Kesi ya Mbowe: Jamhuri yafunga ushahidi kabla ya mashahidi wengine 11 kuhojiwa

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji wakati tunaiomba Mahakama kwenye kifungu cha 41, tuliridhia kwa sababu mahususi kuwa Mahakama inaweza kufanya maamuzi hayo. Tunaporejea kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, tulikuwa aware na kifungu cha 293(1) cha CPA kwa mawakili wa utetezi kwa mazingira ambayo wameomba hapa Mahakamani. Hivyo Mheshimiwa Jaji, katika kuwasilisha hoja yetu hapo, na kama utaona inafaa kufanya hivyo kwa wasilisho basi tunaomba tufanye kwa njia ya maandishi na tuweze kuziwasilisha hapa Mahakamani.

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia, BJ, leo tarehe 15 Februari 2022.

Mwendelezo kesi ya Freeman Mbowe na wenzake leo Jumatatu, Februari 15, 2022 shahidi wa 13 kutoa ushahidi wake katika hatua ya kuhojiwa na mawakili wa utetezi.

Jaji ameingia Mahakamani. Muda ni saa 4:06 asubuhi. Ameshakaa kwenye kiti chake tayari kusikiliza kesi. Na kesi namba 16 ya mwaka 2021 ya Jamhuri dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe inatajwa.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji. Ikikupendeza mimi naitwa Robert Kidando na hapa nipo na wakili:

  1. Pius Hilla
  2. Abdallah Chavula
  3. Jenitreza Kitali
  4. Nassoro Katuga
  5. Esther Martin
  6. Ignasi Mwinuka
  7. Wakili Tulimanywa Majige

Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala. Hapa nipo mawakili:

  1. Livino Haule
  2. Emanuel Chengula
  3. Edward Heche
  4. John Malya
  5. Nashon Nkungu
  6. Fredrick Kihwelo

Jaji anawaita washitakiwa na wote wanne wanaitika kuashiria kwamba wako mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, shauri hili limekuja kwa ajili ya kusikilizwa na sisi tupo tayari kuendelea.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji na sisi pia tupo tayari kuendelea na shauri.

JAJI: Shahidi nakukumbusha kwamba ulikuwa chini ya kiapo na utaendelea kuwa chini ya kiapo.

SHAHIDI: Sawasawa Mheshimiwa Jaji.

JAJI: Wakili endelea kumhoji shahidi.

KIBATALA: Shahidi unakumbuka masuala ya sampuli ambazo ulichukua kutoka kwa mshitakiwa wa kwanza, wa pili na wa tatu?

SHAHIDI: Ni sahihi. Nakumbuka.

KIBATALA: Unakumbuka katika ushahidi wako uliotoa tarehe 7 Februari 2022 ulisema kwamba tarehe 30 Machi 2021 “niilipokea ripoti ya uchunguzi kutoka maabara ya uchunguzi wa maandishi kutoka kwa Koplo Khamis?

SHAHIDI: Nakumbuka.

KIBATALA: Kwa hiyo suala la ripoti mlileta wenyewe mahakamani, na mpaka ukasema mwandiko wa Bwire unafana na ule wa kwenye kidaftari?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Na kumwambia sasa katika ripoti hiyo mwandishi anasema kwamba ulipeleka sampuli 15?

SHAHIDI: Si kweli.

KIBATALA: Lakini ulisoma hiyo ripoti?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Ikija ikaonekana kweli ulipeleka karatasi 15?

SHAHIDI: Nimeshasema si kweli.

KIBATALA: Je, uliambiwa Jaji kwamba kidaftari cha Five Star si kielelezo hapa Mahakamani?

SHAHIDI: Sikuambiwa.

KIBATALA: Na kuhusu hiyo ripoti uliambiwa kuwa haiko hapa Mahakamani?

SHAHIDI: Sikuambiwa.

KIBATALA: Unafahamu kwamba majengo yana anuani, iwe kwa reference ya namba au makutano ya barabara mbili au tatu?

SHAHIDI: Nafahamu.

KIBATALA: In fact hata makao makuu makubwa au madogo ya Jeshi la Polisi Dodoma yana anuani. Unajua?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Na katika context hiyo ndiyo maana hata tumepiga hatua ndiyo maana hata makazi binafsi wanaanza kutoa anuani?

SHAHIDI: Ndiyo. Nafahamu.

KIBATALA: Nilikusikia ukisema kwamba ulitembelea vituo kadhaa wa kadhaa vya mafuta. Ni sahihi?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Ambavyo katika ushahidi wako ulisema kwamba vituo vililengwa kufanyiwa matendo fulani fulani katika vituo hivyo vya mafuta?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Ulitaja vituo vipi vya mafuta mbali na kile cha Morocco?

SHAHIDI: Ni GBP Kilwa Road, Puma Kilwa Road, Big Born Kariakoo…

KIBATALA: Kingine?

SHAHIDI: Puma kilichoko Sinza.

KIBATALA: Je, ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba kipo katika plot namba ngapi hicho kituo cha Morocco?

SHAHIDI: Nilieleza kipo katika barabara, kuhusu plot sikueleza.

KIBATALA: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba mmiliki wa hicho ni nani?

SHAHIDI: Sikumwambia.

KIBATALA: Sasa twende Kilwa Mivinjeni. Je, ulisema kipo Makutano ya barabara zipi?

SHAHIDI: Nilisema kipo Barabara ya Kilwa.

KIBATALA: Kipo plot namba ngapi?

SHAHIDI: Sikueleza.

KIBATALA: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba hicho kituo kinamilikiwa na nani?

SHAHIDI: Sikumwambia.

KIBATALA: Sinza hicho Kituo cha Puma, ulimwambia kipo sehemu gani?

SHAHIDI: Sikumweleza.

KIBATALA: Ulimwambia kipo katika makutano ya barabara zipi?

SHAHIDI: Sikueleza.

KIBATALA: Ulimwambia kipo katika plot namba ngapi?

SHAHIDI: Sikueleza.

KIBATALA: Ulimwambia kinamilikiwa na nani?

SHAHIDI: Sikumwambia.

KIBATALA: Big Bon Kariakoo ulimwambia Mheshimiwa Jaji kipo katika barabara ipi?

SHAHIDI: Sikumwambia.

KIBATALA: Ulimwambia kipo katika plot namba ngapi?

SHAHIDI: Sikusema.

KIBATALA: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba mmiliki wake ni nani?

SHAHIDI: Sikumueleza.

KIBATALA: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba vituo hivyo ulitembelea tarehe ngapi na saa ngapi?

SHAHIDI: Nilimwambia kwa kutaja tarehe.

KIBATALA: Kwa hiyo kwa ushahidi hapa vituo vyote ulitembelea kwa siku moja?

SHAHIDI: Ni sahihi. Ni tarehe 14 Agosti 2020.

KIBATALA: Muda ulitaja?

SHAHIDI: Sikutaja.

KIBATALA: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba ulienda na nani?

SHAHIDI: Sikusema.

KIBATALA: Hizo details kama ulivyozitoa katika maelezo yako ya tarehe 9 Agosti 2021 hakuna.

SHAHIDI: Zipo.

KIBATALA: Ungependa niombe nakala halisi ya kwako ili uweze kuithibitishia Mahakama?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe nakala halisi ya maelezo ya Inspekta Tumaini Swila. Nimejenga msingi wa kutosha na shahidi huyu.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi.

KIBATALA: Naomba ungalie na usome kwa sauti, ukishamaliza nielekeze mahali ambapo umevi- describe hivyo vituo kama ulivyosema.

(Shahidi amepokea na anasoma maelezo yake).

KIBATALA: Unafahamu maana ya details?

SHAHIDI: Hebu fafanua.

KIBATALA: Mwanzo nilikuuliza kwamba vituo vya mafuta ulivyotaja ulivitaja katika details kwamba vinamilikiwa na mtu X?

SHAHIDI: Ndiyo. Lakini si lazima iwe hivyo.

KIBATALA: Katika maelezo yako unasema Mivinjeni Dar es Salaam ulikuta kituo cha kuuzia mafuta cha Puma. Je, kuna mahali umetaja Kituo cha Puma kipo Kilwa Road?

SHAHIDI: Kilwa Road haipo. Ila ndiyo maana nimekuja kutoa ushahidi mahakamani. Kwenye maelezo siwezi kuweka kila kitu.

KIBATALA: Haya! Pia umesema kwamba ulifika Big Bon Kariakoo. Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa umetaja makutano ya barabara ipi.

SHAHIDI: Sikutaja.

KIBATALA: Twende pale unaposema kwamba Morocco kuna kituo cha kuuzia mafuta cha Total. Je, kuna mahali popote umesema kituo cha Morocco kipo katika makutano ya barabara gani?

SHAHIDI: Katika maelezo yangu hakuna.

KIBATALA: Ulikitaja kituo cha Morocco kipo karibu na Mwenendo Kasi, umetaja kituo cha Mwendo Kasi hapa?

SHAHIDI: Sijataja.

KIBATALA: Twende Sinza kwenye kituo cha Puma. Je, umefafanua kwa Jaji kuwa kituo cha Puma Sinza kipo barabara gani?

SHAHIDI: Sijafafanua.

KIBATALA: Si umekuja kutoa ushahidi wa kweli? Je, kuna tatizo Mheshimiwa Jaji akiyaona maelezo yako kama ushahidi wako?

SHAHIDI: Hakuna tatizo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kama shahidi alivyoomba, naomba maelezo yake yapokelewe kama kielelezo.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, Sisi tulichosikia ni “kuna tatizo lolote Jaji akiyaona maelezo yako?” Shahidi akasema hakuna tatizo. Hakuna mahala popote aliposema yapokelewe kama kielelezo. Hapo naona kama kuna tatizo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji. Nakumbuka nimesema akiyaona kama kielelezo? Unless kama kuna maelezo.

JAJI: Rudia swali lako.

KIBATALA: Je, shahidi una tatizo lolote kama maelezo yako yakipokelewa kama kielelezo Mahakamani?

SHAHIDI: Hakuna tatizo.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi.

JAJI: Mahakama inapokea maelezo ya Inspekta Tumaini Sostenes Swila kama kielelezo namba D5.

(Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na kuridhika na uamuzi wa jaji kwa kusimama na kukaa).

(Kuna simu imeita mahakamani na mtu ametolewa hapa).

KIBATALA: Kuna sehemu katika maelezo yako unasema kuwa lakini tangu akamatwe mtuhumiwa Khalfani Bwire, Mheshimiwa Mbowe haijawahi kufika kituo chochote cha Polisi kumuulizia, kitu ambacho kinafanya tuone nia yake iliyo ovu.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji. Katika kifungu cha 154 kinakataza anachokifanya Wakili Peter Kibatala. Ingekuwa ameomba kwa matumizi haya anayofanya basi ilitakiwa ajenge msingi. Kwa mujibu wa kifungu hiki, alimwelekeza katika maeneo ambayo alitembelea vituo vya mafuta kwa madhumuni ya kum- contradict, Sasa anachokifanya kipo nje ya kile alichoombea kielelezo. Procedure hiyo tunai- support kwa uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Lilian Jesus vs Republic_ ambayo ni Criminal Appeal namba 151 ya Mwaka 2018 (Unareported) lakini inapatikana katika mtandao wa TANZII.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, hiyo kesi anayotaja tunayo lakini nakuwa mwangalifu na anachokisema. Acha ni- reorganize. wanza anasema mimi najua, kwanza mimi siyajui hayo. Hayo ni maoni yao. Kwanza hapa Mahakamani kuna uamuzi wako wa kwamba nyaraka ilishaingia Mahakamani kama kielelezo inaweza kutumika.

KIBATALA: Kwanza kifungu cha 154 na 161 ni vifungu vinavyotumika kuingiza nyaraka Mahakamani.

JAJI: Soma kifungu cha 154.

(Kibatala anakisoma kifungu husika).

KIBATALA: Hiyo portion ni permissive. Naweza kumuuliza kwa kumwonyesha nyaraka au bila nyaraka. Nilikuwa nahitaji kum- contradict. Lazima nimuonyeshe the particular portion ambayo nataka kum- contradict. Hakuna mahali inasema kwamba siwezi kutumia kielelezo hapa Mahakamani kikishapokelewa. Kwanza wameweka toroli mbele ya farasi.

JAJI: Nakubalina na wewe na ninakubaliana naye kuwa katika Kifungu 154 inaposema kwamba pale ambapo unataka ku- draw attention yake kabla ya nyaraka inataka kuingia Mahakamani.Suala lako wewe unasema kwamba wameanza kuweka objections kabla hawajajua kuwa unataka kuwa- contradict au la. Kwa maana hiyo nakuacha uendelee tuone unachotaka kufanya kama utafika hapo tutajadili.

KIBATALA: Shahidi tuendelee. Umeiona sehemu unayosema kwamba Freeman Mbowe alikuwa na nia ovu?

SHAHIDI: Ndiyo. Kama asingekuwa nayo angefika kituo cha Polisi.

KIBATALA: Ni sheria gani inayomlazimisha Mbowe kufika kituoni personally yeye mwenyewe kumtafuta Bwire kituoni?

SHAHIDI: Hakuna sheria.

KIBATALA: Ili Freeman Mbowe aweze kufika kituo cha Polisi, lazima awe na information. Je, ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba mlimpatia simu Khalfani Bwire aongee na mke, ndugu na jamaa?

SHAHIDI: Sikueleza lakini ilikuwa inafahamika.

KIBATALA: Hiyo inafahamika na nani?

SHAHIDI: Inafahamika kwa mke wake siku tunaenda nyumbani kwake kumpekua.

KIBATALA: Kwa hiyo mke wake Khalfani Bwire akifahamu ndiyo Freeman Mbowe anafahamu? Je, ulichunguza ukakuta wanafahamiana?

SHAHIDI: Sikuchunguza hilo.

KIBATALA: Je, unafahamu kwamba kabla ya committal Khalfani Bwire alikuwa na uwakilishi wa mawakili kwa maelekezo ya Freeman Mbowe?

SHAHIDI: Sifahamu hilo.

KIBATALA: Je, Freeman Mbowe akitoa maelekezo ya wakili waende kumwakilisha Khalfani Bwire Mahakamani, je, atakuwa hajashiriki?

SHAHIDI: Siwezi kukujibu swali hilo.

KIBATALA: Huwezi kwa sababu hutaki au kwa sababu hujui?

SHAHIDI: Rudia swali lako.

KIBATALA: Kwanza wewe umeandika maelezo tarehe 6 Agosti 2021, na hapa kwenye committal panaonyesha mawakili walikuwapo kwa maelekezo ya Mbowe. Sivyo?

SHAHIDI: Sifahamu hilo.

KIBATALA: Unafahamu kwamba siku watuhumiwa wanafikishwa Mahakamani mlikuwa mnasema upelelezi haujakamilika?

SHAHIDI: Sahihi.

KIBATALA: Ni wewe katika ushahidi wako ulisema uliwapeleka watuhumiwa Kisutu?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Je, ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba ulipoteza interest kiasi kwamba huwezi kujua mawakili waliokuwa wanawawakilisha washitakiwa?

SHAHIDI: Kwa akili yako wewe naweza kusema neno kama hilo? Kwamba nimepoteza interest?

KIBATALA: Wewe jibu swali. Umemwambia au hujamwambia?

SHAHIDI: Sijamwambia.

KIBATALA: Wewe ndiye uliyesema kwamba ndiyo ulishiriki kuwaachia akina Gabriel Muhina na Khalid?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Nitaishia hapo. Naiachia Mahakama.

KIBATALA: Je, shahidi, Freeman Mbowe ina maana alikuwa chini ya uangalizi kabla hajakamatwa?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Je, wakati mnamfuatilia Freeman Mbowe ulikuwa unafahamu anaambatana na akina nani?

SHAHIDI: Sifahamu. Nilichoambiwa na Ramadhan Kingai ni kwamba mtuhumiwa namba nne anafuatiliwa kwa karibu.

KIBATALA: Katika ushahidi wako ulisema kwamba mlimtafuta Khalfani Bwire Sinza na Coco Beach?

SHAHIDI: Sahihi.

KIBATALA: Sasa je, uliwahi kugundua kuwa huyu mliyekuwa mnamtafuta Sinza na Coco Beach alikuwa na kazi ya kumlinda Mbowe na alikuwa katika jukumu la kumpokea Tundu Lissu?

SHAHIDI: Hiyo ilikuwa haifahamiki.

KIBATALA: Na katika maelezo yako umesema kuwa siku mnamkamata Khalfani Bwire alikuwa anatokea kazini kwake, yaani kwa Mbowe?

SHAHIDI: Ndiyo. Nimeandika.

KIBATALA: Kwamba siku anakamatwa alikuwa anatokea wapi?

SHAHIDI: Kazini kwake.

KIBATALA: Kazini Kwake kwa nani?

SHAHIDI: Kazini kwake. Kwa Freeman Aikael Mbowe.

KIBATALA: Luteni Denis Urio ambaye ni mtoa taarifa wenu anasema kwamba alimpatia Ramadhan Kingai namba za simu mshitakiwa wa kwanza, wa pili na wa tatu. Je, uliwahi kufahamu uwepo wa namba za simu?

SHAHIDI: Katika maelezo yake Denis Urio alitaja namba za simu za watuhumiwa wawili. Hizo ndizo alizompatia Afande Ramadhan Kingai.

KIBATALA: Na kwamba katika simu zao na maelezo yao ya onyo hakuna mahali ambapo walikuwa wametaja namba za Khalfani Bwire?

SHAHIDI: Sikumbuki kama wametaja.

KIBATALA: Unafahamu kufanya triangulation ya namba za Simu ili kujua mtuhumiwa yupo sehemu gani?

SHAHIDI: Fafanua.

KIBATALA: Ni neno la kiupelelezi unataka nifafanue nini? Kufanya (triangulation) ni kutumia namba ya simu ili kutaka kujua mtuhumiwa yuko eneo gani.

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Katika kumfuatilia Freeman Mbowe kama suspect wa ufadhili wa ugaidi, je, mlikuwa mnamfuatilia Freeman Mbowe movement zake za ndani na nje ya nchi?

SHAHIDI: Nilikuwa sifuatilii. Ramadhan Kingai alisema yeye anafanya hivyo.

KIBATALA: Je, unafahamu kwamba baada ya uchaguzi mtuhumiwa Freeman Mbowe alikamatwa yeye, Godbless Lema na Ex-Mayor Boniface Jacob? Walipelekwawa kufichwa sehemu mbalimbali zikiwemo Bagamoyo na Pale Oysterbay walipewa dhamana?

SHAHIDI: Sifahamu hilo.

KIBATALA: Pia hufahamu kwamba baada ya kupewa dhamana alikuwa anaripoti ofisi ya RCO Oysterbay mara kwa mara?

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Pia hufahamu kwa utaratibu huo huo Jeshi la Polisi lilimruhusu kusafiri kwenda nje ya nchi?

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Na pia hufahamu kwamba alirejea Tanzania kama mwanachi anayetii sheria?

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Je, ulifahamu logic (mantiki) ya swali la Wakili John Malya alipokuuliza kuhusu Rais Samia Suluhu Hassan kwamba Mbowe alikimbilia nje ya nchi baada ya kutafutwa siku nyingi kuja kujibu tuhuma zake?

SHAHIDI: Nilikuwa sifahamu.

KIBATALA: Lakini wewe kama mpelelezi uliyetakiwa na DCI lakini hujawahi kutoa taarifa kwa wakubwa zako kwamba mtuhumiwa ambaye nilikuwa nampeleleza amekimbia nchi?

SHAHIDI: Sijawahi kutoa taarifa kama hizo.

KIBATALA: Katika jalada CD/IR/2097/2020 uliwahi kuona taarifa kuwa mtuhumiwa Freeman Mbowe ametoroka nchini? Umewahi kuona katika jalada hilo?

SHAHIDI: Sikuwahi kuona.

KIBATALA: Twende kwa washitakiwa ambao umewaleta wewe mwenyewe. Je, washitakiwa Gabriel Muhina na Khalid walifanya nini mpaka wawe kwenye kesi?

SHAHIDI: Sikuwahi kufahamu.

KIBATALA: Ulishawahi jujulishwa kuwa kwanini wapo kwenye kesi?

SHAHIDI: Ramadhan Kingai aliniambia kuna taarifa za kiitelijensia zinazosema kuwa ni wahalifu.

KIBATALA: Wewe kwenye faili uliona jambo lolote ambalo lilikuwa linawahusu watuhumiwa wale?

SHAHIDI: Sijawahi kuona jambo lolote katika jalada kuhusu wale watuhumiwa.

KIBATALA: Je, walikaa muda gani vile?

SHAHIDI: Mwaka mmoja.

KIBATALA: Freeman Mbowe amemaliza mwaka mmoja?

SHAHIDI: Hapana.

KIBATALA: Nikisema huenda baada ya mwaka mmoja pia mtaona hana hatia nitakuwa nawaonea? Je, Luteni Denis Urio alishawahi kuwaambia kuhusu Gabriel Muhina na Khalid?

SHAHIDI: Hapana.

KIBATALA: Unafahamu Keys Hotel?

SHAHIDI: Ya Dar es Salaam au Moshi?

KIBATALA: Wewe unayoipigia kengele katika kesi hii.

SHAHIDI: Keys Hotel Moshi.

KIBATALA: Bila shaka sababu ya Kaaya.

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Je, ulimwambia Mheshimiwa Jaji kwamba Kaaya alikuambia lolote kuhusu Keys Hotel?

SHAHIDI: Hapana. Sikumwambia.

KIBATALA: Kaaya alikuambia kuhusu uwanja wa mpira Longido?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Kuna mahali popote umemwambia Mheshimiwa Jaji kuhusu Kaaya kukueleza mambo ya uwanja wa Longido?

SHAHIDI: Sikueleza.

KIBATALA: Je, katika maelezo…?

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji tunapinga swali hilo.

KIBATALA: Hapa Mahakamani ulitoa ushahidi kwamba baada ya kupokea simu nane kutoka ForensicBureau ukazikabidhi kwa askari polisi anaitwa Charles?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Wakati unakabidhiwa simu hizo nane, uliwahi kufafanuliwa kwanini kuna simu moja ilikuwa na chaji baada ya mwaka mmoja na nusu?

SHAHIDI: Hapana.

KIBATALA: Wewe binafsi uliwahi kufahamu kwanini simu hiyo ikawa na chaji kwa zaidi ya miaka miwili tangu ichukuliwe kutoka kwa Luten Denis Urio?

SHAHIDI: Nilikuwa sifahamu kwa sababu zilikuwa zimefungwa.

KIBATALA: Je, uliwahi kumfahamisha kwamba simu namba P28 iliwahi kugoma kuwaka hapa Mahakamani pamoja na jitihada kubwa za Denis Urio?

SHAHIDI: Sikuwahi kufahamishwa.

KIBATALA: Lakini hukuwahi kuambiwa kuwa kuwa kuna simu moja iligoma kuwaka?

SHAHIDI: Sikuwahi kuambiwa hilo.

KIBATALA: Tarehe 10 Agosti 2020 ulimpigia simu Luteni Denis Urio?

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Jeshi la Polisi lilimuwezesha kuja Dar es Salaam?

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Tarehe 11 ulimwagiza alete tena simu zingine. Je, ulimuwezesha kwenda Morogoro kufuata simu?

SHAHIDI: Sifahamu.

KIBATALA: Na je, Police Form 145 zinatakiwa zibandikwe muda gani?

SHAHIDI: Ni muda wowote tu unapoweka labelling.

KIBATALA: Matumizi ya Police Form 145 unayafahamu?

SHAHIDI: Nayafahamu.

KIBATALA: Yameelezwa na sheria gani?

(Shahidi anakaa kimya bila kujibu).

(Kisha Kibatala anamsaidia kujibu).

KIBATALA: Ni PGO.

SHAHIDI: Ndiyo.

KIBATALA: Unakumbuka PGO ipi?

SHAHIDI: Sikumbuki.

KIBATALA: Nilisikia pia kwamba hukubandika Police Form 145 kwa sababu palikuwa na uhaba wa fomu pale ofisini?

SHAHIDI: Siyo uhaba. Palikuwa hakuna fomu ofisini.

KIBATALA: Je, ulifafanua kwa Jaji kwanini hukumruhusu Luteni Denis Urio aende na simu zake ukipata Police Form 145 … tarehe 13 Agosti 2020?

SHAHIDI: Sikufafanua kwa sababu hapakuwa na umuhimu.

KIBATALA: Shahidi unafahamu kwamba pamoja na sheria na kanuni, kazi za polisi pamoja na wewe kama polisi mnaongozwa na hii Criminal Procedure Act?

SHAHIDI: Ndiyo. Pamoja na miongozo mingine.

KIBATALA: Je, unafahamu kwamba Criminal Procedure Act ina vifungu vinavyoruhusu utendwaji wa kosa?

SHAHIDI: Sikumbuki.

KIBATALA: Kwa hiyo hukumbuki hata sehemu inayosema kwamba unaweza kutoa taarifa kuhusu utendaji wa kosa si tu kwa afisa wa Polisi bali kwa mtu yeyote mwenye mamlaka?

SHAHIDI: Ni sahihi. Nakumbuka.

KIBATALA: Kwa hiyo mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ni mtu mwenye mamlaka kwa tafsiri hii?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Mkuu wa kambi ya Jeshi ni mtu mwenye mamlaka kwa mujibu wa sheria hii?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Mheshimiwa naomba sasa nipewe kielelezi P1 na P13.

KIBATALA: Sasa umezungumzia kuhusu mipango ya kulipua vituo vya mafuta ambao ilikuwa utekelezwe na watuhumiwa wanne, ambapo foot soldiers ni watuhumiwa watatu. Sasa kwa kuwa wewe ulikuwa ni mpelelezi, unaweza kumwambia Mheshimiwa Jaji ni kazi ipi maalumu ilikuwa ifanywe na Khalfani Bwire yeye binafsi katika kulipua hivyo vituo vya mafuta?

SHAHIDI: Alikuwa ana kidaftari cha michoro ya vituo vya mafuta. Alikuwa alipue vituo vyote.

KIBATALA: Wewe umeyatoa wapi?

SHAHIDI: Katika maelezo ya watuhumiwa wote.

KIBATALA: Nitafutie sasa katika maelezo ya Adam Kasekwa anaposema kwamba Khalfani Bwire alikuwa alipue vituo vyote. Tafadhali.

(Shahidi sasa anapekua kutafuta palipoandikwa katika hayo maelezo).

SHAHIDI: (Anasoma) “Mnamo tarehe 1 Agosti 2020 muda wa saa 11 alituita na kutuelekeza kuwa tukatekeleza maelekezo ya kwenda kumdhuru Mkuu wa Wilaya Ole Sabaya, pia alituelekeza kuwa anapenda kutembelea klabu kubwa za Kokoriko na MileStone. Pia tulirudi Dar es Salaam kulipua vituo vya mafuta na mikisunyiko.

KIBATALA: Sasa hapo kwa maelezo hayo ndiyo Khalfani Bwire katajwa anaenda kulipua vituo vya mafuta?

SHAHIDI: Ndiyo. Nimeshajibu.

KIBATALA: Nimekuuliza what is individual role ya Khalfani Bwire, wewe ukasema Khalfani Bwire alikuwa alipue vituo vyote.

SHAHIDI: Hilo ndilo jibu sahihi. Sasa uliza swali lingine.

KIBATALA: Unapokuwa unataka kulipua kila mtu anafanya kazi fulani. Twende kwa mshtakiwa wa pili. Alikuwa na jukumu lipi?

SHAHIDI: Kazi ilikuwa haijakamilika. Ilikuwa ni mipango.

KIBATALA: Ndiyo sasa wewe kama mpelelezi uligundua mshitakiwa wa pili alikuwa na jukumu gani? Majambazi wakivamia benki kuna mtu ataenda kwenye SAFE. Mwingine atashika risasi na mwingine ataweka watu chini. Sasa Adam Kasekwa alikamatwa kuwa na jukumu gani katika kulipua?

SHAHIDI: Katika maelezo ya hawajaeleza hayo.

KIBATALA: Je, katika maelezo hayo, wameeleza Mohammed Ling’wenya alikuwa na jukumu gani katika kulipua?

SHAHIDI: Ni kulipua.

KIBATALA: Ni sahihi shahidi kwamba katika maelezo uliyoshika ya Adamoo anasema “baada ya kufika Dar es Salaam na kumfikisha Mheshimiwa Mikocheni…” Umeiona sehemu hiyo?

SHAHIDI: Nimepaona.

KIBATALA: Hebu pasome.

(Shahidi anasoma).

SHAHIDI: (Anasoma). “Baada ya kufika Dar es Salaam na kumfikisha Mheshimiwa nyumbani Mikocheni mimi na Mohamed tulipewa shilingi 200,000 kwa ajili ya kujiandaa kwa mavazi, kwani kesho yake Tundu Lissu ndiyo alikuwa anakuja na kumpokea uwanja wa ndege. Baada ya kumpokea Tundu Lissu tulibakia Dar es Salaam mpaka tarehe 31 Julai 2020.”

KIBATALA: Sasa wewe kama mpelelezi ulithibitisha hayo katika upelelezi kuwa walirudi Dar es Salaam?

SHAHIDI: Nilithibitisha kupitia maelezo yao.

KIBATALA: Ulithibitisha pia kuwa baada ya kumpokea Tundu Lissu waliendelea kutoa huduma mpaka tarehe 31 Julai 2020?

SHAHIDI: Waliendelea kushiriki vitendo vya uhalifu.

KIBATALA: Soma katika hayo maelezo sehemu ambayo baada ya tarehe 27 na kabla ya tarehe 31 Julai 2020 kama walifanya matendo ya kigaidi.

SHAHIDI: Walikuwa wameshakula njama za kushiriki vitendo vya kigaidi.

JAJI: Elewa swali. Swali ni kilichofanyika kati ya tarehe 27 na tarehe 31 Julai 2020.

(Shahidi anapekuwa ili asome).

(Ameendelea kupekua, halafu anasoma sehemu nyingine hadi Kibatala anaingilia…)

KIBATALA: Nataka (unisomee) wakiwa hapa Dar es Salaam kati ya tarehe 27 na tarehe 31 Julai 2020.

SHAHIDI: Ukitaka nijibu hivyo huwezi kupata … Kwa maana ambayo unataka hakuna maneno hayo … Kwa maana ya maneno yote ukisoma utaona…

(Wasikilizaji mahakamani wanaangua kicheko).

KIBATALA: Twende kwenye maelezo ya Mohammed Ling’wenya pale inaposema kwamba “Baada ya mazungumzo yetu Mheshimiwa Mbowe… “

(Bado ni kama shahidi anatatizika halafu Kibatala anamsaidia…)

KIBATALA: Shuka mpaka sehemu Mheshimiwa Mbowe alikuwa anakunywa bia aina ya Kilimanjaro. Je, umeiona hiyo sehemu?

SHAHIDI: Nimepaona.

KIBATALA: Anza pale “..katika maongezi yetu…”

SHAHIDI: (Anasoma) “Katika maongezi yetu Mheshimiwa Mbowe alianza kwa kuuliza kama siasa tunaijua. Tukamwambia sisi siasa hatujui. Akatueleza kwamba katika jimbo lake la Hai, vijana wale wanapigwa na wengine wanatukanwa. Mheshimiwa Mbowe alisema kwamba alishawahi kufikisha malalamiko mpaka kwa Rais, pia kwa IGP alishampatia taarifa akasema kwamba atalifuatilia hilo.”

KIBATALA: Je, wewe kama mpelelezi ulithibitisha hilo kwamba sehemu ya mazungumzo yao palikuwa na mazungmzo ya siasa?

SHAHIDI: Katika maelezo yao nilithibitisha.

KIBATALA: Na anasema kwamba Mheshimiwa Mbowe anasema watu wake wanapigwa na yeye Mbowe anatukanwa. Je, wewe kama mpelelezi ulithibitisha walichosema?

SHAHIDI: Nilitumia maelezo.

KIBATALA: Maelezo yanasema kwamba Mbowe alimwambia Mohammed Ling’wenya kwamba Mbowe alifikisha malalamiko polisi kwa IGP ambaye ni bosi wako. Je, uliwahi kuthibitisha kwa IGP kama aliwahi kupokea malalamiko yake dhidi ya Sabaya?

SHAHIDI: Hapana.

KIBATALA: Nenda tena katika sehemu pameandikwa kesho yake.

SHAHIDI: (Anaendelea kusoma) “Kesho yake baada ya kuamka muda wa saa 2 asubuhi Dar es Salaam tulifika saa nne usiku. Mheshimiwa Mbowe alituita ndani kwake. Mheshimiwa Mbowe akaanza kutuambia kuhusu malipo yetu kwa mwezi kwamba tutalipwa shilingi 300,000. Na Mheshimiwa Mbowe alitupatia shilingi 200,000 kila mmoja kwa ajili ya kwenda kununua mavazi. Kesho yake tulikuwa tunaenda kumpokea Tundu Lissu. Kesho yake tarehe 27 tulielekea airport kumpokea Mheshimiwa Tundu Lissu ambapo Mheshimiwa Mbowe na Khalfani Bwire binafsi walikuwa katika gari yake nyeusi…”

KIBATALA: Inatosha mpaka hapo. Nina maswali kadhaaa.

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji naomba kwenda WASHROOM.

(Mahakama sasa inamsubiri shahidi arudi kizimbani).

Shahidi amesharejea kizimbani.

KIBATALA: Ni sahihi sasa kwa mujibu wa maelezo hayo kwenye tarehe ambayo Mohammed Ling’wenya anasema walikutana kwa Mbowe Dar es Salaam na content ilikuwa ni kuhusu malipo kwa mwezi na malipo ni shilingi 300,000. Je, ni kweli ulithibitisha kwamba majadiliano hayo yalifanyika?

SHAHIDI: Ni sahihi. Kwa mujibu wa maelezo ndiyo ilivyo.

KIBATALA: Ni sahihi pia kwamba shahidi kwa mujibu wa maelezo hayo Mbowe alimwachia masuala yanayohusu mishahara kwa katibu wake na Mbowe ambaye Ling’wenya anasema hamjui kwa jina. Je, ni sahihi?

SHAHIDI: Hebu rudia hapo.

KIBATALA: Ngoja nisome. “Tulikubaliana malipo ya mshahara itakuwa shilingi 300,000 ambapo Mbowe alimkabidhi majukumu hayo katibu wake.”

KIBATALA: Shahidi ni sahihi pia kwa mujibu wa maelezo hayo Mbowe alimwachia masuala ya mishahara kwa katibu wake ambaye Ling’wenya anasema hamjui kwa jina?

SHAHIDI: Ni sahihi. Ndiyo ilivyo kwenye hayo maelezo.

KIBATALA: Ni sahihi kwamba maelezo yanazidi kusema kuwa tarehe 27 Julai 2020 walikwenda kumpokea Tundu Lissu. Je, ulithibitisha?

SHAHIDI: Ni sahihi kwa mujibu wa maelezo.

KIBATALA: Ni sahihi kwamba wakati wanaenda kumpokea Tundu Lissu walitoka nyumbani kwa Mbowe Mikocheni B wakaelekea ofisi za Chadema?

SHAHIDI: Ni sahihi kwa mujibu wa maelezo.

KIBATALA: Ni sahihi pia kwamba Kasekwa na Mohamed Ling’wenya walienda airport wakitokea ofisi za Chadema?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Na ni sahihi kwamba baada ya kutoka airport walirejea ofisi za Chadema ambapo palikuwa na kikao mpaka saa mbili usiku?

SHAHIDI: Ni sahihi kwa mujibu wa maelezo.

KIBATALA: Je, ulithibitisha kwamba Kakobe na Katibu walienda kutafuta suruali za kaki kama combat, mabuti, suti…?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Je, ni sahihi kwamba suruali za kaki kama combat ni vazi rasmi la Chadema?

KIBATALA: Je, ni sahihi kwamba Mohammed Ling’wenya anasema kama alivyosema Adam Kasekwa walikuwa Dar es Salaam kuanzia tarehe 27 mpaka tarehe 31 Julai 2020?

SHAHIDI: Ni sahihi.

KIBATALA: Swali langu la mwisho kwako. Je, wewe kama mpelelezi tangu kesi hii ifunguliwe umeshawahi kuwa na washitakiwa saba?

SHAHIDI: Sahihi.

KIBATALA: Je, kuna mshitakiwa yeyote ambaye ameshawahi kuhukumiwa kifungo katika kesi hii?

SHAHIDI: Hakuna mshitakiwa ambaye amehukumiwa kifungo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji sina swali lingine kwa shahidi huyu. Naomba kurudisha vielelezo vyote.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji nitaanza mimi na baadaye atakuja wakili mwenzangu.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kupatiwa kielelezo P1 na P13.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa maswali kadhaa kuhusu maelezo ya onyo ya Adam Kasekwa na Mohamed Ling’wenya. Kielelezo namba 13 katika maelezo ya Mohammed Ling’wenya kuna eneo mahususi kuhusu suala la ulipuaji wa visima vya mafuta kama kielelezo namba P1 … Samahani siyo 13 hasa katika maelezo yanayoanzia muda wa saa kumi.

SHAHIDI: (Anapekua kisha anasema) Nimepata.

WAKILI WA SERIKALI: Katika eneo hilo alikuuliza majukumu yapi mahsusi ambayo mshitakiwa wa kwanza ameyafanya katika kulipua vituo vya mafuta. Wewe ukasema mpaka usome yote ndiyo utajua majukumu. Sasa pitia kwanza maelezo.

(Shahidi anasema ameona).

WAKILI WA SERIKALI: Kwanini ulisema kwa mujibu wa eneo alikuwa halipui visima vyote?

SHAHIDI: Kwenye maelezo hapa imeandikwa “ikishakamilika,” alituelekeza kurudi Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya kazi nyingine nyeti ya kulipua vituo vyote vya mafuta.

SHAHIDI: Na kwamba na yeye alikuwa katika njama ya kulipua vituo vya mafuta. Nilikuwa namaanisha hivyo kutokana hilo eneo.

WAKILI WA SERIKALI: Katika maelezo hayo hayo uliulizwa majukumu mahsusi ambayo Adam Kasekwa aliyafanya, ukasema hayajaelezwa. Ni Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Kwa sababu vituo vya mafuta ni vya Dar es Salaam. Na ukisoma utaona kuwa ni kulipua vituo vya mafuta Dar es Salaam.

WAKILI WA SERIKALI: Pia alikurejea katika kielelezo namba 13 ambacho ni maelezo ya Mohammed Ling’wenya. Umeulizwa maswali hapo ilihusiana na maongezi ya mshahara, na kwamba maelekezo sasa ya kukamilisha majukumu aliachiwa katibu wake ambaye alisema hamjui kwa jina. Je, eneo hilo umeliona?

SHAHIDI: Ndiyo nimeona.

WAKILI WA SERIKALI: Ukasema jambo hilo halikutekelezwa. Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Ukijakusoma mbele utaona tulikuwa tunasubiria mahitaji yetu. Kwa hiyo hilo suala halikuwepo, na wao walikuwa wanatumia kama wahalifu baada ya kushawishiwa.

WAKILI WA SERIKALI: Pia katika kielelezo hicho hicho namba 13… Ila ili nikuulize swali, soma kipande hiki (Anamwonyesha pa kusoma).

SHAHIDI: (Anasoma) “Kwamba watu wake Mheshimiwa Mbowe wanapigwa na yeye anatukanwa na vijana wa Sabaya. Alishawahi kufikisha malalamiko yake mpaka kwa Mheshimiwa Rais. Pia aliwahi kufikisha kwa IGP…”

WAKILI WA SERIKALI: Ukasema lakini wewe hukuthibisha.

SHAHIDI: Kwa sababu hili tukio lilikuwa halijaripotiwa na mimi nilikuwa sihusiki kupeleleza hilo.

WAKILI WA SERIKALI: Wakati unaulizwa kuhusu zile PF145, hususan zile ambazo ulijaza tarehe 13 ambapo ulipokea tarehe 12, ukaulizwa kwamba kwanini ulijaza tarehe 13 na hukumwita tena Luteni Denis Urio wakati unajaza tena. Ukasema hapakuwa na umuhimu.

SHAHIDI: Ni kwa sababu tulishajaza hati ya makabidhiano. Na wakati wa kujaza hiyo PF145 hawajibiki kuwapo. Inajazwa na askari.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kama ulifanya upelelezi wowote kuhusu Keys Hotel Moshi, ukasema hakukuwa na umuhimu.

SHAHIDI: Ni kwa sababu yeye alienda Keys Hotel kumsubiria Freeman Mbowe, na baada ya pale ndiyo walienda Aishi Hotel ambapo kule alimkabidhi majina ya watu wa Sabaya.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, tunaona angeishia Aishi Hotel. Lakini naona wanaenda overboard.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji. Sisi hatuoni ni jambo jipya. Sisi tunaona majibu haya ni valid kwa shahidi wetu kuzungumzia.

JAJI: Mr. Kibatala nitakupa muda wa kufanya tena cross examination.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Basi Mheshimiwa Jaji naomba tuishie pale, mwisho Aishi Hotel bila kusema kilichojiri kule ili kupunguza mlolongo.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi ulikuwa pia unaulizwa katika nafasi yako kama mpelelezi ikiwa unafahamu kwamba mshitakiwa wa nne aliwahi kutoroka nchini. Wewe ukasema kuwa halikuwa jukumu lako. Je, ni kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Nilisema hivyo kwa sababu taarifa za kufuatiliwa mwenendo wa mtuhumiwa namba nne Freeman Mbowe nilijulishwa na Afande Ramadhan Kingai bila kuniambia nani anayefuatilia. Na niliposema pia hapakuwa na taarifa zozote za mtuhumiwa namba nne, ni kweli sikujulishwa hizo taarifa wala sikusikia.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, naomba ahirisho fupi ili tukirudi tuweze kuendelea na re examination.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi. Malya alikuwa anatania kuwa nisiombe Jaji amlinde shahidi.

JAJI: Basi tutapata ahirisho mpaka saa 7:45.

Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama.

Jaji ameshaingia katika chumba cha mahakama. Kesi inatajwa tena. Ni kesi namba 16 ya Jamhuri dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji kwa upande wa Jamhuri quorum iko kama ilivyokuwa mwanzoni kabla ya kuahirisha shauri hili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji na sisi pia quorum yetu iko kama ilivyokuwa kabla ya kwenda break. Tupo tayari kuendelea.

JAJI: Karibuni tuendelee.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na vile vituo vya mafuta ulivyokwenda kuvitembelea kwa maana ya Big Bon Kariakoo, Puma ya Sinza na Puma ya Kilwa Road. Sasa uliulizwa swali kuhusu details ambazo umezitoa Mahakamani, ukasema umezitoa kwa maana ulifahamu maana ya details. Ukaulizwa details za plot namba, mmiliki na makutano ya barabara ukasema siyo lazima ziwepo katika maelezo yako.

SHAHIDI: Ndiyo. Nilisema kwamba si lazima kwa sababu mimi nimekuja Mahakamani. Nimeapa na nilieleza maelezo yangu.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa kama ulijibu swali kwamba hukuweka hizo details lakini details hizo umetoa hapa Mahakamani. Kwanini umetoa details Mahakamani na hukuweka kwenye maelezo yako?

SHAHIDI: Ni ili Mahakama iweze kuelewa zaidi ni maeneo gani yaliyo kuwa yamepangwa kufanyiwa vitendo vya uhalifu.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kwa mara nyingine tena tupatiwe kielelezo namba 1 na kielelezo namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusiana na mtu mmoja anaitwa Justine Kaaya kuhusu kushiriki vikao vya kigaidi. Ukasema ni kweli alishiriki bila yeye kufahamu lengo la kikao ila mshitakiwa alifahamu lengo la Kikao. Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba wakati mshitakiwa wa nne kuomba majina ya watu wanaofuatana na Ole Sabaya, alikuwa anajua lengo la kupata vitu hivyo ni kufanya vitendo vya kigaidi. Wakati Kaaya anatoa vitu hivyo hakujua lengo la mshitakiwa namba nne ni lipi.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa na Wakili Nashon Nkungu kama ni kosa kama ilivyojitokeza kwa Luteni Dennis Urio kumtafutia mtu watu wa kufanya vitendo vya ugaidi. Ukasema inategemea. Elezea hapo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba haitakuwa kosa kama utakuwa unamtafutia huyo mtu kwa lengo la kusaidia vyombo husika.

Wakili Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji. Nilichouliza ni kama lilikuwa ni kosa kwa shahidi Denis Urio kukubali mpango wa ugaidi na si kwenda kufuta.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji na mimi ndicho nilichouliza kama ni kosa au siyo kosa kwa Denis Urio kukubali kwenda kumtafutia watu wa kwenda kwa mshitakiwa wa nne wale watu.

SHAHIDI: Niliposema inategemea inaweza kuwa kosa au si kosa nilikuwa namaanisha kuwa kama atatafuta watu hao kwa lengo la kuzia uhalifu na kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vya Ulinzi haitakuwa kosa, na uhalifu huo umezuiwa kwa walengwa kukamatwa na kufikishiwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Umeulizwa maswali kadhaa kuhusiana na taarifa aliyotoa Luteni Dennis Urio kwa DCI kwamba awe anatoa taarifa kwa Kingai, na Dennis Urio alitoa taarifa kwa Kingai kwamba tarehe 18 Julai mpaka tarehe 4 Agosti 2020, ukasema hakukuwa na ufutailiaji bado. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilimaanisha kwamba taarifa ambazo Luteni Dennis Urio alipewa na mshitakiwa wa nne alikuwa bado hajaanza kufanyia kazi. Mpaka tarehe nne alipoanza kuwasiliana na mtuhumiwa namba moja. Na wakati wanawasiliana nao…

WAKILI WA SERIKALI: Bado hujaulizwa swali.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa swali kuhusiana na hati ya makabidhiano baina yako na Dennis Urio tarehe 11 Agosti 2020. Je, ile fomu ilivyo ulionyeshwa hapa ukasema fomu ile haionyeshi kama Dennis Urio ni shahidi.

SHAHIDI: Nilieleza hivyo kwa sababu fomu ile huwa tunatumia askari tunapokabidhiana vielelezo. Nilitumia fomu hiyo kwa Luten Dennis Urio kwa sababu yeye ni shahidi. Niliweza kusaini katika fomu hiyo na yeye akasaini.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusu ile Polisi fomu namba 145 ambayo ilikuwa na vielelezo namba 28 mpaka 35 na kuhusu vielelezo vilivyokamatwa kwa mshitakiwa wa kwanza. Kuna baadhi vinaonyesha kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam au Police Central Dar es Salaam.

SHAHIDI: Fomu hizo zinajazwa kuonyesha jalada la kesi na kituo ambacho jalada hilo limefunguliwa.

Wakili John MALLYA: Objection! Mheshimiwa Jaji napinga hilo swali. Mimi ndiye niliyeuliza fact kwamba linajazwa na linafunguliwa. It’s a new fact ambayo ita- invite further cross examination.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji. Kwanza pingamizi lake halina mashiko. Kwanza ingekuwa sawa kama nauliza kuhusiana na mshitakiwa wa kwanza na wa tatu. Aliulizwa simu za mshitakiwa wa kwanza alipokea akiwa wapi akasema akiwa Central, akauliza kama aliandika mwenyewe akasema hapana. Hapa chini shahidi alisema hawezi kuwasemea Kingai wala Goodluck walijazia wapi. Sisi Mheshimiwa Jaji tunaendelea kusisitiza kuwa swali letu ni valid.

JAJI: Jibu ni nini?

SHAHIDI: Fomu namba 145 unajaza sehemu ya station na namba ya jalada. Kwa sehemu ya station nimejaza Police Central Station na jalada ni CD/IR/2097/2020.

JAJI: Sasa suala la Malya ni kwamba anaposema hivyo anatoa explanations mpya kwa sababu yeye alijaza fomu za Dennis Urio. Kwa hiyo alileta maelezo kuhusiana na hao ambao hajajaza yeye. Inaleta shida kidogo.

WAKILI WA SERIKALI: Sawa Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Inspekta Swila uliulizwa hapa maswali kuhusiana na vifaa vya mshitakiwa wa nne ambavo ni simu na computer kadhaa, ukasema kwamba ulipeleka katika maabara ya uchunguzi, na siku ile ambayo ulianza kutoa ushahidi wako ndiyo uchunguzi wake ulikuwa umekamilika.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba upelelezi wa shauri hili umekamilika tangu tarehe 18 Julai 2021. Kuhusu tarehe ya juzi kuhusu uchunguzi ilikuwa ni kuhusu uchunguzi wa ziada wa vielelezo vya mshitakiwa wa nne ambao ulikuwa unafanywa na maabara ya uchunguzi ya makosa ya mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa kati ya kipindi cha tarehe 14 Julai 2020 mpaka Agosti 5, 2020 kama uhalifu ulikuwa umeshatendeka. Ukasema inategemea na mpango wa uhalifu wenyewe.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kuwa kama kikundi mipango yake ya kutenda uhalifu itakuwa imekamilika basi uhalifu utafanyika, lakini kama kikundi haijakamilisha mipango yake yenyewe ya kutenda uhalifu basi uhalifu hauwezi kutendeka.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Inspekta Swila uliulizwa pia maswali kuhusiana na yale maombi ya uchunguzi wa kisayansi kwenda Airtel, kuhusiana na Khalfani Bwire na Freeman Mbowe pamoja na Dennis Urio, namba zote tatu zilioombewa taarifa, lakini taarifa zikaja za Dennis Urio na Freeman Mbowe lakini taarifa ya Khalfani Bwire haipo. Ukasema ipo katika taarifa ya Mbowe.

SHAHIDI: Katika uchunguzi wa miamala ya Freeman Mbowe palikuwa pia pana taarifa ya uchunguzi wa miamala ya Khalfani Bwire katika miamala ya Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hukusiana na taarifa iliyopo katika kielelezo namba 26 na maelezo ya Dennis Urio. Ulipoulizwa kuhusiana na kilichopo ukasema hakutakuwa na utofauti wa maudhui. Je, ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha ni ujumbe wa maneno uliopo katika vielelezo hivyo kwani unafanywa na mtumaji na mtumiwaji. Inaonekana mwisho katika taarifa iliyoandaliwa na maabara ya uchunguzi Kitengo cha Makosa ya Mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu upokelewaji wa taarifa kutoka kwa Dennis Urio na ukathibitisha aliyepokea taarifa ni DCI wakati huo palikuwa na Deputy DCI Charles Kenyela Ukaulizwa kama mazingira yake si alitakiwa amuachie Deputy DCI kuongozwa Upelelezi? Ukasema si kweli.

SHAHIDI: Niliposema kwamba Afande DCI hakupaswa kumuachia Deputy DCI kuendelea na upelelezi wa sshauri hilo kwa sababu taarifa za uhalifu zilitoka upande mwingine ambapo zilipokelewa na Afande DCI.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali kuhusu taarifa ya jalada la uchunguzi, ukasema kilichokuongoza ni taarifa alizokuwanazo Afande Boazi. Ukaulizwa kuhusu material ya kutosha kufungua jalada ukasema ulikuwa nayo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha taarifa ambayo ilikuwa imeandikwa na Afande Ramadhan Kingai niliweza kupokea na kuifanyia kazi taarifa hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu taarifa iliyotoka kwa DCI kuja kwako kwamba ilikuwa ni hearsay ukasema NDIYO. Ulikuwa na maana gani?

SHAHIDI: Askari anayepokea taarifa anakuwa anafuata moja kwa moja kutoka kwenye chanzo. Hiyo haizuii kufungua jalada.

WAKILI WA SERIKALI: Licha ya kuwa mpokeaji wa taarifa wa kwanza, uliulizwa pia kuhusu ni lini hasa ulichukua maelezo yake tarehe 4 Oktoba 2020. Ukaulizwa kwanini kesi hii isichukuliwe kuwa ni ya kutungwa.

SHAHIDI: Siyo ya kutunga kwa sababu taarifa ilitolewa, watuhumiwa wakakamatwa na hatimaye wakafikishwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kwamba wengine wanasema ni kulipua vituo vya mafuta na wengine wanasema kuchoma masoko katika maeneo ya mkusanyiko, ukasema kulipua na kuchoma ni kitu tofauti na baadaye ukasema kulipua na kuchoma ni terminology. Ulikuwa unamaanisha nini?

SHAHIDI: Ni terminology tu. Watu wanashindwa kutofautisha lakini haiondoi lile kosa la kutenda vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na kielelezo namba nne na namba tano kwa maana ya maganda mawili ya risasi katika kielelezi namba 4 na kielelezo namba 5 ni kielelezo cha risasi. Ukaulizwa kuhusu kutofautiana moja inaitwa Luger na nyingine jina tofauti. Ukasema kwa upande wa risasi ni tofauti. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha risasi si muhimu kuwa na utambulisho. Hazina utambulisho ambao ni tofauti.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji napinga kabisa majibu hayo. Kwamba risasi hazina utambulisho tofauti..

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sisi tulisikia hilo. Sijui kama upande kinzani walisikia hilo. Mheshimiwa Jaji naomba kuendelea na swali lingine.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa swali kuhusiana na Justin Elia Kaaya. Ukaulizwa kama kuna mfanano wowote kati ya maelezo akiwa mtuhumiwa na akiwa shahidi. Wewe ukasema hayawezi kufanana kati ya onyo na ushahidi, isipokuwa yale maelezo ya msingi.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha maelezo ya kwanza yalikuwa yanaelezea kosa wakati haya ya pili ni shahidi na hayaelezei kosa lolote.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali katika kielelezo namba 13 ambayo ni maelezo ya onyo ya mshitakiwa Mohammed Ling’wenya, kwamba katika maelezo yake, hasa ile nia ya kumdhuru Lengai Ole Sabaya ilikuwa siyo kuleta taharuki ila kushambulia viongozi wa Serikali.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika maelezo yake hakusema kwa nia ya kuleta taharuki, lakini kwa malengo yaliyokusidiwa na ambayo shahidi alieleza kutoka kwa mshitakiwa wa nne vitendo vya kumdhuru kiongozi ni vitendo vya kuondoa amani na kufanya nchi isitawalike.

KIBATALA: Objection! Mheshimiwa Jaji samahani. Neno kuondoa amani tulishawahi kutaja hapa Mahakamani?

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji neno kunaondoa amani tunalitoa.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila kuna maswali kadhaa hapa uliulizwa hasa kuhusu mshitakiwa wa pili na wa tatu pale Morogoro kuhusiana na suala la kwenda kwa Freeman Mbowe. Katika maelezo yao ya onyo ya P1 na P13 hawa wote wanasema walipoondoka walikwenda Moshi wakati maelezo mengine ya Dennis Urio wanasema walipoondoa walikwenda Dar es Salaam. Uliulizwa kama kuna mgongano ukasema HAKUNA.

SHAHIDI: Ni kwa sababu maelezo yote lengo ni kwenda kukutana na Freeman Mbowe. Maelezo hayana mgongano wowote kwa sababu mtu ambaye walitakiwa kukutana naye walikutana naye Moshi kama wanavyoeleza katika maelezo yao.

Shaidi: Ni wazi walikutana na mshitakiwa wa kwanza.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno WAZI liondoke. Ni OPINION zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji ni sawa liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na kiwango cha pesa ambacho kila mshitakiwa anadai katika maelezo yake ya onyo alipewa na Luten Dennis Urio, ambapoo Adam Kasekwa anasema walipewa shilingi 87,000 na Urio anasema aliwapa shilingi 199,000. Wakati huo Mohammed Ling’wenya anasema ni shilingi 195,000. Ukaulizwa viwango hivyo vinafanana? Ukasema vinafanana. Kwanini?

SHAHIDI: Kwa sababu wote walipokea pesa kwa Luteni Dennis Urio na kila mtuhumiwa alitoa maelezo yake kwa hiari yake.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kuhusiana na maelezo aliyotoa Adam Kasekwa hasa pale alipotoka Morogoro akanunua shati Chalinze. Ukaulizwa kama shati lile ni ugaidi, ukasema huwezi kutengenisha na ugaidi.

SHAHIDI: Ni kwa sababu pesa ilitumwa na mtu ambaye alikuwa anajua nia ya kuwaleta watu hao kwake ni kwa nia ya kutekeleza vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali hapa kuhusiana na maelezo yale uliyomwandika Dennis Urio kama kuna sehemu alikuambia Kuwa amemwambia Freeman Mbowe kuwa asitumie namba yake bali atumie ya wakala au vijana wake. Wewe ukasema kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya kumweka karibu. Ukasema sehemu hiyo kwenye maelezo haipo.

SHAHIDI: Nilipoeleza hivyo nilikuwa namaanisha kuwa kumzuia asitumie namba yake ya simu ilikuwa ni sehemu ya kukusanya taarifa kutoka kwa mtuhumiwa wa nne.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa swali kuhusiana na kielelezo namba P1 ambayo ni maelezo ya Adam Kasekwa ambayo ni IMEI namba kwa kulinganisha na kielelezo namba 23 ambayo ni ripoti kutoka uchunguzi wa kisayansi. Lakini ikawa na utofauti kwamba katika maelezo y aonyo palikuwa na utofauti wa namba tatu. Wewe ulisema katika maelezo ya onyo kipo ila kwenye cyber ripoti haipo ila ukasema haimaanishi kitu tofauti.

SHAHIDI: Nilimaanisha simu hiyo IMEI ya kwanza ipo katika maelezo lakini kwenye IMEI ya pili ndiyo kuna utofauti. Kwa hiyo kukosea kwa hiyo ya pili haimaanishi ni kitu cha pili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno kukosewa lisiingie. Ni ushahidi mpya anataka kuingiza kwa mlango wa nyuma.

JAJI: Maneno halisi ni kukosekana.

WAKILI WA SERIKALI: Ndiyo Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila jana ulionyeshwa maelezo ya onyo y aAdam Kasekwa ambapo yeye anadai kukamatwa Rau Madukani saa tano asubuhi wakati mtuhumiwa mwenzake anazungumzia kukamatwa saa saba mchana. Ukaulizwa kama huu utofauti uliufanyia kazi. Ukasema kila mmoja alisema kwa ufahamu wake.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba watuhumiwa hawa walitoa maelezo kwa hiari yao. Kwa hiyo kutofautiana kwa muda ni kwa kadri mtu alipokuwa anajaza.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kiwango cha pesa cha shilingi 195,000 ambacho Luteni Dennis Urio aliwapatia kwa namna mbili. Sasa washitakiwa wanaongeala kupewa pesa kiwango hicho? Wewe ukasema ni hali ya kawaida. Eleza kwanini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba kila mmoja alitoa maelezo kwa kadri ya ufahamu wake na kumbukumbu zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapa. Wenzangu pia wataendelea.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji nina maswali machache.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi, kama unakumbuka uliulizwa swali na Wakili Nashon Nkungu, kuhusiana na OC Forensic kukaa na exhibit na kuviandaa kwa ajili ya uchunguzi, ukajibu siyo sahihi kwamba OC Forensic ndiye anakaa na exhibit. Fafanua sasa.

SHAHIDI: Niliieleza Mahakama kwamba siyo sawa kwamba OC Forensic anakaa na vielelezo baada ya kukamatwa, badala yake vielelezo vinakaa kwa mpelelezi aliyekamata na baada ya hapo vitaandakiwa barua kwenda kwa OC Forensic.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa kuhusiana na watuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu kwamba muda gani walianza kuwa na guilty mind, ukasema ni pale walipokuubali kushawishiwa.

SHAHIDI: Mtuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu hawakuwa na taarifa kuhusu njama za mtuhumiwa wa nne. Mara tu baada ya kukutana mtuhumiwa namba nne ndipo walishawishika kuacha kutoa taarifa na kuamua kushiriki katika vitendo vya uhalifu, hali ambayo ilipelekea wao kukamatwa huko Moshi mtuhumiwa wa pili akiwa na silaha. Walipo hojiwa wakakiri kula njama hizo na kukubali kufanya vitendo vya uhalifu ikiwapo tukio la kumdhuru Lengai Ole Sabaya ambapo walikamatwa wakiwa katika utejelezaji wa tukio la namna hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali pia kuhusu uhamisho wako, ukajibu kuwa si kweli kwamba timing ya uhamisho wako Ilikuwa ni ya kimkakati.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba nilihamishwa kwa uhamisho wa kawaida mwezi Januari 2020.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na namna Afande DCI alivyo na maslahi binafsi ukasema si kweli.

SHAHIDI: Si kweli kwamba ana maslahi binafsi. Afande DCI alipokea taarifa kutoka kwa mtu mwingine. Si Kweli kwamba alikuwa ana maslahi binafsi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu register ya 251/2021 ukasema register hizo muhimu katika utunzaji wa vielelezo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ninachokumbuka mimi ni umuhimu wa utunzaji wa register vituo vya polisi.

JAJI: Lakini hapakuwa na neno vituo vya polisi. Hilo neno vituo liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sasa mtu akisema polisi anamaanisha nini? Tutakuwa hatujaisaidia Mahakama yako na sababu ya re examination itakuwa haipo.

JAJI: Sina hakika kama shahidi alitafsiri vituo. Kuleta neni ‘vituo ni concept’ Mpya.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji tunaondoa neno ‘vituo’.

SHAHIDI: Niliposema register hizo ni muhimu kwa Polisi kwa sababu inasaidia kuonyesha kumbukumbu za vielelezo Hivyo, na inaonyesha aliyekabidhi na aliyekabidhiwa. Kama nilivyoeleza kwamba simu nilikabidhi kwa Koplo Charles na silaha kwa Sajenti Nuru.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali mengi kuhusiana na ile miamala, moja ya maeneo uliulizwa kila shillingi iliyotumwa. Katika majibu yako ukasema siyo lazima ku- trace kila shillingi bali ni knowledge ya mtumaji.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika shauri hili mtumaji wa fedha ambaye ni Freeman Mbowe alikuwa anatuma pesa kufadhili vitendo vya ugaidi.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji ya kwangu naomba niishie hapo niwaachie wenzangu.

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji naomba kwenda WASHROOM.

Inaonekana mawakili wa Serikali wanarushiana mpira wa nani aendelee kumfanyia shahidi re examination.

Shahidi amesharejea kizimbani.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatutakuwa na swali zaidi kwa shahidi namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Naomba kukomea hapo.

(Jaji anaandika huku mahakama ikiwa kimya).

JAJI: Shahidi tunakushukuru. Asante kwa ushahidi wako.

(Shahidi anashuka kutoka kizimbani).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, baada ya shahidi huyu namba 13, tumefanya assessment ya kesi yetu kwa maana ya ushahidi ambao umetolewa mpaka sasa. Ni maoni yetu kwamba tume- discharge burden ambayo tunatakiwa kisheria, hivyo tunaialika mahakama yako tukufu chini ya kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa ya 2019 uone kwamba washitakiwa wote wanne wana kesi ya kujibu. Hivyo taratibu za sheria zifuatwe ili shauri hili liweze kuendelea katika hatua zinazifuata za kuanza kujitetea. Baada ya kusema hayo tunaomba kufunga kesi yetu kwa upande wa Jamhuri. Asante Mheshimiwa Jaji.

JAJI: Kabla ya AMRI ya kufunga upande wa utetezi mna chochote cha kusema?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kuhusu amri ya kufunga hapa, hatuna cha kusema. Tutasema baada ya AMRI ya kufunga.

(Jaji anaendelea kuandika).

JAJI: Baada ya kusikia hoja Iliyoletwa na Bwana Kidando kutoka upande wa mashitaka, Mahakama inakubali ombi la kufunga kesi upande wa mashitaka. Natoa AMRI.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kwa Mahakama haizungumzii haya maombi tunayoyaomba, bali baada ya kufunga upande wa mashitaka, basi upande wa utetezi wanapata nafasi ya kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’. Na kama Mahakama itatukubalia kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’, tunaomba maombi madogo mawili

MOJA:
Tunaomba Mahakama hii tukufu ikipendezwa tunaomba tunapatiwe mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo mpaka sasa.

MBILI:
Mahakama ituruhusu tufanye submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’ kwa wasilisho la mdomo. Tupo tayari kwa tarehe yoyote ambayo Mahakama itatupangia baada ya kutupatia nyaraka.

JAJI: Kwanini mnataka submission mfanye kwa wasilisho la mdomo na si kwa maandishi?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji. Tulijadili siku nyingi sana kwamba kufanya wasilisho la mdomo kutasaidia tuwe more focused na itakuwa faida kwetu.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji samahani. Sijajua kwa hatua hii Wakili Peter Kibatala anaweza kusemea washitakiwa wote?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji haina shida. Nimeongea kwa niaba ya jopo. Ila kama mtaamua kuwa kila mmoja aulizwe basi haina shida. Itachukua dakika 10 kufikia malengo yaleyale.

JAJI: Nitauliza kila mmoja.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji nimesikia upande wa mashitaka. Sisi hatuna pingamizi kwa ajili ya kufunga ushahidi wao. Na mheshimiwa Jaji tunaomba ikupendeze mawasilisho ya ‘NO CASE TO ANSWER’ tutafanye kwa njia ya mdomo.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji, pia tunaomba tupatiwe mwenendo wa kesi na kama itabidi na vielelezo. Ni hayo kwa niaba ya mshitakiwa wa kwanza.

John MALLYA: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa pili tumesikia kufungwa kwa kesi ya Jamhuri na hatuna pingamizi. Naona mkono wakili wa mshtakiwa wa nne na mshitakiwa wa kwanza. Na ombi lao la kufanya wasilisho la ‘NO CASE TO ANSWER’ tufanye kwa njia ya mdogo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa tatu pia hatuna pingamizi kwa upande wa Jamhuri kufunga kesi yao. Niungane na mawakili wa upande wa utetezi kwamba tuweze kupewa mwenendo wa kesi na kufanya wasilisho letu kwa njia ya mMdomo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

(Mahakama imekaa kimya huku Jaji akiandika).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji wakati tunaiomba Mahakama kwenye kifungu cha 41, tuliridhia kwa sababu mahususi kuwa Mahakama inaweza kufanya maamuzi hayo. Tunaporejea kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, tulikuwa aware na kifungu cha 293(1) cha CPA kwa mawakili wa utetezi kwa mazingira ambayo wameomba hapa Mahakamani. Hivyo Mheshimiwa Jaji, katika kuwasilisha hoja yetu hapo, na kama utaona inafaa kufanya hivyo kwa wasilisho basi tunaomba tufanye kwa njia ya maandishi na tuweze kuziwasilisha hapa Mahakamani. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Lakini pia Mheshimiwa Jaji tulikuwa tunahangakia katika kifungu cha hoja ya kwanza cha 41 trial hii imechukua muda mrefu. Hatujajua kuwa nyaraka za mwenendo wa kesi zitachukua muda gani ukizingatia umebakia muda machache kuhusu usilikizwaji wa shauri hili.

JAJI: Mpaka leo Karani wangu amechapa kurasa 1,400 za kesi hii. Sijajua itakuwa imebakia kurasa ngapi. Nafikiri jana na leo atakuwa amefikisha kurasa kama 1,500.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, tulikuwa tunawashawishi wenzetu tukaongee ofisini kwako.

JAJI: Nyiye mnaonaje?

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi la kuteta faragha ofisini kwako.

JAJI: Sawa.
[2/15, 15:06] William Shao: Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama

Jaji ameshaingia katika chumba cha mahakama. Ni saa 8:19 alasiri. Kesi inatajwa tena. Ni kesi namba 16 ya Jamhuri dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji kwa upande wa Jamhuri quorum iko kama ilivyokuwa mwanzoni kabla ya kuahirisha shauri hili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji na sisi pia quorum yetu iko kama ilivyokuwa kabla ya kwenda break. Tupo tayari kuendelea.

JAJI: Karibuni tuendelee.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na vile vituo vya mafuta ulivyokwenda kuvitembelea kwa maana ya Big Bon Kariakoo, Puma ya Sinza na Puma ya Kilwa Road. Sasa uliulizwa swali kuhusu details ambazo umezitoa Mahakamani, ukasema umezitoa kwa maana ulifahamu maana ya details. Ukaulizwa details za plot namba, mmiliki na makutano ya barabara ukasema siyo lazima ziwepo katika maelezo yako.

SHAHIDI: Ndiyo. Nilisema kwamba si lazima kwa sababu mimi nimekuja Mahakamani. Nimeapa na nilieleza maelezo yangu.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa kama ulijibu swali kwamba hukuweka hizo details lakini details hizo umetoa hapa Mahakamani. Kwanini umetoa details Mahakamani na hukuweka kwenye maelezo yako?

SHAHIDI: Ni ili Mahakama iweze kuelewa zaidi ni maeneo gani yaliyo kuwa yamepangwa kufanyiwa vitendo vya uhalifu.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kwa mara nyingine tena tupatiwe kielelezo namba 1 na kielelezo namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusiana na mtu mmoja anaitwa Justine Kaaya kuhusu kushiriki vikao vya kigaidi. Ukasema ni kweli alishiriki bila yeye kufahamu lengo la kikao ila mshitakiwa alifahamu lengo la Kikao. Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba wakati mshitakiwa wa nne kuomba majina ya watu wanaofuatana na Ole Sabaya, alikuwa anajua lengo la kupata vitu hivyo ni kufanya vitendo vya kigaidi. Wakati Kaaya anatoa vitu hivyo hakujua lengo la mshitakiwa namba nne ni lipi.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa na Wakili Nashon Nkungu kama ni kosa kama ilivyojitokeza kwa Luteni Dennis Urio kumtafutia mtu watu wa kufanya vitendo vya ugaidi. Ukasema inategemea. Elezea hapo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba haitakuwa kosa kama utakuwa unamtafutia huyo mtu kwa lengo la kusaidia vyombo husika.

Wakili Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji. Nilichouliza ni kama lilikuwa ni kosa kwa shahidi Denis Urio kukubali mpango wa ugaidi na si kwenda kufuta.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji na mimi ndicho nilichouliza kama ni kosa au siyo kosa kwa Denis Urio kukubali kwenda kumtafutia watu wa kwenda kwa mshitakiwa wa nne wale watu.

SHAHIDI: Niliposema inategemea inaweza kuwa kosa au si kosa nilikuwa namaanisha kuwa kama atatafuta watu hao kwa lengo la kuzia uhalifu na kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vya Ulinzi haitakuwa kosa, na uhalifu huo umezuiwa kwa walengwa kukamatwa na kufikishiwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Umeulizwa maswali kadhaa kuhusiana na taarifa aliyotoa Luteni Dennis Urio kwa DCI kwamba awe anatoa taarifa kwa Kingai, na Dennis Urio alitoa taarifa kwa Kingai kwamba tarehe 18 Julai mpaka tarehe 4 Agosti 2020, ukasema hakukuwa na ufutailiaji bado. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilimaanisha kwamba taarifa ambazo Luteni Dennis Urio alipewa na mshitakiwa wa nne alikuwa bado hajaanza kufanyia kazi. Mpaka tarehe nne alipoanza kuwasiliana na mtuhumiwa namba moja. Na wakati wanawasiliana nao…

WAKILI WA SERIKALI: Bado hujaulizwa swali.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa swali kuhusiana na hati ya makabidhiano baina yako na Dennis Urio tarehe 11 Agosti 2020. Je, ile fomu ilivyo ulionyeshwa hapa ukasema fomu ile haionyeshi kama Dennis Urio ni shahidi.

SHAHIDI: Nilieleza hivyo kwa sababu fomu ile huwa tunatumia askari tunapokabidhiana vielelezo. Nilitumia fomu hiyo kwa Luten Dennis Urio kwa sababu yeye ni shahidi. Niliweza kusaini katika fomu hiyo na yeye akasaini.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusu ile Polisi fomu namba 145 ambayo ilikuwa na vielelezo namba 28 mpaka 35 na kuhusu vielelezo vilivyokamatwa kwa mshitakiwa wa kwanza. Kuna baadhi vinaonyesha kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam au Police Central Dar es Salaam.

SHAHIDI: Fomu hizo zinajazwa kuonyesha jalada la kesi na kituo ambacho jalada hilo limefunguliwa.

Wakili John MALLYA: Objection! Mheshimiwa Jaji napinga hilo swali. Mimi ndiye niliyeuliza fact kwamba linajazwa na linafunguliwa. It’s a new fact ambayo ita- invite further cross examination.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji. Kwanza pingamizi lake halina mashiko. Kwanza ingekuwa sawa kama nauliza kuhusiana na mshitakiwa wa kwanza na wa tatu. Aliulizwa simu za mshitakiwa wa kwanza alipokea akiwa wapi akasema akiwa Central, akauliza kama aliandika mwenyewe akasema hapana. Hapa chini shahidi alisema hawezi kuwasemea Kingai wala Goodluck walijazia wapi. Sisi Mheshimiwa Jaji tunaendelea kusisitiza kuwa swali letu ni valid.

JAJI: Jibu ni nini?

SHAHIDI: Fomu namba 145 unajaza sehemu ya station na namba ya jalada. Kwa sehemu ya station nimejaza Police Central Station na jalada ni CD/IR/2097/2020.

JAJI: Sasa suala la Malya ni kwamba anaposema hivyo anatoa explanations mpya kwa sababu yeye alijaza fomu za Dennis Urio. Kwa hiyo alileta maelezo kuhusiana na hao ambao hajajaza yeye. Inaleta shida kidogo.

WAKILI WA SERIKALI: Sawa Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Inspekta Swila uliulizwa hapa maswali kuhusiana na vifaa vya mshitakiwa wa nne ambavo ni simu na computer kadhaa, ukasema kwamba ulipeleka katika maabara ya uchunguzi, na siku ile ambayo ulianza kutoa ushahidi wako ndiyo uchunguzi wake ulikuwa umekamilika.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba upelelezi wa shauri hili umekamilika tangu tarehe 18 Julai 2021. Kuhusu tarehe ya juzi kuhusu uchunguzi ilikuwa ni kuhusu uchunguzi wa ziada wa vielelezo vya mshitakiwa wa nne ambao ulikuwa unafanywa na maabara ya uchunguzi ya makosa ya mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa kati ya kipindi cha tarehe 14 Julai 2020 mpaka Agosti 5, 2020 kama uhalifu ulikuwa umeshatendeka. Ukasema inategemea na mpango wa uhalifu wenyewe.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kuwa kama kikundi mipango yake ya kutenda uhalifu itakuwa imekamilika basi uhalifu utafanyika, lakini kama kikundi haijakamilisha mipango yake yenyewe ya kutenda uhalifu basi uhalifu hauwezi kutendeka.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Inspekta Swila uliulizwa pia maswali kuhusiana na yale maombi ya uchunguzi wa kisayansi kwenda Airtel, kuhusiana na Khalfani Bwire na Freeman Mbowe pamoja na Dennis Urio, namba zote tatu zilioombewa taarifa, lakini taarifa zikaja za Dennis Urio na Freeman Mbowe lakini taarifa ya Khalfani Bwire haipo. Ukasema ipo katika taarifa ya Mbowe.

SHAHIDI: Katika uchunguzi wa miamala ya Freeman Mbowe palikuwa pia pana taarifa ya uchunguzi wa miamala ya Khalfani Bwire katika miamala ya Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hukusiana na taarifa iliyopo katika kielelezo namba 26 na maelezo ya Dennis Urio. Ulipoulizwa kuhusiana na kilichopo ukasema hakutakuwa na utofauti wa maudhui. Je, ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha ni ujumbe wa maneno uliopo katika vielelezo hivyo kwani unafanywa na mtumaji na mtumiwaji. Inaonekana mwisho katika taarifa iliyoandaliwa na maabara ya uchunguzi Kitengo cha Makosa ya Mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu upokelewaji wa taarifa kutoka kwa Dennis Urio na ukathibitisha aliyepokea taarifa ni DCI wakati huo palikuwa na Deputy DCI Charles Kenyela Ukaulizwa kama mazingira yake si alitakiwa amuachie Deputy DCI kuongozwa Upelelezi? Ukasema si kweli.

SHAHIDI: Niliposema kwamba Afande DCI hakupaswa kumuachia Deputy DCI kuendelea na upelelezi wa sshauri hilo kwa sababu taarifa za uhalifu zilitoka upande mwingine ambapo zilipokelewa na Afande DCI.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali kuhusu taarifa ya jalada la uchunguzi, ukasema kilichokuongoza ni taarifa alizokuwanazo Afande Boazi. Ukaulizwa kuhusu material ya kutosha kufungua jalada ukasema ulikuwa nayo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha taarifa ambayo ilikuwa imeandikwa na Afande Ramadhan Kingai niliweza kupokea na kuifanyia kazi taarifa hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu taarifa iliyotoka kwa DCI kuja kwako kwamba ilikuwa ni hearsay ukasema NDIYO. Ulikuwa na maana gani?

SHAHIDI: Askari anayepokea taarifa anakuwa anafuata moja kwa moja kutoka kwenye chanzo. Hiyo haizuii kufungua jalada.

WAKILI WA SERIKALI: Licha ya kuwa mpokeaji wa taarifa wa kwanza, uliulizwa pia kuhusu ni lini hasa ulichukua maelezo yake tarehe 4 Oktoba 2020. Ukaulizwa kwanini kesi hii isichukuliwe kuwa ni ya kutungwa.

SHAHIDI: Siyo ya kutunga kwa sababu taarifa ilitolewa, watuhumiwa wakakamatwa na hatimaye wakafikishwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kwamba wengine wanasema ni kulipua vituo vya mafuta na wengine wanasema kuchoma masoko katika maeneo ya mkusanyiko, ukasema kulipua na kuchoma ni kitu tofauti na baadaye ukasema kulipua na kuchoma ni terminology. Ulikuwa unamaanisha nini?

SHAHIDI: Ni terminology tu. Watu wanashindwa kutofautisha lakini haiondoi lile kosa la kutenda vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na kielelezo namba nne na namba tano kwa maana ya maganda mawili ya risasi katika kielelezi namba 4 na kielelezo namba 5 ni kielelezo cha risasi. Ukaulizwa kuhusu kutofautiana moja inaitwa Luger na nyingine jina tofauti. Ukasema kwa upande wa risasi ni tofauti. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha risasi si muhimu kuwa na utambulisho. Hazina utambulisho ambao ni tofauti.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji napinga kabisa majibu hayo. Kwamba risasi hazina utambulisho tofauti..

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sisi tulisikia hilo. Sijui kama upande kinzani walisikia hilo. Mheshimiwa Jaji naomba kuendelea na swali lingine.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa swali kuhusiana na Justin Elia Kaaya. Ukaulizwa kama kuna mfanano wowote kati ya maelezo akiwa mtuhumiwa na akiwa shahidi. Wewe ukasema hayawezi kufanana kati ya onyo na ushahidi, isipokuwa yale maelezo ya msingi.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha maelezo ya kwanza yalikuwa yanaelezea kosa wakati haya ya pili ni shahidi na hayaelezei kosa lolote.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali katika kielelezo namba 13 ambayo ni maelezo ya onyo ya mshitakiwa Mohammed Ling’wenya, kwamba katika maelezo yake, hasa ile nia ya kumdhuru Lengai Ole Sabaya ilikuwa siyo kuleta taharuki ila kushambulia viongozi wa Serikali.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika maelezo yake hakusema kwa nia ya kuleta taharuki, lakini kwa malengo yaliyokusidiwa na ambayo shahidi alieleza kutoka kwa mshitakiwa wa nne vitendo vya kumdhuru kiongozi ni vitendo vya kuondoa amani na kufanya nchi isitawalike.

KIBATALA: Objection! Mheshimiwa Jaji samahani. Neno kuondoa amani tulishawahi kutaja hapa Mahakamani?

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji neno kunaondoa amani tunalitoa.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila kuna maswali kadhaa hapa uliulizwa hasa kuhusu mshitakiwa wa pili na wa tatu pale Morogoro kuhusiana na suala la kwenda kwa Freeman Mbowe. Katika maelezo yao ya onyo ya P1 na P13 hawa wote wanasema walipoondoka walikwenda Moshi wakati maelezo mengine ya Dennis Urio wanasema walipoondoa walikwenda Dar es Salaam. Uliulizwa kama kuna mgongano ukasema HAKUNA.

SHAHIDI: Ni kwa sababu maelezo yote lengo ni kwenda kukutana na Freeman Mbowe. Maelezo hayana mgongano wowote kwa sababu mtu ambaye walitakiwa kukutana naye walikutana naye Moshi kama wanavyoeleza katika maelezo yao.

Shaidi: Ni wazi walikutana na mshitakiwa wa kwanza.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno WAZI liondoke. Ni OPINION zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji ni sawa liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na kiwango cha pesa ambacho kila mshitakiwa anadai katika maelezo yake ya onyo alipewa na Luten Dennis Urio, ambapoo Adam Kasekwa anasema walipewa shilingi 87,000 na Urio anasema aliwapa shilingi 199,000. Wakati huo Mohammed Ling’wenya anasema ni shilingi 195,000. Ukaulizwa viwango hivyo vinafanana? Ukasema vinafanana. Kwanini?

SHAHIDI: Kwa sababu wote walipokea pesa kwa Luteni Dennis Urio na kila mtuhumiwa alitoa maelezo yake kwa hiari yake.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kuhusiana na maelezo aliyotoa Adam Kasekwa hasa pale alipotoka Morogoro akanunua shati Chalinze. Ukaulizwa kama shati lile ni ugaidi, ukasema huwezi kutengenisha na ugaidi.

SHAHIDI: Ni kwa sababu pesa ilitumwa na mtu ambaye alikuwa anajua nia ya kuwaleta watu hao kwake ni kwa nia ya kutekeleza vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali hapa kuhusiana na maelezo yale uliyomwandika Dennis Urio kama kuna sehemu alikuambia Kuwa amemwambia Freeman Mbowe kuwa asitumie namba yake bali atumie ya wakala au vijana wake. Wewe ukasema kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya kumweka karibu. Ukasema sehemu hiyo kwenye maelezo haipo.

SHAHIDI: Nilipoeleza hivyo nilikuwa namaanisha kuwa kumzuia asitumie namba yake ya simu ilikuwa ni sehemu ya kukusanya taarifa kutoka kwa mtuhumiwa wa nne.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa swali kuhusiana na kielelezo namba P1 ambayo ni maelezo ya Adam Kasekwa ambayo ni IMEI namba kwa kulinganisha na kielelezo namba 23 ambayo ni ripoti kutoka uchunguzi wa kisayansi. Lakini ikawa na utofauti kwamba katika maelezo y aonyo palikuwa na utofauti wa namba tatu. Wewe ulisema katika maelezo ya onyo kipo ila kwenye cyber ripoti haipo ila ukasema haimaanishi kitu tofauti.

SHAHIDI: Nilimaanisha simu hiyo IMEI ya kwanza ipo katika maelezo lakini kwenye IMEI ya pili ndiyo kuna utofauti. Kwa hiyo kukosea kwa hiyo ya pili haimaanishi ni kitu cha pili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno kukosewa lisiingie. Ni ushahidi mpya anataka kuingiza kwa mlango wa nyuma.

JAJI: Maneno halisi ni kukosekana.

WAKILI WA SERIKALI: Ndiyo Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila jana ulionyeshwa maelezo ya onyo y aAdam Kasekwa ambapo yeye anadai kukamatwa Rau Madukani saa tano asubuhi wakati mtuhumiwa mwenzake anazungumzia kukamatwa saa saba mchana. Ukaulizwa kama huu utofauti uliufanyia kazi. Ukasema kila mmoja alisema kwa ufahamu wake.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba watuhumiwa hawa walitoa maelezo kwa hiari yao. Kwa hiyo kutofautiana kwa muda ni kwa kadri mtu alipokuwa anajaza.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kiwango cha pesa cha shilingi 195,000 ambacho Luteni Dennis Urio aliwapatia kwa namna mbili. Sasa washitakiwa wanaongeala kupewa pesa kiwango hicho? Wewe ukasema ni hali ya kawaida. Eleza kwanini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba kila mmoja alitoa maelezo kwa kadri ya ufahamu wake na kumbukumbu zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapa. Wenzangu pia wataendelea.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji nina maswali machache.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi, kama unakumbuka uliulizwa swali na Wakili Nashon Nkungu, kuhusiana na OC Forensic kukaa na exhibit na kuviandaa kwa ajili ya uchunguzi, ukajibu siyo sahihi kwamba OC Forensic ndiye anakaa na exhibit. Fafanua sasa.

SHAHIDI: Niliieleza Mahakama kwamba siyo sawa kwamba OC Forensic anakaa na vielelezo baada ya kukamatwa, badala yake vielelezo vinakaa kwa mpelelezi aliyekamata na baada ya hapo vitaandakiwa barua kwenda kwa OC Forensic.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa kuhusiana na watuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu kwamba muda gani walianza kuwa na guilty mind, ukasema ni pale walipokuubali kushawishiwa.

SHAHIDI: Mtuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu hawakuwa na taarifa kuhusu njama za mtuhumiwa wa nne. Mara tu baada ya kukutana mtuhumiwa namba nne ndipo walishawishika kuacha kutoa taarifa na kuamua kushiriki katika vitendo vya uhalifu, hali ambayo ilipelekea wao kukamatwa huko Moshi mtuhumiwa wa pili akiwa na silaha. Walipo hojiwa wakakiri kula njama hizo na kukubali kufanya vitendo vya uhalifu ikiwapo tukio la kumdhuru Lengai Ole Sabaya ambapo walikamatwa wakiwa katika utejelezaji wa tukio la namna hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali pia kuhusu uhamisho wako, ukajibu kuwa si kweli kwamba timing ya uhamisho wako Ilikuwa ni ya kimkakati.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba nilihamishwa kwa uhamisho wa kawaida mwezi Januari 2020.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na namna Afande DCI alivyo na maslahi binafsi ukasema si kweli.

SHAHIDI: Si kweli kwamba ana maslahi binafsi. Afande DCI alipokea taarifa kutoka kwa mtu mwingine. Si Kweli kwamba alikuwa ana maslahi binafsi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu register ya 251/2021 ukasema register hizo muhimu katika utunzaji wa vielelezo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ninachokumbuka mimi ni umuhimu wa utunzaji wa register vituo vya polisi.

JAJI: Lakini hapakuwa na neno vituo vya polisi. Hilo neno vituo liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sasa mtu akisema polisi anamaanisha nini? Tutakuwa hatujaisaidia Mahakama yako na sababu ya re examination itakuwa haipo.

JAJI: Sina hakika kama shahidi alitafsiri vituo. Kuleta neni ‘vituo ni concept’ Mpya.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji tunaondoa neno ‘vituo’.

SHAHIDI: Niliposema register hizo ni muhimu kwa Polisi kwa sababu inasaidia kuonyesha kumbukumbu za vielelezo Hivyo, na inaonyesha aliyekabidhi na aliyekabidhiwa. Kama nilivyoeleza kwamba simu nilikabidhi kwa Koplo Charles na silaha kwa Sajenti Nuru.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali mengi kuhusiana na ile miamala, moja ya maeneo uliulizwa kila shillingi iliyotumwa. Katika majibu yako ukasema siyo lazima ku- trace kila shillingi bali ni knowledge ya mtumaji.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika shauri hili mtumaji wa fedha ambaye ni Freeman Mbowe alikuwa anatuma pesa kufadhili vitendo vya ugaidi.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji ya kwangu naomba niishie hapo niwaachie wenzangu.

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji naomba kwenda WASHROOM.

Inaonekana mawakili wa Serikali wanarushiana mpira wa nani aendelee kumfanyia shahidi re examination.

Shahidi amesharejea kizimbani.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatutakuwa na swali zaidi kwa shahidi namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Naomba kukomea hapo.

(Jaji anaandika huku mahakama ikiwa kimya).

JAJI: Shahidi tunakushukuru. Asante kwa ushahidi wako.

(Shahidi anashuka kutoka kizimbani).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, baada ya shahidi huyu namba 13, tumefanya assessment ya kesi yetu kwa maana ya ushahidi ambao umetolewa mpaka sasa. Ni maoni yetu kwamba tume- discharge burden ambayo tunatakiwa kisheria, hivyo tunaialika mahakama yako tukufu chini ya kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa ya 2019 uone kwamba washitakiwa wote wanne wana kesi ya kujibu. Hivyo taratibu za sheria zifuatwe ili shauri hili liweze kuendelea katika hatua zinazifuata za kuanza kujitetea. Baada ya kusema hayo tunaomba kufunga kesi yetu kwa upande wa Jamhuri. Asante Mheshimiwa Jaji.

JAJI: Kabla ya AMRI ya kufunga upande wa utetezi mna chochote cha kusema?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kuhusu amri ya kufunga hapa, hatuna cha kusema. Tutasema baada ya AMRI ya kufunga.

(Jaji anaendelea kuandika).

JAJI: Baada ya kusikia hoja Iliyoletwa na Bwana Kidando kutoka upande wa mashitaka, Mahakama inakubali ombi la kufunga kesi upande wa mashitaka. Natoa AMRI.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kwa Mahakama haizungumzii haya maombi tunayoyaomba, bali baada ya kufunga upande wa mashitaka, basi upande wa utetezi wanapata nafasi ya kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’. Na kama Mahakama itatukubalia kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’, tunaomba maombi madogo mawili

Moja:
Tunaomba Mahakama hii tukufu ikipendezwa tunaomba tunapatiwe mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo mpaka sasa.

Mbili:
Mahakama ituruhusu tufanye submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’ kwa wasilisho la mdomo. Tupo tayari kwa tarehe yoyote ambayo Mahakama itatupangia baada ya kutupatia nyaraka.

JAJI: Kwanini mnataka submission mfanye kwa wasilisho la mdomo na si kwa maandishi?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji. Tulijadili siku nyingi sana kwamba kufanya wasilisho la mdomo kutasaidia tuwe more focused na itakuwa faida kwetu.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji samahani. Sijajua kwa hatua hii Wakili Peter Kibatala anaweza kusemea washitakiwa wote?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji haina shida. Nimeongea kwa niaba ya jopo. Ila kama mtaamua kuwa kila mmoja aulizwe basi haina shida. Itachukua dakika 10 kufikia malengo yaleyale.

JAJI: Nitauliza kila mmoja.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji nimesikia upande wa mashitaka. Sisi hatuna pingamizi kwa ajili ya kufunga ushahidi wao. Na mheshimiwa Jaji tunaomba ikupendeze mawasilisho ya ‘NO CASE TO ANSWER’ tutafanye kwa njia ya mdomo.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji, pia tunaomba tupatiwe mwenendo wa kesi na kama itabidi na vielelezo. Ni hayo kwa niaba ya mshitakiwa wa kwanza.

John MALLYA: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa pili tumesikia kufungwa kwa kesi ya Jamhuri na hatuna pingamizi. Naona mkono wakili wa mshtakiwa wa nne na mshitakiwa wa kwanza. Na ombi lao la kufanya wasilisho la ‘NO CASE TO ANSWER’ tufanye kwa njia ya mdogo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa tatu pia hatuna pingamizi kwa upande wa Jamhuri kufunga kesi yao. Niungane na mawakili wa upande wa utetezi kwamba tuweze kupewa mwenendo wa kesi na kufanya wasilisho letu kwa njia ya mMdomo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

(Mahakama imekaa kimya huku Jaji akiandika).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji wakati tunaiomba Mahakama kwenye kifungu cha 41, tuliridhia kwa sababu mahususi kuwa Mahakama inaweza kufanya maamuzi hayo. Tunaporejea kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, tulikuwa aware na kifungu cha 293(1) cha CPA kwa mawakili wa utetezi kwa mazingira ambayo wameomba hapa Mahakamani. Hivyo Mheshimiwa Jaji, katika kuwasilisha hoja yetu hapo, na kama utaona inafaa kufanya hivyo kwa wasilisho basi tunaomba tufanye kwa njia ya maandishi na tuweze kuziwasilisha hapa Mahakamani. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Lakini pia Mheshimiwa Jaji tulikuwa tunahangakia katika kifungu cha hoja ya kwanza cha 41 trial hii imechukua muda mrefu. Hatujajua kuwa nyaraka za mwenendo wa kesi zitachukua muda gani ukizingatia umebakia muda machache kuhusu usilikizwaji wa shauri hili.

JAJI: Mpaka leo Karani wangu amechapa kurasa 1,400 za kesi hii. Sijajua itakuwa imebakia kurasa ngapi. Nafikiri jana na leo atakuwa amefikisha kurasa kama 1,500.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, tulikuwa tunawashawishi wenzetu tukaongee ofisini kwako.

JAJI: Nyiye mnaonaje?

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi la kuteta faragha ofisini kwako.

JAJI: Sawa.

Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama.

Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama

Jaji ameshaingia katika chumba cha mahakama. Ni saa 8:19 alasiri. Kesi inatajwa tena. Ni kesi namba 16 ya Jamhuri dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji kwa upande wa Jamhuri quorum iko kama ilivyokuwa mwanzoni kabla ya kuahirisha shauri hili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji na sisi pia quorum yetu iko kama ilivyokuwa kabla ya kwenda break. Tupo tayari kuendelea.

JAJI: Karibuni tuendelee.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na vile vituo vya mafuta ulivyokwenda kuvitembelea kwa maana ya Big Bon Kariakoo, Puma ya Sinza na Puma ya Kilwa Road. Sasa uliulizwa swali kuhusu details ambazo umezitoa Mahakamani, ukasema umezitoa kwa maana ulifahamu maana ya details. Ukaulizwa details za plot namba, mmiliki na makutano ya barabara ukasema siyo lazima ziwepo katika maelezo yako.

SHAHIDI: Ndiyo. Nilisema kwamba si lazima kwa sababu mimi nimekuja Mahakamani. Nimeapa na nilieleza maelezo yangu.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa kama ulijibu swali kwamba hukuweka hizo details lakini details hizo umetoa hapa Mahakamani. Kwanini umetoa details Mahakamani na hukuweka kwenye maelezo yako?

SHAHIDI: Ni ili Mahakama iweze kuelewa zaidi ni maeneo gani yaliyo kuwa yamepangwa kufanyiwa vitendo vya uhalifu.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kwa mara nyingine tena tupatiwe kielelezo namba 1 na kielelezo namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusiana na mtu mmoja anaitwa Justine Kaaya kuhusu kushiriki vikao vya kigaidi. Ukasema ni kweli alishiriki bila yeye kufahamu lengo la kikao ila mshitakiwa alifahamu lengo la Kikao. Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba wakati mshitakiwa wa nne kuomba majina ya watu wanaofuatana na Ole Sabaya, alikuwa anajua lengo la kupata vitu hivyo ni kufanya vitendo vya kigaidi. Wakati Kaaya anatoa vitu hivyo hakujua lengo la mshitakiwa namba nne ni lipi.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa na Wakili Nashon Nkungu kama ni kosa kama ilivyojitokeza kwa Luteni Dennis Urio kumtafutia mtu watu wa kufanya vitendo vya ugaidi. Ukasema inategemea. Elezea hapo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba haitakuwa kosa kama utakuwa unamtafutia huyo mtu kwa lengo la kusaidia vyombo husika.

Wakili Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji. Nilichouliza ni kama lilikuwa ni kosa kwa shahidi Denis Urio kukubali mpango wa ugaidi na si kwenda kufuta.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji na mimi ndicho nilichouliza kama ni kosa au siyo kosa kwa Denis Urio kukubali kwenda kumtafutia watu wa kwenda kwa mshitakiwa wa nne wale watu.

SHAHIDI: Niliposema inategemea inaweza kuwa kosa au si kosa nilikuwa namaanisha kuwa kama atatafuta watu hao kwa lengo la kuzia uhalifu na kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vya Ulinzi haitakuwa kosa, na uhalifu huo umezuiwa kwa walengwa kukamatwa na kufikishiwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Umeulizwa maswali kadhaa kuhusiana na taarifa aliyotoa Luteni Dennis Urio kwa DCI kwamba awe anatoa taarifa kwa Kingai, na Dennis Urio alitoa taarifa kwa Kingai kwamba tarehe 18 Julai mpaka tarehe 4 Agosti 2020, ukasema hakukuwa na ufutailiaji bado. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilimaanisha kwamba taarifa ambazo Luteni Dennis Urio alipewa na mshitakiwa wa nne alikuwa bado hajaanza kufanyia kazi. Mpaka tarehe nne alipoanza kuwasiliana na mtuhumiwa namba moja. Na wakati wanawasiliana nao…

WAKILI WA SERIKALI: Bado hujaulizwa swali.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa swali kuhusiana na hati ya makabidhiano baina yako na Dennis Urio tarehe 11 Agosti 2020. Je, ile fomu ilivyo ulionyeshwa hapa ukasema fomu ile haionyeshi kama Dennis Urio ni shahidi.

SHAHIDI: Nilieleza hivyo kwa sababu fomu ile huwa tunatumia askari tunapokabidhiana vielelezo. Nilitumia fomu hiyo kwa Luten Dennis Urio kwa sababu yeye ni shahidi. Niliweza kusaini katika fomu hiyo na yeye akasaini.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusu ile Polisi fomu namba 145 ambayo ilikuwa na vielelezo namba 28 mpaka 35 na kuhusu vielelezo vilivyokamatwa kwa mshitakiwa wa kwanza. Kuna baadhi vinaonyesha kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam au Police Central Dar es Salaam.

SHAHIDI: Fomu hizo zinajazwa kuonyesha jalada la kesi na kituo ambacho jalada hilo limefunguliwa.

Wakili John MALLYA: Objection! Mheshimiwa Jaji napinga hilo swali. Mimi ndiye niliyeuliza fact kwamba linajazwa na linafunguliwa. It’s a new fact ambayo ita- invite further cross examination.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji. Kwanza pingamizi lake halina mashiko. Kwanza ingekuwa sawa kama nauliza kuhusiana na mshitakiwa wa kwanza na wa tatu. Aliulizwa simu za mshitakiwa wa kwanza alipokea akiwa wapi akasema akiwa Central, akauliza kama aliandika mwenyewe akasema hapana. Hapa chini shahidi alisema hawezi kuwasemea Kingai wala Goodluck walijazia wapi. Sisi Mheshimiwa Jaji tunaendelea kusisitiza kuwa swali letu ni valid.

JAJI: Jibu ni nini?

SHAHIDI: Fomu namba 145 unajaza sehemu ya station na namba ya jalada. Kwa sehemu ya station nimejaza Police Central Station na jalada ni CD/IR/2097/2020.

JAJI: Sasa suala la Malya ni kwamba anaposema hivyo anatoa explanations mpya kwa sababu yeye alijaza fomu za Dennis Urio. Kwa hiyo alileta maelezo kuhusiana na hao ambao hajajaza yeye. Inaleta shida kidogo.

WAKILI WA SERIKALI: Sawa Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Inspekta Swila uliulizwa hapa maswali kuhusiana na vifaa vya mshitakiwa wa nne ambavo ni simu na computer kadhaa, ukasema kwamba ulipeleka katika maabara ya uchunguzi, na siku ile ambayo ulianza kutoa ushahidi wako ndiyo uchunguzi wake ulikuwa umekamilika.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba upelelezi wa shauri hili umekamilika tangu tarehe 18 Julai 2021. Kuhusu tarehe ya juzi kuhusu uchunguzi ilikuwa ni kuhusu uchunguzi wa ziada wa vielelezo vya mshitakiwa wa nne ambao ulikuwa unafanywa na maabara ya uchunguzi ya makosa ya mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa kati ya kipindi cha tarehe 14 Julai 2020 mpaka Agosti 5, 2020 kama uhalifu ulikuwa umeshatendeka. Ukasema inategemea na mpango wa uhalifu wenyewe.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kuwa kama kikundi mipango yake ya kutenda uhalifu itakuwa imekamilika basi uhalifu utafanyika, lakini kama kikundi haijakamilisha mipango yake yenyewe ya kutenda uhalifu basi uhalifu hauwezi kutendeka.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Inspekta Swila uliulizwa pia maswali kuhusiana na yale maombi ya uchunguzi wa kisayansi kwenda Airtel, kuhusiana na Khalfani Bwire na Freeman Mbowe pamoja na Dennis Urio, namba zote tatu zilioombewa taarifa, lakini taarifa zikaja za Dennis Urio na Freeman Mbowe lakini taarifa ya Khalfani Bwire haipo. Ukasema ipo katika taarifa ya Mbowe.

SHAHIDI: Katika uchunguzi wa miamala ya Freeman Mbowe palikuwa pia pana taarifa ya uchunguzi wa miamala ya Khalfani Bwire katika miamala ya Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hukusiana na taarifa iliyopo katika kielelezo namba 26 na maelezo ya Dennis Urio. Ulipoulizwa kuhusiana na kilichopo ukasema hakutakuwa na utofauti wa maudhui. Je, ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha ni ujumbe wa maneno uliopo katika vielelezo hivyo kwani unafanywa na mtumaji na mtumiwaji. Inaonekana mwisho katika taarifa iliyoandaliwa na maabara ya uchunguzi Kitengo cha Makosa ya Mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu upokelewaji wa taarifa kutoka kwa Dennis Urio na ukathibitisha aliyepokea taarifa ni DCI wakati huo palikuwa na Deputy DCI Charles Kenyela Ukaulizwa kama mazingira yake si alitakiwa amuachie Deputy DCI kuongozwa Upelelezi? Ukasema si kweli.

SHAHIDI: Niliposema kwamba Afande DCI hakupaswa kumuachia Deputy DCI kuendelea na upelelezi wa sshauri hilo kwa sababu taarifa za uhalifu zilitoka upande mwingine ambapo zilipokelewa na Afande DCI.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali kuhusu taarifa ya jalada la uchunguzi, ukasema kilichokuongoza ni taarifa alizokuwanazo Afande Boazi. Ukaulizwa kuhusu material ya kutosha kufungua jalada ukasema ulikuwa nayo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha taarifa ambayo ilikuwa imeandikwa na Afande Ramadhan Kingai niliweza kupokea na kuifanyia kazi taarifa hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu taarifa iliyotoka kwa DCI kuja kwako kwamba ilikuwa ni hearsay ukasema NDIYO. Ulikuwa na maana gani?

SHAHIDI: Askari anayepokea taarifa anakuwa anafuata moja kwa moja kutoka kwenye chanzo. Hiyo haizuii kufungua jalada.

WAKILI WA SERIKALI: Licha ya kuwa mpokeaji wa taarifa wa kwanza, uliulizwa pia kuhusu ni lini hasa ulichukua maelezo yake tarehe 4 Oktoba 2020. Ukaulizwa kwanini kesi hii isichukuliwe kuwa ni ya kutungwa.

SHAHIDI: Siyo ya kutunga kwa sababu taarifa ilitolewa, watuhumiwa wakakamatwa na hatimaye wakafikishwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kwamba wengine wanasema ni kulipua vituo vya mafuta na wengine wanasema kuchoma masoko katika maeneo ya mkusanyiko, ukasema kulipua na kuchoma ni kitu tofauti na baadaye ukasema kulipua na kuchoma ni terminology. Ulikuwa unamaanisha nini?

SHAHIDI: Ni terminology tu. Watu wanashindwa kutofautisha lakini haiondoi lile kosa la kutenda vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na kielelezo namba nne na namba tano kwa maana ya maganda mawili ya risasi katika kielelezi namba 4 na kielelezo namba 5 ni kielelezo cha risasi. Ukaulizwa kuhusu kutofautiana moja inaitwa Luger na nyingine jina tofauti. Ukasema kwa upande wa risasi ni tofauti. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha risasi si muhimu kuwa na utambulisho. Hazina utambulisho ambao ni tofauti.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji napinga kabisa majibu hayo. Kwamba risasi hazina utambulisho tofauti..

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sisi tulisikia hilo. Sijui kama upande kinzani walisikia hilo. Mheshimiwa Jaji naomba kuendelea na swali lingine.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa swali kuhusiana na Justin Elia Kaaya. Ukaulizwa kama kuna mfanano wowote kati ya maelezo akiwa mtuhumiwa na akiwa shahidi. Wewe ukasema hayawezi kufanana kati ya onyo na ushahidi, isipokuwa yale maelezo ya msingi.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha maelezo ya kwanza yalikuwa yanaelezea kosa wakati haya ya pili ni shahidi na hayaelezei kosa lolote.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali katika kielelezo namba 13 ambayo ni maelezo ya onyo ya mshitakiwa Mohammed Ling’wenya, kwamba katika maelezo yake, hasa ile nia ya kumdhuru Lengai Ole Sabaya ilikuwa siyo kuleta taharuki ila kushambulia viongozi wa Serikali.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika maelezo yake hakusema kwa nia ya kuleta taharuki, lakini kwa malengo yaliyokusidiwa na ambayo shahidi alieleza kutoka kwa mshitakiwa wa nne vitendo vya kumdhuru kiongozi ni vitendo vya kuondoa amani na kufanya nchi isitawalike.

KIBATALA: Objection! Mheshimiwa Jaji samahani. Neno kuondoa amani tulishawahi kutaja hapa Mahakamani?

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji neno kunaondoa amani tunalitoa.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila kuna maswali kadhaa hapa uliulizwa hasa kuhusu mshitakiwa wa pili na wa tatu pale Morogoro kuhusiana na suala la kwenda kwa Freeman Mbowe. Katika maelezo yao ya onyo ya P1 na P13 hawa wote wanasema walipoondoka walikwenda Moshi wakati maelezo mengine ya Dennis Urio wanasema walipoondoa walikwenda Dar es Salaam. Uliulizwa kama kuna mgongano ukasema HAKUNA.

SHAHIDI: Ni kwa sababu maelezo yote lengo ni kwenda kukutana na Freeman Mbowe. Maelezo hayana mgongano wowote kwa sababu mtu ambaye walitakiwa kukutana naye walikutana naye Moshi kama wanavyoeleza katika maelezo yao.

Shaidi: Ni wazi walikutana na mshitakiwa wa kwanza.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno WAZI liondoke. Ni OPINION zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji ni sawa liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na kiwango cha pesa ambacho kila mshitakiwa anadai katika maelezo yake ya onyo alipewa na Luten Dennis Urio, ambapoo Adam Kasekwa anasema walipewa shilingi 87,000 na Urio anasema aliwapa shilingi 199,000. Wakati huo Mohammed Ling’wenya anasema ni shilingi 195,000. Ukaulizwa viwango hivyo vinafanana? Ukasema vinafanana. Kwanini?

SHAHIDI: Kwa sababu wote walipokea pesa kwa Luteni Dennis Urio na kila mtuhumiwa alitoa maelezo yake kwa hiari yake.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kuhusiana na maelezo aliyotoa Adam Kasekwa hasa pale alipotoka Morogoro akanunua shati Chalinze. Ukaulizwa kama shati lile ni ugaidi, ukasema huwezi kutengenisha na ugaidi.

SHAHIDI: Ni kwa sababu pesa ilitumwa na mtu ambaye alikuwa anajua nia ya kuwaleta watu hao kwake ni kwa nia ya kutekeleza vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali hapa kuhusiana na maelezo yale uliyomwandika Dennis Urio kama kuna sehemu alikuambia Kuwa amemwambia Freeman Mbowe kuwa asitumie namba yake bali atumie ya wakala au vijana wake. Wewe ukasema kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya kumweka karibu. Ukasema sehemu hiyo kwenye maelezo haipo.

SHAHIDI: Nilipoeleza hivyo nilikuwa namaanisha kuwa kumzuia asitumie namba yake ya simu ilikuwa ni sehemu ya kukusanya taarifa kutoka kwa mtuhumiwa wa nne.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa swali kuhusiana na kielelezo namba P1 ambayo ni maelezo ya Adam Kasekwa ambayo ni IMEI namba kwa kulinganisha na kielelezo namba 23 ambayo ni ripoti kutoka uchunguzi wa kisayansi. Lakini ikawa na utofauti kwamba katika maelezo y aonyo palikuwa na utofauti wa namba tatu. Wewe ulisema katika maelezo ya onyo kipo ila kwenye cyber ripoti haipo ila ukasema haimaanishi kitu tofauti.

SHAHIDI: Nilimaanisha simu hiyo IMEI ya kwanza ipo katika maelezo lakini kwenye IMEI ya pili ndiyo kuna utofauti. Kwa hiyo kukosea kwa hiyo ya pili haimaanishi ni kitu cha pili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno kukosewa lisiingie. Ni ushahidi mpya anataka kuingiza kwa mlango wa nyuma.

JAJI: Maneno halisi ni kukosekana.

WAKILI WA SERIKALI: Ndiyo Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila jana ulionyeshwa maelezo ya onyo y aAdam Kasekwa ambapo yeye anadai kukamatwa Rau Madukani saa tano asubuhi wakati mtuhumiwa mwenzake anazungumzia kukamatwa saa saba mchana. Ukaulizwa kama huu utofauti uliufanyia kazi. Ukasema kila mmoja alisema kwa ufahamu wake.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba watuhumiwa hawa walitoa maelezo kwa hiari yao. Kwa hiyo kutofautiana kwa muda ni kwa kadri mtu alipokuwa anajaza.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kiwango cha pesa cha shilingi 195,000 ambacho Luteni Dennis Urio aliwapatia kwa namna mbili. Sasa washitakiwa wanaongeala kupewa pesa kiwango hicho? Wewe ukasema ni hali ya kawaida. Eleza kwanini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba kila mmoja alitoa maelezo kwa kadri ya ufahamu wake na kumbukumbu zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapa. Wenzangu pia wataendelea.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji nina maswali machache.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi, kama unakumbuka uliulizwa swali na Wakili Nashon Nkungu, kuhusiana na OC Forensic kukaa na exhibit na kuviandaa kwa ajili ya uchunguzi, ukajibu siyo sahihi kwamba OC Forensic ndiye anakaa na exhibit. Fafanua sasa.

SHAHIDI: Niliieleza Mahakama kwamba siyo sawa kwamba OC Forensic anakaa na vielelezo baada ya kukamatwa, badala yake vielelezo vinakaa kwa mpelelezi aliyekamata na baada ya hapo vitaandakiwa barua kwenda kwa OC Forensic.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa kuhusiana na watuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu kwamba muda gani walianza kuwa na guilty mind, ukasema ni pale walipokuubali kushawishiwa.

SHAHIDI: Mtuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu hawakuwa na taarifa kuhusu njama za mtuhumiwa wa nne. Mara tu baada ya kukutana mtuhumiwa namba nne ndipo walishawishika kuacha kutoa taarifa na kuamua kushiriki katika vitendo vya uhalifu, hali ambayo ilipelekea wao kukamatwa huko Moshi mtuhumiwa wa pili akiwa na silaha. Walipo hojiwa wakakiri kula njama hizo na kukubali kufanya vitendo vya uhalifu ikiwapo tukio la kumdhuru Lengai Ole Sabaya ambapo walikamatwa wakiwa katika utejelezaji wa tukio la namna hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali pia kuhusu uhamisho wako, ukajibu kuwa si kweli kwamba timing ya uhamisho wako Ilikuwa ni ya kimkakati.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba nilihamishwa kwa uhamisho wa kawaida mwezi Januari 2020.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na namna Afande DCI alivyo na maslahi binafsi ukasema si kweli.

SHAHIDI: Si kweli kwamba ana maslahi binafsi. Afande DCI alipokea taarifa kutoka kwa mtu mwingine. Si Kweli kwamba alikuwa ana maslahi binafsi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu register ya 251/2021 ukasema register hizo muhimu katika utunzaji wa vielelezo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ninachokumbuka mimi ni umuhimu wa utunzaji wa register vituo vya polisi.

JAJI: Lakini hapakuwa na neno vituo vya polisi. Hilo neno vituo liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sasa mtu akisema polisi anamaanisha nini? Tutakuwa hatujaisaidia Mahakama yako na sababu ya re examination itakuwa haipo.

JAJI: Sina hakika kama shahidi alitafsiri vituo. Kuleta neni ‘vituo ni concept’ Mpya.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji tunaondoa neno ‘vituo’.

SHAHIDI: Niliposema register hizo ni muhimu kwa Polisi kwa sababu inasaidia kuonyesha kumbukumbu za vielelezo Hivyo, na inaonyesha aliyekabidhi na aliyekabidhiwa. Kama nilivyoeleza kwamba simu nilikabidhi kwa Koplo Charles na silaha kwa Sajenti Nuru.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali mengi kuhusiana na ile miamala, moja ya maeneo uliulizwa kila shillingi iliyotumwa. Katika majibu yako ukasema siyo lazima ku- trace kila shillingi bali ni knowledge ya mtumaji.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika shauri hili mtumaji wa fedha ambaye ni Freeman Mbowe alikuwa anatuma pesa kufadhili vitendo vya ugaidi.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji ya kwangu naomba niishie hapo niwaachie wenzangu.

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji naomba kwenda WASHROOM.

Inaonekana mawakili wa Serikali wanarushiana mpira wa nani aendelee kumfanyia shahidi re examination.

Shahidi amesharejea kizimbani.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatutakuwa na swali zaidi kwa shahidi namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Naomba kukomea hapo.

(Jaji anaandika huku mahakama ikiwa kimya).

JAJI: Shahidi tunakushukuru. Asante kwa ushahidi wako.

(Shahidi anashuka kutoka kizimbani).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, baada ya shahidi huyu namba 13, tumefanya assessment ya kesi yetu kwa maana ya ushahidi ambao umetolewa mpaka sasa. Ni maoni yetu kwamba tume- discharge burden ambayo tunatakiwa kisheria, hivyo tunaialika mahakama yako tukufu chini ya kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa ya 2019 uone kwamba washitakiwa wote wanne wana kesi ya kujibu. Hivyo taratibu za sheria zifuatwe ili shauri hili liweze kuendelea katika hatua zinazifuata za kuanza kujitetea. Baada ya kusema hayo tunaomba kufunga kesi yetu kwa upande wa Jamhuri. Asante Mheshimiwa Jaji.

JAJI: Kabla ya AMRI ya kufunga upande wa utetezi mna chochote cha kusema?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kuhusu amri ya kufunga hapa, hatuna cha kusema. Tutasema baada ya AMRI ya kufunga.

(Jaji anaendelea kuandika).

JAJI: Baada ya kusikia hoja Iliyoletwa na Bwana Kidando kutoka upande wa mashitaka, Mahakama inakubali ombi la kufunga kesi upande wa mashitaka. Natoa AMRI.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kwa Mahakama haizungumzii haya maombi tunayoyaomba, bali baada ya kufunga upande wa mashitaka, basi upande wa utetezi wanapata nafasi ya kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’. Na kama Mahakama itatukubalia kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’, tunaomba maombi madogo mawili

Moja:
Tunaomba Mahakama hii tukufu ikipendezwa tunaomba tunapatiwe mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo mpaka sasa.

Mbili:
Mahakama ituruhusu tufanye submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’ kwa wasilisho la mdomo. Tupo tayari kwa tarehe yoyote ambayo Mahakama itatupangia baada ya kutupatia nyaraka.

JAJI: Kwanini mnataka submission mfanye kwa wasilisho la mdomo na si kwa maandishi?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji. Tulijadili siku nyingi sana kwamba kufanya wasilisho la mdomo kutasaidia tuwe more focused na itakuwa faida kwetu.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji samahani. Sijajua kwa hatua hii Wakili Peter Kibatala anaweza kusemea washitakiwa wote?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji haina shida. Nimeongea kwa niaba ya jopo. Ila kama mtaamua kuwa kila mmoja aulizwe basi haina shida. Itachukua dakika 10 kufikia malengo yaleyale.

JAJI: Nitauliza kila mmoja.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji nimesikia upande wa mashitaka. Sisi hatuna pingamizi kwa ajili ya kufunga ushahidi wao. Na mheshimiwa Jaji tunaomba ikupendeze mawasilisho ya ‘NO CASE TO ANSWER’ tutafanye kwa njia ya mdomo.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji, pia tunaomba tupatiwe mwenendo wa kesi na kama itabidi na vielelezo. Ni hayo kwa niaba ya mshitakiwa wa kwanza.

John MALLYA: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa pili tumesikia kufungwa kwa kesi ya Jamhuri na hatuna pingamizi. Naona mkono wakili wa mshtakiwa wa nne na mshitakiwa wa kwanza. Na ombi lao la kufanya wasilisho la ‘NO CASE TO ANSWER’ tufanye kwa njia ya mdogo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa tatu pia hatuna pingamizi kwa upande wa Jamhuri kufunga kesi yao. Niungane na mawakili wa upande wa utetezi kwamba tuweze kupewa mwenendo wa kesi na kufanya wasilisho letu kwa njia ya mMdomo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

(Mahakama imekaa kimya huku Jaji akiandika).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji wakati tunaiomba Mahakama kwenye kifungu cha 41, tuliridhia kwa sababu mahususi kuwa Mahakama inaweza kufanya maamuzi hayo. Tunaporejea kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, tulikuwa aware na kifungu cha 293(1) cha CPA kwa mawakili wa utetezi kwa mazingira ambayo wameomba hapa Mahakamani. Hivyo Mheshimiwa Jaji, katika kuwasilisha hoja yetu hapo, na kama utaona inafaa kufanya hivyo kwa wasilisho basi tunaomba tufanye kwa njia ya maandishi na tuweze kuziwasilisha hapa Mahakamani. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Lakini pia Mheshimiwa Jaji tulikuwa tunahangakia katika kifungu cha hoja ya kwanza cha 41 trial hii imechukua muda mrefu. Hatujajua kuwa nyaraka za mwenendo wa kesi zitachukua muda gani ukizingatia umebakia muda machache kuhusu usilikizwaji wa shauri hili.

JAJI: Mpaka leo Karani wangu amechapa kurasa 1,400 za kesi hii. Sijajua itakuwa imebakia kurasa ngapi. Nafikiri jana na leo atakuwa amefikisha kurasa kama 1,500.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, tulikuwa tunawashawishi wenzetu tukaongee ofisini kwako.

JAJI: Nyiye mnaonaje?

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi la kuteta faragha ofisini kwako.

JAJI: Sawa.

Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama.

Jaji ameshaingia katika chumba cha mahakama. Ni saa 8:19 alasiri. Kesi inatajwa tena. Ni kesi namba 16 ya Jamhuri dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji kwa upande wa Jamhuri quorum iko kama ilivyokuwa mwanzoni kabla ya kuahirisha shauri hili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji na sisi pia quorum yetu iko kama ilivyokuwa kabla ya kwenda break. Tupo tayari kuendelea.

JAJI: Karibuni tuendelee.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na vile vituo vya mafuta ulivyokwenda kuvitembelea kwa maana ya Big Bon Kariakoo, Puma ya Sinza na Puma ya Kilwa Road. Sasa uliulizwa swali kuhusu details ambazo umezitoa Mahakamani, ukasema umezitoa kwa maana ulifahamu maana ya details. Ukaulizwa details za plot namba, mmiliki na makutano ya barabara ukasema siyo lazima ziwepo katika maelezo yako.

SHAHIDI: Ndiyo. Nilisema kwamba si lazima kwa sababu mimi nimekuja Mahakamani. Nimeapa na nilieleza maelezo yangu.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa kama ulijibu swali kwamba hukuweka hizo details lakini details hizo umetoa hapa Mahakamani. Kwanini umetoa details Mahakamani na hukuweka kwenye maelezo yako?

SHAHIDI: Ni ili Mahakama iweze kuelewa zaidi ni maeneo gani yaliyo kuwa yamepangwa kufanyiwa vitendo vya uhalifu.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kwa mara nyingine tena tupatiwe kielelezo namba 1 na kielelezo namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusiana na mtu mmoja anaitwa Justine Kaaya kuhusu kushiriki vikao vya kigaidi. Ukasema ni kweli alishiriki bila yeye kufahamu lengo la kikao ila mshitakiwa alifahamu lengo la Kikao. Kwanini ulisema hivyo?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba wakati mshitakiwa wa nne kuomba majina ya watu wanaofuatana na Ole Sabaya, alikuwa anajua lengo la kupata vitu hivyo ni kufanya vitendo vya kigaidi. Wakati Kaaya anatoa vitu hivyo hakujua lengo la mshitakiwa namba nne ni lipi.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa na Wakili Nashon Nkungu kama ni kosa kama ilivyojitokeza kwa Luteni Dennis Urio kumtafutia mtu watu wa kufanya vitendo vya ugaidi. Ukasema inategemea. Elezea hapo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba haitakuwa kosa kama utakuwa unamtafutia huyo mtu kwa lengo la kusaidia vyombo husika.

Wakili Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji. Nilichouliza ni kama lilikuwa ni kosa kwa shahidi Denis Urio kukubali mpango wa ugaidi na si kwenda kufuta.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji na mimi ndicho nilichouliza kama ni kosa au siyo kosa kwa Denis Urio kukubali kwenda kumtafutia watu wa kwenda kwa mshitakiwa wa nne wale watu.

SHAHIDI: Niliposema inategemea inaweza kuwa kosa au si kosa nilikuwa namaanisha kuwa kama atatafuta watu hao kwa lengo la kuzia uhalifu na kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vya Ulinzi haitakuwa kosa, na uhalifu huo umezuiwa kwa walengwa kukamatwa na kufikishiwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Umeulizwa maswali kadhaa kuhusiana na taarifa aliyotoa Luteni Dennis Urio kwa DCI kwamba awe anatoa taarifa kwa Kingai, na Dennis Urio alitoa taarifa kwa Kingai kwamba tarehe 18 Julai mpaka tarehe 4 Agosti 2020, ukasema hakukuwa na ufutailiaji bado. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilimaanisha kwamba taarifa ambazo Luteni Dennis Urio alipewa na mshitakiwa wa nne alikuwa bado hajaanza kufanyia kazi. Mpaka tarehe nne alipoanza kuwasiliana na mtuhumiwa namba moja. Na wakati wanawasiliana nao…

WAKILI WA SERIKALI: Bado hujaulizwa swali.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa swali kuhusiana na hati ya makabidhiano baina yako na Dennis Urio tarehe 11 Agosti 2020. Je, ile fomu ilivyo ulionyeshwa hapa ukasema fomu ile haionyeshi kama Dennis Urio ni shahidi.

SHAHIDI: Nilieleza hivyo kwa sababu fomu ile huwa tunatumia askari tunapokabidhiana vielelezo. Nilitumia fomu hiyo kwa Luten Dennis Urio kwa sababu yeye ni shahidi. Niliweza kusaini katika fomu hiyo na yeye akasaini.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila uliulizwa maswali kuhusu ile Polisi fomu namba 145 ambayo ilikuwa na vielelezo namba 28 mpaka 35 na kuhusu vielelezo vilivyokamatwa kwa mshitakiwa wa kwanza. Kuna baadhi vinaonyesha kituo cha Polisi Kati Dar es Salaam au Police Central Dar es Salaam.

SHAHIDI: Fomu hizo zinajazwa kuonyesha jalada la kesi na kituo ambacho jalada hilo limefunguliwa.

Wakili John MALLYA: Objection! Mheshimiwa Jaji napinga hilo swali. Mimi ndiye niliyeuliza fact kwamba linajazwa na linafunguliwa. It’s a new fact ambayo ita- invite further cross examination.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji. Kwanza pingamizi lake halina mashiko. Kwanza ingekuwa sawa kama nauliza kuhusiana na mshitakiwa wa kwanza na wa tatu. Aliulizwa simu za mshitakiwa wa kwanza alipokea akiwa wapi akasema akiwa Central, akauliza kama aliandika mwenyewe akasema hapana. Hapa chini shahidi alisema hawezi kuwasemea Kingai wala Goodluck walijazia wapi. Sisi Mheshimiwa Jaji tunaendelea kusisitiza kuwa swali letu ni valid.

JAJI: Jibu ni nini?

SHAHIDI: Fomu namba 145 unajaza sehemu ya station na namba ya jalada. Kwa sehemu ya station nimejaza Police Central Station na jalada ni CD/IR/2097/2020.

JAJI: Sasa suala la Malya ni kwamba anaposema hivyo anatoa explanations mpya kwa sababu yeye alijaza fomu za Dennis Urio. Kwa hiyo alileta maelezo kuhusiana na hao ambao hajajaza yeye. Inaleta shida kidogo.

WAKILI WA SERIKALI: Sawa Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi Inspekta Swila uliulizwa hapa maswali kuhusiana na vifaa vya mshitakiwa wa nne ambavo ni simu na computer kadhaa, ukasema kwamba ulipeleka katika maabara ya uchunguzi, na siku ile ambayo ulianza kutoa ushahidi wako ndiyo uchunguzi wake ulikuwa umekamilika.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba upelelezi wa shauri hili umekamilika tangu tarehe 18 Julai 2021. Kuhusu tarehe ya juzi kuhusu uchunguzi ilikuwa ni kuhusu uchunguzi wa ziada wa vielelezo vya mshitakiwa wa nne ambao ulikuwa unafanywa na maabara ya uchunguzi ya makosa ya mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hapa kati ya kipindi cha tarehe 14 Julai 2020 mpaka Agosti 5, 2020 kama uhalifu ulikuwa umeshatendeka. Ukasema inategemea na mpango wa uhalifu wenyewe.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kuwa kama kikundi mipango yake ya kutenda uhalifu itakuwa imekamilika basi uhalifu utafanyika, lakini kama kikundi haijakamilisha mipango yake yenyewe ya kutenda uhalifu basi uhalifu hauwezi kutendeka.

WAKILI WA SERIKALI: Sasa Inspekta Swila uliulizwa pia maswali kuhusiana na yale maombi ya uchunguzi wa kisayansi kwenda Airtel, kuhusiana na Khalfani Bwire na Freeman Mbowe pamoja na Dennis Urio, namba zote tatu zilioombewa taarifa, lakini taarifa zikaja za Dennis Urio na Freeman Mbowe lakini taarifa ya Khalfani Bwire haipo. Ukasema ipo katika taarifa ya Mbowe.

SHAHIDI: Katika uchunguzi wa miamala ya Freeman Mbowe palikuwa pia pana taarifa ya uchunguzi wa miamala ya Khalfani Bwire katika miamala ya Freeman Mbowe.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali hukusiana na taarifa iliyopo katika kielelezo namba 26 na maelezo ya Dennis Urio. Ulipoulizwa kuhusiana na kilichopo ukasema hakutakuwa na utofauti wa maudhui. Je, ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha ni ujumbe wa maneno uliopo katika vielelezo hivyo kwani unafanywa na mtumaji na mtumiwaji. Inaonekana mwisho katika taarifa iliyoandaliwa na maabara ya uchunguzi Kitengo cha Makosa ya Mtandao.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu upokelewaji wa taarifa kutoka kwa Dennis Urio na ukathibitisha aliyepokea taarifa ni DCI wakati huo palikuwa na Deputy DCI Charles Kenyela Ukaulizwa kama mazingira yake si alitakiwa amuachie Deputy DCI kuongozwa Upelelezi? Ukasema si kweli.

SHAHIDI: Niliposema kwamba Afande DCI hakupaswa kumuachia Deputy DCI kuendelea na upelelezi wa sshauri hilo kwa sababu taarifa za uhalifu zilitoka upande mwingine ambapo zilipokelewa na Afande DCI.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali kuhusu taarifa ya jalada la uchunguzi, ukasema kilichokuongoza ni taarifa alizokuwanazo Afande Boazi. Ukaulizwa kuhusu material ya kutosha kufungua jalada ukasema ulikuwa nayo.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha taarifa ambayo ilikuwa imeandikwa na Afande Ramadhan Kingai niliweza kupokea na kuifanyia kazi taarifa hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu taarifa iliyotoka kwa DCI kuja kwako kwamba ilikuwa ni hearsay ukasema NDIYO. Ulikuwa na maana gani?

SHAHIDI: Askari anayepokea taarifa anakuwa anafuata moja kwa moja kutoka kwenye chanzo. Hiyo haizuii kufungua jalada.

WAKILI WA SERIKALI: Licha ya kuwa mpokeaji wa taarifa wa kwanza, uliulizwa pia kuhusu ni lini hasa ulichukua maelezo yake tarehe 4 Oktoba 2020. Ukaulizwa kwanini kesi hii isichukuliwe kuwa ni ya kutungwa.

SHAHIDI: Siyo ya kutunga kwa sababu taarifa ilitolewa, watuhumiwa wakakamatwa na hatimaye wakafikishwa Mahakamani.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kwamba wengine wanasema ni kulipua vituo vya mafuta na wengine wanasema kuchoma masoko katika maeneo ya mkusanyiko, ukasema kulipua na kuchoma ni kitu tofauti na baadaye ukasema kulipua na kuchoma ni terminology. Ulikuwa unamaanisha nini?

SHAHIDI: Ni terminology tu. Watu wanashindwa kutofautisha lakini haiondoi lile kosa la kutenda vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kadhaa kuhusiana na kielelezo namba nne na namba tano kwa maana ya maganda mawili ya risasi katika kielelezi namba 4 na kielelezo namba 5 ni kielelezo cha risasi. Ukaulizwa kuhusu kutofautiana moja inaitwa Luger na nyingine jina tofauti. Ukasema kwa upande wa risasi ni tofauti. Ulimaanisha nini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha risasi si muhimu kuwa na utambulisho. Hazina utambulisho ambao ni tofauti.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji napinga kabisa majibu hayo. Kwamba risasi hazina utambulisho tofauti..

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sisi tulisikia hilo. Sijui kama upande kinzani walisikia hilo. Mheshimiwa Jaji naomba kuendelea na swali lingine.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi uliulizwa swali kuhusiana na Justin Elia Kaaya. Ukaulizwa kama kuna mfanano wowote kati ya maelezo akiwa mtuhumiwa na akiwa shahidi. Wewe ukasema hayawezi kufanana kati ya onyo na ushahidi, isipokuwa yale maelezo ya msingi.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha maelezo ya kwanza yalikuwa yanaelezea kosa wakati haya ya pili ni shahidi na hayaelezei kosa lolote.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa maswali katika kielelezo namba 13 ambayo ni maelezo ya onyo ya mshitakiwa Mohammed Ling’wenya, kwamba katika maelezo yake, hasa ile nia ya kumdhuru Lengai Ole Sabaya ilikuwa siyo kuleta taharuki ila kushambulia viongozi wa Serikali.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika maelezo yake hakusema kwa nia ya kuleta taharuki, lakini kwa malengo yaliyokusidiwa na ambayo shahidi alieleza kutoka kwa mshitakiwa wa nne vitendo vya kumdhuru kiongozi ni vitendo vya kuondoa amani na kufanya nchi isitawalike.

KIBATALA: Objection! Mheshimiwa Jaji samahani. Neno kuondoa amani tulishawahi kutaja hapa Mahakamani?

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji neno kunaondoa amani tunalitoa.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila kuna maswali kadhaa hapa uliulizwa hasa kuhusu mshitakiwa wa pili na wa tatu pale Morogoro kuhusiana na suala la kwenda kwa Freeman Mbowe. Katika maelezo yao ya onyo ya P1 na P13 hawa wote wanasema walipoondoka walikwenda Moshi wakati maelezo mengine ya Dennis Urio wanasema walipoondoa walikwenda Dar es Salaam. Uliulizwa kama kuna mgongano ukasema HAKUNA.

SHAHIDI: Ni kwa sababu maelezo yote lengo ni kwenda kukutana na Freeman Mbowe. Maelezo hayana mgongano wowote kwa sababu mtu ambaye walitakiwa kukutana naye walikutana naye Moshi kama wanavyoeleza katika maelezo yao.

Shaidi: Ni wazi walikutana na mshitakiwa wa kwanza.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno WAZI liondoke. Ni OPINION zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji ni sawa liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na kiwango cha pesa ambacho kila mshitakiwa anadai katika maelezo yake ya onyo alipewa na Luten Dennis Urio, ambapoo Adam Kasekwa anasema walipewa shilingi 87,000 na Urio anasema aliwapa shilingi 199,000. Wakati huo Mohammed Ling’wenya anasema ni shilingi 195,000. Ukaulizwa viwango hivyo vinafanana? Ukasema vinafanana. Kwanini?

SHAHIDI: Kwa sababu wote walipokea pesa kwa Luteni Dennis Urio na kila mtuhumiwa alitoa maelezo yake kwa hiari yake.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kuhusiana na maelezo aliyotoa Adam Kasekwa hasa pale alipotoka Morogoro akanunua shati Chalinze. Ukaulizwa kama shati lile ni ugaidi, ukasema huwezi kutengenisha na ugaidi.

SHAHIDI: Ni kwa sababu pesa ilitumwa na mtu ambaye alikuwa anajua nia ya kuwaleta watu hao kwake ni kwa nia ya kutekeleza vitendo vya kigaidi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali hapa kuhusiana na maelezo yale uliyomwandika Dennis Urio kama kuna sehemu alikuambia Kuwa amemwambia Freeman Mbowe kuwa asitumie namba yake bali atumie ya wakala au vijana wake. Wewe ukasema kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya kumweka karibu. Ukasema sehemu hiyo kwenye maelezo haipo.

SHAHIDI: Nilipoeleza hivyo nilikuwa namaanisha kuwa kumzuia asitumie namba yake ya simu ilikuwa ni sehemu ya kukusanya taarifa kutoka kwa mtuhumiwa wa nne.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa swali kuhusiana na kielelezo namba P1 ambayo ni maelezo ya Adam Kasekwa ambayo ni IMEI namba kwa kulinganisha na kielelezo namba 23 ambayo ni ripoti kutoka uchunguzi wa kisayansi. Lakini ikawa na utofauti kwamba katika maelezo y aonyo palikuwa na utofauti wa namba tatu. Wewe ulisema katika maelezo ya onyo kipo ila kwenye cyber ripoti haipo ila ukasema haimaanishi kitu tofauti.

SHAHIDI: Nilimaanisha simu hiyo IMEI ya kwanza ipo katika maelezo lakini kwenye IMEI ya pili ndiyo kuna utofauti. Kwa hiyo kukosea kwa hiyo ya pili haimaanishi ni kitu cha pili.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji naomba neno kukosewa lisiingie. Ni ushahidi mpya anataka kuingiza kwa mlango wa nyuma.

JAJI: Maneno halisi ni kukosekana.

WAKILI WA SERIKALI: Ndiyo Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: Inspekta Swila jana ulionyeshwa maelezo ya onyo y aAdam Kasekwa ambapo yeye anadai kukamatwa Rau Madukani saa tano asubuhi wakati mtuhumiwa mwenzake anazungumzia kukamatwa saa saba mchana. Ukaulizwa kama huu utofauti uliufanyia kazi. Ukasema kila mmoja alisema kwa ufahamu wake.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba watuhumiwa hawa walitoa maelezo kwa hiari yao. Kwa hiyo kutofautiana kwa muda ni kwa kadri mtu alipokuwa anajaza.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa pia kiwango cha pesa cha shilingi 195,000 ambacho Luteni Dennis Urio aliwapatia kwa namna mbili. Sasa washitakiwa wanaongeala kupewa pesa kiwango hicho? Wewe ukasema ni hali ya kawaida. Eleza kwanini?

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba kila mmoja alitoa maelezo kwa kadri ya ufahamu wake na kumbukumbu zake.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapa. Wenzangu pia wataendelea.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji nina maswali machache.

WAKILI WA SERIKALI: Shahidi, kama unakumbuka uliulizwa swali na Wakili Nashon Nkungu, kuhusiana na OC Forensic kukaa na exhibit na kuviandaa kwa ajili ya uchunguzi, ukajibu siyo sahihi kwamba OC Forensic ndiye anakaa na exhibit. Fafanua sasa.

SHAHIDI: Niliieleza Mahakama kwamba siyo sawa kwamba OC Forensic anakaa na vielelezo baada ya kukamatwa, badala yake vielelezo vinakaa kwa mpelelezi aliyekamata na baada ya hapo vitaandakiwa barua kwenda kwa OC Forensic.

WAKILI WA SERIKALI: Pia uliulizwa kuhusiana na watuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu kwamba muda gani walianza kuwa na guilty mind, ukasema ni pale walipokuubali kushawishiwa.

SHAHIDI: Mtuhumiwa wa kwanza hadi wa tatu hawakuwa na taarifa kuhusu njama za mtuhumiwa wa nne. Mara tu baada ya kukutana mtuhumiwa namba nne ndipo walishawishika kuacha kutoa taarifa na kuamua kushiriki katika vitendo vya uhalifu, hali ambayo ilipelekea wao kukamatwa huko Moshi mtuhumiwa wa pili akiwa na silaha. Walipo hojiwa wakakiri kula njama hizo na kukubali kufanya vitendo vya uhalifu ikiwapo tukio la kumdhuru Lengai Ole Sabaya ambapo walikamatwa wakiwa katika utejelezaji wa tukio la namna hiyo.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali pia kuhusu uhamisho wako, ukajibu kuwa si kweli kwamba timing ya uhamisho wako Ilikuwa ni ya kimkakati.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba nilihamishwa kwa uhamisho wa kawaida mwezi Januari 2020.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali kuhusiana na namna Afande DCI alivyo na maslahi binafsi ukasema si kweli.

SHAHIDI: Si kweli kwamba ana maslahi binafsi. Afande DCI alipokea taarifa kutoka kwa mtu mwingine. Si Kweli kwamba alikuwa ana maslahi binafsi.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa kuhusu register ya 251/2021 ukasema register hizo muhimu katika utunzaji wa vielelezo.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ninachokumbuka mimi ni umuhimu wa utunzaji wa register vituo vya polisi.

JAJI: Lakini hapakuwa na neno vituo vya polisi. Hilo neno vituo liondoke.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji sasa mtu akisema polisi anamaanisha nini? Tutakuwa hatujaisaidia Mahakama yako na sababu ya re examination itakuwa haipo.

JAJI: Sina hakika kama shahidi alitafsiri vituo. Kuleta neni ‘vituo ni concept’ Mpya.

WAKILI WA SERIKALI: Mheshimiwa Jaji tunaondoa neno ‘vituo’.

SHAHIDI: Niliposema register hizo ni muhimu kwa Polisi kwa sababu inasaidia kuonyesha kumbukumbu za vielelezo Hivyo, na inaonyesha aliyekabidhi na aliyekabidhiwa. Kama nilivyoeleza kwamba simu nilikabidhi kwa Koplo Charles na silaha kwa Sajenti Nuru.

WAKILI WA SERIKALI: Uliulizwa maswali mengi kuhusiana na ile miamala, moja ya maeneo uliulizwa kila shillingi iliyotumwa. Katika majibu yako ukasema siyo lazima ku- trace kila shillingi bali ni knowledge ya mtumaji.

SHAHIDI: Nilikuwa namaanisha kwamba katika shauri hili mtumaji wa fedha ambaye ni Freeman Mbowe alikuwa anatuma pesa kufadhili vitendo vya ugaidi.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji ya kwangu naomba niishie hapo niwaachie wenzangu.

SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji naomba kwenda WASHROOM.

Inaonekana mawakili wa Serikali wanarushiana mpira wa nani aendelee kumfanyia shahidi re examination.

Shahidi amesharejea kizimbani.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatutakuwa na swali zaidi kwa shahidi namba 13.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Naomba kukomea hapo.

(Jaji anaandika huku mahakama ikiwa kimya).

JAJI: Shahidi tunakushukuru. Asante kwa ushahidi wako.

(Shahidi anashuka kutoka kizimbani).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji, baada ya shahidi huyu namba 13, tumefanya assessment ya kesi yetu kwa maana ya ushahidi ambao umetolewa mpaka sasa. Ni maoni yetu kwamba tume- discharge burden ambayo tunatakiwa kisheria, hivyo tunaialika mahakama yako tukufu chini ya kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa ya 2019 uone kwamba washitakiwa wote wanne wana kesi ya kujibu. Hivyo taratibu za sheria zifuatwe ili shauri hili liweze kuendelea katika hatua zinazifuata za kuanza kujitetea. Baada ya kusema hayo tunaomba kufunga kesi yetu kwa upande wa Jamhuri. Asante Mheshimiwa Jaji.

JAJI: Kabla ya AMRI ya kufunga upande wa utetezi mna chochote cha kusema?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kuhusu amri ya kufunga hapa, hatuna cha kusema. Tutasema baada ya AMRI ya kufunga.

(Jaji anaendelea kuandika).

JAJI: Baada ya kusikia hoja Iliyoletwa na Bwana Kidando kutoka upande wa mashitaka, Mahakama inakubali ombi la kufunga kesi upande wa mashitaka. Natoa AMRI.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, kwa Mahakama haizungumzii haya maombi tunayoyaomba, bali baada ya kufunga upande wa mashitaka, basi upande wa utetezi wanapata nafasi ya kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’. Na kama Mahakama itatukubalia kufanya submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’, tunaomba maombi madogo mawili

Moja:
Tunaomba Mahakama hii tukufu ikipendezwa tunaomba tunapatiwe mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo mpaka sasa.

Mbili:
Mahakama ituruhusu tufanye submission ya ‘NO CASE TO ANSWER’ kwa wasilisho la mdomo. Tupo tayari kwa tarehe yoyote ambayo Mahakama itatupangia baada ya kutupatia nyaraka.

JAJI: Kwanini mnataka submission mfanye kwa wasilisho la mdomo na si kwa maandishi?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji. Tulijadili siku nyingi sana kwamba kufanya wasilisho la mdomo kutasaidia tuwe more focused na itakuwa faida kwetu.

WAKILI WA SERIKALI: (Pius Hilla) Mheshimiwa Jaji samahani. Sijajua kwa hatua hii Wakili Peter Kibatala anaweza kusemea washitakiwa wote?

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji haina shida. Nimeongea kwa niaba ya jopo. Ila kama mtaamua kuwa kila mmoja aulizwe basi haina shida. Itachukua dakika 10 kufikia malengo yaleyale.

JAJI: Nitauliza kila mmoja.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji nimesikia upande wa mashitaka. Sisi hatuna pingamizi kwa ajili ya kufunga ushahidi wao. Na mheshimiwa Jaji tunaomba ikupendeze mawasilisho ya ‘NO CASE TO ANSWER’ tutafanye kwa njia ya mdomo.

Nashon NKUNGU: Mheshimiwa Jaji, pia tunaomba tupatiwe mwenendo wa kesi na kama itabidi na vielelezo. Ni hayo kwa niaba ya mshitakiwa wa kwanza.

John MALLYA: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa pili tumesikia kufungwa kwa kesi ya Jamhuri na hatuna pingamizi. Naona mkono wakili wa mshtakiwa wa nne na mshitakiwa wa kwanza. Na ombi lao la kufanya wasilisho la ‘NO CASE TO ANSWER’ tufanye kwa njia ya mdogo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshitakiwa wa tatu pia hatuna pingamizi kwa upande wa Jamhuri kufunga kesi yao. Niungane na mawakili wa upande wa utetezi kwamba tuweze kupewa mwenendo wa kesi na kufanya wasilisho letu kwa njia ya mMdomo. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

(Mahakama imekaa kimya huku Jaji akiandika).

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji wakati tunaiomba Mahakama kwenye kifungu cha 41, tuliridhia kwa sababu mahususi kuwa Mahakama inaweza kufanya maamuzi hayo. Tunaporejea kifungu cha 41(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, tulikuwa aware na kifungu cha 293(1) cha CPA kwa mawakili wa utetezi kwa mazingira ambayo wameomba hapa Mahakamani. Hivyo Mheshimiwa Jaji, katika kuwasilisha hoja yetu hapo, na kama utaona inafaa kufanya hivyo kwa wasilisho basi tunaomba tufanye kwa njia ya maandishi na tuweze kuziwasilisha hapa Mahakamani. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Lakini pia Mheshimiwa Jaji tulikuwa tunahangakia katika kifungu cha hoja ya kwanza cha 41 trial hii imechukua muda mrefu. Hatujajua kuwa nyaraka za mwenendo wa kesi zitachukua muda gani ukizingatia umebakia muda machache kuhusu usilikizwaji wa shauri hili.

JAJI: Mpaka leo Karani wangu amechapa kurasa 1,400 za kesi hii. Sijajua itakuwa imebakia kurasa ngapi. Nafikiri jana na leo atakuwa amefikisha kurasa kama 1,500.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji, tulikuwa tunawashawishi wenzetu tukaongee ofisini kwako.

JAJI: Nyiye mnaonaje?

WAKILI WA SERIKALI: (Robert Kidando) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi la kuteta faragha ofisini kwako.

JAJI: Sawa.

Jaji anaondoka katika chumba cha mahakama.

Mawakili wa pande zote mbili wamerejea mahakamani. Na Jaji naye amerejea Mahakamani saa 11:8

Mahakama imerejea baada ya majadiliano na mawakili wa pande zote.

JAJI: Basi Mahakama baada ya kujadiliana na mawakili wa pande zote mbili, kwa kuzingatia mazingira ya pande zote mbili kwa kutumia kifungu cha 40, Mahakama itapitia yenyewe kwa ushahidi wa upande wa mashitaka iwapo washitakiwa watakuwa na kesi ya kujibu au hapana tarehe 18 Februari 2022. Washitakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya Magereza mpaka tarehe 18 Februari 2022. NATOA AMRI.

Jaji anaondoka mahakamani.

Like