Kesi ya Mbowe: Mahakama yatupilia mbali vielelezo vya mashitaka

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia, BJ, leo 10.01.2022

KESI namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling’wenya  Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: : : Mheshimiwa Jaji Upande wa Jamhuri tupo Kama tulivyo kuwa awali

Jaji baada ya Kukubaliana Pande zote Mbili Tumekubaliana Kuhairisha Shauri hili Mpaka Tarehe 10 January

NDIPO TULIPO ISHIA TAREHE 20 DECEMBER 2021

Nyimbo za Chadema zinaimbwa

Chadema Chadema Chadema, Tanzania Tanzania People’s Power

Jaji ameingia Mahakamani Muda huu Saa 4 kamili

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: : : Mheshimiwa Jaji naomba kuwatambulisha

Pius Hilla

Abdallah Chavula

Jenitreza Kitali

Nassoro Katuga

Esther Martin

Ignasi Mwinuka

Tulimanywa Majige

Wakili Peter Kibatala: : Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala.

Naomba kuwatambulisha

Nashon Nkungu

John Malya

Dickson Matata

Seleman Matauka

Sisty Aloyce

Faraji Mangula

Michael Mwangasa

Gaston Garubindi

Maria Mushi

Jaji anaita washitakiwa wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: : : Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Uamuzi Mdogo, Tupo tayari Kuendelea

Wakili Peter Kibatala: : nasi pia tupo tayari Kupokea Uamuzi na Kuendelea

Anainama

Jaji anainama na Kuandika Kidogo

Mahakama ipo kimya.

Jaji: Ni kweli Shauri hili. Lina kuja kwa ajili ya Uamuzi Mdogo

Kama ambavyo Mahakama Ilihairisha Mwaka Jana

Uamuzi huu Unatokana na kupigwa kwa kupokelewa vielelezo ambavyo vilikuwa vimetolewa na ASP Jumanne

Na Kwamba aliomba Kutoa Vielelezo baada ya Kufanya Upekuzi na Kwamba Upekuzi huo Ulifanyika Mbele ya Mwenye Nyumba Mariam Juma na Mjumbe wa Nyumba kumi pamoja na Mke wa Mshtakiwa

[Na Kwamba alijaza Certificate of Seizure Kwa mlolomgo wa mali ambazo alizo kamata kama ambavyo nimeziorodhesha

Na Kwamba Baada ya Kufanya Upekuzi huo alizo weka alama  X/ HD

Na baadaa akamkabidhi Mtunza Vielelezo Kituo cha Polisi Kati

Na Kwamba alivichukua na Kwenda Kutunza Ofisi ya Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam Tarehe 17 December 2021

Notebook Nyekundu hakutoa Hapa Mahakamani, na Kwamba Baada ya yeye Kupitia na Kugundua haina Uhusiano na Kesi hii alicha Kuitoa hapa Mahakamani

Na alikuwa anavitaja Vielelezo Kwa Kutumia Alama ya X/HD

Alipokuwa anavitoa hapa Mahakamani alipingwa na Mawakili wa Utetezi

Wote Walipinga Vielelezo Vyote vilivyokiwa vinaombwa Kutolewa hapa Mahakamani

Hata hivyo Kila Wakili akisimama na Kutoa Hoja zake

Kwa Maana hiyo Mahakama haitaenda kwa Kila Wakili Bali kwa Hoja Moja moja

 Mapingamizi haya yalijikita Maeneo Mawili:

  1. Chain of Custody
  2. Competence ya Vielelezo Vyenyewe na Shahidi aliyekuwa anaomba Kutoa Mahakamani

Si Jambo Jipya hapa Mahakamani

Mahakama hii kwa kutumia Experience ya huko Nyuma

Sheria Inaelezea Kwamba Upokelewaji wa Vielelezo Mahakamani Kupitia Sheria Kesi ya SHARIF MOHAMMED ATHUMAN AND SIX OTHER, CHARLES GAZILABO AND THE OTHER THREE,

Katika Mashauri yote Mawili Mahakama imeeleza Kwamba Vielelezo Inaweza Kupokelewa Baada ya Vitu Vitatu

Kutumia Criteria ya Competence, Mahakama ili eleza Kuwa test ipo katika Mambo Matatu ya naitwa Authentication

Lazima atambue unique features

Unique features ya Kielelezo hicho

Atambue Chain of Custody

 Kwa Maana hiyo Mapingamizi yaliyoletwa yameltwa kwa Jambo Moja la Competence

Mhakama Ita adopt namna ambavyo Mapingamizi yameletwa kwa Chain of Custody na Competence

Ishu ya Chain of Custody imeelezwa na Mawakili Wote wa Utetezi

Nitaamua kwa Kufuata Ishu kama ambavyo zime letwa na Mawakili Wa Utetezi

Maelezo ya jumla yanaeleza Chain of Custody ni nini.? Na Wakili Nashon Nkungu: Alieleza nini Maana ya Chain Of Custody

Mahakama ina kubaliana kwamba ni namna ambavyo kielelezo kilikamatwa na kikitunzwa wapi kam ambapo kilikuwa mahakamani

Kielelezo Ambacho Kilikuwa kimelengwa Kuletwa hapa Mahakamani Kilichezewa na Kwamba hii inaonyesha kwamba Vielelezo Vilikuwa Pamoja ndiyo Maana Notebook Nyekundu Imetolewa

Kwa Upande wa Utetezi walikuja na Hoja Kadhaa

Kwa Mujibu wa Sheria Vielelezo ambavyo vimekamatwa kwamba vielelezo ambavyov imekuwa Commited vinatakiwa  kuja vyote Mahakama Kuu

Kwa sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200 inataka afisa wa polisi ambaye anataka kutoa kielelezo mahakamani anatakiwa anarudishe kwa amtu aliyepata kwake

Inaonyesha kuwa shahidi Namba nane hakutoa Hoja zake kwanini Kielelezo Hicho Hakikuletwa Mahakamani

Kama hajarudisha inaonyesha kielelezo hicho kimechezewa

Waliendelea kuikimbusha mahakama kwamba PGO 229  Afisa wa Polisi anatakiwa kushika kielelezo hicho mpaka atakapo kitoa mahakamani

Na kwamba wakati anakamatwa aliamini kina husika ndiyo maana alikikamata, hivyo sisSawa kutokutoa hapa mahakamani

Wakili Malya: alisema Kwamba haieleweki Huenda Kwamba Kielelezo hicho Kilikuwa kinamnufaisha Mashitakiwa namba Moja

Kwa hoja wakasema kwamba \wanaomba mahakama ione kwamba kielelezo kimechezewa

Kwa sababu Vielelezo hivi Vingine vilikamatwa na notebook nyekundu basi mahakama ione kuwa vielelezo hivyo vimechezewa.

Kwa Upande wa Mawakili Wa Mashitaka Walisema Kwamba Mawakili Wa Utetezi wametafsiri vibaya

Kwamba upande wa mashitaka awalazimishwi kutoa vielelezo vyote mbele ya mahakama

Shahidi aliona kwamba kielelezo hicho hakihusiki hapa mahakamani

Kwa maelezo hayo waliendelea kusema kielelezo kipokelewe mahakamani kama ambavyo Vilikamatwa

Sasa hapa mahakamani, mahakama ni kweli inaona kwamba kielelezo hicho hakikutolewa hapa mahakamani.

Kutokana na shahidi namba 8 alisema kwamba hakutoa kielelezo hicho hapa mahakamani kwa sababu aliona kwamba haihusiani na kesi hapa mahakamani.

Kwa upande wa utetezi, wanamaoni kuwa vielelezo vyote ambavyo vimekuwa commited vinatakiwa kuja mbele ya Mahakama Kuu na kama siyo basi mchakato wa kurudisha kielelezo hicho ulipaswa uwe umefuatwa.

Kwa namna hiyo, waliomba mahakama ikatae vielelezo vyote.

Ukisoma pande zote mbili, ni wazi kuwa kielelezo hiki kwa kutolewa kwake kimekiuka sheria ukizingatia kuwa kilikuwa tayari imekuwa commited.

Hakuna sheria inayosema kwamba kila kielelezo ambacho kimekuwa commited kinatakiwa lazima kiletwa mahakamani

Kifungu cha 246 CPA na kanuni ya 8 ya mwaka 2016 inasema kuwa vielelezo vyote ambavyo vimekuwa commited kutoka kwenye a Mahakama ya Hakimu Mkazi ni vile ambavyo Mkurugenzi wa mashitaka atataka kuvitumia

Ni wazi atakuwa amepitia kielelezo hicho kuona kama kinatemgeeza kesi au akitengenezi kesi

Siyo lazima kwa ushahidi au shahidi ambao umekuwa commited anatakiwa lazima aje kutoa ushahidi mahakamani

Kama Kifungu cha 110 na 114 cha CPA pamoja na sheria ya ushahidi kifungu cha 1,3 na 4 katika mazingira hayo basi Mahakama Inaona kwamba Pingamizi hili limekosewa

Mahakama inaona pingamizi hili halina msingi na kutupilia mbali.

Kuhusiana na chain of custody imeelezwa kwamba kielelezo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine mahakama lazima itazame sana

Endapo mnyororo wa kielelezo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine Inapokuwa umevunjika basi upande wa mashitaka wanakuwa wamekuwa wameshindwa

(c)

Hakuna maelezo yaliyotolewa na shahidi namba 8 kwamba aliwezake kutoa kielelezo hicho kutoka kwa Sargeant Johnson. PGO Hiyo inasema kwamba funguo ya chumba cha vielelezo inatakiwa itajwe ni nani alikuwa anatunza

Kwa kushindwa kueleza hilo wa naona kwamba chain of custody imevunjika

Bwana kidando nayeye alitoa maelezo yake kwamba pingamizi hili limekosa substance kwamba PGO ya 229 4(a) inavyotakiwa

Kidando alieleza namna ambavyo shahidi namba 08 aliviepeleka kwa Sarjent Johnson na kwenda kuchukua tarehe 17 December 2021 na kwamba shahidi ajahojiwa kuona ambavyo ushahidi wake unavyotetereka

Akaendelea kusema kwa kina kuwa shahidi alieleza kwa kina namna ambavyo alitunza kielelezo hicho hapa mahakamani

Akaomba mahakama Itumie sheria kesi ya IGNATUS MKOKA

Kesi namba 245 ya mwaka 2013

Pia akaomba Mahakama Itumie sheria kesi ya KENNEDY SHAYO 84 ya 2017 ukurasa wa 31 na 34

Na akaendelea kusema kwamba Shahidi anaeleza mahakama vile vielelezo ambayo alivi kamata na kuvitunza kwa sarjent Johnson

Upande wa utetezi walisema kwamba utunzaji wa vielelezo katika sheria Imetungwa kulinda vielelezo visichezewe

Na kwamba sheria inasema kwamba polisi anatakiwa  kuwa na notebook namna ambavyo alikuwa anaviorodhesha

Na kwamba shahidi hakuonyesha paper trade na vithibitisho vya paper havikuonyeshw akama ambavyo inatakiwa

Wakaomba kutumia kesi ya ILUMINATUS MKOKA pamoja na kesi ya MAYALA MBITI 177 ya 2015.

Kuhusiana na kesi ya KENNEDY SHAYO wakaomba kwamba kesi hiyo I inaunga mkono hoja za utetezi, kwa sababu Bunge liliona kuwa kielelezo ambacho ni nguo kina what za kuchezewa na kwamba mnyororo huo unakuwa umevunjika

Na kuhusiana kupokelewe kwa vielelezo hivyo kuwa vitaathiri washtakiwa au lah

Walisema kuwa bunge kinapotunga sheria na sheria hiyo inapokuwa haifuatwi basi washtakiwa wanakuwa wameathirika

Kwenye suala hili ni seme ni kweli kwamba suala la upokelewaji wa vielelezo limeelezwa

Na suala zima la upokelewaji wa vielelezo Inategemea ambavyo vielelezo vimetunzwa

Na chronological paper trade inaonyesha namna ambavyo kielelezo kilikuwa kimekamatwa mpaka kutunzwa

Suala zima la upokelewaji wa vielelezo na chain of custody limeelezwa na sheria kwa kifungu cha 38 cha CPA, sura ya 322, sheria ya polisi na polisi wasaidizi, PGO ya 229

Suala la kufuatwa kwa mnyororo wa kielelezo kuna vipingili vingi.

Unapokuwa unaangalia kipingili kimoja likiwa kimekatika kimoja basi mnyororo huo unakuwa umekatika

Katika kushughulika na vielelezo hivyo kuwa vipo namba ambavyo vimakatwa mpaka vinagika mahakamani.

Siyo sahihi shahidi mmoja tuh anapotoka ushahidi kueleza kwa niaba ya wengine kuhusiana na mnyororo kuvunjia au kutovunjika

Kwenye kesi ya CHARLES GAZILABO, mahakama ilitoa uamuzi kwamba Mahakama ya Rufani inaamini uthibishwaji wa utunzaji wa mnyororo hauwezi kuthibitishwa na shahidi mmoja, kwamba mahakama Itaweza kuona baada ya ushahidi wote kutolewa.

Katika kesi ya CHRISTINA Vs JAMHURI, ukurasa wa 5 na 7 kufuatia mfano huu Mahakama Ya Rufani inasisitiza kuwa kama hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwamba mnyororo ulichezewa

 Na kwamba kama upande wa Jamhuri hawatoleta mashahidi wengine kuthibitisha mnyororo huo basi mahakama inaweza kusema mnyororo huo haujathibitishw kwenye kesi ya ABASI KONDO Vs JAMHURI kesi 472 ya 2017

Pia Mahakama Ya Rufani imetoa malekezo kwemye kesi ya ANANIA  Vs JAMHURI mahakama Iliyoketi Dar es Salaam

Hizo authorities nilizo sema hapo juu ni authorities ambazo zimetolewa na Mahakama Ya Rufani

Kwa maana hiyo mahakama ya chini inapotoa maamuzi lazima izingatie maamuzi hayo ya juu

Katika mazingira hayo basi kwa kutizama shahidi ambaye amekuja kutoa ushahidi hapa mahakamani kwamba vielelezo ambavyo alivikamata hakubaki navyo bali alimkabidhi sarjent Johnson

Kwakuwa bado upande wa jamhuri awajashindwa kumuita sarjent johnson ajaitwa mahakamani kutoa ushahidi at uwezi kusema kuwa shahidi aliyepo mahakamani ameshindwa kutoa mnyororo wa ushahidi

Kuhusiana na mwaliko niliopata kutumia kesi ya MKOKA NA MAYALA MBITI nakubalina na upande wa utetezi kuwa kanuni zilizotumika katika mashauri hayo ni mzuri lakini ikumbukwe maamuzi hayo yalifanyika baada ya ushahidi huo kutolewa

Naona hoja za utetezi zimeletwa kabla ya wakati labda kama ingeletwa wakati wa final submission

Kwa sababu hiyo mahakama hsiwezi kuzingatia na kwa sababu hiyo pingamizi hili nalitupilia mbali

Ikumbukwe pia shahidi aliyopo mahakamani, yeye ndiye aliye fanya search na alizikamata

Hoja za kwamba shahidi amethibitisha kwamba mali ambazo zinatolewa mahakamani ni mali ya JWTZ wakati hakuna mahala aliyothibitisha kuwa vielelezo hivyo ni mali ya JWTZ na pia hakuna mahali ambapo JWTZ walikuja kuthibitisha kuwa ni mali yao

Aliendelea kusema wakili JOHN Malya: kuwa shahidi alishindwa kutaka vizuri hapa mahakamani, ikumbukwe ni vifaa vya kijeshi na vina majina yake ya kijeshi

Akatoa mfano kuwa shahidi amesema kuwa kielelezo ni PONJOL wakati ni sleeping bag

Akaendelea kuomba mahakama kwamba shahidi ameshindwa kuvitambua vielelezo hivyo

Na kwamba vielelezo ambavyo vilikuwa vinatolewa hakuna sleeping bag na akaomba kwa kusema shahidi hana knowledge ya kutosha

Shahidi alisema vielelezo ni mali ya JWTZ na JKT wakati shahidi hajawahi kufanya kazi JKT wala JWTZ

Kwa sababu vielelezo hivyo ni vya jeshi na shahidi hana knowledge basi mahakama isipokee vielelezo hivyo kwa sababu shahidi siyo competent

Kwa upande  wa mashitaka walikuja kusema kwamba likuka kutoa ushahidi wa kile ambacho alikikamata

Na kwamba kwa hatua ya sasa siyo sawa kutoa ushahidi wa kitaalamu

Shahidi alieleza kwa kina kuwa aliweka alama hiyo baada ya kuvikamata

Aliomba Mahakama ione kwamba shahidi huyo ameweza kutambua vielelezo hiyo

Mr Malya: hajaonyesha pia kuwa yeye alivitambua je hapa mahakamani

Kwa sasa mahakama inatazama kama vinaweza kupokelewa na siyo kuthibitisha kuwa ni mali ya jeshi au siyo mali ya jeshi

Wakasema kuwa imeelezwa kwenye kesi ya Jamuhuri Vs CHARLES GAZILABO

Kwamba mahakama ishughulike na kuvipokea

Kuhusu alama aliyo weka aliomba kusema kwamba mahakama ione kuwa vielelezo hivyo vilishughulikiwa vizuri

Katika rejoinder walieleza upande wa utetezi ni kwamba kwakuwa shahidi alitaja kwa majina vielelezo hivyo basi alionyesha kuwa anavitambua

Upande wa mashitaka wanasema kwamba swala la utalaam siyo suala la sasa

Maelezo ambayo yameletwa pande zote mbili kuwa kukosekana kwa uelewa kuhusu vielelezo hivyo inatosha kum disqualifie

Katika kesi ya SHARIF MOHAMMED ATHUMAN AND SIX OTHER VS DPP I asema kwamba katika ushahidi kuna identification ikifanyika inatosha

Utambuzi kwa kuangalia features pekeee

Utambuzi kwa kuangalia unique futures

Kwa alama ambayo shahidi maeiweka yeye mwenyewe, ambayo nimeweka hapo juu kuwa kielelezo kinaweza kutambuliwa kwa unique features

Lakini features ambayo ni  X/HD ilikuwa inatosha

Features ambayo ni mabaka inapatikana katika vielelezo vyote

Nafahamu maelezo ambayo ya inasema kuwa features X /HD siyo features ya kisheria

Mahakama inaona hoja hii itashughulika nayo katika hoja inayofuata

Hoja ya utaalamu tuta shughulika nayo baadae siyo kwa sasa

Hoja ya kidaftari cha five star, kuhusu kikaratasi ambacho kilikuwa ndani yake,

Kuwa hakikufuata mchakato wa sheria juu ya kuongeza kielelezo

Upande wa mashitaka awajafuata utaratibu wa kisheria kutumia kifungu cha 289 cha CPA sura ya 20 juu ya kutaarifu mahakama katika kuingiza kielelezo ambacho halikuwa commited

Vielelezo ambavyo havikuwa commited katika trial court

Kidando wakati anajibu alieleza mahakama kuwa swala zima la commital limeelezwa katika kanuni ya 8(2) ya 2019 GN ya 277

Katika Ukurasa wa 32,33 wa commital proceedings, inaonyesha kuwa ilisha tajwa

Katika hali hiyo waliomba mahakama ipokee kielelezo hicho

Katika hali hiyo waliomba mahakama ipokee kielelezo hicho

Katika Kesi ya RONJINO walisema Kwamba Hai hausiki na urodheshwaji wa vielelezo

Wakaomba mahakama kuwa katika certificate of seizure kuna vingine vimetwajwa

Upande wa utetezi wakasema kuwa kielelezo ambacho kinatajwa hakikupokelewa

Kwa kuangalia kwa ujumla naona kuwa ni kweli

Vielelezo vinavyolengwa kutolewa hapa mahakamani havikutolewa hapa mahakamani haviku orodheshwa wakati wa commital

Kifungu cha 246 linataka kuwa kielelezo au ushahidi wowote unapotakiwa kupokelewa mahakamani unatakiwa uwe umekuwa commited mahakamani

Nikisona Kanuni ya 8 (2) ya mahakama hii inataka mahakama hii kusoma maelezo kwa lugha wanayo ufahamu, kusoma ushahidi wanaoshtakiwa nao, nyaraka za ushahidi unalotarajiwa kutolewa mbele ya mahakama

Kinachotakiwa kufanywa na mahakama husika ni kusoma mashitaka, kusoma ushahidi lakini pia kusoma nyaraka zinzo contain substance ya ushahidi unapotakiwa kusomwa mahakamani

Kinachotakiwa kufanywa ni kungaliwa kama ni kweli kilisomwa.?

Hayo ndiyo masharti ambayo yapo kifungu 289 (1) hakuna shahidi atakaye itwa kama ushahidi wake haukusomwa wakati wa commital, shahidi ataitwa endapo kama ushahidi wake ulisomwa na ushahidi huo ulienda upande wa mashitaka

Katika haki hiyo basi kumbe kinachomatazwa ni shahidi kuitwa bila kutolewa notisi upande wa utetezi, kama kuna nia ya kumuita shahidi huyo na mahakama ita angalia notisi hiyo ni toahelezi au siyo toahelezi

Hakuna takwa la kisheria kuwa kuna takwa la kuleta kielelezo ambacho

Ni physical.

Kwa maelezo hayo naona hakuna sheria ambayo imevunjwa

Na upande wa utetezi waliomba kwamba ili kusudi tukubali au kupokea kielelezo chochote lazima pawe na sheria inayokataza

Kama hakuna sheria wala sheria kesi mahakama hii itakuwa inafanya makosa kukataa kielelezo

Vielelezo vyote ambavyo vinalengwa kutumika hapa mahakamani, hakuna sheria ambayo imevunjwa

Kwa upande wa mashitaka hawalazimishwi kusoma kielelezo ambacho ni physical

Na sheria ambayo zimeorodheshwa hazikatazi

Kwa maana hiyo naitupilia mbali hoja hii

Lakini pia Suala la Mr. Malya: aliomba mahakama kuwa kidaftari ambacho kilikuwa commited siyo kilicho letwa hapa mahakamani

Mahakama imeona kilikuwa commited na kiliorodheshwa na karatasi zimo ambazo zinamichoro michoro

Kwa Hoja hiyo ya Malya: Pia siyo ya Msingi

Mr Malya: ni kama alitaka ku impeachment kumbukumbu za mahakama, na mahakama inaona hoja aliyoleta haina msingi

Katika mazingira hayo basi mahakama hii imeona hoja yake haina msingi

Kuhusiana na kibali cha kufanya seizure of certificate kwamba baada ya kukamata vielelezo hivyo vitakiwa kupelekwa kwa hakimu

Kesi ya NESTORY Vs Maryland Jaji Masabo alisema kuwa pale ambapo kuna hoja ya kutaka kuwa na wasiwasi na kumbukumbu za mahakama ushahidi unatakiwa kuwa wakutosha

Hoja za kupinga za Bwana Kidando PGO 226 (2)c kwamba afisa wa upelelezi alikuwa anahusika na kukamata na kuhifadhi

Kesi ya Mbowe Vs DPP  ya 420/2018 Mahakama ya Rufani ilisema kwamba kutokutolewa Kwa Taarifa kwa  Hakimu  haizuii Ushahidi Kupokelewa

Utetezi Wao walisema kwamba hakuna ushahidi kwamba vielelezo vilienda kuthibitishwa kwa hakimu

Mahakama ione kuwa kutofuatwa kwa utaratibu wa kuvalidate search

Kuhusiana na Kesi ya Mbowe Waliomba mahakama ione kuwa kesi hiyo siyo relevant

Nakubalina na utetezi kuwa search inatakiwa kuwa validated na hakimu kama ambavyo PGO 226 (2)c   na kifungu cha 38 (2) kwamba kama hukupata kibali cha search basi unatakiwa kupeleka vielelezo kwa hakimu kwa ajili ya ku validate

Nakubalina  na utetezi kuwa kesi ya Mbowe ni distinguishable

Nakubakina  kuwa hakimu anatakiwa kutoa kibali cha ku validate search

VUYO Vs DPP ya 334 ya 2016

Lakini ikumbukwe kuwa kesi hiyo ilielekeza kuwa ipo kesi nyingine

Kutokana na maamuzi hayo ya Mahakama ya Rufani kuwa siyo automatic kuwa kielelezo hicho kisipokelewe mahakamani

Bali kitaangaliwa kuwa kielelezo hicho kupokelewa kwake kuna muathiri mshitakiwa

Ndipo inapoweza kuoekana kuwa kutofuatwa kwa kifungu hicho kumeathiri mshitakiwa

Katika mazingira hayo mahakama inaona pia pingamizi hilo halina msingi

Katika hoja nyingine ya vielelezo ambavyo vinalengwa kutolewa mahakamani vinatakiwa kuwa lebeled kwa kufuata sheria na mahakama iliombwa kungalia PGO 229 (10) inaeleza namna ya kuweka alama katika nguo kama lebel ya kielelezo

Na Lebel ya X / HD siyo moja ya lebel ambayo inatajwa katika sheria

Imeelezwa kuwa kilicho fanyika siyo lebeling bali ni kuharibu kielelezo

Kanuni zinasisitiza kuwa alama inayowekwa ni kwa ajili ya kutofautisha

Ikumbukwe kuwa jambo hili limefanyika bila kuwepo kwa mashahidi wakiokwepo

Kukiuka masharti ya PGO hii ni kukiuka sheria hii

Kwenye hoja hii wakili wa serikali alisema kuwa vielelezo ambavyo vinalengwa kutolewa hapa mahakamani, zilikuwa lebeled na kumsaidia shahidi kukumbuka vielelezo hivyo

Na wakaomba kuwa hoja hii haina msingi na mahakama itupilie mbali

Kwamba vielelezo ambavyo vinatolewa hapa mahakamani lebeling ilikuwa sahihi

Katika mazingira hayo mahakama imeelekezwa katika PGO 229 (8) kwamba askari anatakiwa kuweka lebel katika ushahidi unaingia katika mikono yake

Eneo la ku lebel limeelezwa vizuri

Katika PGO hii imelekeza vielelezo ambavyo ni nguo vinatakiwa kuwa lebeled, mahakama imeelezwa kuwa inatakiwa akuwekwa lebel kwa kamba ambayo itapita katika vishikizo na ining’inie

Na exhibit ambayo inatakiwa kulebel inatakiwa kuwa paper pin

PGO 229 (8) I eleza kuwa lebel hiyo inatakiwa kuwa ni minor number, na vingine

Kutokana na malekezo hayo ya kisheria yakiyoelezwa katika PGO hiyo ni wazi kuwa alama iliyiwekwa siyo alama ambayo PGO 229 Imeitambua na kuelekeza

Hata kama alama hiyo ingekuwa imevumiliwa basi kama ingekuwa alama hiyo iliwekwa mbele ya mashahidi hao basi ingevumilia

Katika utaratibu huo mahakama ina maoni kwamba alama hiyo iliyiwekwa imekiuka PGO 229 kwa maana hiyo inaathiri afya ya kielelezo hicho na kuathiri competence

Na nikutafute matakwa ya adminsibility kuwa polisi ofisa alitakiwa kutoa risiti ya ku acknowledge kukamata vielelezo hivyo

Katika hoja hiyo upande wa utetezi wanasema kuwa mtu yoyote ambaye anafanya upekuzi lazima atoe risiti baada ya upekuzi kama ambavyo sheria inalekeza

Wakasema kuwa shahidi namba 08 ajasema kuwa ametoa risiti wala ajatoa nakala yoyote mahakamani kama alitoa risiti

Kwa namna hiyo wakialika kuwa kutokutoa risiti kulikiuka sheria

Bwana Kidando anasema kwa kufanya upekuzi na kukamata mali, shahidi namba 08 alitoa seizure certificate

Upende wa mashitaka wakasema kuwa kwa kutolewa seizure certificate ambayo ina content sawa na risiti wakaomba mahakama wa one kuwa seizure certificate ionekane kama risiti

Nakubaliana na upande wa utetezi kama ambavyo wameieleza mahakama kuwa panapokuwa oamefanyika upekuzi katika nyumba, box au eneo afisa ambaye amekamatwa mali anatakiwa kutoa risiti juu ya mali alizokamata

Wakaomba mahakama izingatie sehemu ya pili katika sehemu A ya CPA, 2 (a) D mahakama ione kuwa kuwepo kwa seizure certificate ni sawa na kutolewa risiti

Nanukuu  kifungu cha 38 (3)  ya CPA

Kifungu pia cha 22(3)d  cha sheria ya uhujumu uchumi inasema pia kuwa ni lazima. kutoa risiti

Kifungu kingine kinachohusika kutolewa na risiti ni kifungu cha 35(3) ya sheria ya polisi na polisi wasaidizi sura ya 322

Lakini pia PGO ya 226 (2,5) na yenyewe inasema kuhusiana na utolewaji wa risiti

Anasoma……. kwa kingereza

Na mwisho guidelines ya mahakama chapter 05 paragraph ya 5 (f) inasema kuwa inatakiwa kutolewa risiti ya mali zilizokuwa zinakamatwa

Hakuna sehemu inayosema kuwa pale mahala ambapo risiti haijatolewa basi seizure certificate itumie kama mbadala wa risiti

Kwa upande wa utetezi walikataa mwaliko huo kwa kuomba mahakama ikatae mwaliko huo kwamba risiti na seizure certificate ni nyaraka mbili tofauti

Katika eneo hilo mahakama inamaoni kuwa suala la risiti mahakama imewekwa wazi na ni muhimu itumike

Mahakama ilipo itwa kuona kuwa risiti itumike mbadala wa certificate of seizure ilisema kuwa

Swala la seizure certificate kutumika badala ya risiti kuna maamuzi ya Mahakama Ya Rufani ya ANDREA AGUSTINO na wenzake ikiwa imeamliwa huko Tanga katika Rufani ya Jinai

Basi ni wazi kuwa a Mahakamani ya Rufani ilisha ona kuwa jambo hili no vitu viwili tofauti na mahakama inaona kuwa kutokutolewa kwa risiti ni mambo mawili tofauti

Baada ya kuwa tumeona kutokutolewa kwa risiti kuna athari, mahakama ya rufani iliyoketi iringa na ilikuwa aime quote with approval katika kesi ya PATRICK JEREMIAH Vs JAMHURI 34 / 2016

Kwa sababu hiyo mahakama hii inaona kuwa kushindwa kutoa kwa risiti ni fatal na jambo hili lina athiri admissibility

Katika hali ya kawaida mahakama ilitakiwa kuishia hapa, lakini kuna mwaliko wa Kibatala kuwa mahakama izingatie kuwa unatafuta nini kila inapokuwa sheria inakiukwa lakini wanapewa nafasi upande wa mashitaka

Nimeona hakuna cha ku reconcile katika maamuzi ambayo nimeshayatoa, maamuzi yote niliyo yatoa ni maamuzi halali hivyo mahakama inaona hoja hiyo halikuwa na mashiko  na naitupilia mbali

Mahakama inaona hoja zote zilizo letwa na upande wa utetezi haya kuwa na  mashiko isipokuwa mapingamizi mawili ya lebeling na kutokutoa risiti

Na Kwa Mapingamizi haya Mahakama Inaona Yana Merit na Sababu nilizo toa Mahakamani Nakataaa Vielelezo Hivyo NINATOA AMRI!

Mtoto wa Shahidi Ling’wenya (kulia)

Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na uamuzi Jaji kwa kusimama na kumuinamia

Wakili wa Serikali Robert Kidando: : tuna shahidi mmoja namba 08 aliyekuwa anatoa ushahidi wake, tupo tayari kuendelea

 Wakili Peter Kibatala: : Na sisi Pia tupo tayari Kuendelea

Shahidi anapanda Upya Kizimbani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: : Shahidi nini kilichofuata baada ya hapo

Shahidi: Shughuli niliyo fanya ilikuwa ni kufuatilia taarifa au michoro ambao ni kuwa nimeona kwenye kidaftari

Wakili Peter Kibatala: :: OBJCECTION shahidi anazungumzia kielelezo ambacho kimekataliww mahakamani, naona wanaongoza kwa mlango wa nyuma

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji mimi sioni kama kuna sheria inakataza juu ya swali hilo

Kibatala: Sija object swali bali majibu ya shahidi, anazungumzia kidaftari ambacho kimeshakatazwa na mahakama

Jaji: Mimi sioni kama kuna tatizo na hilo kama anaongelea jambo ambalo. limekatazwa mahakama itaona mbeleni

Shahidi: nimefuatilia baadhi ya maeneo ambayo yalikuwa yamechorwa na taarifa za a baadhi ya  maeneo uhalifu ulikuwa umepangwa

Wakili wa Serikali: Lini na Wapi?

Shahidi: Tarehe 24 August 2020 nilifika eneo moja ambalo lilikuwa kwenye mchoro ambalo lilikuwa limeandikwa sokoni Kilombero. 

Kwa Kulifuatilia eneo hilo nililitembelea ni Soko ambalo lipo Mkoani Arusha ambapo Lipo Uhuru Road

Kati kati ya kesi chupa ya soda inandoka na kesi inasimama, jaji anaomba kilicho lia kitafutwe kimtokea wapi

Kina kutwa ni chupa ya fanta chini ya miguu ya mawakili wa serikali

Jaji anaagiza kuwa chup ya soda ni silaha, isiingie tena mahakamani na kuanzia kesho ukaguzi uimarishwe

Shahidi : Tarehe 25 August 2020 anakamatwa Mtuhumiwa mwingine anayeitwa justin kaaya ambaye alikuja kuachiwa baaadae

Jaji: tuendelee

Wakili wa Serikali: Kwanini Justin Kaaya aliachiwa?

Shahidi: Aliachiwa baada ya ushahidi kuonyesha hausiki na tuhuma tuliokuwa tunampeleleza

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine Ulifanya

Shahidi: Upelelezi uliendelea katika kutafuta taarifa za watuhumiwa wengine tuliokuwa tunawataufa

Ambapo Tarehe 10 September 2020 tulimkamata mtuhumiwa mwingine aliyekuwa anaitwa Khalid Ally Athuman  ambaye na yeye aliachiliwa baada ya upelelezi kufanyika

Wakili wa Serikali: Kwanini Khalid Ally Athuman alikamatwa

Shahidi: Alikamatwa kama mtuhumiwa ambaye alikuwa analemgwa  kushiriki kwemye kikundi, pia aliwahi kuwa ni mwanajeshi wa kikosi cha 92 KJ alimakatwa hapa Dar es Salaam eneo la Kinondoni

Wakili wa Serikali: Baada ya ukamatwaji Khalid Ally Athuman kitu gani kingine ulifanya?

Shahidi Tarehe 19 September 2020 Tulimkamata Gabriel Muhina huko Tabora, aliwahi kuwa Mwanejeshi wa JWTZ katika kikosi Cha KJ 92

Wakili wa Serikali: :Mlimkamata kwa Tuhuma gani

Shahidi: Kwa tuhuma za a kutaka kwenda kushiriki vitendo vya kigaidi vilivyokiwa vinataka kutendwa hapa nchini

Wakili wa Serikali: :Gabriel Muhina sasa hivi Yupo wapi?

Shahidi: Aliwahi Pia kuwa Mwanajeshi wa JWTZ Kikosi cha  92 KJ

Nikiwa Mwanza nilitembelea maeneo ya Mabatini  Mwanza na BOT kwa kufatisha mchoro uliokuwa kwenye kidaftari

MALIMA BURONGO Tulimkamata  maeneo ya Pasiansi

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo kitu gani kiliendelea?

Shahidi: Tarehe 22 July 2021 usiku aliletwa mtuhumiwa namba nne ambaye ni Freeman Aikael Mbowe ili nimhoji

Baada ya kuletwa mbele yangu na yeye kunipatia majina particular zake zote

 Ndipo nilimuonya kwa makosa ya kula njama kutenda ugaidi

Chini ya sheria ya kuzia ugaidi

Wakili wa Serikali: Baada ya kumuona..?

Shahidi: Alipomaliza kutaja majina yake, wakili wake fredrick kihwelo hakwepo na hakuwezi kupatikana wakili wake

Hivyo mpaka kesho yake tarehe 22 July 2021 hiyohiyo ndipo alipatikana wakili wake

Siku fanikiwa kumuhoji mtuhumiwa, alisema mpka atakapo fika mahakamani ndipo atakapo toa maelezo yake

Wakili wa Serikali: Umekuwa ukieleza kuhusiana na Khalfani Bwire, hebu onyesha hapa mahakamani yupo sehemu gani

Shahidi: Ni yule aliye vaa tshirt yenye maandishi ya njano

Wakili wa Serikali: Wakati unaandika seizure certificate uliandika HALIFANI BWIRE elezea jina  hilo ulilipata wapi

Shahidi:  Ni kutokana. na matamshi aliyokuwa anataka mwenyewe

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh kwa sasa katika examination in chief.

Wakili Peter Kibatala: : Mheshimiwa Jaji tunaoemdekeza tupate mapumziko kwa dakika 45 mpaka saa 7 na nusu turudi

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi

Walikuwa wametushiriksha

Jaji: Basi tuna break kwa muda wa dakika 45, tutarudi saa saba na nusu

Jaji anatoka

Jaji amerejea saa 8 kamili mchana

Kesi namba 16 ya mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa mahakamani kwa mara nyingine

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji quorum yetu ipo kama awali, tupo tayari kuendelea.

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi pia quorum yetu ipo vilevile tupo tayari kuendelea.

 Wakili NashonNkungu: Shahidi habari!

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Maswali yangu nitataka ujibu kwa sauti.

Shahidi: Ndiyo nitajibu

Wakili Nashon Nkungu: Kwamba ulihusika kukamata washitakiwa wa kwanza, pili na watatu

Shahidi: Sahihi

 Wakili Nashon Nkungu: Hata Mahita alieleza hivyo

Shahidi: Miye sijui Kama Mahita kasema hivyo

Wakili Nashon Nkungu: Na ulikuwa na Mahita

 Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Mahita anasema mlifika kituoni

Shahidi: Ndiyo kituoni tulifika

Wakili Nashon Nkungu: Mweleze Mheshimiwa Jaji kama ni muhimu kumuandikisha mtuhumiwa kwenye detention register mtuhumiwa anapo fikishwa kituo cha polisi

Shahidi: Kufikishiwa na kupokelewa ni vitu viwili tofauti

Wakili Nashon Nkungu: Unaweza kumfikisha mtuhumiwa na asipokelewe..?

Shahidi: Mtuhumiwa analokelewa Kituo cha Polisi ndiyo anarekodiwa

Wakili Nashon Nkungu: Mweleze Mheshimiwa Jaji kama ni kitu che pesi kwa askari kwa vitu anavyofanya kwa kutumia memory yake

Shahidi: Ni Vyepesi kwakuwa ni moja ya sifa ya askari

Wakili Nashon Nkungu: unafahamu kwamba PGO inasema kinyume kwamba askari ategemewi kutumia kumbukumbu zake

 Shahidi: Miye sifahamu, ila nafahamu sifa ya askari ni kumbukumbu

Wakili Nashon Nkungu: Kwa hiyo PGO Unaposema kuwa askari asitegemee memory yaje inadanganya

Shahidi: Haidanganyi

Wakili Nashon Nkungu: Mida ya kukamata, kusachi na kuchukua vielelezo ni mida sahihi au makadirio.?

Shahidi: Mida sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Kwa hiyo mida yite mliyikuwa mna andika ilikuwa ni muda sahihi na siyo makadirio

Shahidi: Ni mida sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Mheshimiwa Jaji naomba kielelezo namba 12 na 13

Nashon Nkungu Ulielezea kuwa mlifika Rau madukani saa saba kamili mchana

Ni kweli.?

Wakili Nashon Nkungu: Nilisema saa saba

Wakili Nashon Nkungu: Kwa kuwa hatukadirii tuambie ilikuwa Saa Saba na Dakika Ngapi..?

Shahidi: Nilikuwa siangalii Muda kuangalia dakika nakumbuka ni saa saba mchana tuh

Wakili Nashon Nkungu: sasa ulisema mlifika saa saba mchana Rau Madukani mkapaki gari

Shahidi: Ni Kweli

wakili nashon nkungu: na ukasema kingai akamtuma mahita kuangalia kama wale watu bado wapo

Shahidi: Sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Kisha   Mahita akarudi?

Shahidi: Sahihi

Nashon Nkungu Sasa kwa kukadiria ulichukua dakika ngapi

Shahidi: Hatufanyi kazi kwa kukadiria

Wakili Nashon Nkungu: Nikisema ulichukua muda wa nusu saa nitakuwa sahihi

Shahidi: Wewe ndiyo umesema ila sisi hatufanyi kazi kwa kukadiria au kungalia muda wa kila kitendo

Wakili Nashon Nkungu: Alipo rudi akasema wale watu wapo?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Nyinyi Sasa mkatelemka mkaanza kuji panga

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Kwa kukadiria mazoezi yite haya sita yalifanyika kwa muda gani?

Kama utaki kujibu ni ruksa pia unaweza kuiambia mahakama kwamba utaki kujibu

Shahidi: Vyote vili fanyika ndani ya saa moja

Shahidi: Ndiyo tuliwapekua..?

Wakili Nashon Nkungu: Baada ya matukio yote kufanyika, sasa mkawapekua wale watuhumiwa, ni sahihi.?

Shahidi: Ndiyo tuliwapekua..

Wakili Nashon Nkungu: Hapa nimeshika vielelezo P11 na P12 nakuletea karibu uvione na kuvitambua? 

Shahidi: Ndiyo nimevitambua

Wakili Nashon Nkungu: Mwambie Mheshimiwa Jaji hii imeandikwa P ngapi

Shahidi: Imeandikwa  P 12

Wakili Nashon Nkungu: Na hii Imeandikwa Ngapi Ukitizana?

Shahidi: Nimeona ni Exhibit P 11.

Wakili Nashon Nkungu: Sehemu za muda ambao upekuzi ulifanyika unasomeka saa ngapi..?

Shahidi Saa saba mchana

Wakili Nashon Nkungu: Hapo ndiyo panasomeka hivyo?

Shahidi: Ni 13:00 mchana

Wakili Nashon Nkungu: Sasa 00 si saa saba kamili mchana

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Sasa ni sahihi kwamba upekuzi (search) ikifanyika kabla hamjafika..?

Shahidi: Sasa si tulifika saa saba mchana

Mahakama Kichekoooooo

Wakili Nashon Nkungu: Sawa miye nitaishia hapo

Wakili Nashon Nkungu: Ni sahihi Kuwa nyie mlitembea na watuhumiwa na mkawarudisha kituoni, ingepata nguvu kama ungetuoa detention register ya moshi

Shahidi: Nguvu ni huu ushahidi ninaotoa hapa

Wakili Nashon Nkungu: Ni sahihi kuwa zaidi ya mara moja mlienda na watuhumiwa Moshi  Police Central?

 Shahidi: Ni kweli

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kuwa detention register ni muhimu kama mtu alifika kituoni na kutoka

Shahidi: Ni muhimu kuonyesha kumbukumbu

Wakili Nashon Nkungu: Na pia ni ushahidi.?

Shahidi: Kama utaamua huo ndiyo ushahidi

Wakili Nashon Nkungu: Kutokwepo kwa nyaraka hakuna mtu mwingine kwa hakika ataeleza kuwa watu hawa walifikishwa Moshi

Shahidi: Sasa mimi si nipo hapa ndiyo nina uhakika

Wakili Nashon Nkungu: Kwa hiyo nyaraka hizi ni urembo?

Wakili Nashon Nkungu: Ushahidi Wa Nyaraka Muhimu zinazoelezwa na Sheria hujatoa hapa Mahakamani?

Shahidi: Mimi sijaleta nyaraka hiyo

Wakili Nashon Nkungu: Wakati mpo Moshi Watuhumiwa walikuwa wanalala wapi..?

Shahidi: Sijui kama walilala maana yake walikaa kituo cha polisi

Wakili Nashon Nkungu: Kama kweli mlisafiri na kama kweli mlisafiri muda huo, si tungeona kwenye polisi log book?

Wakili Nashon Nkungu: Nyinyi safari yenu mlisafiri kwa gari ya polisi.?

Shahidi: Ndiyo Kwa Gari ya Polisi

Wakili Nashon Nkungu: Je unafahamu kuwa kama mnasafiri kwa gari ya polisi, kila safari kuna watu wanatoa vibali vya nyinyi kusafiri, je unafahamu.?

Shahidi: Ndiyo Nafahamu

Wakili Nashon Nkungu: Mweleze Mheshimiwa Jaji kama ulisema safari yenu ilikuwa authorized na nani

Shahidi: Sikusema

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kuwa mnapo anza safari CRO officer anatakiwa  kurekodi muda na dhumuni la safari kabla mjaanza safari

Shahidi: Inategemea safari inaanzia wapi

Wakili Nashon Nkungu: Unaweza kuwa recorded au siyo lazima?

Shahidi: Inategemea Siyo Lazima

Wakili Nashon Nkungu: Je unafahamu gari ya polisi inapoyoka nje ya mkoa inatakiwa kupata ruhusa ngapi?

Shahidi: Si Kweli

Wakili Nashon Nkungu: Je unafahamu kuwa mnapo pata hitilafu gari hiyo inatakiwa kuripotiqa kwenye kituo cha karibu?

Shahidi: Si kweli

Wakili Nashon Nkungu: Unaifahamu Police Form Fomu EMI?

 Shahidi: Hapana siifahamu

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kuwa gari ya polisi inatakiwa kuwa na motor vehicle logbook

 Shahidi: Naifahamu

Wakili Nashon Nkungu: Basi hiyo Fomu EMI ndiyo logbook

Wakili Nashon Nkungu: Je umeitoa logbook hapa mahakamani?

 Shahidi: Hapana sijaitoa

Wakili Nashon Nkungu: Ni kweli kwamba gari zote za polisi zina registration namba

Shahidi: Ndiyo, zina registration namba

Wakili Nashon Nkungu: Na Kweli hapa mahakamani hukutoa registration ya gari yoyote ya polisi mliyotumia

Wakili Nashon Nkungu: Unakumbuka kuwa tarehe 9 mwezi august 2020 mliwapeleka watuhumiwa Mbweni?

Shahidi: Si kweli tarehe 09 august 2020 sikuwapeleka watuhumiwa Mbweni

Wakili Nashon Nkungu: Lakini unakumbuka kuwa uliwapeleka watuhumiwa Mbweni

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Sasa unakumbuka registration namba ya gari mliyotumia kuwapeleka watuhumiwa Mbweni?

Shahidi: Sikumbuki

Wakili Nashon Nkungu: Lakini wewe ukisema hapa moja ya sifa ya polisi ni kuwa na kumbukumbu

Wakili Nashon Nkungu: Sasa hapa kuna kauli mbili za mashahidi, ni sahihi kwamba mlikuwa kwenye gari ya pamoja wewe na Mahita mkitoka pale Rau madukani?

 Shahidi: Ni sahihi

[1/10, 14:42] +255 767 206 226: Wakili Nashon Nkungu: Na Watuhumiwa.?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Na kwamba mlikuwa mkiwa uliza maswali mbalimbali

Shahidi: Hapana, siyo maswali mbalimbali.

Wakili Nashon Nkungu: Mahita anasema kwenye ushahidi wake kuwa aliwauliza kuhusu mwenzao wa tatu yupo wapi

Shahidi: Ndiyo hilo waliulizwa

Wakili Nashon Nkungu: Ni sahihi Kwamba ulisema waliibu kuwa hawajui kuwa aliondokaje ondokaje katika lile eneo?

Shahidi: Ni sahihi walijibu hivyo

Wakili Nashon Nkungu: Tuambie nani muongo kati yako wewe na Mahita aliyesema walijibu tumeamwacha pale Rau Madukani na wewe waliokujibu kuwa hatujui

Shahidi: Hakuna mwongo

Wakili Nashon Nkungu: Je shahidi unafahamu kuwa watuhumiwa wanakataa kuwa hakuna sehemu yoyote mliyozunguka nao

Shahidi: Miye nimeeleza ushahidi wangu

Wakili Nashon Nkungu: Na moja sehemu mliyo enda Aishi Hotel?

Shahidi: Ndiyo tulifika

Wakili Nashon Nkungu: Mlijua mnaenda Aishi Hote?l

Shahidi:Ndiyo kwa kuongozwa na watuhumiwa

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Unajua Kuwa Hotel ni Private Premises?

Shahidi: Sisi hatukuingia Ndani ya Hotel, kiongozi wetu alishuka akasogea maeneo yake ila haku ingia ndani

Wakili Nashon Nkungu: Bado upo serious unataka mahakama iamini mlienda Aishi Hotel kumtafuta mtuhumiwa?

Wakili Nashon Nkungu: Hiyo ndiyo sababu pekee iliyoawafanya mvunje sharia?

Shahidi? Hatukuvunja sheria

Wakili Nashon Nkungu: Mliwaandikisha maelezo ndani ya masaa manne

 Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Anita na Esther maelezo yao yaliandikwa wapi?

Shahidi: Yaliandikwa Moshi

Wakili Nashon Nkungu: Pamoja na kwamba kesi ilifunguliwa Dar es Salaam?

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Wakati mnawaandika maelezo mlikuwa mnajua Mbowe na yeye  mtuhumiwa

 Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Na mliwaandika maelezo bila. MBOWE kukamatwa?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon Nkungu: Kwa hiyo kutokukamatwa suala la Mbowe Freeman halikukwamisha suala la kuandika maelezo wengine

Wakili Nashon Nkungu: Ni kweli Mbowe ulimuandika saa 6 na dakika 51

Wakili Nashon Nkungu: Kwa hiyo inawezekana kuandika maelezo usiku?

Shahidi: Ndiyo kutoka na upelelezi ulikuwa bado haujakamilika

Wakili Nashon Nkungu: Ni wewe ndiyo ulifanya upekuzi wa maungoni.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Na ulipofika kiunoni ukahisi ni kitu kigumu?

Kuna maeneo matatu ambayo ndiyo ukaguliwa fingerprints

Shahidi Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Ni sahihi Kuwa finger inaweza kuonyesha possession ya bastola hiyo?

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kwamba PGO inasema kuwa possession ya bastola inathibitishwa na finger prints?

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Je umeleta hapa mahakamani ushahidi wa finger prints kuonyesha possession ya hiyo bastola.?

Shahidi: Hapana siku leta kwasababu  halikuwa na sababu

Wakili Nashon Nkungu: Ni sahihi Kwamba PGO inasema silaha (exhibit) kisiwe loaded?

 Shahidi: Inategemea PGO

 Wakili Nashon Nkungu: PGO ipi.?

Wakili Nashon Nkungu: Je wewe ulimweleza Sébastien Madembwe kwamba atakiwi. kufanya hiki na hiki?

Shahidi: Mimi sijaongea kuhusu Madembwe na katika ushahidi wangu sija taja Madembwe

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kwamba madawa yakikamatwa yanatakiwa  kupelekwa kituo cha karibu yakabidhiwe kwa officer incharge?

Shahidi: Inategemea

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu kuwa mtu (Mtuhumiwa) anapokiri anatakiwa afikishwe kwa hakimu?

Shahidi: Inatemea na mtu mwenyewe kama anahitaji

Wakili Nashon Nkungu: Je unafahamu huo ukiri wa mtu wa tatu unaongeza nguvu ya ushahidi?

Shahidi: Ndiyo ni hitaji la mtuhumiwa mwenyewe siwezi kulazimisha

Wakili Nashon Nkungu: Wakati wa adamoo anaandika ukiri kwa kushiriki kwake kuweka magogo na ugaidi hukuona haja ya kwenda kwa mlinzi wa amani

Shahidi: Mimi sikuandika maelezo ya Adamoo

Wakili Nashon Nkungu: Unafahamu Inspector Mahita

Shahidi: ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Na ulisema ulikuwa naye mlipofika kwa Bwire?

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Ni kweli mlieleza kwenye ushahidi wako mlimkamata Bwire na simu mbili za techno na nyingine

Shahidi: Ndiyo

Wakili Nashon Nkungu: Je ulitoa hapa mahakamani simu hizo?

Shahidi: Hapana

Wakili Nashon Nkungu: Je ulisema zipo wapi simu hizo?

Shahidi: Zipo mahala salama

Wakili Nashon Nkungu: Ulizihusisha na Mashitaka haya?

Shahidi: Hapana

Wakili Nashon Nkungu: Nimesikia umrhojiwa Kuhusu HALIFAN BWIRE

Je ulisema hapa Mahakamani kuwa Mtu huyu ndiyo Khalfani Bwire? 

Shahidi: Sijasema labda kuna mtu mwingine atakuja 

Wakili Nashon Nkungu: Ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji

Wakili John Malya

Malya: unajua Kuwa Mamlaka inayotoa Leseni ya Kufanya Biashara ya Mafuta?

Shahidi Hapana sifahamu

Malya: inaitwa EWURA Leo nitakufahamisha

Malya: Unafahamu kuwa masoko yanasajiliwa?

Shahidi: Hapana sijui

Malya: : Basi Masoko yanasajiliwa na mamlaka za serikali

Malya:Shahidi unajua kuwa wauzaji wa mafuta uliowataja wana leseni za biashara katika halmashauri husika?

Shahidi” Sijui kama wanapewa leseni

Malya: Mimi sasa nakubishi kuwa katika yale makutano jirani na BOT hakuna kituo cha mafuta, sasa ithibitishe mahakama kama kweli kuna kituo cha mafuta Shahidi: Kwenye ushahidi wangu nimesema hakuna

Wakili: Wewe unasajili vituo vya mafuta.?

 Shahidi: Hapana

Malya: ulijaribu hata Kununua Mafuta Lita 5

Shahidi: Hapana

Malya: Vipi  kama ni road show tu?

Shahidi: Sijui sasa wewe

Malya: Umesema kuwa pale Arusha ulienda kwenye soko je ulimtaja hata kiongozi wa soko? 

Shahidi: Hapana

Malya: Hata sanduku la posta  la soko?

Shahidi: Sijui

Malya: Shahidi ushawahi kufanya kazi ofisi za DCI?

Shahidi: Ndiyo

Malya: Muda gani.?

Shahidi: Kwa miaka 7 ofisi ya utawala wa upelelezi

Malya: Unakumbuka kesi yoyote ambayo umesha wahi kupeleleza?

Shahidi: Ni nazo nyingi lakini siwezi kutaja hapa

Malya: Vipi Kuhusu Kesi ya Tito Magoti ambayo alikamatwa na ZCO na baadae kunyimwa dhamana na akatoka kwa kulipa pesa baadae, ushiriki wako ukoje

Shahidi: Siwezi kueleza hapa hilo

Malya: Wakati Unatoa ushahidi wako ulisema wewe ni Msukuma? 

Shahidi: Ndiyo

Malya: Unafahamu Kuwa Boaz na yeye ni Msukuma?

Shahidi: Miye sijui

Malya: Unafahamu pia kuwa Makonda ni Msukuma?

Shahidi: Miye sijui

Malya: Vipi ushiriki wako katika kumkamata Eric Kabendera.? 

Shahidi Si Kweli

Malya: Na wala hukwepo Wakati anachukuliwa maelezo?

Shahidi: Sijafanya sijafanya sijafanya!

Malya: Wakati ukiwa kwa DCI  Dar es Salaam ulishiriki ana na Makonda mliwahi kumtuhumu Mbowe kwa akuuza madawa ya kulevya?

Shahidi: Si kweli

Malya: Washitakiwa wanasema hawakukamatwa na bali walitekwa 

Shahidi: Sijui

Malya: Mshitakiwa Namba 4 alikuwa na msaidizi wake anaitwa Ben Saa Nane alikamatwa na mamlaka za serikali ukiwa ofisi ya DCI

Shahidi: Miye sijui lolote

Malya: Lakini ulisikia kuwa Ben Saa Nane amepotea..?

Shahidi: Nilisikia kwenye vyombo vya habari

Malya: Ukiwa ofisi ya DCI ulichukua hatua gani baada ya Ben Saa Nane kupotea ukiwa ofisi ya DCI?

Shahidi: Miye siyo jukumu langu,DCI  anajua kazi yake

Malya: Mbowe wakati anatekwa Mwanza simu zake walimpeleka wapi?

Shahidi: Mimi sijui nilikutana naye tarehe 22 July 2021

Malya: Alisachiwa nyumbani kwake walikamatwa computer, rooter na nyaraka zingine pamoja na hizo simu mmepeleka wapi hapa mahakamani hakuna?

Shahidi: Wanajua waliovi kamata miye sijui lolote

Malya: Fomu ya kukamatia mali unajaza  kitu chochote au kilichoandaliwa Mle?

Shahidi: Kilichoandaliwa Mle

Malya: Zile particular alizojaza ulijaza kabla ya kumpekua au baada ya kumpekua?

Shahidi: Alijaza mwenyewe

Malya: Alijaza baada ya kupiga makofi kidogo au kwa hiari yake?

Shahidi: Kwa hiyari yake

Malya: Wakati una mpekua alijibu anakaa wapi..?

Shahidi: Alijaza Chalinze

Malya: Kwa hiyo ukaamini anakaa Chalinze?

Shahidi: Anapokaa haikuwa muhimu

Malya: Jina lake muhimu?

Shahidi: Ndiyo

Malya: Address yake hukumuuliza?

Shahidi: Sikumuuliza

Malya: Maelezo hayo ya Chalinze  ulitoa wapi?

Shahidi: Hata mwenzie alisema hivyo

Malya: Mheshimiwa Jaji atasoma hapo umeandika address ya wapi wala sikupi faida kukutajia

Malya: Mheshimiwa Jaji naomba kielelezo P 13

Malya: Kwemye maelezo haya kuna sehemu wamesema kuwa walikutana Morogoro kupanga ugaidi.?

Shahidi: Ndiyo walikutana kupanga ugaidi

Malya: Sawa chukua maelezo haya nionyeshe sehemu palipoandikwa walikaa kikao cha kupanga ugaidi

Shahidi anapekua Maelezo

Shahidi anasoma sasa

Shahidi anasoma na mahakama inacheka tena

Mallya Kuna sheria yoyote inakata kiongozi kuwa na mlinzi.?

Shahidi: Hapana sifahamu

Malya: Kuna sheria yoyote inakataza kuwa mlinzi ambaye ni mwanajeshi mstaafu au aliye acha kazi?

Shahidi: Hapana

Malya: Ukiwa ofisi ya DCI mwezi 9 2017 kiongozi mwenzake alishambuliwa na risasi

Shahidi: Kuhusu kumshambulia Nina taarifa ila kuhusu riport sifahamu

Malya: Na Watu waliomshambulia Tundu Lissu wanamafunzo ya kutumia hizo silaha

Shahidi: Hata wahalifu wanajua kutumia

Malya: Sasa mtu a naona mwenzake alishambuliwa na risasi, anatafuta watu waka kusaidia kukabiliana na uhalifu kam huo, we utaki ajilinde..?

Malya: Shahidi nitafutie kwenye Kielelezo P 13 sehemu ambayo Ling’wenya alikiri Kufanya Ugaidi kwenye Mikoa ya Mwanza na Mbeya

Shahidi anapekua

Shahidi: Kuna sehemu anapo sema nchi nzima, mikoa unayosema ipo kwenye nchi nzima

Malya: Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji aandike sehemu inaposomeka kwamba watafanya maandamano nchi nzima ndiyo kupanga ugaidi Mwanza na Mbeya

 Shahidi: Ndiyo

Malya: Kwenye hati ya kukamatia bastola sehemu zote umejaza adamoo ila hapa Umejaza Adamo, je ulisha wahi kueleza utofauti huu?

Shahidi: Hapana sijaelezea

Malya: Mheshimiwa Jaji yangu ni Hayo tu!

Wakili Dickson Matata: Mheshimiwa Jaji nitakuwa na maswali machache sababu mengi washaukiza wenzangu

Shahidi nikikurudisha nyuma hapa, Malya: alikuuliza Swali kwamba kuna sheria inayokataza mtu aliye staafu jeshi au kuacha kazi ya jeshi kulinda mtu binafsi ukasema hakuna je nipo sahihi?

Shahidi: Ndiyo upo sahihi

Shahidi Aliitwa na Denis Urio Kuja Kufanya VIP protection

Matata: : Huko Kwingine hakunihusu jibu ni nacho kuuliza tuh

Matata: Kama aliitwa kwa vipi protection, alitumiwa nauli na pesa ya matumizi njiani?

Shahidi: Kama zinamalengo mazuri siyo kosa

Matata: Soma hapo

Shahidi: Baada ya hapo Mheshimiwa Mbowe alisema kuwa atarudi Dar es Salaam, ambapo kuna kazi kubwa ya kuweka magogo

Matata: Sasa kwenye hiyo sehemu uliyosoma kuna sehemu imesema au kutaja hivyo vituo vya mafuta vya kuchoma

Matata: Ukiachana na hapo Uliposema Kuna sehemu amekiri Kuwa ataweka Magogo Mkoa fulani au Barabara fulani

Shahidi: Hakuna sehemu iliyoa andikwa

Matata: Kuna sehemu specific ambapo wamesema kwamba kuna maandamano yatafanyika mkoa fulani na mkoa Fulani?

Shahidi: Hakuna specific ilipo tajwa mkoa

Matata: Kwa uelewa wako kufanya maandamano ni kosa kisheria au siyo kosa?

Shahidi: Inategemea Maandamano yamefanyikaje

Matata: Nilisikia unasema mtu akikiri ni hitajio lake kama ata hitaji kwenda kwa mlinzi wa amani

Shahidi: Ndiyo mpaka yeye atakapo hitaji

Matata: Kwa kifungu kipi cha sharia?

Shahidi: Sikumbuki

Matata: Kwa Sheria Ipi?

Shahidi: Sikumbuki Sheria ipi ila Kwa uzoefu wangu

Matata: ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji

Kibatala :Nafahamu wewe ni shaidi mzoefu

:Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Unafahamu kuwa wanao fuatilia kesi hii wanafuatilia wajibu wa utendaji kazi wa jeshi la polisi?

Shahidi: Miye natimiza majukumu yangu kama shahidi, suala la watu wanasema nini huko, siyo kazi yangu

Kibatala:Unafahamu unatakiwa kuwa na adabu unapokuwa kwenye kizimba cha mahakama na mchakato huu?

Shahidi: Nafahamu

Kibatala: Na unafahamu kuwa unapoambiwa uje mahakamani siku fulani lazima uje

Kibatala: Uliambiwa Kwamba Mheshimiwa Jaji Alitoa Amri katika Mahakama ya Wazi Kuwa 14 December 2021 alisema Ukija Tarehe 15 December 2021 kuwa Uje na Uthibitisho 

Shahidi: Niliambiwa lakini nilikuwa Njiani

Kibatala: Haya iambie mahakama ulifanya hivyo ulipokuwa mahakamani kutoa uthibitisho kuwa ulikuwa unaumwa

Shahidi: Si Kufanya

Kibatala: Kuna siku yoyote ile ambayo ulinyoosha mkono kumwambia Mheshimiwa Jaji nafahamu kuna amri yako

Shahidi: Sikunyoosha mkono

Kibatala: Kwa hiyo tukuchukuliaje sasa, kwamba umeizoea sana mahakama?

Shahidi: Si kweli kwamba nimeizoea mahakama

Kibatala: Haya tulikuwa na likizo ya mahakama ya wiki mbili je ulishawahi kuandika barua kupitia mawakili wako kuwa unasababu Fulani? 

Shahidi: Sikufanya

Kibatala: Umefanya kazi kwa miaka mingapi huko polisi

Shahidi: Miaka 20

Shahidi Miye mwanadamu, uwezi kunipiga kwa kukosea jambo moja

Kibatala: Wakati wa upelelezi ulikuwa ASP sasa hivi umepanda cheo, Je ulipanda cheo lini?

Shahidi: Mwaka jana mwezi sita

Kibatala: Ni sahihi umepandishwa cheo baada ya kufanya hizi shughuli ambazo ziliwapelekea hawa kupelekwa mahakamani?

Shahidi: Ni kweli matokea yalikuwa yameshatokea

Kibatala: na Sasa ni nani? 

Shahidi: Ni ACP

Kibatala Kwenye mkoa alikuwa ni nani?

Shahidi: Mpelelezi wa mkoa

Kibatala: Mahita alikuwa nani? 

Shahidi: Alikuwa assistant inspector

Kibatala: Nilisikia Mlikuwa Mnafanya kazi na Mahita 

Shahidi: Ndiyo

Kibatala Sasa hivi anacheo gani

Shahidi: Inspector

Kibatala: Amepanda cheo au ameshuka cheo?

Shahidi: Amepanda cheo

Kibatala: na Goodluck na yeye alikuwa nani?

Shahidi: Alikuwa Constable

Kibatala: Na yeye ni nani sasa hivi?

Shahidi: Yupo kozi anasoma

Kibatala: Nilisikia unasema kuwa wakati Bwire anakamatwa ulikwepo?

Shahidi: Ndiyo nilikwepo

Kibatala: Kuna mtu yoyote anamawasiliano ya dereva?

Shahidi: Mimi si mchukua mawasiliano

Kibatala: Namba, zake, root yake, namba ya daladala

Shahidi : Hakuna Details

Kibatala: Nilisikia kuna askari ulisema aaliwekwa ku intercept ile daladala, je unataarifa za huyo traffic

Shahidi: Sina

[1/10, 16:31] +255 767 206 226: Kibatala: Je kazi aliyoifanya ilikuwa ya Msingi au Haikuwa Msingi

Shahidi: Alifanya shughuli ya muhimu

Kibatala: Kwa ushahidi wako wewe ukisema kwamba Bwire alipofanyiwa search alikutwa na simu mbili za techno na bundi 

Shahidi Ndiyo nilizungumzia ila nikasema kuhusu disposal yake watakuwa kuzungumzia  wengine

Kibatala: Wakati Manazichukua Palikuwa na Shahidi Huru Mwingine? 

Shahidi: Hapakuwa na shahidi huru yoyote

Kibatala Ulimwambia mheshimiwa jaji kwanini hapaku a na shahidi huru.? Shahidi: Ila  kwa Jambo hili hamkuina Umuhimu wa Shahidi Huru

Kibatala Nilisikia ulihusika kukamatwa na Muhina na Khalid, kwa ufahamu wako walikaa ndani wakiwa wamebebeshwa kesi ya ugaidi mpaka nyie mlipoamua muwaachie huru

Shahidi: Sikusema

Mimi sikushughulika na hizo simu

Kibatala Baada ya Upelelezi Kukamilika ndiyo Mkagundua kuwa hawakuwa na Kosa 

Shahidi: Mwaka Mmoja

Shahidi: taratibu zinataka wakae ndani mpaka upelelezi unapokamilika

Kibatala: Jeshi La Polisi limepanga kuwafidia nini? 

Shahidi: Miye siwezi Kuingolea hilo

Kibatala: Ushawahi kufuatilia juu ya afya zao hasa Muhina ambaye amepata stress disorder ambayo mlimsababishia nyie ukiongozwa na wewe 

Shahidi Walikuwa ni wahalifu

Kibatala: Kama wahalifu kwanini mliwaachia

Shahidi: Kwa sababu hapo kuwa na ushahidi wa kutosha

Kibatala: Sasa watu ambao umekosa ushahidi unakwaita wahalifu?

Kibatala Kwanini mahakama isione kwamba wewe ni shahidi ambaye unamaslahi kama unawaita watu ambao hawajakuwa convicted kuwa ni wahalifu tena amewaaachia mwenyewe?

Kibatala: Nilisikia Unasema Kuwa mpango wa kulipua vituo vya mafuta na kupanga magogo barabarani

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Sasa ulisema lolote hapa mahakamani kwamba ulitoa taarifa kwa Ubalozi wa Uingereza waweze kuwakinga watu wao

Shahidi: Sikufanya

Kibatala: Ulitoa taarifa kwa Ubalozi wa Marekani

Shahidi: Sikutoa taarifa popote

Kibatala: Ubalozi wa Kenya?

Shahidi: Sikutoa taarifa

Kibatala: Hili soKo la Kilombero, Je Kuna sehemu yoyote umemwambia Mheshimiwa Jaji kuwa Soko la Kilombero kipo Arusha tuh

Kibatala: Maswala ya Ugaidi ni Global, Je kuna taasisi yoyote mliwataarifu kusaidiana kukabiliana na ugaidi?

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala Nimesikia mara kadhaa sheli, sheli sheli hivi sheli ndiyo nini?

Shahidi: Sheli kwa mtaani ni vituo vya kuuza mafuta

Kibatala: Miye nafahamu ROYAL Dutch Shell ni kampumi ya  kuuza  mafuta kama Puma au Bp

Shahidi: Miye sijui, nasikia watu wanasema sheli najua ni kituo cha mafuta

Kibatala: Zoezi la wakili wa serikali kuchukua hati ya mashitaka, kuhusu kuandika  HALIFANI je uliongozwa kuhusu kulimhanisha majina 

Shahidi: Si kuongozwa kuringanisha majina

Kibatala Wakati Ling’wenya anatoka Mtwara akasimama Chalinze na Kumchukua Mshitakiwa Wa Pili Kwenda Morogoro kwenda Kwa Urio Je walikuwa tayari Wana Nia Ovu au hawajui

Shahidi: Miye siwezi kufahamu kama walikuwa wana nia ovu

Kibatala: Wakati wanatoka Morogoro kwenda Moshi walikuwa wa nafahamu kuwa wanaenda kufanya matendo ya Ugaidi Moshi

Shahidi: Walikuwa wanafahamu

Kibatala: Nani aliye wa recruit kati ya mheshimiwa Mbowe au Urio

Shahidi: Aliye wafadhili

Kibatal: Nani aliye watongoza Ling’wenya na Adam pale Morogoro Kwenda kufanya Ugaidi, Ni Urio au Mbowe? 

Shahidi Ni Urio

Kibatala: Urio ana umri gani?

Shahidi: Ni mtu mzima

Kibatala: Alitoka Mtu Mwanza akaniomba nimtafitie Watu wa Kumuua Mtu Mwanza Je, Mimi niliyewatafuta watu Kwa ajili ya Kwenda Kuua nitakuwa Nina tenda Kosa la Jinai au siyo

Shahidi: Inategemea

Mheshimiwa Jaji bado Nina Maswali Mengi, Naomba tuhairishe hadi kesho

Kibatala: Basi Kama nilivyokueleza mwanzo watu wangapi a weledi wako wewe na jeshi la polisi

Jaji anaandika Kidogo

Wakili wa Serikali Robert Kidando:  Mheshimiwa Jaji Hatuna pingamizi na Ombi lililo Wasilisha na Wakili Msomi Kibatala kwa sababu ule muda tuliokubaliana umesha fika

Jaji: kufuatia maombi yaliyoletwa na upande wa utetezi na kukubaliwa na upande wa mashitaka nina ahiirisha shauri hili hadi kesho saa 3 asubuhi

Washitakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi

Shahidi namba 08    ataendelea Kuwa Kizimbani hapo Kesho

Like
1