RIPOTI YA UTAFITI JUU YA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU KATIKA MAENEO YA HIFADHI NCHINI TANZANIA YAZINDULIWA

Kondo Kikunda, mkazi wa Bagamoyo, ni miongoni mwa waathirika wa dhuluma za vyombo vya serikali dhidi ya raia. Alishiriki uzinduzi wa ripoti na kutoa ushuhuda wa mateso aliyopitia.

MASHIRIKA matatu yenye dhamana mtambuka katika habari, sheria, na haki za binadamu leo yamezindua ripoti ya utafiti juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu katika maeneo ya hifadhi nchini Tanzania.

Mashirika hayo ni the Centre for Strategic Litigation (CSL) lenye makao makuu Zanzibar, SK Media East Africa lenye makao makuu Nairobi (Kenya), na Media Brains la Dar Es Salaam.

Katika hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, miongoni mwa walioshiriki ni wanahabari, watetezi wa haki za binadamu, wanasheria nguli, na baadhi ya waathirika wa ukiukwaji wa haki za binadamu kutoka maeneo mbalimbali Tanzania.

Utafiti uliozaa ripoti hii ulifanyika kati ya 2022 na 2023, ukishirikisha waandishi wa habari walioteuliwa kutoka mikoa yote ya Tanzania, Bara na Visiwani. Walipewa mafunzo maalumu ya utafiti, ufuatiliaji na ukusanyaji wa taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu katika mikoa waliyopangiwa.

Ripoti ya utafiti, ambayo imeambatanishwa hapa.chini, inaonyesha, kwa kifupi, hali halisi katika kila mkoa.

Mpiga picha wetu, Fidelis Felix, alikuwepo. Zifuatazo ni baadhi ya picha za hafla ya uzinduzi huo.

Neville Meena, Jesse Kwayu, Absalom Kibanda, na Jabir Idrisa (wahariri na wasimamizi wa utafiti wa ripoti hiyo).
Wakili Bahama Nyanduga, Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu Tanzania. Ndiye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.
Wakili Rugemeleza Nshala, akisisitiza jambo katika mjadala wa ripoti hiyo kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu.
Kassim Mkwanga (kushoto), mkazi wa mkoa wa Lindi, akitoa ushuhuda wa dhuluma aliyofanyiwa na jinsi ilivyomwathiri. Aliye katikati ni Angelina Nassari, mkazi wa Arusha, mwathirika mwingine wa dhuluma za dola dhidi ya haki za binadamu. Jesse Kwayu, Mkurugenzi Mtendaji wa Media Brains (kulia) ndiye aliongoza mjadala.

NAKALA YA RIPOTI INAPATIKANA HAPA:Conserving Our Rights -Uncovering Human Rights Violations in Tanzania's Conservation Sector

Habari kamili itachapishwa katika ukurasa huu, na uchambuzi wake kwa video utafanyika katika ukurasa wetu wa SK Media Online TV kwenye mtandao wa YouTube.

Like