Kesi ya Mbowe: Mawakili wa utetezi wawashika uchuku jaji na shahidi kwenye kumbukumbu halisi za mahakama

AWALI ILIKUWA HIVI:
Wakili wa Serikali: Wakati mnaenda Moshi Kutoka Arusha mlikuwa watu wangapi?
Shahidi: Wakati tunatoka Moshi tulikuwa watu sita ila wakati wa ukamataji tulikuwa watano. Mmoja alikuwa dereva
Mtobesya: OBJECTION Jambo la dereva ni jipya; hakutaja dereva
Jaji: Wewe hukusikia, alitaja dereva. Mimi nilisikia. Na nilisikia akisema mmoja ya waliotoka Arusha, mmoja alikuwa dereva wa RCO.
Jaji: Anasoma majina, DC Aziz likiwemo, lakini hakuna neno dereva
Mtobesya: Neno DC AZIZI nilisikia ila hakusema hapo DEREVA.
Mallya: Wale waliohusika na ukamataji ni sita ndio alitaja
Mtobesya: Na akija mtu mwingine akisema mlikuwa watano, siyo sita, yeye akasema watano?
Mallya: Wale waliohusika na ukamataji ni sita ndio alitaja
Jaji: kama jibu muhimu mnalihitaji tutawapa re-examination.
BAADAYE IKAWA HIVI
Mtobesya: Unakumbuka ulisema wakati mnamkamata mlikuwa sita?
Shahidi: Nilikwambia watano.
Mtobesya: Ni ushahidi wako kwamba hukusema watu sita?
Shahidi: Mimi nilisema watu watano. Ndiyo tulienda kuwakamata
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba utukumbushe
Jaji: “Tulitoka Arusha kwenda Moshi tukiwa sote na sisi ndiyo tuliokamata.
Tuliokamata tulikuwa sita.”

Kama ilivyowasilishwa na ripota raia, BJ leo tarehe 05 Novemba 2021.

Jaji ameingia Mahakamani
Kesi namba 16 ya Mwaka 2020 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling’wenya na Freeman Mbowe, imeshatajwa.
Wakili wa Serikali Robert Kidando anatambulisha jopo lake

2.Abdallah Chavula
3.Jenitreza Kitali
4.Pius Hilla
5.Nassoro Katuga
6.Esther Martin
7.Tulimanywa Majige
8.Ignasi Mwinuka

Wakili Peter Kibatala anatambulisha jopo la mawakili wa Utetezi
2.Jeremiah Mtobesya
3.John Malya
4.Fredrick Kihwelo
6.Idd Msawanga
7.Hadija Aron
8.Evaresta Kisanga
9.Maria Mushi
10.Nashon Nkungu
Kibatala anakaa
Jaji anaita washitakiwa kwa namba 1, 2, 3 na 4
Wote wanaitika wapo na kunyanyuka
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji, shauri linakuja kwa ajili ya kusikilizwa na leo tuna shahidi mmoja. Tupo tayari kuendelea.

Jaji anaandika na kuhoji, “upande wa utetezi?”
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia kwa ruhusa yako tupo tayari kuendelea.

Wakili wa Serikali: anaenda nje kumuita shahidi.

Jaji: atakuwa shahidi wa saba Siyo?

Wakili wa Serikali: Ndiyo

Tunamuona Inspector Mahita karejea

Jaji: Majina yako

Shahidi: Inspector Mahita Mohamed

Jaji: Umri

Shahidi: 36

Jaji: Kabila

Shahidi: Mluguru

Jaji: Kazi

Shahidi: Askari Polisi

Jaji: Dini

Shahidi: muislam

Shahidi: Wallah wabillah watallah, Nathibitisha Kutoa Ushahidi Wa Kweli

Wakili wa Serikali: Ataongozwa na Wakili Pius Hilla

Wakili wa Serikali: Mahita Wewe ni Mkazi wa wapi

Shahidi: Mkazi wa Morogoro

Wakili wa Serikali: Tangu lini

Shahidi: Mwezi 04 Mwaka 2021

Wakili wa Serikali: Kabla Mwezi wa Nne ulikuwa Ukiishi wapi

Shahidi: Arusha

Wakili wa Serikali: Kazi yako ni Ipi

Shahidi: Polisi

Wakili wa Serikali: Tangu lini

Shahidi: Mwezi wa 03 2011

Wakili wa Serikali: Upo Kitengo gani

Shahidi: Idara ya Polisi Upelelezi wa Jinai

Wakili wa Serikali: Kwa Muda gani

Shahidi: Kwa Miaka 08

Wakili wa Serikali: Arusha Ulikwenda Lini

Shahidi: Tangu Mwaka 2014

Wakili wa Serikali: Mwaka 2020 ulikuwa kituo gani

Shahidi: Central Police Arusha

Wakili wa Serikali: Ulikuwa na nafasi gani

Shahidi: Msaidizi wa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Arusha

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama ukiwa Kama Afisa wa Polisi Majukumu Yako yalikuwa ni yapi

Shahidi: Ukamataji wa wahalifu, Upekuzi wa tuhumiwa na Maeneo, Kusafirisha Watuhumiwa

Wakili wa Serikali: Unamaanisha Nini

Shahidi: Kuwatoa Watuhumiwa kuwatoa na kuwapeleka Sehemu Nyingine

Wakili wa Serikali: Kingine

Shahidi: Kuzuia na Kupambama na Uhalifu

Wakili wa Serikali: Kingine

Shahidi: Uandishi Wa Maelezo, ya Mashahidi na Watuhumiwa pamoja na Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kusimamia Askari waliopo Chini yangu

Wakili wa Serikali: Tarehe 04 August 2020 nini Kilotokea

Shahidi: Nikiwa Ofisini Arusha Nilipogiwa Simu na Afande Wangu ACP Ramadhan Kingai, aliniita Ofisini kwake Aliniagiza Kutafuta Askari Wawili Ambapo niliwatafuta Detective Francis na koplo Goodluck Tulienda Ofisi ya Afande RCO akatuambia tunatoka Kwa ajili ya Safari ya kazi

Kuna kazi ya kwenda Kufanya

Wakili wa Serikali: Ilikuwa Majira ya Saa ngapi

Shahidi: Saa 11

Wakili wa Serikali: Kingai alisema mnapenda Kufanya kazi wapi

Shahidi: Tunaenda Kufanya kazi Moshi

Wakili wa Serikali: Ukiwa pale sasa na Goodluck pamoja na Francis kitu gani kilifuata

Shahidi: Tulijiandaa na Safari pamoja na Askari Mwingine anayetokea Ofisini Kwake ASP Jumanne alikuwa na Yeye anatusubiria pale tujiunge naye kwa Pamoja twende Moshi Alikuwa anatusubiria Arumeru

Wakili wa Serikali: Baada ya Kufika Arumeru Mlielekea Wapi

Shahidi: Tukiingiza Ofisi ya Polisi OC CID Arumeru, Mimi Afande Kingai, ASP Jumanne, PC GOODLUCK na PC Francis ili Kupata Briefing Ya kazi tunayo kwenda Kufanya

Shahidi: Tukiingiza Ofisi ya Polisi OC CID Arumeru, Mimi Afande Kingai, ASP Jumanne, PC GOODLUCK na PC Francis ili Kupata Briefing Ya kazi tunayo kwenda Kufanya

Wakili wa Serikali: Nani aliye fanya Briefing Siku hiyo

Shahidi: Afande Kingai ambaye ndiye alikuwa Kiongozi wetu wa Msafara

Wakili wa Serikali: Kwenye Briefing Mlielezwa Mambo gani

Shahidi: Afande Kingai alituambia Kuwa amepewa Maelekezo ya Kuunda Kikosi Maalum, na Kikosi Hilo Ndiyo MIMI, ASP Jumanne, Goodluck, Francis, na PC Aziz Kwamba Kuna Kikundi Cha Watu kinataka Kufanya Vitendo Vya kigaidi

Wakili wa Serikali: Vitendo gani hivyo Shahidi: Kuwa Kikundi hicho kinataka Kufanya Vitendo Vya Kigaidi Mikoa Mbalimbali ikiwemo Arusha, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya Uhalifu walipokuwa wanataka Kufanya ni KUCHOMA Vituo Vya Mafuta, Kuzuia Barabara, Kukata Miti, kuwadhuru Viongozi Wa Serikali Ikiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Hai, Ole Lengai Sabaya Maandamano ambayo haya Ukomo, na Pia alitueleza Washirika ambao wanataka Kufanya Matukio hayo

Wakili wa Serikali: Aliwataja akina nani

Shahidi: Afande Kingai alisema Mpango huo ulikuwa unaratibiwa na Mheshimiwa Freeman Mbowe

Shahidi: alisema Wahalifu Wengine wapo Moshi, Kwa hiyo tuwazuie Twende Mkoani Kilimanjaro Wilaya Ya Moshi Alisema Kuna watuhumiwa 4 ambao walikuwa Moshi

Wakili wa Serikali: Wakina nani

Shahidi: Walikuwa wanakamilisha Mpango wa kwenda Kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya

Wakili wa Serikali: Kingai alisema Madhumuni ya Mpango yote ni nini

Shahidi: Kuleta Taharuki, Ili Nchi is iweze Kutawalika Tunapoelekea Kwenye Uchaguzi Akasema tuzuie Matendo hayo, Ili Nchi eindelee Kuwa Salama

Wakili wa Serikali: Mengine

Shahidi: Hayo tu kwenye Briefing

Wakili wa Serikali: Baada ya Briefing?

Shahidi: Tukianza Safari Kuelekea Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro

Wakili wa Serikali: Ilikuwa Saa ngapi

Shahidi: Ilikuwa kwenye Saa Mbili Kuelekea Saa 03

Wakili wa Serikali: Mlipofikq Moshi Usiku huo kitu gani Kilifuata

Shahidi: Tuliendelea na Upelelezi wa watuhumiwa ilituweze Kuwakamata

Tulisubiri Taarifa Kutoka kwa Afande Kingai Lakini kwa Siku ile hatukupata kiru

Wakili wa Serikali: Mlifanya Ufutiliaji Kwa Muda gani Kuanzia Saa 6 Mpaka Saa 7 Afande akasema Tubreak tutaendelea Siku inayofuata

Wakili wa Serikali: Siku inayofuata ilikuwa Siku gani

Shahidi: Siku ya 05 Mwezi 08 Mwaka 2020

Shahidi: Ambapo tuliamka Saa 11 alfajiri, Afande akawa anacordinates, Ilipofika Saa 06 Afande alituita Wote,

Jaji: ukisema Afande ni Jumanne au Mtu gani

Shahidi: Afande Kingai Ambaye ndiyo Mkuu wa Msafara

Wakili wa Serikali: endelea Shahidi’ alipotuita alituambia Kuwa wale Watuhumiwa wameonekana Maeneo ya RAU Madukani

Wakili wa Serikali: Rau ya wapi Shahidi Moshi

Shahidi: Tulichofanya ni kupewa description ya Watuhumiwa Jinsi walivyo

Wakili wa Serikali: description ya nini

Shahidi: Muonekano wao

Wakili wa Serikali: Unakumbuka description Zao zilikuaje?

Shahidi: Mmoja alikuwa amevaa Jacket na Ndani Shati la kitenge, Wa pili alikuwa amevaa Shati na Wa tatu alikuwa amevaa Jezi

Wakili wa Serikali: Baada ya Kupata description Ilikuwaje

Shahidi: Kwenda Kujipanga kwa ajili ya ukamataji Detail ya kwanza alikuwa nayo Afande Kingai na Afande Jumanne Na Detail ya Pili nilikuwa nayo Mimi na Coplo Fransis

Wakili wa Serikali: Kwani hilo Eneo Likoje Mpaka Muwe na Details Mbili

Shahidi: Hilo Eneo lina Barabara ya Lami, Kushoto Kuna Flemu za Maduka

Wakili wa Serikali: Maduka Yametizama Upande Upi wa Barabara

Shahidi: Ukiwa unapelekea ni Kushoto na wale watu wa Madukani wanaangali Barabara

Wakili wa Serikali: Upande Mwingine

Shahidi: Kuna Kibanda ambapo Mbele yake a watuhumiwa ndiyo walipokwepo na Baada ya kuwaona wakina Afande kingai Wakaanza Kusimama Kuelekea Upande wangu

Shahidi: Mimi nikawasimamisha

Wakili wa Serikali: Hicho Kibanda cha Namna gani

Shahidi: Kama Cha Wazi tuh, Mtu akipita anawaona Ni kama Ki shelter alafu Pembeni yake kuna Ki Glocery

Wakili wa Serikali: Karibu palikuwa na nini

Shahidi: Pana Kiuwazi, MAma Mmoja alikuwa anapika

Wakili wa Serikali: Watu walipokuwa wamekaa kwenye Kibanda unasema walinyanyuka

Shahidi: Kwa Mujibu wa Taarifa tuliambiwa wapo Watatu lakini walipokuwa wanakuja wapo Watatu Nikawa simamisha Nikamwambia Wanyooshe. Mikono Juu, nikawaeleza Mimi Inspector Mahita natokea Arusha

Wakili wa Serikali: Ukiwaeleza Nini

Shahidi: SIMAMA, KAA CHINI

Wakili wa Serikali: Wakafanyeje

Shahidi: Walisrespond

Wakili wa Serikali: Sasa Baada ya Kuwa simamisha ukafanyeje

Shahidi: Nilijitambulisha Nikawaambi wanatuhumiwa Makosa ya Kutaka Kutenda Vitendo Vya Kigaidi

Baada ya Muda afande Kingai akafika Lakini baada ya Kutumia Sauti Kali ikazua Taharuki ikabidi Watu waaanze Kusogea

Wakili wa Serikali: Alifika afande Kingai na nani

Shahidi: Afande Kingai na Afande Jumanne Afande Kingai kamuamuru afande Jumanne kuwapeleka wale Watuhumiwa

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Baada ya Jumanne Kupewa Maelekezo, Jumanne alifanya nini

Shahidi: Kwanza aliwaita Mashahidi huru wawili walikuwa wanashuhudia

Wakili wa Serikali: Walikuja hao Mashahidi wa Namna gani

Shahidi: Wanawake

Wakili wa Serikali: Baada ya Mashahidi huru Kufika Kitu gani Kilifanyika

Shahidi: alijitambulisha kwa washtakiwa, akatoa Vitu vyake mfukoni, akaanza Upekuzi

Wakili wa Serikali: Alianza Upekuzi Kwa Mtu yupi

Shahidi: Alianza kwa Mtu anaye Itwa Adam Kasekwa

Wakili wa Serikali: Ulifahamu Adam Kasekwa Muda gani

Shahidi: Wakati Afande Jumanne anajitambulisha na wao walijitambulisha

Wakili wa Serikali: Matokeo ya Upekuzi yalikuwaje

Shahidi: afande Jumanne alitoa Pistol Upande wa Kushoto wa Mtuhumiwa

Wakili wa Serikali: Upande wa Kitu gani Shahidi Wa Suruali

Wakili wa Serikali: Ulitambua Vipi wewe Kwamba ni Pistol

Shahidi: kwa Mwonekano wake na ilikuwa na namba ya A5340

Wakili wa Serikali: Tofauti na Pistol Kitu gani Kingine Kilionekana

Shahidi: Ndani ya Hiyo post palikuwa na Magazine yenye Risasi 3, Ilikuwa aina ya Luger

Wakili wa Serikali: Tofauti na Pistol na Risasi zake, Je kitu gani Kingine

Shahidi: alikutwa na Unga unaosadikiwa kuwa ni Madawa ya Kulevya

Shahidi: Alikutwa pia na simu, Na Line za Simu, Airtel na Hallotel,

Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi ASP JUMANNE alifanya Kitu gani,

Shahidi: alijaza Hati ya Upekuzi

Wakili wa Serikali: Zilikuwa Hati ngapi

Shahidi: Zilikuwa Mbili

Wakili wa Serikali: baada ya hapo walifanya nini

Shahidi: Mtuhumiwa aliweka Sahihi na baada ya pale Akaendelea na Upekuzi wa Mtuhumiwa wa pili

Wakili wa Serikali: ambaye anaitwa nani Shahidi Mohamed Ling’wenya

Wakili wa Serikali: na Yeye alikutwa na nini

Shahidi: alikutwa na Simu, na Kete za Unga zinazosadikiwa kuwa ni Madawa ya Kulevya 25

Wakili wa Serikali: Madawa yalipatikana eneo gani

Shahidi: Kwenye Mfuko wa suruali

Wakili wa Serikali: baada ya hapo nini Kilifanyika

Shahidi: Afande Jumanne alijaza Hati mbili

Wakili wa Serikali: Baada ya Kujaza hizo Hati Mbili nini Kilifanyika

Shahidi: Mtuhumiwa aliweka Saini yake na wale Mashahidi huru

Afande Jumanne akampatia afande Goodluck Vielelezo, Afande kingai akaita Gari Nyingine

Wakili wa Serikali: Aliita kutoka wapi

Shahidi: Kwa Kamanda Wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Kwa kuwa tulishakuwa wengi wale Mashahidi huru wakapanda Gari Nyingine

Wakili wa Serikali: Tueleze hapa Mahakamani

Uliowakamata wapo hapa?

Shahidi: Ndiyo wapo hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali: Elezea Wapo wapi

Shahidi: Upande wa Pili

Wakili wa Serikali: Wamevaaje vaaje

Shahidi: Mohamed Ling’wenya ni yule aliye Vaa Shati na Adam Kasekwa ni yule Mwenye Tshirt yenye mistari Mistari

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Kwamba Kwemye Gari walipokuwa Watuhumiwa kuelekea Central Moshi Mlikuwa kwenye Gana akina nani

Shahidi: Afande Kingai, ASP Jumanne, Mimi na Watuhumiwa na Goodluck

Francis yeye alikuwa na wale Mashahidi

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kilifuata Mlipokuwa Njiani

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kilifuata Mlipokuwa Njiani

Shahidi: afande kingai aliwaambia Kwa Taarifa zake walikuwa watatu, akawa uliza yule Mwingine Yupo wapi

Wenyewe kwa Ushirikiano Kabisa wakasema Kuwa kweli walikuwa watatu

Wakili wa Serikali: Walikuwa na nani

Shahidi: Moses Lijenje

Wakili wa Serikali: Ambapo walisema yupo wapi

Shahidi: Kwa Maelezo yao walituambia wamemuacha pale Rau Madukani

Wakili wa Serikali: baada ya Kuelezea hivyo kitu gani kiliendelea

Shahidi: kwakuwa tulikuwa tumekaribia kufika Kituoni, tukiingia Kituoni Afande Kingai akatoa Maelekezo Francis aendelee Kuchukua Maelezo

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kikafuata

Shahidi: Tukarudi na Watuhumiwa Mpaka Rau Madukani Lakini hatukupata, Watu wakawa wanasema Kapita hapa Kapita tuh

Tukarudi kwa Washitakiwa Wetu wakasema Basi watatu onyesha Maeneo anayopenda Kwenda

Wakili wa Serikali: Ilikuwa ni sehemu gani

Shahidi: Naweza Kusema Ilikuwa ni Vibanda Umiza tuh pale Moshi Mjini

Wakili wa Serikali: Baada ya Pale Moshi Mjini, Kwanini Mlifika Mpaka Aishi Hotel

Shahidi: Kwa sababu walituambia wenyewe anaweza Kuwa ameelekea Kule

Wakili wa Serikali: Ufutailiaji huo wa Moses Lijenje Uliendelea Mpaka Lini au saa ngapi

Shahidi: Tuliendelea Mpaka Boma Majira ya Sa 4 au Saa 5

Wakili wa Serikali: Saa 4 au 5 ya Majira gani

Shahidi: Usiku

Wakili wa Serikali: Baada ya Kufika Boma

Shahidi: Tuliendelea Kumtafuta pale Boma, tukala nao Chakula. Afande Kingai akasema turudi kuwarudisha Lock up Watuhumiwa

Wakili wa Serikali: Lock Up wapi

Shahidi: Kituo cha Moshi

Shahidi: Kesho yake Majira saa 11 tuliamka na Kwenda kuwa chukua watuhumiwa pale Moshi Upelelezi Uliendelea Wa Kumtafuta Moses Lijenje Kama atakuwa amepanda Basi Kuelekea Sehemu Nyingine

Wakili wa Serikali: Matokea ya Upelelezi wenu Siku hiyo sa Tarehe 06 -08 -2020

Shahidi: Hatukumpata, ikabidi turudi tena Kwenye Vile Vijiwe Vya tarehe 05 Lakini wakati tunazunguka, Adam Kasekwa alisema Moses Lijenje NaDada Yake Sakina Arusha Safari Ikaanza Upya Kuelekea Huko Arusha

Wakili wa Serikali: Kitu gani kilitokea Huko Arusha

Shahidi: Tulifika Arusha lakininhawakuweza Kutambua Nyumba ya Dada yake Moses Lijenje Tukawarudisha Moshi Na Kisha Afande Kingai akasema tuwatoe Watuhumiwa tuwarudishe Moshi

Wakili wa Serikali: Safari ailianza Muda gani

Shahidi: Kuelekea Moshi Ilianza Saa 2 Jioni

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Baada ya Kutoka Moshi na Safari ya Kuja Dar Kitu gani Kilifuata

Shahidi: Tulilofila Njia panda Ya Himo Gari yetu ilipata Pacha, afande Kingai Ikabidi Aombe Gari Nyingine Tukiwa tunasubiria Gari tulipata Nguvu Tumbo (Refreshments) au Chakula

Baada ya Gari Kufika tuliendelea na Safari

Wakili wa Serikali: Kwenye Safari mlikuwa na akina nani Shahidi: Mimi, Afande Kingai, ASP Jumanne, PC GOODLUCK na wale Watuhumiwa

Wawili wa Serikali: watuhumiwa gani

Shahidi: Mohamed Ling’wenya na Adam Kasekwa

Wakili wa Serikali: Tangu tarehe 05 Mpaka tarehe 06 walikuwa Kwenye Uangalizi wa nani

Wakili wa Serikali: Walikuwa na Hali gani

Shahidi: Hali Nzuri

Wakili wa Serikali: Unamaanisha Nini Kusema Hali Nzuri

Shahidi: Walikuwa na Afya Nzuri

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Dar es Salaam Mlifika lini

Shahidi: Tulifika Siku ya Tarehe 07 Majira ya Saa 11 kuelekea Saa 12 Asubuhi

Wakili wa Serikali: Mlipofika Dar es Mlielekea wapi

Shahidi: Tulifika Central Police Dar es Salaam Baada ya Kufika Central Police Dar es Salaam Tukiwakabidhi pale CRO ili wawaingize Lockup

Wakili wa Serikali: Baada ya Kuwa weka Luck up nini Kikifuata

Shahidi: afande Kingai alitoa Malekezo Kwamba tuka awe Uso alafu turudi

Wakili wa Serikali: Mlirejea Saa ngapo

Shahidi: Saa 1 Asubuhi

Wakili wa Serikali: Mlipewa Malekezo Gani sasa

Shahidi: Afande alituambia tujiunge na Assistant Inspector Swila tuendelee Na Ufutailiaji wa Mtuhumiwa Mwingine anayeitwa Bwire

Wakili wa Serikali: ambaye alikuwa wapi

Shahidi: Alikuwa Dar es Salaam

Wakili wa Serikali: Mlikuwa na akina nani

SHAHIDI: Mimi, PC GOODLUCK, Assistant Inspector Swila

Wakili wa Serikali: Mliendelea na nini

Shahidi: Tuliendelea na Upelelezi, Hatua za Upelelezi mbalimbali Kutafuta ma Informer

Wakili wa Serikali: Nini Kikatokea

Shahidi: Siku hiyo Hatukufanikiwa

Shahidi: Siku inayofuata ya tarehe 08 Afande Kingai akatoa Maelekezo Kwamba Tuwatoe Watuhumiwa pale Central tuwapeleke Kituo Cha Mbweni

Wakili wa Serikali: ulitekeleza Vipi hayo Maelezo

Wakili wa Serikali: Maelezo yapi Mengine Ulipewa

Shahidi: Afande Kingai akasema Kutokana na Mafunzo watuhumiwa walivyo nayo, Tuwapeleke Mbweni ilikila Mtuhumiwa akae Chumba Chake cha Mahabusu Wakili wa Serikali Unakumbuka zoezi la Kuwatoa Central Lilikuwa Kwenye Majira ya Saa 4

Shahidi: Nilienda Kuwatoa Mahabusu Watuhumiwa na Nikiwa na Afande Jumanne nikawapeleka Kituo cha Mbweni

Wakili wa Serikali: Maelezo yapi Mengine Ulipewa

Shahidi: Afande Kingai akasema Kutokana na Mafunzo watuhumiwa walivyo nayo, Tuwapeleke Mbweni ilikila Mtuhumiwa akae Chumba Chake cha Mahabusu

Wakili wa Serikali: Unakumbuka zoezi la Kuwatoa Central Lilikuwa Kwenye Majira ya Saa 4

Wakili wa Serikali: Tarehe 09 Mwezi wa 08 2020 nini kilitokea

Shahidi: Taarifa za Bwire tulizokuwa tumezipata kwamba Mtuhumiwa alikuwa anatokea Buguruni kwenda Maeneo ya Chang’ombe tukaweka Mtego

Wakili wa Serikali: Mtego gani huo

Shahidi: Tukiweka Askari Track wa Usalama Barabarani akalisimamisha Basi aina ya Costa ambayo Mtuhumiwa alikuwa amepanda Afande Kingai Aliniambia nipande Kumuangala Ndani Nikamkuta kakaa zile Siti za Kati

Wakili wa Serikali: Baada ya Kumuona Shahidi Nikajitambulisha Kwamba naitwa Inspector Mahita na Kwamba natokea Arusha na Kwamba anashitakiwa kwa Makosa ya Kutaka Kutenda Ugaidi Afande: Kingai na Yeye akajitambulisha akamuonya na baadae akawekwa Mahabusu ya pale pale Chang’ombe

Wakili wa Serikali: Ilikuwa Majira ya Saa ngapi

Shahidi: Saa 4 Usiku

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Kwamba Baada ya Tarehe 09 ulishughulika namna gani na watuhumiwa

Shahidi: Tuliendelea Kuwatafuta Watuhumiwa na Kufanya Upelelezi akwa kwenda sehemu Mbalimbali

Wakili wa Serikali: Kama zipi

Shahidi: Mwanza na Tabora

Wakili wa Serikali: Unasema Ulishiriki Kumkamata Bwire, je yupo hapa Mahakamani

Shahidi: Ndiyo amevaa kanzu na Barakha Sheikh

Wakili wa Serikali: Mliwakamata watuhumiwa wote kwa tuhuma zipi

Shahidi: Kwa kula Njama za Kutenda Matendo Ya Ugaidi

Wakili wa Serikali: Umeshiriki Kumkamata watu watatu

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Mbowe yeye amekamatawa lini

Shahidi: Mwaka huu

Wakili wa Serikali: Kwanini yeye Kipindi hicho hakukamatwa

Shahidi: Afande Kingai alisema Mpaka Uchunguzi Ukikamilika

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Swali lingine


Mtobesya ananyanyuka anaweka Joho Vizuri na Kumfuata Shahidi

Mtobesya: Afande Kingai alikwambia Siku ya Kwanza Kwamba Kuna watu wamepanga Kufanya Matendo ya Ugaidi

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: alikuwa anakwambia here say Kutoka kwa nani

Shahidi: alikuwa anaambiwa na Msiri wake

Mtobesya: Kwa hiyo Kingai ni Mtu wa Ngapi Kupokea Taarifa

Shahidi: Wa kwanza Kwa Uelewa wangu

Mtobesya: Mliweza Ku verify Source

Shahidi: Siyo Jukumu langu

Mtobesya: Nilisikia Unasema Kingai Aliwapa description Ya Mavazi

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Mweleze Jaji Rau ina ukubwa gani na Ipo busy vipi

Shahidi: Ni Center ambayo ipo busy

Mtobesya: Nitakuwa Sahihi Nikisema Kuna Mwingiliano Wa watu wengi

Shahidi: Ndiyo sahihi

Mtobesya: Kwamba pale Rau Madukani pasingeweza kuwa na Mtu Mwingine Mwenye Shati Jekundu?

Shahidi: Nilisha Jiridhisha Kama Ulinisikikiza Vizuri, Ndiyo Maana tunafanya Surveillance

Mtobesya: Kwa hiyo kwa huo Ushahidi Wako kwa Siku ile Rau Madukani hapakuwa na Mtu Mwingine aliye Vaa Shati Jekundu

Shahidi: Ndiyo Kwa Siku hiyo

Mtobesya: Detail Mliyoenda nayo Moshi Mlikuwa watu wangapi

Shahidi: Sita

Mtobesya: Na Watu hao Sita Ndiyo Mlioshughulika kukamata

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Kwa hiyo akitokea Mtu akisema mlikuwa watano kwenye ukamataji atakuwa sahihi au siyo Sahihi

Shahidi: Wakati Wa Ukamataji tulikuwa Wawili watatu wakaja baadae

Mtobesya: Unarukaruka swali, Nauliza Nyie Ambao Mlitoka Moshi Kwamba akitokea Mtu akisema Mlikuwa watano na siyo Sita atakuwa hayupo sahihi

Shahidi: itakuwa Hayupo Sahihi

Mtobesya: Baada ya upekuzi Jumanne alimkabidhi nani vielelezo?

Shahidi: PC GOODLUCK

Mtobesya: Unaifahamu fomu ya polisi inaitwa Fomu namba 45

Shahidi: Sifahamu

Mtobesya: Je, unafahamu kwamba hiyo fomu ndiyo anahitajika kujaza vielelezo anapotoa vielelezo sehemu ya tukio?

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: na unafahamu anayetokea vielelezo anatakiwa kujaza fomu+

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Wewe Unasemaa umeona Jumanne Akimkabidhi Goodluck vielelezo, Je uliona wakijaza hiyo fomu

Shahidi: Ndiyo niliona

Mtobesya: hiyo fomu ya 145

Shahidi: Kimya

Mtobesya: na Unakumbuka ulichokiandika au Unahitaji Ku’ refresh Memory

Shahidi: Hapana nakumbuka

Mtobesya: Kwenye Maelezo yako uliyoandika Polisi Hakuna Sehemu ambayo umeandika Afande Jumanne alijitambulisha kabla ya Upekuzi

Shahidi: Ndiyo Hayapo

Mtobesya: Kwenye Maelezo yako wewe Ndiye Uliyemkamata Bwire hayo Maneno hayapo, Ni sahihi

Shahidi: Sahihi hayapo

Mtobesya: Kwenye Maelezo yako umeandika zile Kete kuwa ni Heroine, kwanini ulidhani ni Heroine na siyo Cocaine

Shahidi: Kwa uzoefu wa Kazi yangu Heroine Ina Mfano wake na Cocaine Kwa Mfano wake

Mtobesya: Kwa hiyo zikiwa in Powder form unaweza Kufanya Utambuzi, Mwambie Mheshimiwa Jaji

Shahidi: Unaweza Kufahamu zikiwa in Powder Form

Mtobesya: Umesema kwamba mlizurura na Watuhumiwa sehemu mbalimbali Moshi, Je unafahamu Kwamba Kuna Kielelezo Hapa Mahakamani Kwamba 24 July 2020 walienda Moshi halafu tarehe 31 July 2020 waliondoka Moshi Kuja Dar es Salaam

Shahidi: Hapana Sifahamu

Jaji anaomba atajiwe tena hizo tarehe

Mtobesya: Nikuulize sasa Swali la Mwisho, Wakati Mnamkamata huyu uliyemuita Bwire Ilikuwa Majira ya Saa ngapi

Shahidi: Saa 2 Usiku

Mtobesya: Wewe Uliacha Kuonana naye lini

Shahidi: Kwa Siku ile Hapana

Mtobesya: Kwa hiyo huwezi kuisaidia Mahakama Kwamba aliandika Maelezo au hakuandika

Shahidi: Wakati anaandika Maelezo Sikuwepo

Mtobesya: Je Upekuzi

Shahidi: Upekuzi wa Nini

Mtobesya: wa yeye Mwenyewe na alipokuwepo

Shahidi: Sikuwepo

Mtobesya: naomba Kuishia Hapo

Anasimama Wakili John Mallya

Mallya: Umewahi Pia kutoa Ushahidi Mahakamani Kwenye kesi zingine

Shahidi: Sahihi

Mallya: Ni sahihi Unapokuwa Shahidi Kama wewe, Kama arresting person Mnakuwa mnaandika Maelezo Kwa Kingereza baada ya kuwakamata Watuhumiwa

Shahidi: Ndiyo yakihitajika tunaandika

Mallya: ulisema Mlienda Mpaka Mwanza Mpaka TABORA

Shahidi: Ndiyo

Mallya: kunaruhusiwa Kuweka Maelezo ya Nyongeza

Shahidi: Additional Statement Inaruhusiwa

Mallya: Mwambie Jaji Kwa Mazingira yapi

Shahidi: Kama ikitokea kuna Maelezo umesahau

Mallya: Maelezo Ya Nyongeza yanasomeka Pamoja au Tofauti

Shahidi: Yanasomeka Pamoja

Mallya: Mtobesya alikuuliza Unakumbuka Uliandika Maelezo

Shahidi: Ndiyo nakumbuka

Mallya: Uliandika Mwezi gani

Shahidi: Tarehe 09 Mwezi 10 2020

Mallya: Sasa sisi tuna Maelezo yako Hapa Kwamba uliandika Maelezo Mwezi 08

Mallya: Tushike lipi

Shahidi: Mwezi wa 10

Mallya: Ulikuwa Lini TABORA

Shahidi: Mwezi 10

Mallya: Sasa Hapa Kuna shahidi kaja anaitwa Kaaya anasema Tarehe hizo Ulikuwa Arusha na siyo TABORA

Shahidi: Ndiyo niliitwa Kuchukua Maelezo

Mallya: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa huyo Kaaya wakati Unamkamata na Kumchukua Maelezo alikuwa anatuhumiwa kwa Makosa gani

Shahidi: Alikutwa na Noti bandia

Mallya: Kuhusu Ugaidi

Shahidi: Hakushtakiwa na Ugaidi

Mallya: Una uhakika

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Je Kaaya alishawahi kushtakiwa kwa Kesi ya ugaidi

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Je Kaaya anahusika na Kesi hii au hausiki

Shahidi: hahusiki

Mallya: Alikuja hapa kama Shahidi

Shahidi: Ndiyo anahusika

Mallya: Ulishawahi kuwakamata Magaidi wa Arusha

Shahidi: siwezi kuongelea Hapa

Mallya: naomba Mheshimiwa Jaji anijibu

Jaji: JIBU SWALI

Shahidi: Ndiyo nilishawahi Kuwakamata

Mallya: Sasa eleza Wakati Unawakamata Ulishawahi Kuonyeshwa na Gaidi gani Mwenzao

Shahidi: Sikumbuki

Mallya: Sasa Umesema hapa Kwamba Ulimkamata Bwire

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Ulimjuaje

Shahidi: Palikuwa na Informer Ndani

Mallya: ulisema Ulifanya Uhakiki kabla ya Kuwakamata, Je ulitoa description Kwamba walikuwa wanafanya Kitu gani

Shahidi: Sikueleza

Mallya: wakati unasema Umeona Cocaine Ulisema Rangi

Shahidi: Hapana

Mallya: Wakati Unasema Cocaine Ulisema ya Uzito gani

Shahidi: Hapana

Mallya: ulishuhudia Upekuzi Kwa Maelezo yako, Vitu Vyao kama Vitambulisho na Pesa vilikwenda wapi

Shahidi: Walikuwa hawana

Mallya: Wa Kwanza Ulifahamu Baada ya Jumanne Kujitambulisha kwake

Shahidi: Sahihi Kabisa

Mallya: na Hati za Uchukuaji Mali zilijazwa eneo la Tukio

Shahidi: Sahihi Kabisa

Mallya: Naomba Kielelezo Mheshimiwa Jaji

Mallya: we Umemtambua Adam Hassan Kasekwa, Je Soma Hati ya Kuchukua Mali imeandikwaje

Shahidi: Adam Hassan Kasekwa AKA Adamoo

Mallya: Umesema Sababu ya kuwahamisha ni Security yao

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Je Central Kuna Polisi Wangapi

Shahidi: Sifahamu

Mallya: hufahamu kwa sababu hujawahi kufanya kazi central?

Shahidi: Nishafanya kazi central..

Mallya: sasa elezea Central Dar es Salaam

Shahidi: Sijawahi kufanya kazi

Mallya: pale Central Mlikuta Polisi Wangapi

Shahidi: Mapokezi Kama wanne na Walinzi Nje

Mallya: Na Mbweni Mlikuwa wa ngapi Mapokezi

Shahidi: Kama wawili

Mallya: Kwa hiyo Mnawatoa Watuhumiwa Kwemye polisi Wengi ila wewe na Jumanne na Watu wawili tuh Mnawabeba Makomandoo

Shahidi: Tulikuwa tumewafunga Pingu

Mallya: Kwamba Ulinzi wa kituo ni kazi yako au Mkuu wa kituo

Shahidi: Mkuu wa Kituo ila Watakuwa waliwasiliana na Afande Kingai

Mallya: Wakati wakili wa Serikali anakuongoza Ulisema hayo

Shahidi: Hapana

Mallya: Wewe Ndiyo Mahita aliyekuja hapa kutoa Ushahidi Kwenye kesi Ndogo?

Shahidi: Ndiyo mimi

Mallya: Ulisema Central ni Class A

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kwa sababu anakaa RPC?

Shahidi: hapana

Mallya: Kwa sababu gani

Shahidi: Anakaa OCS na Mkuu wa Kituo na Idadi Kubwa ya Polisi

Mallya: Sasa hao OCS na Mkuu wa Kitu na hiyo Idadi wapo Mbweni

Shahidi: Hapana

Mallya: Ulielezea kwamba Madawa ya Kulevya mliyoyapata Kwa Adam Kasekwa Uliyatoa Upande Gani

Shahidi: Hapana

Mallya: Ulieleza Kwamba Madawa Ya kulevya ya Mohammed Ling’wenya mmetoa Upande gani

Shahidi: Hapana

Mallya: Kukaa Chini na Kuchuchumaa ni Kitu Kimoja

Shahidi: Hapana

Mallya: Sasa Kuna Mtu mmoja kaja mahakamani kasema ulisema wachuchumae siyo wakae Chini

Shahidi: Nilichokisema ndiyo Nilichokisema

Mallya: atakuwa anaongea Uongo

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mpaka tunapoongea Maelezo Ya Bwire yameshachukuliwa

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Ulisema Umeenda Kuwachukua watuhumiwa Central Ukawapeleka Mbweni, Je Ulieleza Kwamba Ulifanya Nini baada ya Kufika pale mbweni

Shahidi: Sikueleza

Mallya: Ulieleza wakati Wa Upekuzi namna walivyo Hesabu hizo Kete

Shahidi: Sikueleza

Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Wakili Fredrick anasimama

Fredrick: Ulisema Baada ya ukamataji wa Khalfani Bwire Mlikuwa mnasubiri Maelekezo ya Viongozi

Shahidi: Sahihi

Fredrick: na baada ya hapo Mkaelekea Mwanza SHAHIDI: Ndiyo Fredrick: Mkumbushe Mheshimiwa Jaji ulienda Mwanza Tarehe Ngapi Shahidi Sikumbuki

Fredrick: Ulisema moja ya tuhuma ni kuwa dhuru Viongozi akiwemo Sabaya, wengine wakina nani

Shahidi: Sabaya

Fredrick: Wengine wakina nani?

Shahidi: Sabaya…

Fredrick: Sabaya ushamtaja hao wengine ni wapi?

Shahidi: nimemtaja Sabaya

Fredrick: Ulizungumza Kuhusu Kurudi Moshi Kutoka Boma, Je Ulieleza Mfika Saa ngapi

Shahidi: Sikueleza

Fredrick: Ulipowafikisha Moshi mkaandikisha

Shahidi: Ndiyo

Fredrick: Hiyo Register hapa Mahakamani Ipo au Haipo

Shahidi: Siyo Kazi yangu Kuitunza

Fredrick: Umezungumzia Kuhusu Afya za watuhumiwa, Kwamba walikuwa Vizuri

Shahidi: Ndiyo

Fredrick: ulijuaje

Shahidi: Kwa kuwaangalia na Majibu yao

Fredrick: Asante Mheshimiwa Jaji

Wakili Kibatala anasimama

Kibatala: Mahita mambo Vipi!?

Shahidi: Poa

Kibatala: Una elimu gani

Shahidi: Digrii

Kibatala: Ya Nini

Shahidi: Ya Sheria

Kibatala: ooohhh kwa hiyo naongea na learned brother

Shahidi: Wewe ndiyo learned brother, maana Mimi nimesema sheria tu..

Kibatala: Kuna Sehemu yoyote Kwenye Dictionary Grocery inasema ni sehemu ya Kunywa Pombe

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: katika Ushahidi Wako umetaja Popote Kuhusu Bar au Kufananisha Grocery na Bar

Shahidi: Hapana

Kibatala: kwahiyo wewe Hukutaja Bar

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: umesema kuhusu Kibanda umiza

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: umemfafanulia Jaji Maana Ya Kibanda Umiza

Kibatala: Je unafahamu Kingai aliambiwa na DCI Boaz Kuwa ndiye aliyetoa Maelezo Kwamba Baada ya Watuhumiwa Kukamatwa waletwe Dar es Salaam

Shahidi: Alituambia tarehe 6

Kibatala: Twende kwenye description sasa, Ni sahihi katika statement Yako mliweka mtego kuwakamata watuhumiwa wawili

Shahidi: Katika statement sikusema hivyo

Kibatala: Statement Yako ya Tarehe 10.8.2020 tulifika Moshi, Tuliweka Mtego mbalimbali kwa ajili ya Kuwakamata Watuhumiwa lakini hatukuwakuta….. Huu Mstari upo au Haupo

Shahidi: Upo

Kibatala: Kingai hajawahi Kuwaambia Kuwa ana Informer wake mwanajeshi anaitwa Urio

Shahidi: hajawahi

Kibatala: Kingai alikuwa anakwambia Kwamba ana wasiri wake au Informer wake

Kibatala: Hakusema hivyo

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Ushahidi Wako wewe Hukusema Neno wasiri au Informers

Shahidi: Nimesema

Kibatala: aliwaambia ana Informer Wangapi

Shahidi: Hakutuambia

Kibatala: Pale Rau Madukani Personally Ulifanya Surveillance

Shahidi: Tulifanya Kibatala Wewe Personally Ulifanya au Hukufanya

Kibatala: Wewe Personally Ulifanya au Hukufanya

Shahidi: Nilifanya

Kibatala: na Ukawaona Watu wote watatu

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Kuna sehemu umesema Kwamba Ulibreak au Ukawa Divated

Shahidi: Hapana

Shahidi: Hapana

Kibatala: Kuna sehemu Ambayo umemwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Uliwaona watatu lakini Ghafla ukawakuta wawili

Shahidi: Nilieleza

Kibatala: Na Katika Ushahidi Wako Ulisema Kwamba Kuna Kibanda Cha Mbege

Shahidi: Hapana

Kibatala: Unafahamu wa Kibanda Cha Mbege Katika Kesi hii

Shahidi: Mimi nafahamu Kuhusu Kumkamata watuhumiwa

Kibatala: Kwa hiyo ufahamu lolote Kuhusu Kibanda Cha Mbege

Shahidi: Mimi sikwenda kukamata Kibanda Cha Mbege, Siyo Priority

Kibatala: Ulizungumzia Kuhusu Kibanda Cha Tigo?

Shahidi: Sikuzungumzia Kibatala: Ni Kuuliza pia Umuhimu wa Kibanda Cha Tigo Pesa Utasema siyo Priority Yako

Shahidi: Ndiyo ilikuwa My Primary Objective

Kibatala: Ulipokuwa Unawakamata Ukitumia Maneno gani

Shahidi: NILIWAAMBIA WASIMAME NILIWAAMBIA WAKAE CHINI

Kibatala: ilikuwa kwa Sauti Kubwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ukajitambulishaje

Shahidi: MAHITA OMARY MAHITA

Kibatala: Umezungumzia wewe au afande Jumanne kwenda Kuwaita kwenye Biashara zao

Shahidi: Nilieleza

Kibatala: kwa hiyo walienda Kuitwa Kwenye Biashara zao au Walitoka kutoka Kwenye Watu walipokuwa wameshuhudia

Shahidi: Walikuwa among the Crowd

Kibatala: wewe Yote Uliyashuhudia

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na wote walipekuliwa kwenye Maungo yao

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Zoezi lilishuhidiwa na Mashahidi, Mwanamke

Shahidi: Ndiyo nilivyosema

Kibatala: Katika Ule Umati Wanamume walikwepo au hawakwepo

Shahidi: walikuwepo

Kibatala: ukiwa na suspect wa kike anatakiwa apekuliwe na nani?

Shahidi: Mtu yoyote

Kibatala: Kwamba upekuzi wa mwanamke unaweza kushuhudiwa na mtu yoyote

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa sheria ipi?

Shahidi: sikumbuki

Kibatala: Upande wa Kulia wa eneo la Tukio palikuwa na frame 4, Moja Ni Duka la Vipodozi na Duka Moja la Jumla

Shahidi: Upande wa Kulia kama palikuwa na M-pesa na TigoPesa…. Mimi sifahamu.. mimi nilikwenda kuwakamata

Kibatala: Unakubaliana na Mimi kama Kweli Mliwakamata Pale Watuhumiwa pana frame 4

Shahidi: frame zipo Upande wa Kushoto

Kibatala: Upande wa pili pana frame?

Shahidi: Kuna Barabara

Kibatala: Kumbukumbu zako Uliwahi Kutoa Ushahidi Kuhusu Juhudi Kufanyika Kumtafuta Kiongozi wa Mtaa

Shahidi: Juhudi zilikuwa kumtafuta Shahidi. Mashahidi tuliwapata

Kibatala: Ufahamu wako pale kuna Kiongozi wa mtaa au Hakuna

Shahidi: Kila Eneo lazima kuna Kiongozi Wa Mtaa

Kibatala: Hao Mashahidi wawili uliwahi Kuwafuatilia Kama ni Viongozi wa Mtaa

Shahidi: Kimya

Kibatala: Mpaka mnaanza Kupata Taarifa kwa Washtakiwa Wa Pili na Watatu, Si palikuwa na Maulizo ya Maswali

Shahidi: Sahihi kabisa

Kibatala: Unafahamu Unapoanza Kumuhoji Mshtakiwa Inakuwa ni sehemu ya Uchukuaji wa Maelezo

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Digrrii Yako ya Sheria umepata lini

Shahidi: 2009

Kibatala: unafahamu Mohammed Ling’wenya alikuwa hajaishi Moshi kwa zaidi ya wiki Moja

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je kwa Uchunguzi wenu Lijenje au alitoroka baada ya kuwagundua na kuwaona

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je wasiri wenu Walikwambia nini Juu ya kutoweka Kwa Lijenje

Shahidi: Mimi sifahamu

Kibatala: Hati ya mashtaka inasema hivyo Vitendo vilivyotakiwa kufanywa vinajumuisha MOROGORO, ARUSHA, DAR ES SALAAM na MWANZA… Je ulieleza Kama kuna Mpelelezi alifika Morogoro?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je Katika ushahidi wako umeeleza kwenda mwanza Kwa kesi hii

Shahidi: Sikueleza

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji wewe Kama Msaidizi Wa RCO, Ulizungumzia Kuhusu Uwepo wa Njama za Kulipua Vituo Vya Mafuta Arusha… Kwa sisi wenyewe tuligundua kuhusu Arusha Kuna Mipango inaendelea

Shahidi: Ndiyo nimeongea

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Arusha Kituo A na B kilitaka Kulipuliwa

Shahidi: Sijamwambia

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama ARUSHA Kuna Kiongozi A na B walitaka Kudhuriwa

Shahidi: Kimya

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwa Mujibu wa Upelelezi watu tuligundua Maandamano haya yalipangwa Tarehe ngapi na Eneo la Kuanzia

Shahidi: Hapana Siku Mwambia

Kibatala: Unakumbuka Kuzungumzia Chochote Kuhusu Mkoa wa Mbeya

Shahidi: Nilitaja Mkoa wa MBEYA kuwa Upo Miomgoni Mwa eneo linalotakiwa Kufanywa tukio

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kati yenu Kuna Mpelelezi alienda Mbeya

Shahidi: Sijamwambia

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kuna Vituo Vya Mafuta MBEYA Vilitakiwa Kulipuliwa

Shahidi: Sijamwambia

Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kiongozi gani alipangwa Kudhuriwa

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Morogoro Vituo gani kwamba vinatakiwa Kulipuliwa

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Maandamano yalitakiwa kufanyika Wapi Mkoa wa Morogoro

Shahidi: Si kumwambia

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Sabaya alitakiwa Kudhuliwa tarehe ngapi Mwezi Gani na Mwaka gani

Shahidi: Hapana Sikumwambia

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Vituo Vinavyotaka Kulipuliwa Kilimanjaro

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mshitakiwa wa Kwanza alitakiwa anatakiwa kufanya katika Mipango hiyo ya Ugaidi

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Je specific Role aliyotakiwa Kufanya ADAM Kasekwa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Je Specific Role ya Mohammed Ling’wenya Kwamba alitakiwa Kufanya nini

Shahidi: Si kumwambia

Kibatala: Je Specific Role ya Freeman Mbowe katika Kutaka kutenda Ugaidi

Shahidi: Ndiyo nilimwambia

Kibatala: Ulimwambia Nini

Shahidi: Kwamba Ndiye aliyekuwa anaratibu

Kibatala: kuratibu ni suala pana, Nataka Kujua Kazi yake Katika huo Uratibu

Shahidi: Hapana Sijamwambia

Kibatala: Je unafahamu katika Maelezo yako Umemtaja ADAM HASSAN na Siyo ADAM HASSAN KASEKWA Maarufu Adamoo

Shahidi: Nimemtaja ADAM HASSAN ila nimemtambua

Kibatala: Je unafahamu Kwamba Mshitakiwa wetu hapa Mahakamani Anaitwa ADAM HASSAN KASEKWA Maarufu Kama Adamoo

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Hwa wote wawili ADAM HASSAN ndiyo ADAM HASSAN KASEKWA

Shahidi: Ndiyo Nimefanya Kwa Kumtambua

Kibatala: Unafahamu Kwamba Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya amehukumiwa na Mahakama kwa Makosa ya Ujambazi

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Je unafahamu Kwamba Sabaya Amehukumiwa Makosa ya Ujambazi Wakati wewe Ukiwa Afisa wa Polisi Arusha na ACP Kingai

Shahidi: Ndiyo natambua

Kibatala: Wewe Ulifanya Jukumu gani katika Kuzuia uhalifu Wa Sabaya

Shahidi: Siyo lazima Mimi lakini kuna wasaidizi waliopo Chini yangu walizipata

Kibatala: Na Unafahamu Kwamba Matendo Yake yalijirudia rudia

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji iwapo wewe na Afande Kingai Kama mlipata Taarifa za Intelijensia kuhusu Uhalifu wa Sabaya

Shahidi: Sikupata Taarifa

Kibatala: lakini unajua Mipango ya Uhalifu wa Wilaya ya Hai Nje ya eneo lako la kazi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwanini tusiseme Kwamba Kesi hii ninyi na Sabaya Mlitengeneza Kesi Kwa ajili ya mambo ya Kisiasa

Shahidi: Siyo Kweli kabisa

Kibatala: Huyu ASP Jumanne Yupo wapi

Shahidi: Yupo Arumeru

Kibatala: Kwamba hufahamu kwamba Jumanne amesimamishwa kazi baada ya kumbambikia Mzee mstaafu kuwekewa meno ya tembo kwenye mzinga wake wa nyuki chini ya usimamizi wa ASP Jumanne ambaye ni shahidi wenu?

Shahidi: Sifahamu najua yupo kazini..

Kibatala: Muda huu tunapo ongea yupo Ofisini?

Shahidi: Sifahamu sababu siwasiliani naye siku nyingi

Kibatala: Unajua tukio lake la kusimamia kumuwekea Mzee wa watu meno ya tembo

Shahidi: Nafahamu

Kibatala: Je ulimfahamisha huyu aliyetaka kudhuriwa Sabaya

Shahidi: Sijamwambia

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ukimfahamisha Kamati ya Ulinzi ya Wilaya Hai au Mkoa wa kilimanjaro

Shahidi: Hapana Siku Mwambia

Kibatala: katika Briefing zenu Je Kingai aliwambia kwamba kwamba ametoa Taarifa Kwa Kamati za Ulinzi na Usalama

Shahidi: Hakutuambia

Kibatala: Je katika Briefing Zenu Kingai aliwahi kuwaambia kuwa amemtaarifu Rais ambaye ni Kiongozi wa Nchi

Shahidi: hajatuambia

Kibatala: Labda Kufahamisha watu wa USALAMA WA TAIFA FA

Shahidi: Hapana hakutuambia

Kibatala: katika Maelezo Yako umezungumzia Kuhusu Jumanne Kuweka Sahihi yake Katika Hati ya Uzuiaji Mali

Shahidi: Hapana Sijasema

Kibatala: Statement Yako inasema “Tuliwa chukua watuhumiwa hao na kuwapeleka kituo cha Polisi Central kwa Mahojiano na tuliendelea Kumtafuta Mtuhumiwa Mwingine Moses Lijenje ambaye hatukuweza Kumpata, Je Kuna sehemu umesema Kwamba Mahojiano hayakufanyika

Shahidi: Hapo hakuna ila Ndiyo Maana Nimeelezea

Kibatala: Mheshimiwa Jaji tulikubaliana kuwa na health break, tunge’ Break kwa sababu bado ninayo maswali mengi na huyu shahidi.

Wakili wa Serikali: sawa mheshimiwa

Jaji: unategemea muda gani zaidi

Kibatala: Labda nusu saa na zaidi

Jaji: Mpaka saa 8:30 tutarudi kuendelea

Jaji Kaingia, Kesi inatajwa na Kibatala anaendelea na shahidi.

Kibatala: Nani alimpekua Adam Kasekwa!?

Shahidi: Afande ASP Jumanne alimpekua Akamkuta Adam Kasekwa na Karatasi yenye Majina Mbalimbali

Kibatala: Je Karatasi hii yenye namba za Simu mli’ connect na tuhuma au ilikuwa ya kwake binafsi

Shahidi: Ilikuwa Connected

Kibatala: Kwa hiyo Ipo kwenye Hati ya Kumiliki Mali

Shahidi: Ipo

Kibatala: Na Ikija Karatasi ya Hati ya Kushikilia Mali nitaiona

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Nani anayo Shahidi: Sijui

Kibatala: Unaweza Kujua Kama hizo namba za Simu zinahusika a na Shauri hili hapa Mahakamani

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Pale Rau Madukani, nani alikuwa Arresting Officer

Shahidi: Mimi hapa

Kibatala: Unafahamu au hufahamu kwamba ukisoma pamoja kifungu cha 23 cha CPA pamoja na PGO, arresting person ndiyo anapaswa kufanya search, Je unafahamu hilo?

Shahidi: Siyo lazima

Kibatala: Kwa ruhusa ya Mahakama nakuonyesha PGO 357(2) nakuletea Shahidi: KAA NAYO TU, SOMA TU

Kibatala: Anasoma 357(2) ya PGO

Kibatala: Kwa ufahamu wako nilivyosema anayetakiwa kushikilia mali ni Arresting Officer au Siyo?

Shahidi: Siyo lazima

Kibatala: Ukishapata offensive Weapon Ikishakuwa Seized inakabidhiwa CRO, Unakubaliana na Mimi

Shahidi: Inategemea na Kituo

Kibatala: Mwambie Jaji hii offensive weapon Luger C100 Iliingizwa Kwenye CRO

Shahidi: Atazungumzia Mwingine

Kibatala: Ufahamu wako ipo au haipo Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Chain of custody ikoje Imeanza kwa nani

Shahidi: Kwa Goodluck

Kibatala: Siyo Jumanne?

Shahidi: Jumanne

Kibatala: Unafahamu au hufahamu Kwamba Goodluck alikaa na hiyo Bastola kuanzia ameichukua kwa Jumanne Mpaka Dar es Salaam

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je ulishuhudia watuhumiwa wakikabidhiwa kwa CRO Dar es Salaam

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Ulishuhudia Handing over ya Bastola Kutoka kwenu kwenda CRO

Shahidi: Sikushuhudia

Kibatala: baada ya Makabidhiano ya Watuhumiwa ulishuhudia Mpaka Mwisho au Uliondoka Kabla

Shahidi: Handing over unawapa Watuhumiwa na Karatasi ya Reference

Kibatala: Ulizungumzia Chochote kwamba Ulishuhudia Jumanne na Goodluck wakibadilishana Makaratasi

Shahidi: Sikushuhudia

Kibatala: Je kwa ufahamu wako Wewe Kama Askari Mwenye LLB, Je Palipaswa kuwa na Makabidhiano ya Makaratasi au Siyo lazima

Shahidi: Lazima yawepo

Kibatala: Je kuna kazi Nyingine 10 Mwezi 08 2020 ya Kiupelelezi ulishiriki Kufanya

Shahidi: Ndiyo nilishiriki

Kibatala: Na Kati ya hao ni Maafisa wa Jeshi wa zamani

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mmoja wapo ni Gabriel Mhina

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kama ni vikao gani vilifanyika Aishi Hotel

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Morogoro Katika sehemu fulani washtakiwa Walikaa Kupanga Ugaidi

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mshitakiwa wa 4,3,2, 1 kwamba walikaa Mkoani Arusha Kupanga Njama za Ugaidi

Shahidi: Hapana Sijamwambia Kibatala: Ni wakati gani mlikuwa na description za Watuhumiwa Mlipata Muda gani kabla

Shahidi: Masaa 6 kabla

Kibatala: Ulisema kuhusu ku’ procure search warranty au hukusema

Shahidi: SIWEZI KUJIBU

Jaji: SHAHIDI JIBU SWALI

Shahidi: SIKUSEMA…….

Kibatala: Nilikusikia Kwamba Ulisema Arusha Lijenje alikuwa na Dada Yake, Je Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulimtajia Mheshimiwa Jaji

Shahidi: Hapana Sikumwambia

Kibatala: Je unayajua Majina ya huyo Dada

Shahidi: Hatukutajiwa

Kibatala: Kwa hiyo Mlienda Arusha Kumtafuta Dada Wa Lijenje

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: katika Maelezo Yako Ukiweka Muda ulifika Dar es Salaam Muda gani

Shahidi: Niliweka Muda

Kibatala: Kwamba Asubuhi au Uliweka na Saa na Dakika

Shahidi: Niliweka

Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba tupewe nakala halisi ya statement ya Mahita kwa mujibu wa 154 na 155 ya Sheria ya Ushahidi Mawakili wa Serikali Wananong’onezana hapa.

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi

Kibatala: Shahidi Soma Kote kisha Taja Exactly Sehemu Uliyo andika Muda

Shahidi: Nisome Kwa sauti

Kibatala: Ndiyo kwa Sauti

Shahidi: Usiku wa Tarehe 06.8.2020 tuliondoka kuelekea Dar es Salaam na kufika 07.8.2020 Asubuhi

Kibatala: Hapo wapi Umetaja 11?

Shahidi: Leo kwenye kiapo

Kibatala: Mimi nakuuliza maelezo yako

Shahidi: Hakuna

Kibatala: Je ungependa maelezo yako yapokelewa MAHAKAMANI?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mheshimiwa Jaji tunaomba Maelezo yake ya pokelewa Kama Kielelezo Cha Upande wa Utetezi

Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi Mheshimiwa

Jaji: Yanapokelewa Kama Kielelezo namba p3

Wakili wa Serikali: Tunaomba kipokelewe na kusomwa kwa Ule ule utaratibu Shahidi Mahita Omary Mahita anasoma Kielelezo

Shahidi, Inspector Mahita Omary Mahita kamaliza kusoma Kielelezo…

Kibatala: Katika Maelezo yako hakuna mahala umezungumzia kuhusu kumpekua Mohamed Ling’wenya

Shahidi: Sijazungumzia

Kibatala: Na Ulishiriki au Hukushiri

Shahidi: Sikushirki

Kibatala: Na Hukuwahi Kufika Nyumbani Kwake Kimara ukiwa Chini ya Kiapo

Shahidi: Sijawahi

Kibatala: Katika Statement hujazungumzia lolote kwamba Gari iliharibika Njia panda Himo

Shahidi: Sijazungumzia

Kibatala: Pia katika Statement Yako Ujazungumzia kuhusu Kwenda Boma Ng’ombe Kula Nyama

Shahidi: Sikuzungumzia

Kibatala: Katika Ushahidi Wako hakuna Mahala Umezungumzi kuhusu Kuchukua Finger Prints katika Eneo la tukio

Shahidi: Sijazumgumzia

Kibatala: PGO ya 229 Order 4 ambayo Heading ni Handing of Exhibit Kibatala anasoma yote (ni makingereza)

Shahidi: Inazelezea Scene of Crime, Eneo ambalo Kimetokea Tukio, lakini siyo On Possession ambapo Mtu amekutwa Kizibiti

Kibatala: Kwa hiyo ni sahihi Kwamba PGO inasisitiza Kutunzwa kwa Finger Prints eneo ambalo Kielelezo kinakutwa

Shahidi: Kwa Eneo la Tukio (Scene of Crime)

Kibatala: Ulimwambia Mhe Jaji Kwamba ni sehemu ya Mpango wenu Kuweka Surveillance

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kwamba Freeman Mbowe alishiriki Uchaguzi wa Mwaka Jana Jimbo la Hai, sahihi

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Kwa kuwa tayari mlikuwa na Maelezo ya Onyo tayari ya Washtakiwa baadhi, Je Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulitaarifu Mamlaka zingine Kuhusu Mbowe Kwamba alikuwa na Tuhuma Za Ugaidi.

Shahidi: Kimya

Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kwamba Freeman Mbowe alishiriki Uchaguzi wa Mwaka Jana Jimbo la Hai, sahihi

Shahidi: Ndiyo nafahamu

Kibatala: Kwa kuwa tayari mlikuwa na Maelezo ya Onyo tayari ya Washtakiwa baadhi, Je Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulitaarifu Mamlaka

Kibatala: Kwa ufahamu wako wewe Mpaka wewe Unauliza Majukumu yako Kuhusu suala hilo, Uliwahi Kujulishwa na Afande Kingai kuhusu Kuchukua Hatua kama hizi

Shahidi: Hapana Sijawahi

Kibatala: Uliwahi Kumshauri ACP kingai atoe Taarifa kwa Afisa wa Uchaguzi

Shahidi: Hapana

Kibatala: Uliwahi kumshauri ACP Kingai ili aweze kudhibiti huyu mastermind wa vitendo vya kigaidi kuhusu mienendo ya kusafiri nje ya nchi

Shahidi: Hapana

Kibatala: Kingai aliwahi kukwambia kwamba alishawahi kuwashauri watu wa USALAMA WA TAIFA kuhusu kumdhibiti Master Mind wa Ugaidi?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ulishawahi wewe au wenzio kwa kesi hii kuwa na voice records za Mbowe au kuagiza zikachukuliwe kwenye makampuni ya simu?

Shahidi: Hapana sijawahi

Kibatala: Ulishawahi kumshauri Boss wako Kingai kuwasiliana na makampuni ya simu kuhusu kwenda kuchukua sauti za simu za Mbowe

Shahidi: Sijawahi kumshauri

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama wewe wenzio mlishawahi kuweka vinasa sauti nyumbani kwa Mbowe au ofisini ilitusikie pasipo shaka alipanga mipango ya ugaidi

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Umesema mshtakiwa 1, 2 na 3 hawakuwa na mali zozote zile

Shahidi: Ndiyo Kibatala: Je unafahamu kwamba palifanyika jitaihada za kwenda kutafuta vitambulisho vyao vya kupiga kura na NIDA

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Wewe unaona Kwako ni sawa Kwamba washtakiwa hawana chochote hata Pesa

Shahidi: Mbona watu wengi wanatembea na Pesa

Kibatala: Umemwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba washtakiwa Walikuwa wanaishi Moshi pale Rau

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wakati unafanya surveillance washtakiwa Walikuwa wanafanya nini

Shahidi: walikuwa wamekaa tu

Kibatala: ulisema ulimuona yoyote akifanya Usajili wa Simu

Shahidi: Hapana

Kibatala: wakati unawakamata walikuwa wanafanya nini?

Shahidi: Walikuwa wanatembea kuja kwangu

Kibatala: Wakati unamkamata Bwire, Kingai alikuwepo

Shahidi: Alifika Jioni

Kibatala: Je Urio alifika lini Mbweni

Shahidi: Sifahamu kabisa

Kibatala: Mpaka leo hujawahi kumuona Urio

Shahidi: Sijawahi kumuona kabisa

Kibatala: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Wakili wa Serikali: Wakati mnaenda Moshi Kutoka Arusha Mlikuwa watu wangapi?

Shahidi: Wakati tunatoka Moshi tulikuwa watu sita ila wakati wa ukamataji tulikuwa watano. Mmoja alikuwa dereva

Mtobesya: OBJECTION Jambo la Dereva ni Jipya, Hakutaja Dereva

Jaji: Wewe Hukusikia, alitaja dereva. Mimi nilisikia. Na nilisikia akisema mmoja ya waliotoka Arusha, mmoja alikuwa dereva wa RCO.

Jaji: anasoma majina, DC Aziz likiwemo, lakini hakuna neno dereva

Mtobesya: Neno DC AZIZI nilisikia ila hakusema hapo DEREVA..

Mallya: Wale waliohusika na Ukamataji ni Sita Ndiyo alitaja

Mtobesya: Na akija mtu mwingine akisema mlikuwa watano siyo sita, yeye akasema watano?
Mallya: Wale waliohusika na Ukamataji ni Sita Ndiyo alitaja
Jaji: kama jibu Muhimu mnalihitaji tutawapa Re-examination.
Wakili wa Serikali: Sawa
Wakili wa Serikali: Elezea wakati wa ukamataji
Shahidi: Tulikuwa watu watano na Mmoja alikuwa Kwenye Gari
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali huhusiana na surveillance ukasema ulijiridhisha mwenyewe. Uliulizwa kuhusu tarehe ya maelezo yako. Je tarehe sahihi ni ipi?
Shahidi: Baada ya kupita tukaona ndiyo wale, na ilikuwa hakuna description ya nguo ya watu kama wale.

Shahidi: Tarehe 10 Mwezi 08 siyo Mwezi wa 09.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kwenye Maelezo umeandika Uhalifu na siyo Ugaidi, Je uhalifu ulimaanisha nini?
Shahidi: Uhalifu ni jumla inayobeba Matendo mbalimbali ya kigaidi kama kuchoma vituo vya mafuta, maandamano ambayo hayana kokomo na kuwadhuru viongozi wa serikali.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Kibandaumiza, ikaleta maneno. Hebu fafanua.
Kibatala OBJECTION itakuwa sawa kweli?

Jaji: Nakubaliana na wewe.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa ukiwa Moshi uliwapiga, ukajibu hayo ni maoni yake. Je, ulimaanisha nini?
Shahidi: Sikuwapiga, tulikaa nao vizuri.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana specific role ya kila mtu. Ieleze Mahakama sasa wewe aulichoambiwa katika briefing ni kitu gani uliambiwa.
Shahidi: Niliambiwa kuhusiana na kikundi kinachotaka kufanya vitendo vya kigaidi, nikisema kuchoma moto vituo vya mafuta, maandamano ya Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Mwanza na Morogoro, kuzuia barabara na mamiti.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana kukabidhiwa kwa pistol, eleza ulichoshuhudia.

Shahidi: Nilishuhudia wakikabidhiana kama nilivyoeleza Mahakam

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa ya kwangu ni hayo tu.

Re-cross examination

Jaji: Kuhusiana na hilo ambalo mlikuwa mnahitaji kufanya re-cross examination.

Mtobesya: Mheshimiwa Naomba nifanye re-cross examination

Jaji: Specifically kwenye eneo hilo tu.

Mtobesya: Unakumbuka ulisema wakati mnamkamata Mlikuwa sita.
Shahidi: Nlikwambia watano

Mtobesya: Ni ushahidi wako kwamba hukusema watu sita?

Shahidi: Mimi nilisema watu watano. Ndiyo tulienda kuwakamata

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba utukumbushe

Jaji: “Tulitoka Arusha kwenda Moshi tukiwa sote na sisi ndiyo tuliokamata.
Tuliokamata tulikuwa sita.”

Mtobesya: Ni sahihi, ndivyo nilivyokuuliza?

Wawili ndio tuliowazuia na kuwawekachini ya ulinzi.

Shahidi: wawili ndio tuliokamata

Mtobesya: Rekodi za Mahakama zinasemaje sasa?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji, naomba maelezo yangu haya Ndiyo yachukuliwe

Mtobesya: Kwenye Maelezo Yako Uliyoandika Ulieleza Kama mlikuwa watano au Sita

Shahidi: Sikueleza

Mtobesya: Mheshimiwa, ni hayo tu.

Jaji: Shahidi tunakushukuru kwa ushahidi wako

Jaji: Shahidi tunakushukuru kwa ushahidi wako

Jaji: Kama jibu muhimu mnalihitaji tutawapa

Re:Examination

Wakili wa Serikali: Sawa

Wakili wa Serikali: Elezea Wakati wa Ukamataji

Shahidi: Tulikuwa watu watano na Mmoja alikuwa Kwenye Gari

Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana na Surveillance Ukasema Ulijiridha Mwenyewe

Shahidi: Baada ya Kupita tukaona ndiyo wale, Alikuwa hakuna description ya nguo ya watu wale

Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Tarehe ya Maelezo yako, Je tarehe Sahihi ni Ipi

Shahidi: Tarehe 10 Mwezi 08 siyo Mwezi wa 09

Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kwenye Maelezo umeandika Uhalifu na siyo Ugaidi, Je uhalifu ulimaanisha nini

Shahidi: Uhalifu ni jumla inayobeba matendo mbalimbali ya kigaidi kama a Kuchoma vituo vya mafuta, maandamano ambayo hayana kikomo na kuwadhuru viongozi wa serikali

Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu kibanda umiza, ikaleta maneno, hebu fafanua

Kibatala: OBJECTION itakuwa sawa kweli

Jaji: nakubaliana na wewe

Wakili wa Serikali: Uliulizwa ukiwa Moshi uliwapiga, ukajibu hayo ni maoni yake, Je ulimaanisha nini

Shahidi: Siku wapiga tulikaa nao vizuri

Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana specific Role ya Kila Mtu Ieleze Mahakama sasa wewe aulichoambiwa Katika Briefing ni Kitu gani uliambiwa

Shahidi: Niliambiwa Kuhusiana na Kikundi Kinachotaka Kufanya Vitendo Vya Kigaidi, Nikisema Kuchoma Moto Vituo Vya mafuta.

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji huyo ndiyo Shahidi Tuliyekuwa naye. Tunaomba hairisho mpaka Jumatatu Tarehe 08 ya Mwezi wa 11 ilituweze kuendelea na mashahidi wengine

Jaji: Utetezi

Kibatala: Hatuna Pingamizi Jaji anaandika kidogo

Jaji: Maombi ya hairisho yamekubaliwa. Shauri linaahirishwa Mpaka Jumatatu 8/11/2021 Washtakiwa watabaki rumande chini ya magereza mpaka tarehe hiyo

Like