa Kifupi

Shahidi: Uchunguzi wa hivi Vifaa Unafanyika Kwa Hatua tatu

Wakili wa Serikali: Hatua zipi

Shahidi: Ya Kwanza ni Aquirezation Maana yake Unafanya Extraction ya Kifaa Husika

Wakili wa Serikali: Una Extract nini

Shahidi: Taarifa zinazotokana na Kielelezo

Shahidi: Hatua ya Pili Unafanya Analysis Hatua ya Tatu Unafanya Reporting

Wakili wa Serikali: Hivi Vielelezo ni Vielelezo Vya Namna Gani ambavyo Vinafanyiwa hizi Hatua

Shahidi: Vielelezo Vya Electronics, Mobile Phone, Gard Disk, Flash Disk, Sim Card, Memory Card, na Vifaa Vingine Vyenye Asili Kama hiyo

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Uchunguzi Wa Vifaa Vya Namna hii Unafanyika Kwa Vifaa gani

Shahidi: Kwa Kutumia Vifaa Vya Uchunguzi wa Kimaabara kwa Vifaa Vinaitwa CELEBRITE MACHINE

Wakili wa Serikali: hiyo CELEBRITE MACHINE Inafanyaje kazi

Shahidi: Inakuwa na Kifaa Kinaitwa LAGADIZZED ambacho ni Computer ambayo inakuwa na Windows ndani yake ambayo ni UNIVERSAL FORENSIC EXTRACTION DEVICE (UPC)

Wakili wa Serikali: Mbali na hicho, Kingine ni nini

Shahidi: Forensic Cables pamoja na Adapter Pia Kuna Kifaa Kingine Kinaitwa CELEBRITE PHYSICAL ANALYISER

Wakili wa Serikali: Software ambazo mnazotumia ni nini

Shahidi: Ni CELEBRITE PHYSICAL ANALYISER NA UPC unakuwa na Kifaa Kinaitwa DONGLE license kwa ajili ya Kufanyia Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Hujaielezea Mahakama Extractions Zinafanyika Vipi

Shahidi: Extraction inafanyika Kwa Kufanya Kifaa Husika Kama ni simu au kingine, kinaunganishwa na Mashine ya Uchunguzi Kwa Kutumia Forensic Cables

Wakili wa Serikali: Ili hicho Kilichopo kwenye Kielelezo ili kiweze Kuchukuliwa ni Nini Kinafanyika

Shahidi: Kwanza Ile UPC lazima Ui run kwenye Mashine, Ukiwa tayari umesha connect Device Yako Kwenye ile Mashine kile Software Ina Detect Kile Kifaa

Wakili wa Serikali: Kwa sababu gani

Shahidi: Kwa sababu Architecture ya Kile Kifaa Kinaundwa na Software mbalimbali za Zile Devices

Wakili wa Serikali: Inapo Detect Kuwa Umeunganisha Devices na Kifaa Je Ni taarifa ipi Inatoa

Shahidi: Ina Tegemea Na Kifaa Ulicho tumia, Itakuoa aina ya Extraction ambayo Inaweza Kufanya Katika hicho Kifaa

Wakili wa Serikali: Kingine

Shahidi: Kikubwa ni hicho.

Wakili wa Serikali: Nimekuuliza Information ambazo Zinakuwa Detected na zile simu ni zipi

Shahidi: Kama IMEI namba na Mobile Phone Namba

Wakili wa Serikali: Kina Kuwa ni Kielelezo gani

Shahidi: Kwanza lazima Ufanye Isolation, Kwa kutumia Flight Mode au Faraeay Forensic

Wakili wa Serikali: Kwanini Iwe hivyo Shahidi: Kwa sababu ya Forensic principles ili Ku’ mantain Data zilizopo Ndani, na Ushahidi Utakaotoa uweze Ku’ Sound

Wakili wa Serikali: Na Kifaa unachotumia Kufanya Uchunguzi Kinatakiwa Kuwa Katika hali gani

Shahidi: Kwanza Kinatakiwa Kuwa na Software ambazo zipo Updates kwa Maana ya Windows pamoja na Severs, Pamoja pia na Physical analyser, Lazima Wakati wote Kifaa Kisiwe na Any Connection ya Internet Wakati wote wa Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Kwanini Shahidi?

Shahidi: Ili Kuzuia kwa namna yoyote ile Mtu ambaye hayupo Physical asiweze Ku’ access Kile Kifaa

Wakili wa Serikali: Baada ya Ku’ Extract Vitu Vyote Unaviweka wapi Shahidi

Shahidi: Unaviweka Katika Storage ambayo Inakuwa Ndani ya Computer

Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Ambapo Extraction inakuwa Imekwisha

Shahidi: Pale ambapo Mashine inakwambia Imemaliza, Una accept YES

Wakili wa Serikali: Unasema Inafanya Storage Ndani

Shahidi: Ndiyo ni Kifaa kinachokuwa na Hard Disk Ndani, Kwahiyo Unachagua Kuweka katika Partition Baada ya Kufanya Kazi yake

Shahidi: Hatua inayo fuata ni analysis ya Extracted Data Analysis Inafanyika kwa Kutumia CELEBRATE PHYSICAL ANALYISER Mfumo huu una kazi Kuu tatu, KAZI ya Kwanza ni Kufanya RECORDING, ANALYISIS kwa Kufanya Advanced Search ya Stored Data na ya Tatu ni DECORDING

Wakili wa Serikali: unaposema DECORDING ina maana gani

Shahidi: Huwa tunapata Extraction ambazo kwa Jicho la Kawaida huwezi Kuziona, Sasa Mfumo unafanya Kuona Taarifa kwa Usahihi Kabisa, Process Nzima Ndiyo tunaita DECORDING

Wakili wa Serikali: Unaposema Search katika Uchunguzi Wenu Maana yake ni Nini?

Shahidi: Tunapo fanya Uchunguzi Maana yake Tunatafuta Ushahidi, Kwa Mfano Kwenye terms of reference Unapata Unachotafuta na inakuletea Majibu

Shahidi: Hizo nazipata Katika Barua

Wakili wa Serikali: Barua Ipi

Shahidi: Ya Mpelelezi ambaye ameomba Uchunguzi Wa Kisayansi ufanyike

Wakili wa Serikali: Elezea Vizuri Madhumuni ya hiyo search ni Kitu gani

Shahidi: Ni Kusaidia Uchunguzi, Kwa kuwa tuna simu ambazo Zina hifadhi Data Nyingi, Kama GB 200 Sasa yenyewe Inakusaidia Kwenda Direct katika Kitu unachokitafuta Unaenda Moja Kwa Moja kwenye Text Meseji, Mult Media,

Wakili wa Serikali: Pia Ulitaja Advanced Search, Je hiki ni Kitu gani

Shahidi: Inafanya Indepths Diving Hiden, Pale ambapo Kitu ambacho unatafuta Kina Kuwa Hiden au Kimekuwa Deleted, Sasa Yenyewe inatafuta ili Kuleta Majibu

Wakili wa Serikali: Na hii Madhumuni yake ni Nini

Shahidi: Kutafuta Ushahidi Ulipo

Wakili wa Serikali: Hapo Mwanzoni Ulisema Kuwa Mashine Ulisha connect kupitia Forensic Cables kupitia Profile yake, Je Kama Hakuna Profile Yake

Shahidi: Kama Profile ya Kifaa Haipo, Manufacturer amekupa Option Ya Kufanya Extraction Ku’ base Kwa Operating System au Kwa Chip Search ya Simu

Wakili wa Serikali: Tuongelee sasa reporting, Je inafanyikaje?

Shahidi: inafanyika pale ambapo Imetambulisha zoezi la Analysis, Kwenye Mfumo ambapo kisha funga Zoezi hilo inaenda Next Stage ambayo ni Reporting ambapo Inakuoa Fursa Mchunguzi Kuweka Details ambazo Zinahusiana na Kesi

Wakili wa Serikali: Reporting hizi zinfanyikia wapi

Shahidi: Zinafanyika kama Segment ndani ya Mfumo wa Physical analyser

Wakili wa Serikali: Inafanyikaje

Shahidi: Mchunguzi anaweka Jina la Mtuhumiwa, Namba ya Kesi, Taasisi ambayo Inafanya Uchunguzi, Majina yake, pamoja na namba ya Kesi, Lab Namba pia

Wakili wa Serikali: Tofauti na Taarifa hizo, Kwenye Segment ya Report Kuna Taarifa zipi Nyingine

Shahidi: Taarifa zingine ni zile zimekuwa generate katika Mfumo ambazo Zinahusiana na Mfumo

Wakili wa Serikali: Muda wote Extraction, na Reporting zile Data znazokuwa Katika Kielelezo Zinakuwa katika Hali gani

Shahidi: Wakati wote Wa Process inafanyika Mashine Ina Kitu Kinaitwa….ambacho Kina ruhusu Kutoa Taarifa lakini hakirihusu Manipulation ya Taarifa ya aina yoyote

Lakini Pia Lengo la analysis hatutaki Content yote ya kwenye simu, Mchunguzi anakuwa anahitaji Taarifa ambazo anazitaka kwa ajili ya Uchunguzi wake

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kwamba Mambo yote Yamefanyika, baada ya hapo ni Kitu gani Kinafuata

Shahidi: Baada Reporting Kufanyika Kama Content si Kubwa Unaweza Ku Print kama ni Kubwa Unaweza Kwenye Storage, Kama DVD, FLASH DISK kutegemeana na Ukubwa

Wakili wa Serikali: Kwa Content ambazo ni Chache Unasema Unaprint, Je Ulisha Print ni Kitu gani Kinafuata

Shahidi: Kama Ume’ print na Kulinganisha Taarifa Yako, verification Kuangalia Usahihi

Wakili wa Serikali: Baada ya Hapo

Shahidi: Ni Kujiridhisha Kama Ulicho nacho na Kwenye Mfumo ni sawa

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama tofauti na print out, Vielelezo vinakuwaje

Shahidi: Kwanza Mtu wa Maabara Unatakiwa Uweke MARK Kwa ajili ya Utambuzi na Ndiyo utayotumia katika Report yako

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo

Shahidi: Unaweka Muhuri Ambao Una Nembo ya Polisi na FORENSIC BEAURRIAL, unasaini

Wakili wa Serikali: Ile Report yako sasa Unayoandaa Inakuwaje

Shahidi: Ya Kwanza inakuwa na Extract ambazo tumezipata, Lazima iwe na Vielelezo Vyote ambavyo Vimeletwa Pale, lazima iwe na Majina ya Uchunguzi

Shahidi: Ya Kwanza inakuwa na Extract ambazo tumezipata, Lazima iwe na Vielelezo Vyote ambavyo Vimeletwa Pale, lazima iwe na Majina ya Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Kuhusiana na Uchunguzi wenyewe

Shahidi: Taarifa Yangu itajibu Maombi ya Taarifa iliyoomba

Wakili wa Serikali: Baada ya Kusaini kitu gani unafanya

Shahidi: Mchunguzi anakuwa na Jina lake, namba ya Simu, Tarehe ya Uchunguzi ambao Umefanyika Unaenda Kuzihifadhi katika Roka lako la Kuhifadhi Kazi za Uchunguzi zilizokamilika

Wakili wa Serikali: Kuhifadhi kwa Madhumuni gani

Shahidi: Kuhifadhi sababu wewe Ndiyo Responsible na Utatoa Siku Vinavyohitajika

Wakili wa Serikali: Tarehe 13 August 2020, Unakumbuka Siku hiyo ulikuwa wapi

Shahidi: Nilikuwa katika Kituo Changu Cha kazi Katika Maabara Ya Uchunguzi wa Kisayansi

Wakili wa Serikali: Siku hiyo ulitekeleza Majukumu yapi

Shahidi: Nilikuwa Ofisa wa Zamu Mapokezi

Wakili wa Serikali: Ofisa wa Zamu Mapokezi Wapi?

Shahidi: Katika Ofisi yetu ya Cyber Crime

Wakili wa Serikali: Majukumu yako yalikuwa yapi

Shahidi: Kupokea Kazi zinazo kuja Kwa ajili ya Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Siku hiyo ulipokea Kazi Ipi

Shahidi: Moja ya Kazi niliyopokea ilikuwa ni Kutoka Katika Ofisi ya DCI

Wakili wa Serikali: Siku hiyo Ulipokea Kazi gani

Shahidi: Nilipokea Barua na Simu ambazo ambazo zilikuwa zipo Nane

Simu hizo ziliambatana na Barua

Wakili wa Serikali: Barua Ilikuwa ina kazi gani

Shahidi: Barua Ilikuwa inaomba Kufanya Uchunguzi katika Vile Vielelezo, Maombi yalikuwa sehemu Kuu tatu

  1. Sehemu ya Kwanza ilikuwa inaomba Kuangalia Mawasiliano Kupitia Mitandao ya Kijamii Kama Telegram, WhatsApp, Mawasiliano ya Jumbe za Simu, Mawasiliano ya Miamala ya Fedha, Mawasiliano ya Kupiga na Kupigiwa, Kati ya Vielelezo Vyote Nane against kwa namba za simu Kadhaa ambapo sikumbuki zilikuwaje 2. iliomba Usajili Wa Namba Tajwa, 3. Taatifa zingine zozote zitakazo saidia Katika Upelelezi

Wakili wa Serikali: Ukiwa kama Afisa Wa Zamu Baada ya Kupokea Ulifanya Nini

Shahidi: Kwanza Nilikagua Kwa Maana ya Kufanya Verification Kama Kile Kilichopo Kwenye Barua Lipo sawasawa

Wakili wa Serikali: Baada ya Hapo

Shahidi: Baada ya Verification na Kuona Vipo sahihi nilivisajili na Kuvipa Kumbukumbu namba ya Maabara ILIKUWA NO. FB/CYBER /2020/LAB/479

Wakili wa Serikali: Baada ya Usajili Kumalika Kitu gani Kilifuata

Shahidi: Ni lifungua Jalada, na Kwenda Kuhifadhi Katika Roka Langu

Wakili wa Serikali: Roka gani Shahidi Kila Mchunguzi ana Roka lake, Kwa hiyo Mimi peke yangu Ndiyo Nina Access na Roka. Langu

Shahidi: Kila Mchunguzi ana Roka lake, Kwa hiyo Mimi peke yangu Ndiyo Nina Access na Roka. Langu

Shahidi: Commanding Officer Wangu a lini assign Kufanya Ile kazi

Wakili wa Serikali: Nani alikuwa assigned

Shahidi: Mimi Assistant Inspector Innocent Ndowa

Wakili wa Serikali: Assistant Inspector Innocent Ndowa ni yupi

Shahidi: Ni Mimi hapa kabla Sijapanda Cheo ndiyo Nilikuwa naitwa Assistant Inspector

Wakili wa Serikali: Baada ya Kuvisajili

Shahidi: Nili hifadho Katika Roka Langu

Wakili wa Serikali: Kingine?

Shahidi: Sikufanya Lolote zaidi ya Kuhifadhi Mpaka Siku nafanyia Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Katika Kutekeleza Uchunguzi wa Vielelezo hivi Vitu gani Ulifanya. Je Maelekezo Ya Kupata KYC na Miamala ya Simu Ulifanyeje Kutekeleza?

Shahidi: Taarifa za KYC na Miamala hazipo Katika Himaya yangu niliwajibika Kuomba kutoka kwa Watoa Huduma

Wakili wa Serikali: Je, ni Watoa huduma wapi hao

Shahidi: Niliandika Barua kwenda Tigo pamoja na Airtel

Wakili wa Serikali: Kwa Watoa huduma uliomba nini na Nini Shahidi: Niliomba KYC Kwa Maana (KNOW YOUR CUSTOMER) na Miamala Ya simu

Shahidi: Nakumbuka Ilikuwa Tarehe 01 July 2021, NILIOMBA kwa kutumia namba ya Kesi. Nakumbuka CD IR /2027/ 2020

Wakili wa Serikali: Hiyo namba ni ya Kitu Gani

Shahidi: Namba ya Kesi Kutoka Kwa Mpelelezi

Wakili wa Serikali: Madhumuni ya ku Indicates hiyo namba ni nini

Shahidi: Ku verify Kuwa kweli Pana Jinai Kuhusiana na Kesi namba hiyo, Kwa Chochote kama atahitaji Na Yeye Kuhakiki

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama sasa ni lini Ulipata Majibu Kutoka kwa hao Watoa huduma Shahidi: Majibu nilipata Tarehe 02 July 2021

Wakili wa Serikali: Kitu Gani Kingine Sasa Ulifanya

Shahidi: Kwanza Nilitaka Kuthibitisha hicho, nikawa nimehifadhi

Wakili wa Serikali: Jambo Jingine ulilofanya.?

Shahidi_ Baada ya Kupata hizo Taarifa Nikaanza Kufanya Uchunguzi Wa Vile Vielelezo

Wakili wa Serikali: Vielelezo gani

Shahidi: ambazo zilikuwa Ni simu nane

Wakili wa Serikali: Ulifanya Uchunguzi Kwa Kufanya nini

Shahidi: Nilitoa Vielelezo Vyangu Kutoka Kwenye Roka, nikaweka Mark

Wakili wa Serikali: Eleza Jinsi Ulivyo weka Mark

Shahidi: zilikuja Zikiwa na Mark, lakini Bado nikazipa Alama za Kimaabara kwa kuzipa A Mpaka H Pembeni Nikazipa Maneno LAB 479

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine Kilifuata

Shahidi: Kwa Maana ya Identification nilizipa Mark Nikianza kwanza Kwa Kuandaa Vitendea Kazi Mashine Kama CELEBRITE

Wakili wa Serikali: Hiyo Mashine Uliyotumia ya CELEBRITE Ukitumia ina Namba gani

Shahidi: ilikuwa U face for PC 7:4:4 lakini namba Nyingine Sizikumbuki

Wakili wa Serikali: Version Ya Mwaka gani

Shahidi: Ya 2021

Wakili wa Serikali: Wakati Unafanya Uchunguzi Software Zilikuwa za Mwaka gani

Shahidi: Kwa ajili ya Kufanyia Uchunguzi ilikuwa ni 7:4:4 ya Mwaka 2021 na Kufanyia Extraction ni 7:4:0 WS: Umadhubuti Wa Vifaa hivyo ulikuwaje

Shahidi: Vifaa Vile vinatumia Genuine Windows, za LICENSED SOFTWARE kutoka Microsoft

Wakati Mwingine wa zoezi Zima tulikuwa tunafanya Updates…

Wakili wa Serikali: Mara ya Mwisho Kufanyia Updates ilikuwa ni lini

Shahidi: Kwa Upande wa CELEBRITE Ilikuwa NI Mwezi July

Wakili wa Serikali: Jambo Jingine?

Shahidi: tuna Install Mashine, Pia Vifaa hivi Vina Rights Broke Hakuna any internet Connection,

Wakili wa Serikali: Baada ya Hapo Shahidi: Unachukua Cable na Ile simu, Unaunganisha kwenye ile simu

Wakili wa Serikali: simu 8 ulizokuw nazo zilikuwa simu za aina gani

Shahidi: Tecno zilikuwa Nne, Itel zilikuwa Mbili, Samsung Ilikuwa Moja na Simu Moja inaitwa BUNDI

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Kila simu Ilkuwa Connected, Je kwenye Extraction ya kila simu ilikuwa Wapi

Shahidi: Kila simu Destination ilikuwa Kwemye Mashine (Computer)

Wakili wa Serikali: Hali ya Hizo Simu zilikuwaje

Shahidi: Kila simu Ilikuwa katika Flight Mode

Wakili wa Serikali: Fafanua Flight Mode Unamaanisha Nini

Shahidi: Ni Mode ambayo Simu haiwezi Kupata Communication

Wakili wa Serikali: Intergrity ya Vifaa ilikuwaje

Shahidi: inaposoma Hakuna Uwezo Kuongeza au Kupunguza Kufuatia Uwepo Right Broke

Wakili wa Serikali: Mashine yako ili Detect Kwa Kusema nini Shahidi Baadhi ya su ili Detect lakini baadhi ya Simu Ili Detect kupitia Sim Card, Na OS yake

Wakili wa Serikali: Shahidi Sasa Mpelelezi anataka Kubaini Mawasiliano, Kwenye analysis sasa Katika simu zote Nane analysis yako ili baini Kitu Gani

Shahidi: Katika analysis Simu ambazo zilikuwa na Majibu Positive tulibaini Simu Nne ambapo tulibaini kupitia Mitandao ya Kijamii

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kwamba Kwenye Process ya analysis ulibaini nini

Shahidi: Software Zote Zina fanya katika Same Technology

Wakili wa Serikali: Kwenye Baadhi ya Simu Ulipata nini

Shahidi: Mawasilisho ya Mitandao ya Kijamii Kama WhatsApp, Telegram, Facebook, Call Logs, call za social Network..

Wakili wa Serikali: Shahidi Sasa analysis ushakamilisha, Je Kitu Ulifanya?

Shahidi: Katika zile simu Nne Zenye Majibu, Nilienda Kwenye Reporting, unaweka Details na Baadae Nika print Taarifa

Wakili wa Serikali: Taarifa ya Simu Ngapi Shahidi Ya Simu Nne

Wakili wa Serikali: Baada ya Ku Print Ukafanya nini

Shahidi: Nilipata Muda wa Kuandaa Taarifa yangu ya findings zangu

Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni Lini

Shahidi: Ilikuwa ni Tarehe 09 July 2021

Wakili wa Serikali: Report Ilikuwa ni Kuhusu nini

Shahidi: Kuelezea Uchunguzi Niliofanya

Wakili wa Serikali: Baada ya kumaliza kuanda report ulifanya nini

Shahidi: Nikajiridhisha Kama zipo Sahihi, nikagonga Muhuri

Wakili wa Serikali: Muhuri gani

Shahidi: Wa Forensic Beaural, Tanzania, Dar es Salaam

Wakili wa Serikali: Je Vielelezo Vyenyewe Ikawaje

Shahidi: Baada ya Kukamilisha, Vile Vielelezo nikaviweka Seal ya Plastic Bag ambapo ilikuwa na Majina yangu, Tarehe na Sahihi na Kwenda Kuhifadhi Katika Roka Langu

Wakili wa Serikali: Ukasema Umehifadhi Kwenye Roka, Je Kwa Madhumuni gani

Shahidi: Kuhakiksha Vipo Salama na Kwa Ajili ya Usalama Wake Kuwa Hivi Ndiyo Nilivyo Viacha

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kwamba ni Lini sasa, Hiyo Taarifa ilichukuliwa

Shahidi: Tarehe 06 August 2021

Wakili wa Serikali: Ni nani uliye Mkabidhi

Shahidi: Anaitwa Inspector Swila

Wakili wa Serikali: Ulimkabidhi Vitu gani

Shahidi: Vielelezo Vyote Nane, Taarifa ya Vifaa Kwa Maana Simu Nne, Nilimkabidhi Taarifa yangu ya Findings

Nilimkabidhi Taarifa Nne kutoka kwenye zile Simu Nne Zenye Ushahidi Nilimkabidhi Taarifa kutoka kwa Watoa Huduma

Wakili wa Serikali: Baada ya Kumkabidhi Uliendelea na Jambo gani

Shahidi: Niliendelea na Mambo yangu Sababu nilikuwa Nimeshamaliza

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Hairisho, Sasa ni saa Saba Kasoro 4

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Inategemea Kabakisha Kiasi gani, ila amekuwa anarudia sana Maswali Mpaka Shahidi anamkumbusha Kama nilivyosema..

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Hairisho Bado sana

Jaji: Kwa Muda Gani

Wakili wa Serikali Pius Hilla: Naomba Hairisho la Lisaa Moja

Kibatala: Tulikubaliana na Wakili wake Kiongozi Dakika 45 sijui 1hr anatoa wapi

Jaji aandika Kidogo

Jaji: Dakika 45 zinatosha tutarudi hapa Saa Nane Kasorobo

Jaji anatoka…

Jaji amerudi Mahakamani

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa, Quorum ipo Kama awali

Kibatala: Mhe Jaji Kama utakumbuka Niliomba Wakili Nashon Nkungu atakapofika nitamtambulisha na Kwamba Anabadilishana na Wakili Mtobesya ambaye ameitwa na Rais wa TLS

Jaji: Shahidi nakukumbusha Bado Upo chini ya Kiapo

Wakili wa Serikali Robert Kidando: kwenye Ku access ile Mashine PALE LAB ikoje

Shahidi: Kila User ana akaunti Password za ku-log in kuweza Ku access

Wakili wa Serikali: Akaunti Zina nini

Shahidi: User name na Password

Wakili wa Serikali: Nani anaye Create Password

Shahidi: Unapokuwa Unaingia mara ya kwanza Ofisi Ina Utaratibu Wa Kutengeneza User akaunti Pale ambapo Mashine imenunuliwa

Wakili wa Serikali: Password Inatengenezwa na nani

Shahidi: Wewe Mwenyewe unayetumia ile Mashine

Wakili wa Serikali: USER name yako ni nani

Shahidi: Nina Reserve Sababu za Kiofisi

Wakili wa Serikali: Shahidi Tumeshaongea Vitu Vingi baada ya Kutengeneza Taarifa na attachments Kutoka Tigo na Airtel ina Vitu gani

Shahidi: Kwanza Itakuwa na Barua niliyo tumia Kuomba Taarifa, Itakuwa na Barua Kutoka Ofisi ya Uchunguzi Kwenda Tigo ambayo imesainiwa na Ofisa anaitwa NAFTALI JOSEPH kwa Niaba ya Kamishina, itakuwa na Kumbukumbu namba

Wakili wa Serikali: Ile Barua ya Kutoka Tigo inakuwa na Vitu gani

Shahidi: Inakuja Barua ina Nyaraka ya KYC na Miamala ya Fedha

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Taarifa hizo ziliwasilishwa Zikiwa na Kitu gani

Shahidi: Barua ambayo Imetoka Kampuni ya Tigo

Wakili wa Serikali: Report Kutoka Tigo ambayo Umeletewa, Unaweza Kuitambua Kwa Vipi

Shahidi: Kwanza Ina Nembo Kutoka Tigo, Muhuri umeandikwa MIC Tanzania

Wakili wa Serikali: Nyaraka ambayo imegongwa Muhuri Unakumbuka ni zipi

Shahidi: KYC na Miamala ya Fedha

Wakili wa Serikali: Report Kutoka Airtel Utaitambuaje

Wakili Dickson Matata: Mheshimiwa JAJI tunapata taabh sana, Tangu Asubuhi Hatusikii kabisa labda kwa sababu Shahidi amesogeleana na Wakili.

Jaji: Shahidi Jitahidi Kutoa Sauti

Shahidi: Kutoka Airtel Nilipokea KYC na Mihamala ya Fedha ya Namba Mbili

Wakili wa Serikali: Nyaraka hizi zinaambatana na nini

Shahidi: Barua ya Airtel

Wakili wa Serikali: Taarifa kutoka Airtel Ukiona Utaitambua Kwa lipi

Shahidi: Logo ya Airtel, Sahihi Imesainiwa na Gladdys Fimbari, na zile namba Ambazo nikiwa Nimeomba Kwenye Barua. Lakini pia Kwenye Attachments Kuna Mihuri pamoja na Logo

Wakili wa Serikali: Shahidi Kamata Nyaraka hii, Tizama Mwanzo Mpaka Mwisho

Shahidi….. Anakagua Makaratasi

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama sasa Nyaraka Uliyo nayo hivi sasa ni Kitu gani Shahidi: Ni KYC na Miamala ya Fedha, pamoja na Barua ya Uchunguzi

Wakili wa Serikali: Nyaraka hizo Unazikumbukaje

Shahidi: Kwanza Kuna namba ya Kesi Katika Barua hii

Wakili wa Serikali: Una Uhusiano gani nazo

Shahidi: Niliombea Taarifa Za Namba za Simu

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama sasa Nyaraka hizo Zina namba zipi

Shahidi: Ni 0784779944, 0782237913, 0787555200

Wakili wa Serikali: Namba hizo Ulizitumia Kuombea Vitu gani

Shahidi: Kuomba KYC pamoja na Miamala Ya Fedha

Wakili wa Serikali: Lwa Mujibu wa Taarifa Ya Airtel, KYC holder ni akina nani

Shahidi: Namba ya 0784779944 ina Usajili wa Jina la Kwanza FREEMAN na Jina la Kati ni AIKAEL na Jina la Mwisho ni MBOWE

Wakili wa Serikali: Shahidi namba ya Pili KYC yake ina taarifa zipi

Shahidi: KYC ilikuwa ya Namba 0782237913 Ambayo ilikuwa na Usajili Jina la Kwanza ni KHALFANI Jina la Kati ni BWIRE na Jina LA Mwisho ni HASSAN

Wakili wa Serikali: KYC inayofuata

Shahidi: Ni ya namba 0797555200 ambayo ilikuwa na Jina LA Kwanza DENIS Jina la Kati LEO na Jina la Mwisho ni URIO

Wakili wa Serikali: Ulisema Taarifa Ya Airtel Ilikuwa ina Miamala, Ieleze Mahakama Miamala Ilikuwa ya Namna gani

Shahidi: Ilikuwa ni Miamala kuanzia 01 June 2020 Mpaka 31 July 2020

Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa ile Barua Walitaka Kujua au Kupata kitu gani

Shahidi: Walitaka Kujua Miamala ya Namba za Simu

Wakili wa Serikali: Wewe Ulibaini nini

Shahidi: Nilisaini Kuna Baadhi ya Namba Ambazo zilikuwa zimeainishwa na Mpelelezi Zilikuwa na Miamala, Zimefanya Miamala (Transactions)

Wakili wa Serikali: Kama utakumbuka Elezea Mahakamani ni Nmab zipi au Mihamala ipi Uliyo baini

Shahidi: Kuna Muhamala wa Tarehe 31 July 2020 ambao Ulitoka Kwenye 0784779944 kwenda namba 0782237913

Wakili wa Serikali: Huo ulikuwa Muamala Wa Pesa Kiasi gani

Shahidi: TSh Elfu Themanini Wakili wa Serikali: Ulikuwa Unaenda Kwenye namba ipi

Shahidi: 0782237913

Wakili JOHN MALLYA: Mheshimiwa Jaji Kama Shahidi anasoma namba Kwa Vielelezo ambavyo Vipo Mahakamani Tunaomba asome kwa usahihi..

Wakili wa Serikali: Sema kutoka lnamba ipi kwenda Ipi

Shahidi: Kutoka 784779944 kwenda 782237944

Wakili wa Serikali: Namba hizo Zina Uhusiano gani na zile walizo Omba Wapelelezi

Shahidi: Ni namba Walizoomba Wapelelezi

Wakili wa Serikali: Je, Kuna Mihamaa Mingine?

Shahidi: Upo Tarehe 20 July 2020 Mumala Kutoka Namba ya Simu 780900174 kwenda 787555200

Wakili wa Serikali: Muamala Wa Pesa Kiasi gani

Shahidi: TSh 500,000 WS anaenda Kuteta Jambo na Jopo la Mawakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: Dakika Moja Mheshimiwa Jaji Jaji anaitikia kwa kichwa.

Wakili wa Serikali: Baada ya Kupokea hizi Taarifa za Airtel unasema Ulifanya nini

Shahidi: Nili report kwenye Taarifa Yangu

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba p6

Wakili wa Serikali: Shahidi Kwa Ujumla Hizo Nyaraka Ni Kitu gani

Shahidi: Ni Taarifa za KYC kutoka Kampuni ya Tigo

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kimekutambulisha Kuwa hiyo ni Taarifa kutoka Tigo

Shahidi: Barua ina Nembo Kutoka Kampuni ya Tigo, Ina Muhuri, Sahihi ya Mwanasheria

Wakili wa Serikali: Ni zile za miamala pia

Shahidi: Na zenyewe Zina Muhuri Wa MIC Tanzania

Wakili wa Serikali: Nyaraka ya KYC inahusiana na namba zipi

Shahidi: Ina husiana na 0719933386

Wakili wa Serikali: Na kwa Mujibu wa KYC Namba hiyo inamuhusu Usajili wa nani

Shahidi: Unahusu Jina la Kwanza FREEMAN Middle namba AIKAEL na Last name MBOWE

Wakili wa Serikali: Kwenye Miamala Ulifanya Ukabiani ni Namba ipi

Shahidi: Nilbaini Muamala Wa Kiasi cha TSh Laki 5, Tarehe 20 July 2020

Shahidi: Muamala Unatoka namba % 255719933386 WS: Kwenda namba ipi

Shahidi: Namba 255787555200

Wakili wa Serikali: Na Kwamba Sasa Shahidi, Hiyo Nyaraka ya Miamala Ilikuwa ya Kipindi Gani

Shahidi: alikuwa Mihamala ya Fedha Kuanzia 01 June 2020 Mpaka 31 July 2020

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Sasa Kwenye report yako Mbali na Taarifa za Tigo na Airtel Uliambatanisha Kitu gani

Shahidi: Niliambatanisha report Kutoka simu zile Nne Zenye Matokeo

Wakili wa Serikali: Simu hizo ni zipi

Shahidi: Tecno Tatu na Itel

SHAHIDI ana nyoosha mkono wake Juu anasema “SAMAHANI MHESHIMIWA JAJI, KICHWA KINANIGONGA NASHINDWA KUONGEA KWA SAUTI”

Jaji: Wakupe Maji?

Jaji: au uondoe kitambaa usoni (Barakoa)

Shahidi: Hapana sababu ya kiafya ibakie tu

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba tuwasiliane Maana Shahidi Ndiyo Kaibua Concern Hapa

Jaji: Mmewasiliana naye?

Wakili wa Serikali: Hapana

Jaji: Wasiliana naye

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi ananiambia Kichwa Kinamgonga sana na hayupo Kwenye Position ya Kuendelea na Ushahidi

Jaji: Unaposema Kichwa Kinamgonga Maana yake Kinamuuma, si Ndiyo?

Wakili wa Serikali: Ndiyo

Kibatala: Mheshimiwa Jaji, inategemea suala la Shahidi mwenyewe, kama tunaweza Ku’ Break kidogo ni sawa, lakini kuhairisha ni Jambo la mwisho kabisaaaaaa

Jaji: Wasiliana naye Kama anaweza kuendelea Kidogo, Tu’ break Kwa muda aje tuendelee

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Samahani Nilipoongea naye kasema Hayupo Kwenye Position ya Kuendelea Ila Sisi Kama Wenye Kesi Shahidi akisema anaumwa tunaona akiendelea anaweza Kutoa Ushahidi Wa Vitu visivyo..

Jaji: Haya Inspector Unasemaje

Shahidi: Mheshimiwa Jaji nimekuja Asubuhi Kichwa kikiwa kinanigonga, ila kadiri Muda Unapoendelea Kinauma zaidi ndiyo Maana Unaona Sauti Ipo Chini..

Jaji: Nafikiri tumpe Benefits of Doubt

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Wakati Shahidi akiendelea Kutoa Ushahidi Wake Mahakamani, Yeye Mwenyewe Ame raise Concerns Kuhusiana na Afya yake, Tumewasiliana naye Mheshimiwa Jaji na ametueleza Kuwa Kichwa kinamuuma.

Na Kwamba Kwa Jinsi anavyojisikia hayupo Kwenye nafasi ya Kuendelea Kutoa Ushahidi Kwa sasa.. Mheshimiwa Jaji ni Utaratibu kwamba ili Shahidi aendelee Kutoa Ushahidi anapaswa awe Sawa Ki Afya, na Kwakuwa Shahidi ameeleza Kichwa Kinauma na Kwakuwa amesema hayupo Kwenye nafasi ya Kuendelea Kutoa Ushahidi Kwa sasa ni Busara tuhairishe ili Shahidi aweze Kupata Medical attention ili aweze Kupata Matibabu Nachelea Kusema turudi lini sababu sijui atakuwa Sawa KiAfya Sawa lini..

Jaji: Tunaye Askofu Mahakamani baada ya hapa atamfanyia maombi na mimi nitakuombea shahidi Ili kesho shahidi uweze kuwa Mahakamani…

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwakuwa Shahidi amewasiliana na Mahakama Mwenyewe sisi hatuna Shida na hilo lakini Premises za kuhairisha ndiyo sijafahamu..

Mimi nafikiri Tuhairishe mpaka Kesho, MUDA ambao Mahakama Itapanga na Kama atakuwa bado sheria ya ushahidi inaruhusu kufanya

Deferment ya ushahidi wake, tuendelee na shahidi mwingine, alipo atakuja kuendelea Na shahidi mwingine

Jaji: Sijui kwanini nahisi kesho atakwepo (Shahidi) Mahakamani

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa tutafanya hivyo Ingawa hatuombei hivyo, Ikitokea imeshindikana tutatafuta shahidi mwingine

Jaji anaandika Kidogo kwenye makbrasha yake..

Jaji: tunahairisha shauri kama ambavyo mashtaka wameomba na Mahakama ika observe. Tunahairisha mpaka kesho Saa 3 Asubuhi Upande wa Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Upande wa Jamhuri kama Itashindikana mtatakiwa mlete shahidi mwingine

Jaji anatoka

Like
1